Je, ni Speed gani kubwa zaidi ushawahi kutembea na gari au pikipiki?

Je, ni Speed gani kubwa zaidi ushawahi kutembea na gari au pikipiki?

Hiii wanayoiita mishangingi wakuu iacheni.
Tu siku nyingine tunatoka bagamoyo kuna ile sehemu pana roundabout tupo na crown nyeusi mbele mbele kidogo tumefika LC amazon hiyo nikasema huyu nanyooka nae mda huo ni saa 12 tochi zishaaanza kupungua nikamuacha atakuangulie kidogo..

Nikaanza sasa kukanyaga jamaa nilipo mfikia karibu nikampigia pasi kumuomba..
Tunyooshe mguu kidogo aka-respond...
Jamaa akawa kila akijitahidi wapi![emoji16] tukafika maeneo ya tegeta kuna kafoleni akatanua nikaungaa nikawasha hazad nae kawasha mwenge ndo tulikuja kuachana!

Yeye anaelekea ubungo mimi nanyoosha.
Nikiwa barabarani njia nyeupe namuona mtu kanipita alafu namuweza huwa sikubali[emoji16] lazima nipiane nae kidogo.
Watu pekee naowaheshimu ni watu wenye
Benz,Bmw,LC, na mjerumani yeyote.
Mie nikipitwa huwa napatwa na hasira sana kiukwel. [emoji16]
 
Kuna siku naenda Manyara mida ya saa 4 usiku, nipo 170kph aisee nilikutana na kona kali haishi, nililala nayo tairi zinalalamika hatare.

Naimaliza nakutana na nyingine kushoto ina daraja, nimevuka daraja nikapaki gari pembeni siamini kilichotokea.

Wakati nashusha pumzi, Mwenyeji wangu akanipigia simu "ukifika maeneo flani kuna kona kali sana, kuwa makini". Ananijua mi ni mtu wa spidi kali

Bimmer - Germany Machine
Ilibaki robo niangushe Noah kwenye kona kali kabla ya Manyoni, niliilaza 150 ikainua miguu ya kushoto, ikabidi niikubalie ninyooshe nikatoka nje ya road na brake za kunyunyiza.
 
Kwan speed ndogo kuna faida gani? Speed kali ni ipi kwa uelewa wako....maana kuna nchi mfano Germany kuna njia ni free tembea vile unaweza kule ndo unakuta bike ya 1000cc 4cyl inaaibishwa ...tena bike ambayo 1st gear inaenda hadi 140 gia ya pili 200kph kule unaaibishwa japo kwa bongo bike ya hata cc 400 unasumbua gari nyingi sana
Kuna bike usipokuwa na roho mbaya unaweza ukaishia gear 2 tu tena hapo kwa tabu haswaa.
 
Inategemea na uwezo wa gari, gari kama inachelewa changanya basi hizo speed utakuwa unasikia tu kwa watu, crown hizo 180 ni kugusa tu, na magari mengi sasa ukianza jarbu futa sahani kwenye rumion ndo shida inaanza
Zingne mpk zipate down ndio zichanganye. [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom