Je, ni kweli kuwa ulimwengu huu ni kifungo cha nafsi?

Je, ni kweli kuwa ulimwengu huu ni kifungo cha nafsi?

Nondo
Dada nikupongeze sana kwa kuleta elimu hii ya utambuzi.
Ni kwanini watu wengi hushikilia mawazo yao hasa mawazo mabaya badala ya kushikilia mawazo mazuri?

Umeshawahi kuongea na nafsi yako kibinafsi? Umeshawahi kujaribu kuchunguza kinachoendelea akilini mwako? Mfano kuchunguza unawaza nini? Kuna wakati unakuta unawaza mawazo mabaya na unaweza ukajisemea mwenyewe "Acha kuwaza mawazo mabaya, hayana umuhimu" huku ukijiambia mwenyewe.Unaweza kuwa makini na mawazo yako na kujiuliza kama unavyouliza mtu mwingine au kuyachunguza kama unavyochunguza hali ya nje.

Kushindwa Kuwa makini na Jambo.
Tunaposhindwa kuelewa jambo kwa kina wengi hujikuta wanaweka fikra duni na kushikiliwa na mawazo hasi. Tunaposhindwa kuelewa hali iliyopo basi tunaweza kuzidi kutawaliwa na wasiwasi, hasira, ujinga woga n.k lakini tukielewa jambo au hali kwa uhalisia wa pande zote mbili yaani kwa upande unaotetea na upande unaopinga au kwa upande hasi na upande chanya tunaweza kufanya maamuzi sahihi na kutoshikiliwa na mawazo bila kujiongoza.

Badili wazo au Fikra mbaya kwa Kuipa Fikra nzuri/chanya kipaumbele.
Huwezi kuondoa mawazo au fikra mbaya kwa fikra mbaya bali vyote hivyo huondolewa kwa fikra nzuri. Mfano unapoona hasira inakutawala, ili kuiondoa hasira weka mtazamo wako kwenye upendo na hasira yenyewe itaondoka bila kipingamizi. Ibadili hasira kwa kutanguliza upendo na hasira yenyewe itaondoka kwani hakuna upendo unaokaa na hasira. Kama vile hakuna giza linalokaa na mwanga ndivyo hakuna mawazo au fikra mbaya inayoweza kukaa na fikra nzuri. Fikra nzuri huondoa fikra mbaya na mawazo mazuri huyaondoa mawazo mabaya.
Vivyo hivyo kinyume chake pia.

Ni vyema kujitawala kwa kinachoendelea akilini na kukishinda badala ya kukiruhusu kitoke katika ulimwengu wa nje. Na ndio maana wengi hujifunza meditation/taamuli kuweza kujizoesha kujitawala na kutawala hisia zao.

Mawazo huumba!
Unapokuwa unayapa kipaumbele mawazo mabaya au mazuri, basi yataumbika kwenye maisha yako. Yawe ya uongo au ya kweli, basi tegemea matokeo yake. Na matokeo hayo ni moja ya kazi ya ufahamu wako lakini wengine wanakuwa wanalalamika na kutupia lawama mara kwa shetani, mungu, binadam wenzao nk jambo ambalo sio.
Kuna matokeo ya mawazo yetu ya aina nyingi

Kuna matokeo ambayo hujitokeza ambayo ndio mabaya sana! Matokeo hayo ni yale yanayomuwekea mtu kizuizi cha kupokea ukweli.
Kuna mawazo mengine pia humfanya mtu kuwa huru kupokea ukweli muda wowote.

Wazo ni mbegu.
Unapopanda wazo na kulipalilia hugeuka neno na hatimae kitendo. Hivyo chunga sana ufahamu wako usijekutekwa na mawazo mabaya maana ndio yatakuwa maisha yako.

Kusema dunia ni kifungo cha nafsi sio kweli.
Tunaposema nafsi tunamaanisha mtu halisi/ufahamu au yule mtu wa ndani. Hivyo mtu huyo nafsi/binafsi aweza kujifunga mwenyewe kwa kujua au kwa kutokujua kwa mawazo yake mwenyewe. Nasema yake mwenyewe kwasababu hata akiyasikia kwa watu/mtu lazima kwanza yatapita kwenye ufahamu wake ndio achague kuyaamini au kwa kutokuyaamini.
Mfano unaambiwa kuna kiumbe anaeitwa shetani, wewe badala uchunguze, upime, na kuhoji, unayaamini moja kwa moja alafu hutaki kusikia zaidi ya hayo. [emoji30]UMEJIBLOCK.

Ishi ukiwa upo tayari kupokea ukweli muda wowote. Hapaswi kujifungia ndani ya sheria walizoweka watu fulani.sheria zao zipokee na uzichunguze... Je? Ni za kweli? Kama sio za kweli jiulize zina walau ukweli kidogo? Kama upo ukweli walau kidogo, uchukue uuishi huku ukijua siku zote ukweli unaendelea kuvumbuliwa.

Nimalizie kwa kusema kwamba hakuna mtu yoyote awezae kuufunga ufahamu wa mtu mwingine. Aweza kufunga ufahamu wake lakini sio wako.
Hata akikufundisha mafundisho gani! Ni hiyari yako kuyaamini au kuyakataa.
Aweza kuufunga mwili lakini sio nafsi. Nafsi yako wewe mwenyewe ndio waweza kuifunga na kuifungua au kuifunga na kuifunga zaidi.

Binadamu wenzako waweza kuufunga mwili wako lakini sio wewe halisi.
 
Hahaha dahh nimecheka sana
1:uongo wa hii falsafa ni nini?
2:NI KWELI ndugu tuliumbwa tukiwa wakamilifu, na swala la kuingia gizani si kweli tuliingia wote... labda ungesema uliingia wewe na baadhi ya unaowajua ulioingia nao, hilo linajidhihirisha katika mfano wako wa kuua kwamba si wote walio gizani ila ni wachache tu walioamua kuingia kwa mapenzi yao binafsi
3:upo sawa kusema ukamilifu bado tunao, nakupongeza kwa hilo hivo basi wakati wa kurudi kwenye chanzo chako halisi upo pia
4:kumbuka kinachokufa ni mwili tu bali ufahamu wako utaendelea kubaki hivyohivyo... je unaamini mungu ataweza kukuhukumu wakati ufahamu wako wote umepotea na huna kumbukumbu yoyote ile ya kile ulichofanya duniani... je hii huoni kama itakuwa uonevu?
#nategemea maswali zaidi kutoka kwako mpaka pale utakaporidhika...
 
Asante sana.
Ni matumaini yangu kuwa wote kwa pamoja tutajitahidi kuendeleza elimu hii itakayosaidia watu kuamka na kujitambua
Hiki ulichokiandika kinatoa picha ya mambo makuu matatu.
Kwanza, elimu. Pili, uelewa. Na tatu, utafiti. Una matatizo kwenye hivi vitu vitatu.
Hujui ukweli ni nini? Na hujui nini kilichomo ndani ya mtu? Na hicho kilichomo ndani ya mtu ni mali ya nani?
Bado hujaweza kujua jambo dogo la mwili wako unafanyaje kazi? Lakini pia hujui kama kujitambua ni jambo lililo la kisayansi au lililo nje ya sayansi? Haya machache huyajui, lakini umeandika!
 
Mkuu huu uzi Umenifanya nifikirie vitu kadhaa kwa wale wenzangu wanaokariri vitu..
Mf;,Mtu anaenda kusali ili siku moja asijekuchomwa moto.
Nawakati hajui.
Yeye ni nani.
Ametoka wapi.
Anakwenda wapi.
Maisha ni nini?
Mungu ndo nini?.
Umhimu wa uhai wako ni upi?
Haki ya Mungu ndo ipi?
Umeshahitimu kutimiza mapenzi ya kile unachokitegemea?

Ujinga wa waumini wengi ndo hufany mambo kuwa Magumu zaidi kwasababu wannasema wanatimiza mapenzi ya Mungu ili siku moja nisiendeMotoni nami najiuliza unaweza kweli kutimiza mapenzi ya Kitu kilicho nje ya uwezo walko? Kwasababu weww umekuwa mtu wa kutubu je siku ukifa na bado
Kimsingi unachojaribu kutuambia hapa kwamba unakielewa siyo sahihi.

Wakati wa maisha ni vizuri Kutafakari, kutafuta na kujiuliza mambo mengi.
Hivi: unachokiona, unachokiwaza au unachokihisi ndiyo ukweli?

Je, ni makubaliano, au ni kadiri ilivyo katika jamii ndiyo ukweli?

Umesema Mungu ni nadharia tu. Lakini je, nadharia ni nini?
 
Kwa maana walio hai wanajua kwamba watakufa;+ lakini wafu, hawajui lolote kamwe,+ wala hawana malipo tena, kwa maana kumbukumbu lao limesahauliwa.+ 6 Pia, upendo wao na chuki yao na wivu wao tayari zimepotea, 10 Yote ambayo mkono wako unapata kufanya, yafanye kwa nguvu zako zote, kwa maana hakuna kazi, wala utungaji wala ujuzi wala hekima katika Kaburi, mahali unapokwenda.” *Mhubiri 9:5, 6 10
Kuhusu hiki ulichokiandika hapa kutoka kitabu cha Mhubiri, maana yake ni kwamba, Watu hawajui wapi wanaelekea - hawajui nini hufuata baada ya kufa. Huu ndiyo hasa ukweli na maana ya hicho ulichokiandika hapo.
Kwa ujumla kitabu cha Mhubiri kinahusu "Nini thamani ya Maisha?" Kitabu hiki ni mtazamo wa kiulimwengu. Tafiti na fikara za mwandishi wa kitabu cha Mhubiri ni, hasa za ulimwengu.
 
na sisi pia kwa kiasi kikubwa huendeleza maisha yao kuwa kweli kwa kuwekeza nguvu(energy) zetu kwao.
 
The path society ndio wewe, ukiangalia kwa umakini ni sawa tu Christianity.
 
Kwa kipindi kirefu sasa nimesikia mafundisho ya kwamba dunia hii ni kifungo cha nafsi na roho za watu... na pia wapo watu mahsusi kwa kazi ya kufungua hizi nafsi na roho zilizofungwa.

Kwanza kabisa ningependa ndugu zangu tutambue ya kwamba sisi binadamu tupo katika ASTRAL, inamaana kwamba hakuna tofauti yeyote ile katika ulimwengu unaoonekana na usiooneka, Vitu ambavyo unaweza kuvijua au kuexperience wakati umekufa pia unauwezo wa kuvitambua sasa, hivyo basi jukumu ni lako kama utataka kuvijua sasa au hadi pale utakapoonja mauti,

Katika hii dunia tunayoishi kila kitu kipo katika kanuni au sheria ambazo zinawezesha huu ulimwengu kufanya kazi zake sawia, hivyo kwa kila jambo ambalo linapata kutokea hapa duniani lina sababu zake, na sababu ndio huleta matukio... sasa ningependa mtambue hapa duniani hakuna aina yeyote ile ya miujiza, kwa sababu miujiza ni kitu ambacho hutenda kazi kinyume cha sheria za ulimwengu huu, hivyo basi ili miujiza ili iweze kutenda kazi ni lazima ifuate kanuni na sheria...

Je, tutaendelea kuita ni miujiza? Kuibuka kwa neno muujiza ni kukosa kwetu maarifa ya kutambua kanuni na sheria za ulimwengu huu.

Hii dunia au ulimwengu sio jela wala kifungo cha nafsi wala roho za watu na wala haitakuja kuwa hivyo.

Kama utakuwa unajua chochote kuhusu LAW OF ATTRACTION utaweza kutambua ya kwamba kitu chochote unachokielekezea nguvu(energy) ndivyo kitu hicho kitazidi kukua au kuongezeka, ina maana kwamba kama watu watazidi kuelekeza nguvu zao katika mambo wasiyoyataka au mabaya ndivyo watakavyozidi kuzalisha na kuyakaribisha wasiyoyataka na mabaya zaidi ya hapo mwanzo, au utashangaa kitu gani kuona mpingaji au mkemeaji wa vitu asivyovitaka akivifanya hivyohivyo anavyopinga?

Jaribu kuchunguza maeneo ambayo kuna mafundisho mengi ya kukemea vitu vibaya au vile wasivyovitaka hali ikoje? Ndugu zangu ningependa mtambue ya kwamba vitu vibaya au vile tusivyovitaka kamwe haviwezi kuondolewa kwa kuvifikiria vitu hivyo au kuviwekea nguvu... labda kama tutakuwa na uhitaji wa makubwa yake.

Ni watu pekee ambao huleta matatizo na kukimbia matokeo ya kile walicho kileta ndio hukimbilia kusema uwepo wa kufungwa kwa nafsi na roho zao katika huu ulimwengu, na ndio aina ya watu hawahawa hubaki kunyosha vidole vyao katika mambo mabaya tu, huona mabaya yanayofanya na papa au vatican, huona mabaya ya Rothischilds family, huona mabaya ya malkia wa uingereza, huona mabaya ya U.S.A n.k bila ya kujua watu hawa huelekeza nguvu(energy) zao katika maisha na mambo yao wenyewe kuwa kweli, na sisi pia kwa kiasi kikubwa huendeleza maisha yao kuwa kweli kwa kuwekeza nguvu(energy) zetu kwao.

Ndugu zangu hapa duniani hakuna nafsi wala roho ya mtu yeyote iliyo kifungoni... ila matatizo yote haya yameanzia pale tulipo ukimbia mwanga,mwanga wa kweli hivo tukaanza uoga na kuamini tusivyovijua, na kwa uoga huohuo hatuwezi kuhoji juu ya kile tunachoamini, imefika hatua kwamba watu wanatamani kufa na kwenda kuishi mbinguni, lakini swali la kujiuliza ni kwamba kama maisha ya duniani umeyashindwa je una uhakika upi kama ya mbinguni utayaweza? Maana mbinguni ni kama duniani(As above as below).

Ndugu zangu baada ya kupita na kukua kimwili huu ni wakati muafaka wa kukua kimaarifa, tuache kuwa kama watoto wadogo wanaolalamika bila ya kuchukua hatua zozote zile, huu ni wakati wa kushika majukumu yako na kuacha kunyosha vidole na kuhukumu wengine, maana pale unavyomhukumu mtu pia ujue hata wewe pia unajihukumu, ila mbaya zaidi hutaishi.....

Watu ambao huwataki ndivyo wao wenyewe walivyoamua kuwa hivyo, je ni vipi kwa wale ambao hawakutaki pia? Je si kwa jinsi wewe ulivyoamua kuwa hivyo?... Ni vigumu sana ndugu zangu kuibadilisha dunia ila dunia ni rahisi sana kukubadilisha wewe, lakini jambo la kufurahi ni kwamba dunia haiwezi kukubadilisha bila mwenyewe kukubali, hivyo lengo la mhimu ni kubadilika mwenyewe, Vatcan sio wamiliki wa hii dunia, Alpha draconis hawatatengeneza maisha yako, Reptlians hawana mamlaka yeyote juu yako, Freemasons, Illuminat Rosscrucian, Skull & bones je hawa wote wana nini na wewe? Kwanini unapoteza nguvu zako kwao?

Wana jamvi mimi nimeona wakati unakuja, na saa imeshafika na ndio tunayo sasa ya kila mmoja wetu kuitambua kweli, kweli ambayo itakuweka huru, na hii kweli ndio itakuwa mwanga wako, nawe utakuwa nuru hapa ulimwenguni, na jambo la kuzingatia ni kuwa hii kweli haiuzwi wala haitolewi bure.

Huu si wakati tena wakushika vitu usivyovijua wala kuwa na uhakika nao, ila kweli ya kweli ipo ndani yako mwenyewe... je hamkusikia ya kwamba unabii hutoka ndani ya mtu mwenyewe? Maana humo ndimo kuliko na kweli yake. Huu ndio wakati wa kila mtu kujiunganisha na chanzo halisi kutoka ndani yako mwenyewe bali si kutoka nje...

Hapo ndipo utagundua uwezo na nguvu ulizonazo, hapo ndipo utagundua wewe ni nani na umetoka wapi na kwanini upo hapa duniani.

Najua itakuwa ni vigumu kueleweka maana lengo la mtumwa ni kuwa huru ila sio habari za kufikiri kuurithi ufalme. Na hapa duniani hakuna mtu yeyote aliyemfungwa, na kama ingekuwa hivyo basi watu wote tungekuwa wafungwa wenye hali sawa, je hizi tofauti zilizipo zinatokea wapi? Je nitakuwa nimekosea kusema hawa wanaotutoa kifungoni ndio waliotuweka? Je wanashindwa nini kumkamata na kumfunga yule anayetufunga? Na je kama ni kweli wanatoa watu vifungoni inakuwaje tena ufalme wao unazidi kuimalika siku hadi siku? (Hamtachelewa kusema nakufuru)

Ndugu zangu sisi tu huru, na hakuna mtu yeyote awezaye kutufunga zaidi ya sisi wenyewe, hakuna kiongozi yoyote wa dini wala mganga yeyote mwenye mamlaka juu yako isipokuwa wewe mwenyewe... na hakuna mtu yeyote awezaye kuifungua kweli iliyo ndani yako zaidi yako mwenyewe, ni wewe tu uliye na hizo funguo, je mpaka sasa hujatambua wale wa kutoka nje wanaosema kukufungua ndivyo huzidi kukufunga zaidi kwa kukuamrisha kipi ufanye na kipi usifanye, na hata wao ndio huamua ni jinsi gani wewe uishi?

Hii ndiyo kweli ambayo leo kwa ujasiri nimepata kuja kuishuhuduia mbele yenu, kwa sababu sasa umefika wakati wa kuamka... AMKA...AMKA...AMKA. sitaweza kukwambia hiyo kweli ni nini, na inatafutwaje maana ipo ndani yako wewe na wala sio kwangu... sitataka kuendeleza kukupa mafunzo ya uongo ili uipate hiyo kweli yako... ila cha kukusaidia ni wewe kufungua macho na ubongo wako na sasa jaribu kuangalia dunia yako katika kona tofauti...

Ni kwa njinsi hii tuliupenda ulimwengu... hivyo tupo hapa kwa dhamira zetu wenyewe... na hakuna yeyote anayepaswa kulaumiwa kwa chochote kile.

Msisahau ya kuwa hakuna kitu kinachotokea kwa bahati mbaya, kila unachokifanya kina matokeo yake yawe ni mabaya au mazuri.

TUENDELEE KUISHI KWA AMANI NA UPENDO!!
KWELI au NAFSI YA KWELI au TRUESELF.

Nimesoma bandiko lako na michango yako wakati ukijibu kwa wachangiaji wengine humu jamvini. Nashindwa alewa ume maandi yako umeyatoa wapi? Yaani source of backing, where it came from, your intellect or your conciousness? Maelezo yana ukweli lakini it seems huishi katika kweli bali umesimuliwa tuu. Kwa sababu ukweli ni kuwa (it is about to be) na hapo ndio unapata mwanzo na mwisho. In short kuwa kwenye nafsi ya kweli ni kuwa kwenye moment where there is no time or space (to be in moment state). Hapo utakutana na mwanzo wako na mwisho wako na ndio Mungu. Hii ndio kweli aliyoifundusha Issah bin Mariam (Yesu) aliposema wakati umefika Waabudio wa kweli watamwabudu Mungu katika Roho na Kweli kwa sababu Mungu ni Roho.

Yatupasa kuitafuta Kweli na Tukiwa katika hali ya kweli ndio tunamwabudu Mungu, kweli ambayo ipo indani yetu lakini kuipata na kuifikia inahitaji juhudi kubwa, vizuizi vilivyopo kuifikia, ni kifungo tosha ya Nafsi zetu, unless ulichokiandika kimetoka akilini (intellectaul thinking) sio matekeo ya matendo yako, kwani kama matokeo ya matedo ungelitambua kwa nini dunia hii ni kifungo cha nafsi zetu na mungu yupo.

Kila hali tuitambuayo, kwa kuona, kusikia kugusa, kula, kunywa inabadilika. Kweli haibadiliki, ilikuwa kweli kabla hata baadaye, milile na milele daima, lakini tunaona miili yetu haiko kama jana, inachakaa, inazeheka na kuharibika, tunakufa, vitu vinachaakaa, hii inaashiria vyote ni vya uongo, kweli haiko nje yetu bali ndani yetu, ilikuwepo kabla hutujazaliwa na itakuwepo baada kifo cha miili yetu kwani kweli au nasfi ya kweli ndio iliyoumbwa kwa mfano wa Mungu. Hiyo ndio twapasa kuitafuta, kuitafuta ni process, na yatupasa kushindana na majaribu mengi.

Baada ya kuzaliwa tunajenga miili na kukuza akiri na utambuzi wetu unafifia, kupitia akiri tunapata utambuzi wa uwongo uliotafsiriwa katika vigezo vya Muda na Wakati, tunajiona, tunafungwa una vaa ubinafsi, unapata hasira na furaha, Uchoyo na Uroho, Umaskini na Tamaa. Tunakuwa utumwani kutumikia Miili yetu, kuilisha, kuivalisha, kuisafisha, kukidhi tamaa na haja zake, kuilimbikizia mali na kuipatia familia tukizani kuwa sisi mwili na akiri na tuko hai. Tumejikuta tunautumikia ulimwengu wa mawazo (ideas), kumbuka kila ulionalo kuzunguka wewe ukamilishani wazo lililopita akilini kwa mwanadamu. Siku pekee tuna kuwa kwenye nafsi ya kweli ni siku ya kukata roho (KIFO CHA MWILI), tunakumbuka wajibu wetu kuwa na mwili na kuwa hatuja timiza huo wajibu tujajutia but its too late, tunapoteza kumbukumbu, kila tulichozani ndio mafanikio yetu tunachana nacho, mali, familia, elimu, utajiri, tunatafuta mwili mwinine na kuzaliwa tena, tunakuwa watumwa wa mzunguko wa kuzaliwa na kifo. Mpaka utakapo bahatika kupata siri ya kutafua nafsi ya kweli, ukibahatika unaweze pata ukweli in lifetime lakini many lifes.

Dini nyingi au kwa kusudi au bahati mbaya hazitufundishi ipasavyo, mafundisho halisi yamefichwa, lakini kila dini inazungumzia kukutana na Mungu yaani ONENESS. Lakini ukisoma sehemu fulani ya vitabu utagundua kurudi kwa mungu ni kupitia mwili not otherwise . Tafuta Spiritual knowledge achana Imani. Tafuta Kweli ungali hai, usidanganywe na eti kunakufufuliwa. Mwili by nature udongo, ulikuwa udongo, ukapitia kwenye mimea, ukafika mezani kwetu kamachakula, ukaumba miili yetu, siku ya kifu unaanza safari ya kurudi ulikotoka.
 
KWELI au NAFSI YA KWELI au TRUESELF.

Nimesoma bandiko lako na michango yako wakati ukijibu kwa wachangiaji wengine humu jamvini. Nashindwa alewa ume maandi yako umeyatoa wapi? Yaani source of backing, where it came from, your intellect or your conciousness? Maelezo yana ukweli lakini it seems huishi katika kweli bali umesimuliwa tuu. Kwa sababu ukweli ni kuwa (it is about to be) na hapo ndio unapata mwanzo na mwisho. In short kuwa kwenye nafsi ya kweli ni kuwa kwenye moment where there is no time or space (to be in moment state). Hapo utakutana na mwanzo wako na mwisho wako na ndio Mungu. Hii ndio kweli aliyoifundusha Issah bin Mariam (Yesu) aliposema wakati umefika Waabudio wa kweli watamwabudu Mungu katika Roho na Kweli kwa sababu Mungu ni Roho.

Yatupasa kuitafuta Kweli na Tukiwa katika hali ya kweli ndio tunamwabudu Mungu, kweli ambayo ipo indani yetu lakini kuipata na kuifikia inahitaji juhudi kubwa, vizuizi vilivyopo kuifikia, ni kifungo tosha ya Nafsi zetu, unless ulichokiandika kimetoka akilini (intellectaul thinking) sio matekeo ya matendo yako, kwani kama matokeo ya matedo ungelitambua kwa nini dunia hii ni kifungo cha nafsi zetu na mungu yupo.

Kila hali tuitambuayo, kwa kuona, kusikia kugusa, kula, kunywa inabadilika. Kweli haibadiliki, ilikuwa kweli kabla hata baadaye, milile na milele daima, lakini tunaona miili yetu haiko kama jana, inachakaa, inazeheka na kuharibika, tunakufa, vitu vinachaakaa, hii inaashiria vyote ni vya uongo, kweli haiko nje yetu bali ndani yetu, ilikuwepo kabla hutujazaliwa na itakuwepo baada kifo cha miili yetu kwani kweli au nasfi ya kweli ndio iliyoumbwa kwa mfano wa Mungu. Hiyo ndio twapasa kuitafuta, kuitafuta ni process, na yatupasa kushindana na majaribu mengi.

Baada ya kuzaliwa tunajenga miili na kukuza akiri na utambuzi wetu unafifia, kupitia akiri tunapata utambuzi wa uwongo uliotafsiriwa katika vigezo vya Muda na Wakati, tunajiona, tunafungwa una vaa ubinafsi, unapata hasira na furaha, Uchoyo na Uroho, Umaskini na Tamaa. Tunakuwa utumwani kutumikia Miili yetu, kuilisha, kuivalisha, kuisafisha, kukidhi tamaa na haja zake, kuilimbikizia mali na kuipatia familia tukizani kuwa sisi mwili na akiri na tuko hai. Tumejikuta tunautumikia ulimwengu wa mawazo (ideas), kumbuka kila ulionalo kuzunguka wewe ukamilishani wazo lililopita akilini kwa mwanadamu. Siku pekee tuna kuwa kwenye nafsi ya kweli ni siku ya kukata roho (KIFO CHA MWILI), tunakumbuka wajibu wetu kuwa na mwili na kuwa hatuja timiza huo wajibu tujajutia but its too late, tunapoteza kumbukumbu, kila tulichozani ndio mafanikio yetu tunachana nacho, mali, familia, elimu, utajiri, tunatafuta mwili mwinine na kuzaliwa tena, tunakuwa watumwa wa mzunguko wa kuzaliwa na kifo. Mpaka utakapo bahatika kupata siri ya kutafua nafsi ya kweli, ukibahatika unaweze pata ukweli in lifetime lakini many lifes.

Dini nyingi au kwa kusudi au bahati mbaya hazitufundishi ipasavyo, mafundisho halisi yamefichwa, lakini kila dini inazungumzia kukutana na Mungu yaani ONENESS. Lakini ukisoma sehemu fulani ya vitabu utagundua kurudi kwa mungu ni kupitia mwili not otherwise . Tafuta Spiritual knowledge achana Imani. Tafuta Kweli ungali hai, usidanganywe na eti kunakufufuliwa. Mwili by nature udongo, ulikuwa udongo, ukapitia kwenye mimea, ukafika mezani kwetu kamachakula, ukaumba miili yetu, siku ya kifu unaanza safari ya kurudi ulikotoka.
Kaka kwenye mambo haya huwa nakuelewa sana ngoja nisome tena na tena ili nielewe kama kuna swali nikuulize.
 
KWELI au NAFSI YA KWELI au TRUESELF.

Nimesoma bandiko lako na michango yako wakati ukijibu kwa wachangiaji wengine humu jamvini. Nashindwa alewa ume maandi yako umeyatoa wapi? Yaani source of backing, where it came from, your intellect or your conciousness? Maelezo yana ukweli lakini it seems huishi katika kweli bali umesimuliwa tuu. Kwa sababu ukweli ni kuwa (it is about to be) na hapo ndio unapata mwanzo na mwisho. In short kuwa kwenye nafsi ya kweli ni kuwa kwenye moment where there is no time or space (to be in moment state). Hapo utakutana na mwanzo wako na mwisho wako na ndio Mungu. Hii ndio kweli aliyoifundusha Issah bin Mariam (Yesu) aliposema wakati umefika Waabudio wa kweli watamwabudu Mungu katika Roho na Kweli kwa sababu Mungu ni Roho.

Yatupasa kuitafuta Kweli na Tukiwa katika hali ya kweli ndio tunamwabudu Mungu, kweli ambayo ipo indani yetu lakini kuipata na kuifikia inahitaji juhudi kubwa, vizuizi vilivyopo kuifikia, ni kifungo tosha ya Nafsi zetu, unless ulichokiandika kimetoka akilini (intellectaul thinking) sio matekeo ya matendo yako, kwani kama matokeo ya matedo ungelitambua kwa nini dunia hii ni kifungo cha nafsi zetu na mungu yupo.

Kila hali tuitambuayo, kwa kuona, kusikia kugusa, kula, kunywa inabadilika. Kweli haibadiliki, ilikuwa kweli kabla hata baadaye, milile na milele daima, lakini tunaona miili yetu haiko kama jana, inachakaa, inazeheka na kuharibika, tunakufa, vitu vinachaakaa, hii inaashiria vyote ni vya uongo, kweli haiko nje yetu bali ndani yetu, ilikuwepo kabla hutujazaliwa na itakuwepo baada kifo cha miili yetu kwani kweli au nasfi ya kweli ndio iliyoumbwa kwa mfano wa Mungu. Hiyo ndio twapasa kuitafuta, kuitafuta ni process, na yatupasa kushindana na majaribu mengi.

Baada ya kuzaliwa tunajenga miili na kukuza akiri na utambuzi wetu unafifia, kupitia akiri tunapata utambuzi wa uwongo uliotafsiriwa katika vigezo vya Muda na Wakati, tunajiona, tunafungwa una vaa ubinafsi, unapata hasira na furaha, Uchoyo na Uroho, Umaskini na Tamaa. Tunakuwa utumwani kutumikia Miili yetu, kuilisha, kuivalisha, kuisafisha, kukidhi tamaa na haja zake, kuilimbikizia mali na kuipatia familia tukizani kuwa sisi mwili na akiri na tuko hai. Tumejikuta tunautumikia ulimwengu wa mawazo (ideas), kumbuka kila ulionalo kuzunguka wewe ukamilishani wazo lililopita akilini kwa mwanadamu. Siku pekee tuna kuwa kwenye nafsi ya kweli ni siku ya kukata roho (KIFO CHA MWILI), tunakumbuka wajibu wetu kuwa na mwili na kuwa hatuja timiza huo wajibu tujajutia but its too late, tunapoteza kumbukumbu, kila tulichozani ndio mafanikio yetu tunachana nacho, mali, familia, elimu, utajiri, tunatafuta mwili mwinine na kuzaliwa tena, tunakuwa watumwa wa mzunguko wa kuzaliwa na kifo. Mpaka utakapo bahatika kupata siri ya kutafua nafsi ya kweli, ukibahatika unaweze pata ukweli in lifetime lakini many lifes.

Dini nyingi au kwa kusudi au bahati mbaya hazitufundishi ipasavyo, mafundisho halisi yamefichwa, lakini kila dini inazungumzia kukutana na Mungu yaani ONENESS. Lakini ukisoma sehemu fulani ya vitabu utagundua kurudi kwa mungu ni kupitia mwili not otherwise . Tafuta Spiritual knowledge achana Imani. Tafuta Kweli ungali hai, usidanganywe na eti kunakufufuliwa. Mwili by nature udongo, ulikuwa udongo, ukapitia kwenye mimea, ukafika mezani kwetu kamachakula, ukaumba miili yetu, siku ya kifu unaanza safari ya kurudi ulikotoka.
In short kuwa kwenye nafsi ya kweli ni kuwa kwenye moment where there is no time or space (to be in moment state).

Nawezaje kuishi bila ya muda au nafasi?
Je mtu anaiyeishi kwakuijua kweli akifa anaenda wapi?
Watu wote wanaozaliwa je washawahi kuishi kabla?
Kama ndio je wote tukifa huku tukiijua kweli hakutazaliwa tena watu wengine?
Ahsante.
 
In short kuwa kwenye nafsi ya kweli ni kuwa kwenye moment where there is no time or space (to be in moment state).

Nawezaje kuishi bila ya muda au nafasi?
Je mtu anaiyeishi kwakuijua kweli akifa anaenda wapi?
Watu wote wanaozaliwa je washawahi kuishi kabla?
Kama ndio je wote tukifa huku tukiijua kweli hakutazaliwa tena watu wengine?
Ahsante.
Nimekuona dumbi niko busy nikipata nafasi nitakujibu.
 
Back
Top Bottom