Je, Rais Magufuli alikuwa na Pacemaker au Defibrillator? Ilidukuliwa?
Pia tusisahau kuchunguza wauaji waliokusudia kuondoa uhai wa Lisu, waliowapoteza AzoryGwanda, Ben saanane, Kanguye, maiti kukutwa kwenye viroba ufukweni mwa bahari, wauaji wa Alphonce Mawazo nk nk nk
 
Mfano angejufa kwa miwaya pia tungeitaji uchunguzi maana mbona kitaa wapo wengi wanadunda uongo?
 
Attackers wanaweza kutumia radio signals au mobile phone ambayo unaweka kwenye mfuko wa shati!
kwamba hizi njia zote usalama walikua hawazijui ama inakuaje mtu apite/akae karibu na rais na aachiwe simu?

kama itakua mobile phones basi mishen imekamilishwa na moja ya wakuu wanaomtembelea rais,wale VIP wasiokaguliwa.
 
Akiwa Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan (sasa Rais) alituambia tu "Rais Magufuli amekufa kutokana na tatizo la mfumo wa umeme katika moyo wake, tatizo alikokuwa nalo zaidi ya miaka 10 iliyopita". Hivi, hili jibu linatosha kuaminiwa?

Ni wangapi Wana tatizo kama hilo lakini bado wanadunda? Mbona Rais alikuwa mzima bukheri wa afya ziarani Dar? Nini kauli ya Daktari wake? Hakujua dalili au ishara ya Rais kupata shida? Nini maana ya Ulinzi madhubuti kwa Rais? Nini hasa kilimsibu Magufuli? Na kwanini wapambe wa mabeberu ndio wawe wa kwanza kubaini hali dhoofu ya Rais Magufuli?

Tunajua JPM hakuwa rafiki na mabeberu katika vita ya uchumi. Kwa nini Rais SSH asiunde Tume ya Kitabibu kuchunguza kifo cha kipenzi chetu? Yaani tukubali tu kirahisi maelezo ya umeme moyoni?! Hapana. Nakataa, muda utaongea.
Kuna haja yakufanya hivo, ata mimi nina mashakha sana na kifo chake, ukifatilia kwa makini wanafamilia wanasema aliomba mpaka maaskofu waje kumfanyia kitubio sijui na Muft akamuombea, pia kama haitoshi alimpigia dimu askofu Gwajima tarehe 6 ambapo inasemekana alienda MOI lakini mwisho kabisa nasaha zake kwa Taifa ambazo zilisomwa juzi na familia japo moja wanasema hawajaikumbuka lakini naamini inajulikana ila imefichwa kutokana na usalama labda kuna vitu kaviongea ambavyo si vya kawaida.
 
Nimejiuliza na kufikiria sana sana kuhusu kifo cha Rais Magufuli kilichosababishwa na mfumo wa umeme wa moyo uliokuwa unaratibiwa na pacemaker/defibrillator.

Kujiuliza na kufikilia kwangu kumetokana onyo la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Marekani (Department of Homeland Security-DHS) lililotolewa mwaka 2019 linaloonya makampuni yanayotengeneza pacemaker/defibrillator kuhusu hatari ya kifaa hicho kudukuliwa na wataalam wa udukuzi na kupelekea hata kifo kwa watu waliopandikizwa kifaa hicho.

Ukitaka kusoma onyo hilo unaweza kugonga hapa;
Link>>> Pacemakers and Hacker Dangers

Wizara hiyo ilibainisha kuwa wadukuzi wanaweza kuingilia mifumo ya pacemaker/defibrillator na kuweza kubadilisha mawasiliano yake ambapo inaweza kupelekea mtu aliyewekewa kifaa kufariki.

Wizara hiyo ilienda mbali zaidi na kusema hata wadukuzi ''mwenye uwezo mdogo'' wanaweza kudukua pacemaker/defibrillator na kufanikiwa kuleta madhara makubwa kwa watu waliopandikizwa vifaa hivyo kwa sababu vifaa hivyo havina mfumo wa uhakiki au idhini (authentication or authorization) ambao ni kinga ya mwanzo dhidi ya udukuzi.

Onyo hili lilipelekea watoa huduma ya afya nchini Marekani kuwaita wananchi wa Marekani zaidi ya nusu milioni waliopandikizwa vifaa hivyo na kuwaeleza ukweli wake.

Kama kifaa hiki kinaweza kudukuliwa hata na wadukuzi wenye uwezo mdogo na kuleta madhara au kifo, inafikirisha sana kusikia kifo cha Rais Magufuli kimesababishwa na mfumo wa umeme wa moyo uliokuwa unaratibiwa na pacemaker/defibrillator. Bear in mind, Rais Magufuli amekuwa na hii pacemaker/defibrillator kwa zaidi ya miaka 10. Why now?

Inafikirisha zaidi baada ya kusoma makala iliyoandikwa na Tundu Lissu kupitia gazeti la Afrika ya Kusini liitwalo Maverick akidai alidokezwa kuhusu hali ya Rais Magufuli na chanzo cha ''uhakika'' kutoka Marekani tarehe 6 Machi.

Ukitaka kusoma makala hiyo gonga hapa;
Link>>> OP-ED: Tanzania’s five years of devastation under the presidency of John Pombe Magufuli

Ukiyachanganua maelezo ya Tundu Lissu utagundua kuwa chanzo cha ''uhakika'' walijua wamefanikiwa ''mission'' ya kudukua hasa baada ya Rais Magufuli kwenda katika hospitali ya Muhimbili tarehe 6 Machi kutibiwa ambapo inaonekana daktari/madaktari walitoa siri hiyo nje lakini baada ya kutoka Muhimbili siku ya pili hawakujua yuko wapi kutokana na usiri wa hali ya juu wa ulinzi wa Rais Magufuli.

Hata gazeti ya Kijasusi liitwalo Africaintelligence halikuweza kujua aliko na likadai habari zinazosema yuko Kenya au India sio za kweli kwa sababu limefanya uchunguzi na kugundua sio kweli.

Kama chanzo cha kifo cha Rais Magufuli kitakuwa ni kudukuliwa kwa pacemaker/defibrillator, hii itakuwa ni aibu na udhaifu mkubwa kwa vyombo vilivyopewa mamlaka ya ulinzi na usalama wa taasisi ya Urais nchini Tanzania. Taasisi ya Ulinzi na Usalama inawezekana ilikuwa imejikita katika ulinzi wa mwili(Physical security ) pekee bila kujiandaa kwenye ulinzi wa saibenetiki(cybersecurity).

Kuna baadhi ya watu watajiuliza, kwa nini pacemaker/defibrillator ya Rais Magufuli idukuliwa kwa sasa?

Mtu mwenye upeo mkubwa atajua muda huu ndio ulikuwa ni muda mwafaka kiujasusi baada ya uchaguzi mkuu 2020 kwa sababu nguvu zilizokuwa zimewekezwa katika Uchaguzi Mkuu 2020 ili kumuondoa Rais Magufuli madarakani kwa njia ya sanduku la kura au maandamano kupitia kwa Tundu Lissu kutofanikiwa.

Ukisikiliza sauti ya tatu utagundua kuwa Tundu Lissu aliwaaminisha ''majasusi'' ana uwezo wa kumtoa Rais Magufuli madarakani kwa kura au maandamano.

Ieleweke kuwa, katika baadhi ya misheni hasa za kijasusi zenye changamano na tata huwa kuna mpango(plan) zaidi ya mmoja. Baada ya mpango wa kwanza kushindwa, mpango wa pili ulichukua nafasi yake na kufanikiwa!

Nadhani hoja za kinadharia kutoka kwa baadhi ya wanasiasa hasa wabunge za kutaka kubadilisha katiba ya Tanzania ili kumuongezea Rais Magufuli muda wa Urais pia zimeharakisha sana ''mission'' hii kabla hawajaanza kuandika ''miswaada binafsi'' na kupeleka bungeni kwa sababu ungepitishwa bila kikwazo chochote!

Mission accomplished, the rest is history!

NOTA BENE.
Kwa wasiojua, pacemaker/defibrillatorni ni kifaa kidogo cha umeme chenye ukubwa kama kiberiti ambacho hufuatilia na kudhibiti wimbo wa moyo ambacho huingizwa kwenye kifua ili kufuatilia na kudhibiti sauti ya moyo isiyo ya kawaida ili kusukuma damu kwa kiwango kinachotakiwa.
View attachment 1733899
Mwanangu lolote linawezekana hasa unapokaa kwenye ulaji wa juu na mkubwa kama huu hasa ukawa noma kwa washenzi
 
Adui wa ndani anaekubali kutumika na beberu ni mbaya kuliko beberu mwenyewe.
Naunga mkono uchunguzi ufanyike tumtafute yuda isakariote.
 
Akiwa Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan (sasa Rais) alituambia tu "Rais Magufuli amekufa kutokana na tatizo la mfumo wa umeme katika moyo wake, tatizo alikokuwa nalo zaidi ya miaka 10 iliyopita". Hivi, hili jibu linatosha kuaminiwa?

Ni wangapi Wana tatizo kama hilo lakini bado wanadunda? Mbona Rais alikuwa mzima bukheri wa afya ziarani Dar? Nini kauli ya Daktari wake? Hakujua dalili au ishara ya Rais kupata shida? Nini maana ya Ulinzi madhubuti kwa Rais? Nini hasa kilimsibu Magufuli? Na kwanini wapambe wa mabeberu ndio wawe wa kwanza kubaini hali dhoofu ya Rais Magufuli?

Tunajua JPM hakuwa rafiki na mabeberu katika vita ya uchumi. Kwa nini Rais SSH asiunde Tume ya Kitabibu kuchunguza kifo cha kipenzi chetu? Yaani tukubali tu kirahisi maelezo ya umeme moyoni?! Hapana. Nakataa, muda utaongea.
Jikumbushe walipouawa akina Eddie Moringe Sokoine ole Severe na Horace Kolimba. Hakuna kilichofanyika. Ukishafukiwa kila kitu kinafukiwa na kufutika. Hata JFKennedy alipotea hivyo ukiachia mbali Patrice Lumumba, Samora na wengine wengi tu.
 
Yaani hao mabeberu wanaotuonea wivu wa kibiashara walioshindwa kutupata hadi kutumia mbinu za kuweka virusi kwenye barakoa badala ya kwenye misaada lukuki wanayotupa ndio waweze kumfikia kiongozi wa nchi ?

Ukitumia logic mambo mengi hayatakupa shida (husasan propaganda za ajabu ajabu)....
 
Akiwa Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan (sasa Rais) alituambia tu "Rais Magufuli amekufa kutokana na tatizo la mfumo wa umeme katika moyo wake, tatizo alikokuwa nalo zaidi ya miaka 10 iliyopita". Hivi, hili jibu linatosha kuaminiwa?

Ni wangapi Wana tatizo kama hilo lakini bado wanadunda? Mbona Rais alikuwa mzima bukheri wa afya ziarani Dar? Nini kauli ya Daktari wake? Hakujua dalili au ishara ya Rais kupata shida? Nini maana ya Ulinzi madhubuti kwa Rais? Nini hasa kilimsibu Magufuli? Na kwanini wapambe wa mabeberu ndio wawe wa kwanza kubaini hali dhoofu ya Rais Magufuli?

Tunajua JPM hakuwa rafiki na mabeberu katika vita ya uchumi. Kwa nini Rais SSH asiunde Tume ya Kitabibu kuchunguza kifo cha kipenzi chetu? Yaani tukubali tu kirahisi maelezo ya umeme moyoni?! Hapana. Nakataa, muda utaongea.
Walisema ni maradhi ya Moyo. Case closed.
 
Back
Top Bottom