Je ni sawa kwa kijana wa miaka 20 kuoa mwanamke mwenye miaka 27?

Je ni sawa kwa kijana wa miaka 20 kuoa mwanamke mwenye miaka 27?

Isomeke hivi.

Je ni sawa kwa kijana wa miaka 20 kKUOLEWA na mwanamke mwenye miaka 27?
 
Mapenzi hayaongozwi na umri,bali hisia na muonekano!

Unaweza ukawa na miaka 19 ukawa na muonekano was Mzee,wakati ukawa na Miaka 32 kijana kabisa Tena mbichi!!
Sikiliza hisia zako baada ya muda mtafanana na kuwa kama kaka na dada!
 
Kijana Kuoa sio Sahihi.

Kuoa Aliekuzidi Umri, Haikubaliki
 
Inawezekana vizuri tu.

Kama wote wanatoshelezana kikamilifu kwenye vitu wavitakavyo katika mahusiano/ndoa.

Masuala ya rika ni mtambuka sana, watu waliopishana miaka 15 wanaweza kupatana vyema kabisa na kuwa maswahiba, ili hali waliopishana miaka 2 wakashindwa kutengeneza urafiki.

Kuna ule mpatano flani hivi(Synergy), kila mmoja anaridhika na mwezake, mambo yataenda tu.
 
Aisee sio poa miaka saba kabisa
Mtume Muhammad (S.A.W), kipenzi cha Allah, akiwa na miaka 25 alimwoa Mwanamke Mhasibu Bi Khadija akiwa na miaka 40...na ndoa yao ilidumu ndio useme gap ya miaka 7?

You are not serious at all
 
Inawezekana vizuri tu.

Kama wote wanatoshelezana kikamilifu kwenye vitu wavitakavyo katika mahusiano/ndoa.

Masuala ya rika ni mtambuka sana, watu waliopishana miaka 15 wanaweza kupatana vyema kabisa na kuwa maswahiba, ili hali waliopishana miaka 2 wakashindwa kutengeneza urafiki.

Kuna ule mpatano flani hivi(Synergy), kila mmoja anaridhika na mwezake, mambo yataenda tu.
Zari na wanaume zake anawazidi miaka 9-12 na wanaishi, japo kibinafsi siwezi hata anaenizidi 5yrs tu namuona bado mdogo napenda mwanaume anizidi 12-18yrs mwisho
 
Back
Top Bottom