Je, ni kweli flyovers na ndege zetu hazina msaada wowote kwa mwananchi anayeishi Nanyamba au Kyabakari?

Je, ni kweli flyovers na ndege zetu hazina msaada wowote kwa mwananchi anayeishi Nanyamba au Kyabakari?

Huyo Jiwe wenu atapigiwa kura na flyover , Madaraja Stiegersgorge , Standard Gauge na Bombadier zake sisi hazituhusu na uwanja wake wa chato na mbuga yake ya Burigi ndio vitampigia kura si ndio ameona vya muhimu kuliko binadamu.
 
Hivyo ulivyovitaka ni vitu muhimu lakini ni vidogo sana kwa Taifa. Havihitajiki kuwa wimbo wa kila siku.

Kuna wakati niliishi Bamako, Mali - nchi ambayo robo 3 ni jangwa. Ndani ya mwaka mmoja flyovers zinajengwa hata 3, husikii hata kwenye TV wakitangaza. Unapita barabarani, unashangaa "ala, kumbe na hapa wanajenga flyover!". Tena zilikuwa ni flyovers kamili siyo kama lile daraja la TAZARA.

Tunapiga kelele sana za mafanikio kwa vitu vidogo sana kwa Taifa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hata hapo Kenya,wamejenga maflyover Nairobi, Mombasa,naivasha na kule eldoreti Ila huwezi kusikia makelele Kama haya ya hapa kwetu kwa watu waliokosa exposure na washamba
 
mimi sipingi kupishana kwa hoja.
"BALI SIASA CHAFU"..
tangu dunia iumbwe hakuna +ve bila -ve..
Kwa hyo kila mtu haheshimu upande wa mwenzie bila chuki,kupigana,kutekana,kuuana n.k..
Sisi ni watanzania tupendane.

Sent from my SM-G928F using JamiiForums mobile app
 
Mafanikio makubwa yanagharama zake. Mwaka huu mshahara umeongezwa.
Kuhusu ajira ni lazima ujue haiwezekani kila mtu akaajiriqa na serikali. Serikali inatengeneza mazingira mazuri kupitia PPP na huko ajira rasmi na zisizo rasmi hutokea.
Ajira za walimu zimetangazwa. Najua bado eneo hilo lina changamoto ila tutafika pazuri zaidi
Mazingira gani ya PPP yanatengenezwa? Huoni wafanyabiashara wakibambikwa makodi na kubughuziwa hadi kufunga biashara na wengine kufariki?

Unajua Ali Mufuruki mlimfanya nini nyie watu kwenye kodi?

Unajua Shamte marehemu mlimfanya nini nyie watu???

Unajua Manji mmemfanya nini nyie watu???
 
Uliyoyasema ni mambo ya msingi kabisa na yana faida kubwa mno, tatizo la babu yenu ni kuwa mkali hovyo anapokumbushwa kutekeleza shughuli za maendeleo kwa kufuata katiba na sheria za nchi, yuko tayari kuua kisa kakoselewa, hizi ni kodi za watz tunapaswa kujua kila senti imetumikaje na asilete ukali wake tunapohoji, kama anakereka kushauriwa na kukosolewa akae pembeni wapo wanaoweza kuendesha nchi kwa kuzingatia katiba na aheria
 
Kwa hiyo hayo mengi aliyofanya ndo yamepelekea kuongeza only USD 100 kwenye GNI na kuvuga kabisa market systems za mazao ya korosho,kahawa,mbaazi na tumbaku huku ukuaji wa uchumi ukiongezeka kutoka 7% hadi 4% si ndiyo mkuu?

Shida Ni pesa yote ifike hazina na ipangiwe majukumu...

Bureue change zilifungwa na Sheria taratibu kubadilishwa maamuzi yote Ni bot...

Serikali haiwezi kufanya biashara wajifunze kupitia Tanesco... Sekta binafsi Ina umuhimu wake ...
 
Mazingira gani ya PPP yanatengenezwa??? Huoni wafanyabiashara wakibambikwa makodi na kubughuziwa hadi kufunga biashara na wengine kufariki???

Unajua Ali Mufuruki mlimfanya nini nyie watu kwenye kodi???

Unajua Shamte marehemu mlimfanya nini nyie watu???

Unajua Manji mmemfanya nini nyie watu???

Hiyo ppp Haina Cha maana... Wapi mwendo Kasi dar... Hakuna faida na mkopo unaatakiwa kulipwA...
 
Shida Ni pesa yote ifike hazina na ipangiwe majukumu...

Bureue change zilifungwa na Sheria taratibu kubadilishwa maamuzi yote Ni bot...

Serikali haiwezi kufanya biashara wajifunze kupitia Tanesco... Sekta binafsi Ina umuhimu wake ...
Kuna genius anaitwa Magu anaetaka kuifanya Tanzania kuwa Kama ulaya in 5 years baada ya kuongeza USD 100.00 kwa miaka mitano
 
Kwa kifupi vina msaada kwa kuwa ni miundombinu na ni vyombo vya usafiri,Ila pia tunaona kuna mengi sana ya kukosoa
 
Kuna genius anaitwa Magu anaetaka kuifanya Tanzania kuwa Kama ulaya in 5 years baada ya kuongeza USD 100.00 kwa miaka mitano

👆😆😆

Hata kigoma na bukoba walikua na ndoto hizo...

Usinipotezee muda Kuandika ndoto za mchana... Miaka 59 madarakani na bado watu Wana shida ya maji?
 
Tujenge uchumi ulioshifikishi.

Acha kuangalia Economic Growth focus na Economic Development.

CCM inatakiwa kuangalia sanaa na sekta ya uchumi inayoshirikisha wengi na tuache hizo sekta zinazohusu wachache.

#YNWA
 
Hivi kwa akili tu ya kawaida huu uchumi wetu wa kuvuta na kamba Mtu anasifia kununuliwa ndege kwa cash??..

By the way maendeleo ni hatua kwa hatua hata ww ipo siku ubongo wako utaendelea na utausoma huu Uzi wako tena, ninaamini utajidharau sana na utajiona mjinga kwa kutetea mambo unayodhania kuwa unayajua kumbe hujui.
Ajabu ni kwamba hizo ndege wanazojisifu nazo, Tangu zinunuliwe na zianze kupiga rooute hazijaweza kurudhisha ata nusu ya pesa iliyotumika kuzinunua
 
Yaaani Vinachekeshaga sanaaa...

Sasa Mtu Anapoitumia Huduma Ya Serikali Mfano Barabara,Flyovers,Shule,Zahanati,Viwanja vya michezo....

Kote huko inakuwa Ni KODI YAKE TU iliyotumika KUYAWEKA HAYO?!!!

Jamii Nikutegemeana Maana Ninavyopenda KULA UBWABWA wa Kutoka Mbeya Haina Maana nimekula PESA YANGU....yaani ile NOTI NYEKUNDU ya buku 10 iweze kuyeyushwa na kunyonywa na PARIETAL cells za UTUMBO WANGU MDOGO?!!!
Barabara, Flyovers, Shule,Zahanati, Viwanja vya michezo Viko wapi hapa kwetu kijiji sijaona hata komoja
 
Tujenge uchumi ulioshifikishi.
Acha kuangalia Economic Growth focus na Economic Development.
CCM inatakiwa kuangalia sanaa na sekta ya uchumi inayoshirikisha wengi na tuache hizo sekta zinazohusu wachache.

#YNWA
Sawa. Kipi Ni kipi? Ni lazima mmoja aanze halafu anamvuta mwenzake. Economic growth si ndio inapelekea economic development?
 
Sawa. Kipi Ni kipi? Ni lazima mmoja aanze halafu anamvuta mwenzake. Economic growth si ndio inapelekea economic development?
Economic growth ya TZ haiakisi ECONOMIC DEVELOPMENT hataa..

Ndio maana tunajenga na kununua vyotee ila hali ya wananchi maskini imebaki kuwa MASIKINI.

Tujikite na sekta zilizo shirikishi.

#YNWA
 
Back
Top Bottom