Je, Rais Samia anayo haki na misingi ya kuongoza Tanzania Bara (Tanganyika) kwa mambo yasiyo ya Muungano?

Hii shida yote hii wakumlaumu ni nyerere, muungano wenyewe umekata kimtego mtego tuu, nguvu zinatunika kuulinda,sisi watanganyika ndiyo tunaulazimisha sijui tunaumwa nini?

Yes wa kumlaumu ni Nyerere, lakini hatuwezi kuendelea kumlaumu milele, inafika wakati tuchole mstari na tuseme sasa basi.
We need reforms zakutosha kwenye katiba juu ya muungano wetu
 
Hayupo anayepinga uwepo wa Samia, yeye yupo kwa mujibu wa Katiba iliyopo, Ila madhaifu ya hii Katiba na aina ya muungano tulionao unaonekana zaidi kipindi hiki. Muungano mzuri wa serikali moja tuu na sio vinginevyo

Welldone aisee, umeongea mawazo yangu
 
Mtoa mada ana hoja za msingi sana, ingawa kuzitoa muda huu inaonekana kama hapendi kuwe na rais kutoka visiwani, ila hii hoja hata kama ingetolewa kipindi cha hayati bado ina mantiki.

Sina ugomvi wowote wa Mama kuwa Rais wa Taifa letu, lakini kwa kipindi chake mapungufu mengi sana juu ya Muungano yanaonekana wazi wazi,

Sio sawa kukimbia hoja hii kwa sababu tu tuna Rais Mzanzibari kwa sasa, ni busara kujadili na ikiwezekana kushawishi mabadiriko yatakayo ondoa mkanganyiko huu.
 

Nadhani wakati wa kurekebisha katiba yetu ni sasa, tusisubiri mpaka tugombane na kufukuzana,
Ni dhahiri kwamba, Mzanzibari kuongoza Bara kwa mambo yasiyo ya muungano inaleta utata, kwani hatukuungana kwa kila kitu.

Na katiba ya sasa inaeleza wazi juu ya mambo 22 ya muungano, nilitegemea Rais wa muungano kama anatoka Zanzibar ahusike na mambo ya muungano exclusive, na katiba iseme mambo yasiyo ya muungano yawe chini ya???? Makamu wa Rais, PM, etc
 
Si mambo ya kuhitaji kuumiza kichwa chako haya, miaka yote tumeimba, tumetisha, tumesingizia watu kuwa WANAHATARISHA MUUNGANO,
kwamba MUUNGANO ULINDWE KWA GHARAMA ZOZOTE.
Acha mambo yaende hivyo hivyo; ndiyo gharama yenyewe

Usinipangie cha kufanya, hii nchi ni yetu sote.
Kwani ni nani aliitisha referendum kuhusu muungano wetu kupata popular puplic opinion? Yupo?

Tanzania ya 1961 sio ya sasa, wengine hatukuwepo, tuna haja ya kuhoji
 
Rais Mh Mama Samia hajaanza kuongoza Tanzania leo. Amekuwa kiongozi mkubwa namba mbili Tanzania takriban miaka sita sasa.
Hapakuwa na swali wala figusi kipindi chote hicho.
Amepanda kuwa namba moja sasa maneno yamekuwa mengi mnoo..
Kipindi chote cha nyuma mlikuwa wapi? Au kwa vile haja toka kanda iliyo haribu tasnia na utu wa Watanzania?
Kwa taarifa tuu, Mama Samia ni Rais HALALI wa Tanzania. Kama mlitegemea genge la Wasukuma poleni sana.
Miaka mitano ilikuwa kama tuko jehanam.
Sasa mama kaja kutupa tabasamu mmeanza na uchokonozi.
Tulieni Mama Samia atupeleke Kaanan nchi ya maziwa na asali.
Mungu wanMbinguni amkinge Mh. Samia na macho ya husda.
 
Swala la urais ni la Muungano, kwa hiyo lina-override eceptions zingine zote ndani ya JMT
 
Kama mngrjikita kujibu hoja basi tungefika mbali sana. Je, nimeandika uongo? Au kuna sehemu nimekosea?
Magufuli kaingiaje hapa?

Hoja ni hii, ni sahihi kwa Mzanzibar kuongoza Bara kwa mambo yasiyo ya Muungano??
Tubaki hapa jamani
Hawa vijana akili zao ni ndogo Sana wanachojaribu kufanya ni kuahirisha kujadili tatizo na sio kuliondoa tatizo kwa kuleta Mambo nje ya mada
 
Je, anakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sababu yeye ni Mzanzibari au kwa sababu yeye ni Mtanzania?

Anyway, tusichoshane kwa maswali... hapa sio bungeni!

Kwanza, tuweke pembeni suala la kuwa rais kwa sababu alikuwa makamu wa rais! Umakamu wake wa rais ulitokana na Uzanzibari wake!

Lakini hapa tunaujadili urais, ambao mtu haupati kwa Uzanzibari wake bali kwa Utanzania wake! Na tunaposema Utanzania, tunazungumzia jamhuri ya muungano!

Sasa kwavile umeshasema mambo yasiyo ya muungano kwa Tanzania Bara yanashughulikiwa na serikali ya muungano; serikali hiyo ya muungano rais wake ndo huyo Samia, ambae, kimsingi urais wake hautokani na Uzanzibari wake bali na Utanzania wake!!!

Na kwavile urais wake unatokana na Utanzania wake, hakuna shaka kwamba, ana haki na mamlaka ya kusimamia yale yote yanayopaswa kusimamiwa au kushughulikiwa na serikali ya muungano!!
 

Naona unatetea uZanzibari na Utanganyika tu, sioni mantiki katika hoja yako. Hujajibu hoja iliyoko mezani!!!!!

Ni kwamba, Mama ni Rais wa muungani hatujabisha, lakini katika muungano kuna mambo baadhi ya muungano(22) na nilitegemea ange base kwenye hayo 22 kwa upande wa Zanzibar, lakini anatoa wapi authority ya kudeal na mambo yasiyo ya muungano, ilhali yeye ni zao la muungano, na anaamini katika mambo ya muungano, hapo sijui
 
Yeye kuwa zao la muungano haimpotezei uhuru wake wa asili wa kuwa rais wa Jamhuri ya muungano.

Alipokuwa makamu wa rais hakuwa na huo uhuru wa kushughulika na masuala yote kwa ujumla wake?.
 

Hakuna nchi inayojulikana Zanzibar duniani kote, nenda UN, AU, EAC, SADC etc hakuna bendera ya Zanzibar inayopepea huko.

Kwa hiyo kusema Tanzania Bara (Tanganyika) sio nchi na haijulikani popote ila Zanzibar ni nchi nadhani ni uwendawazimu tu, kwa sababu hivi vitu havina tofauti
 
 

Exactly, na kama tuko makini yunaweza kuepusha kufika huko
 
Kwani Mzanzibari si Mtanzania? Mbona Mwinyi na Jumbe waliongoza Zanzíbar ilhali si Wazanzibari?
Je katiba inasemaje kuhusu Zanzíbar kutoa raisi au inasema MTANZANIA tu ?

Acha uongo, rudi kwenye hoja mezani
 
G55 ya nini kwa sasa. Lets give time kwa mama atulie kwenye kiti kisha haya Muungano tutayazungumza baadaye na yeye kuyafanyia kazi kwa mujibu wa Katiba na atakavyoona inafaa. Kwa sasa yupo kwenye nafasi hiyo kwa mujibu wa katiba iliyopo. Fullstop.

When is baadaye? Afanyie kazi asifanyie kazi, the bottom line ni kujadili haya mapungufu ya katiba na kuyatatua sasa
 

Asante sana mkuu, nimeheshimu sana mawazo yako.
Thank you
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…