Je ni kweli Waisrael wamebarikiwa kuliko binadamu yeyote duniani?

Je ni kweli Waisrael wamebarikiwa kuliko binadamu yeyote duniani?

mbona unatuongopea ndudu kuna nchi gani ambayo inaweza kuanzisha vita na urusi,iyo Nato ina nchi 28 lakini kila siku inaongeza ulinzi kwa ajiri ya kuofia kuvamiw na warusi.iyo china yenyew inauziwa siraha na warusi au ulikuwa ujui
Mkuu sio kwamba NATO haiwezi kupigana na Russia.

Number isn't a matter but size of the fight.

Kwa Historia tu, NATO ndio iliiangusha Urusi (USSR)/kupitia Proxy War. Mfano kule Afghanistan etc.1990.

KUna mkataba waliingia kati ya Urusi na United States unaitwa MAD (Mutually Assured Destruction).
Ni kwamba haya mataifa yana silaha ambazo zinaweza kuifuta Dunia kwa sekunde.

Ndio maana yako very sensitive kuhusu kupigana vita yenyewe kwa yenyewe kwakua wanajua Wanaweza kujiangamiza wote.na ndio maana Wameelekeza vita yao zaidi kwenye ku-Influence (Allience) na Uchumi.

Ambapo huko bado USA ni Leader wa Dunia.


Russia ya Putin aliwahi kusema ikitokea anapigana na USA, hatatumia silaha za kawaida. Ataanza na silaha zA nuclear. Anajua Nukes ndio suluhisho. Hizi silaha zingine ni mbwembwe tu katika kuishinda USA.
 
iyo ugerumani iliyokuwa bora ilipigwa mpaka berlin.80% ya jeshi la ugeruman liliangamia katika mikono ya warusi

Urusi ndio.walikua wakwanza kuingia Jiji la Berlin kumuondoa Führer kwa upande mmoja.

Ila majeshi washirika wa Marekani, UK, France, Italy walikua wakiongeza Pressure upande mwingine.

Usitake kuamini kua Urusi pekee ingeweza ku- withstand nguvu ya Ujerumani iliokua Bora, thanks to the extremely cold weather kwa kuwapa backup warusi dhidi ya ujerumani imara.
Usisahahu major intention ya Hitler ilikua kuichukua Urusi yote. Hizi nchi nyingine kama Poland ziliangukia tu mikononi mwake kama sehemu ya mpango.
 
Kuna vitu unatakiwa kuvielewa. Ni kweli aliyepigana na mataifa ma5 ya kiarabu ni mwisrael na mataifa hayo yalikubali kusitisha vita ndani ya siku 6 tu. Lakini mwisrael hakupigana peke yake alikuwa na usaidizi wa washirika wake hasa marekani. Waisrael katika hiyo vita walisaidiwa siraha, pesa, mahitaji ya kijamii kwa ajili ya jeshi na pia taarifa za kiintelijensia.
Vita hiyo inafanana na kung'olewa kwa Ghadaffi, ama vita ya kule iraq na afghanistan kila mmoja anajua marekani amepigana hivyo vita. Je alipigana peke yake? Jibu ni hapana alikuwa anasaidiwa na Uingereza, ufaransa n.k
Ni vita chache sana duniani ambazo vimepiganwa bila kuhusisha washirika mf vita ya kagera na vita ya urusi dhidi ya Poland
Hata vita ya sasa ya israel dhidi ya palestina, israel inasaidiwa na marekani, Uingereza na ufaransa huku palestina walisaidiwa na mataifa ya kiarabu
Mkuu umesoma vibaya hiyo historia.

Kwa kifupi USA alijiingiza baada ya kuona kumbe Israel wanajiweza.
Lakini hata Urusi ilikua ikitoa sapoti kwa waarabu na ilipoona hasara inayowakuta waarabu wakaamua kutishia kuingia vitani, ndipo USA akiwa hataki influence ya Urusi pale middle east akaharakisha Egypt ipatane na Israel ili vita iishe .

Kuhusu Palestine, nachoweza kusema Wapalestina sio Taifa. Sihesabu kua wanapigana na wapalestine, ila magaidi wa Hamas na Hezbollah.
 
anaefahamu naomba anijuze ?nasikia hawa watu wanaakili sana na ndio maana hitla aliwaua mamia kwamaelfu navilevile nasikia kwamba nchi za kiarabu zimeshindwa kabisa kuifyeka hii israel eti wanabaki kubweka huku wameficha mkia kama mbwa alie mface chatu sijui nikweli? Great tel me plz
Wenye majibu mazuri kuhusu hawa watu, tungepata mmisri au mpalestina hawa ndio wanaijua stori kamili ya hawa watu. au Tungemuuliza Idi Amin Dadaa Nduli. pale walipokuja chukua ndugu zao pale Entebbe.
 
anaefahamu naomba anijuze ?nasikia hawa watu wanaakili sana na ndio maana hitla aliwaua mamia kwamaelfu navilevile nasikia kwamba nchi za kiarabu zimeshindwa kabisa kuifyeka hii israel eti wanabaki kubweka huku wameficha mkia kama mbwa alie mface chatu sijui nikweli? Great tel me plz
Ni WANAFIKI DUNIA NZIMA...HATA MUNGU WALIMFANYIA VITIMBWI KIBAO...EXODUS utawakuta...
 
anaefahamu naomba anijuze ?nasikia hawa watu wanaakili sana na ndio maana hitla aliwaua mamia kwamaelfu navilevile nasikia kwamba nchi za kiarabu zimeshindwa kabisa kuifyeka hii israel eti wanabaki kubweka huku wameficha mkia kama mbwa alie mface chatu sijui nikweli? Great tel me plz
Yani hapo ni sawa na kusema waislael wa kipindi cha musa ni sawa na hawa wa nertanyau ,,,au daud kipenzi cha Mungu ni sawa na daud ba,,she[emoji12] [emoji12] [emoji12]
 
Israel kama sio mmarekani na Muingeleza tusingekuwa tunawaskia duniania hapa, wangekuwa nchi kama Guinea huko
 
Wa Israel halisi hawapo pale Israel,wako kwenye mataifa wamesambaa wakifanya kazi.biblia inamaanisha watakua utumwani.na ni kweli wana akili nyingi sana.unaowaona sasa hivi pale Israel ni wazungu fulani tu wakorofi korofi hivi.Israel wenyewe halisi wako duniani pote hasa mataifa hayo hayo makubwa wanatumikishwa kufanya kazi za kitaalamu.na kadri miaka inavyoenda kuna siku watajikusanya wote na vizazi vyao na kurudi pale Israel,binafsi nachoamini hao watakapoamua kurudi na kujenga Israel halisi ndipo utakapoona hakuna cha mmarekani wala mrusi wala mchina atakaekua na nguvu kuliko wao
Umetunga stori na kujiaminisha kama itakuja kuokeaa hivyo!!!! Hongera
 
Ni kweli hawa jamaa wamebarikiwa.

Utaona story ya Daudi na Goliath inavyojirudia pale middle east.
Mwaka 1967 Waisrael waliwapiga mataifa matano ya Kiarabu kwa siku sita. Siku ya saba wakapumzika, kama vile Mungu alivyoumba Mbingu na dunia sikU sits , na siku ya 7 akapumzika.

Walikua na jeshi dogo, silaha chache, ndege chache lakini walishusha kichapo kilichowaogopesha hadi Taifa la Kisovieti LA Urusi.

Haya hayawezi kutokea bila kua na Baraka za Mungu.

Yapo majaribio kadhaa ya kuwafuta katika Uso wa nchi yamefanywa na waarabu, wajerumani, yakashindwa vibaya sana.
Utaona kila taifa lililoiunga mkono Israel lilipiga hatua kubwa kinyume na Yale yaliopingana nayo hata Leo.

USA ilibarikiwa sana ilipoanza juhudi za kuwaunga mkono, hali yao ilizorota pale walipokua wakiwakandamiza kisera.
Urusi iliangushwa.
Waarabu mpaka Leo wameshindwa kuungana dhidi ya Israel.

Obama aliwapinga sana matokeo yake chama chake kikashindwa dhdi ya bwana Trump,

Nyerere alikataa kuwasaidia wasiokoe mateka wao Uganda lakini Kenya walikubali matokeo yake IDD Amin akavamia Tanzania.na so Kenya.

Kwa ufupi hata Leo wako watakaosema waisrael si lolote kwasababu ya uchache wao nk. Ila wakithubutu wanaangamia.

Israel ndio INA asili ya manabii, mitume watakatifu wanaosomwa zaidi duniani, akiwemo mkombozi Yesu Kristo.
Kupitia Israel mataifa yote yatabarikiwa.
So kwa ufupi IPO baraka katika Israel
Mkuu,
Wewe unaamini katika haki na usawa..?
 
Naamini Mkuu.

Lakini jua kua usawa uliopo ..ni wakati mwingine mmoja kua bora zaidi ya mwingine.
Kwanini mmoja awe bora zaiidi ya mwingine, huku ikiwa wote ni binadamu Tulioumbwa na mwenye upendo,usawa na uweza
 
Kwanini mmoja awe bora zaiidi ya mwingine, huku ikiwa wote ni binadamu Tulioumbwa na mwenye upendo,usawa na uweza


I think... Uumbaji wa Pale Bustani ya Eden ndio ulikuwa na dhana ya usawa unaouzungumzia ambao ni tofauti sana na baada ya Mwanadamu kutolewa Eden. Hapa mambo mengi yalibadilika.

Tumeumbwa kwa Upendo, usawa na uweza tofauti. hii wanaita Talent.(Kipaji)

Aftermath.*
USAWA WA ki -MUNGU HUKO HIVI:-

Utakuta Mmoja ameumbwa kua kichwa na mwingine kua Tail.

Kwa Mfano:- By default, Mwanamke ameumbwa kua Chini ya Mwanaume kimamlaka.
Hii haijalishi Mwanamke ana pesa, akili, kiasi gani kumshinda Mumewe au ni mrefu kuliko Mume.. Sikuzote Mwanamke Anatakiwa kua submissive mbele ya Mumewe.

Mungu ameweka furaha kwa kila MTU na nafasi yake.Atimize lengo La kuwepo kwake hapa Duniani. Kumsaidia Mumewe, nk.

Ni Kama ufalme wa Nyuki, ambapo kuna makundi ya soldier, workers, male na Queen.

Sikuzote workers hawalalamiki kwanini wao sio soldiers, wanaendelea kuchapa Kazi, ndivyo walivyoumbiwa. nk.

Lakini katika Dunia, unapotaja Mungu na kwa bahati mbaya pia yupo shetani.

Kupitia Dhana hii ya mythology, Mungu anakua ni Positive force na Shetani ni Negative force.

Mungu alishagawa talents na shetani halali kutwa akihangaika kuitwa mungu wa hii dunia naye anagawa talents zake ambazo zipo opposite na zile alizogawa Mwenyezi Mungu.

Utakuta.. (..After Eden)
Mmoja anakua bora Kwasababu mwingine haridhiki na nafasi yake aliopewa na Mungu anajaribu kuwania nafasi ya mwingine...Like anaishia "kufoji cheti " ili astahili asipostahili.
Mwishowe hatatimiza mpango wa Mungu katika Kazi zake na jamii yake ipasavyo.

Hapo ndipo walio bora dhidi ya wengine wanapoibuka.

Kwa case ya waisrael, utakuta wapo waisrael wanaamini kua ile ardhi pale middle east wamepewa wao na Mungu kihalali kabisa, na kwamba wakiigawa Mungu atawaadhibu, lakini kuna waarabu hawakubaliani na hiyo imani wanajaribu kupingana na huo unaoitwa mpango huu wa Mungu kwa sana wa israel.
Matokeo yake ni self evident.
 
Israel ya mapigano ilikuwa ile ya Musa ya jino kwa jino na kufuata misimamo mikari ya kushika sabato katika torati yaani agano la kale, sasa watu wanashindwa kuelewa kuwa Yesu Kristo kaanzisha agano jipya ambalo sasa taifa la mungu sio wayahudi hawa wa leo tena bali mataifa yote yako treated the same ili kuwa taifa la Mungu (Israelit’s), unatakiwa kumuamini Mungu katika kristo Yesu ndiyo maana biblia inasema kasha nikaona Yerusalem mpya ikishuka kutoka juu, manake siyo hii ya leo na waisrael hawa wa leo bali wote wanaomuamini Mungu katika roho na kweli na hii ndo sababu kuu ya lile hekalu la Yerusalemu kubomolewa na kushindikana kujengwa upya kwa wote waliojaribu kulijenga makusudically ili hekalu hilo lijengwe katika miili ya wanadamu wote ili Mungu abudiwe katika roho na kweli kila mahali. Mwisho ili uwe muisrael lazima umpokee Yesu kama bwana na mwokozi wako, umuuamini Mungu kupitia yeye na usaidia wenye shida kama una uwezo, hapo ndipo utakapowashinda maadui zako, na kuwa hekima ya Mungu katika mambo yako na hivyo lazima akili zako ziwe tofauti kabisa yaani high level mind and thought.
 
Israel ya mapigano ilikuwa ile ya Musa ya jino kwa jino na kufuata misimamo mikari ya kushika sabato katika torati yaani agano la kale, sasa watu wanashindwa kuelewa kuwa Yesu Kristo kaanzisha agano jipya ambalo sasa taifa la mungu sio wayahudi hawa wa leo tena bali mataifa yote yako treated the same ili kuwa taifa la Mungu (Israelit’s), unatakiwa kumuamini Mungu katika kristo Yesu ndiyo maana biblia inasema kasha nikaona Yerusalem mpya ikishuka kutoka juu, manake siyo hii ya leo na waisrael hawa wa leo bali wote wanaomuamini Mungu katika roho na kweli na hii ndo sababu kuu ya lile hekalu la Yerusalemu kubomolewa na kushindikana kujengwa upya kwa wote waliojaribu kulijenga makusudically ili hekalu hilo lijengwe katika miili ya wanadamu wote ili Mungu abudiwe katika roho na kweli kila mahali. Mwisho ili uwe muisrael lazima umpokee Yesu kama bwana na mwokozi wako, umuuamini Mungu kupitia yeye na usaidia wenye shida kama una uwezo, hapo ndipo utakapowashinda maadui zako, na kuwa hekima ya Mungu katika mambo yako na hivyo lazima akili zako ziwe tofauti kabisa yaani high level mind and thought.
 
Wana akili kwenye nini? Umetumia standard gani mpaka ukafikiria kwamba wana akili?

Mfano angalia hizi ni nchi 15 bora duniani kwa uvumbuzi wa vitu

The 15 most innovative countries in the world

Kati ya nchi hizo 15 israel haipo,

Mimi nimetumia standard yangu kwamba ili uonekane na akili inabidi uvumbue na israel hawamo kwenye wavumbuzi bora.

Ukija kwenye iq nchi zenye watu wenye uwezo mkubwa zaidi wa kufikiri baadhi ya research nilizoziona hata top 40 hawamo

https://iq-research.info/en/page/average-iq-by-country#
Israel kama nchi haipo kwenye list ya wavumbuzi .. lakini Waisrael (watu wenye asili ya Israel) ndo wavumbuzi wengi
 
Israel ni Taifa masikini linaishi kwa kutegemea misaada ya Wamarekani.........hawajawahi kutengeneza hata sabuni ya kuogea ki ufupi ni vilaza hawajui chochote
Kuendelea kusema kwamba Israel wapo juuu ni sawa na kukariri kwamba wasomi ni Wahaya
Na wafanyabiashara ni wachaga

Sasa ivi kila mtu yupo vizuri akuna cha mchaga wala muhaya

Ivyo ivyo ni kama ilivyo kwa awo waisrael, sasa ivi wamekuwa wa kawaida sana.
Sema anagalizo awa jamaa wana kitu kinaitwa Matrinual system, kwamba watoto ni wa upande wa mama ni waisrael na ndio wametapaa dunia nzima na ndio wanafanya uchunguzi wa technology ya vitu vingi katika mataifa makubwa na wanapoenda katika Hekalu zao za kuabudu wanajalibu kuwa na mahusiano na wayahudi wote waliopo duniani
Na suala la watu kuwachukia ni kwa sababu wao ndio walioanzisha Ubaguzi wa Rangi, dini na kubagua mzungu huyu ana macho ya brown, blue na black na mzungu huyu ana nywele Nyeusi na huyu ana ana nywele za Goldish
 
Back
Top Bottom