Je, ni kweli Idd Amini alikuwa shujaa wa Afrika, Nyerere alitumiwa na wazungu kumchafua?

Dah mwisho wa siku Kenya akatupiga bao....bila ile vita sisi ndo tungeongoza East afrika kiuchumi

..Ni kweli uchumi wetu uliyumba kwasababu ya vita vya Kagera.

..lakini vita sio sababu pekee iliyosababisha uchumi wetu uyumbe.

..naamini Mwalimu Nyerere alichelewa kufuata ushauri wa kurekebisha uchumi na matokeo yake nchi ikaenda mrama.

..makada wa Ccm waliokuwa wanatoa hoja za kurekebisha uchumi kwa wakati huo waliitwa WASALITI na " chawa " waliokuwa wakisisitiza tukomae na Ujamaa na uchumi dola.
 
Lakin mkuu kama Urusi ingeshinda vita baridi na Ujamaa kutawala dunia,tungetoboa
 
Lakin mkuu kama Urusi ingeshinda vita baridi na Ujamaa kutawala dunia,tungetoboa

..sina uhakika.

..kwasababu pamoja na kuwa Wajamaa Soviet Union hakuwa mfadhili namba moja wa miradi yetu ya kiuchumi.

..Mwalimu alikuwa mbishi sana kubadilika nadhani mpaka nchi za Skandinavia zikatuchoka.
 
Aliwatimuaga wahindi- waliokuwa wafanya biashara uganda

Wahindi wakatimkia marekani na wakafanikiwa huko balaa kwenye biashara zao na badala ya kumlaani Iddy Amini wakamshukuru kwa kutimuliwa kulee na Iddy Amini na kusema wangekaa hata miaka mia uganda wadingepata mafanikio yalee waliyoyapata marekani kwa mda mfupi sana kwenye biashara zao

Wameweka picha za Iddy Amini kwenye maduka yao huko marekani kama shukrani kwa walibyofukuzwa na huyo jamaa
 
Wa kufkuza mabepari mchana kweupe,
Wazungu, waarabu na wahindi wote kwaooo

Sasa hii nadhani iliwaumiza wazungu wakamtumia nyerere kumuangusha mwafrika mwenzake, kisa wazungu?
hao ndio adui wa mwafrika? baada ya kuwaondoa Uganda ilinufaika nini?
 
Nia ya kumpiga tunayo sababu ya kumpiga tunayo na uwezo wa kumpiga tunao kumbe nyerere alikuwa na nia ya kumpiga iddi amin toka muda mrefu na vita ile imetutia umasikini haswa kisa tu kumuweka madarakani mkatoliki mwenzie obote
 

Nyerere ndiye alianza kwa kumchokonoa Amin, Nyerere alihifadhi waasi wa Uganda akina Museveni na kuwapa mafunzo ya kijeshi na matunzo.
Huo ulikua uchokozi mbaya sana, hebu waza hapo msikie Kenya inawapa mafunzo maelfu ya wapiganaji waje kuipindua serikali ya Tanzania.
Historia ya huu ugomvi huwa hamtaji hiki alichokifanya Nyerere, huwa mnaanzia pale pa Amin kuvamia Kagera.
Nimekua Uganda, ukitaja mabaya ya Amin unaweza hata ukapigwa, wanamkumbuka sana, hususan leo ambapo wengi wanaamini Wahindi wameachiwa nchi wafanye watakavyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…