Je, Rais Samia anayo haki na misingi ya kuongoza Tanzania Bara (Tanganyika) kwa mambo yasiyo ya Muungano?

Je, Rais Samia anayo haki na misingi ya kuongoza Tanzania Bara (Tanganyika) kwa mambo yasiyo ya Muungano?

Nionavyo mimi: Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Tanganyika na Zanzibar. Kwa lugha rahisi hakuna Tanzania Bara, kuna Tanganyika na Zanzibar. Huyu ni Raia wa Tanzania. Unapozungumzia Muungano, ondoa akilini mwako Tanzania Bara, sema Tanganyika. Hivyo kwa maana hiyo, Raia wa Tanzania anayo haki zote za kuwa Rais wa Tanzania ili mradi anatimizi vigezo vya kuwa Rais- Umri, akili timamu, uraia halali.
Ni sawa, ila mtoa hoja anachouliza ni kwa mantiki gani Mzanzibari aongoze mambo ya Tanganyika yasiyo ya Muungano wakati Mtanganyika (Hata alipokuwepo Magufuli) asiongoze mambo yasiyo ya Muungano Zanzibar? Mimi nona hapa dawa ni serikali 3 au moja, hizi mbili zina utata.
 
Hoja ni kwamba rais anapotoka Zanzibar kuwe na kiongozi mwingine mkuu anaesimamia Mambo ya bara yasio ya Muungano, Kama wanavyofanya wao Zanzibar
Labda ingefaa, lakini nayo inahitaji mabadiliko ya Katiba
 
Yaan mzanzibari aongoze bara kwa mambo hata yasiyo ya muungano ila Mbara asiingilie mambo yasiyo ya muungano Zanzibari! asee Nyerere alikosa hekima katika hili.
Kimsingi Nyerere aliweka mambo yote ya Tanganyika ndani ya serikali ya muungano ndiyo maana tanganyika mambo yote ni ya muungano na ndiyo maana hakuna serikali ya tanganyika hivyo tumsapoti mama aendelee kuongoza nchi.
 
Kimsingi Nyerere aliweka mambo yote ya Tanganyika ndani ya serikali ya muungano ndiyo maana tanganyika mambo yote ni ya muungano na ndiyo maana hakuna serikali ya tanganyika hivyo tumsapoti mama aendelee kuongoza nchi.
Unachoongea haki make sense hats kidogo.

Mambo ya muungano yapo 22, any thing out of hizo 22 haihusiani Na muungano!!

Rais wa muungano ( ambaye sio wa bara) ana pata wapi mandate ya kumanage mambo yasio katika muungano Tanzania bara.

Huu ni mtego hatari sana ( a ticking bomb) nalitakuja kulipuka siku ambayo rais wa jamhuri Na wa Zanzibar watatoka vyama tofauti


Na ndio maana ili kuepusha ili itabidi chama chenye nguvu kushinda muungano urais itabidi kitumie nguvu ya ubabe ama wizi kuiba kura Na Zanzibar kishinde hata kama hakipendwi ili kuepusha hili balaa.

Ndomana Mimi sipendi kuilamu CCM inachofanyaga Zanzibar najua it is a necessary evil maana wanajua mfano

Wangeruhusu siku maalim akachukua urais Zanzibar Na CUF ( au ACT ) nchi haiwezi tawalika aisee kutakuaa Na mkanganyiko mkubwa mno wa kimadaraka maana katiba Mpya ya Zanzibar nayo changamoto tupu
 
Nime quote vifungu vya katiba ku-support arguments zangu, nimeuliza kuna mahala nimeongea uongo?
Sijajibiwa zaidi ya matusi yako,

I quit arguing will stupid zero brain like you.
Acha usen&&ge! Hivyo vifungu ndiyo umevijua leo? Mtawala yoyote huwa anataka katiba inayomlinda akiwa madarakani. Dikteta Magufuri alijua wazi kwa katiba hii mbovu itampa mamlaka ya kufanya lolote na hakuna wa kumuuliza. Kumbuka Mwl. Nyerere aliwahi kusema kuwa kwa katiba hii akitokea mwendawazimu akawa Rais basi atakuwa Dikteta. Sasa alipoingia huyo mtu wako ikulu na kuambiwa arekebishe katiba unakumbuka alitoa jibu gani la kifedhuli?
 
Mtaota mpaka muote tena.

Sio nyinyi mnaosema Zanzibar ni kama Mkuranga?? Imekuwaje tena Leo?? Eti yaani tungeuua utaifa wa Zanzibar!!!!!!!! Mungu wetu tunaemuabudu ataziepushia mbali husda na njama zenu mbaya kwa Zanzibar na Zanzibar itaishi milele mpaka mwisho wa dunia.

Wakati nyinyi mkifikiria serikali 3 Leo, Wazanzibari kwa umoja wao wanafikiria mambo makubwa zaidi, time will tell.
You got it all wrong sina husda yeyote Na wazenji why should I?

Ninachosema huu mfumo unamapungufu mengi yanayofunikwa Na CCM kwakuwa inashika madaraka both sides.

Siku ikitokea JMT Na Zanzibar zina marais from different political parties tutaona mengi sana
 
You got it all wrong sina husda yeyote Na wazenji why should I?

Ninachosema huu mfumo unamapungufu mengi yanayofunikwa Na CCM kwakuwa inashika madaraka both sides.

Siku ikitokea JMT Na Zanzibar zina marais from different political parties tutaona mengi sana
Nakuuliza kwa nini huu mjadala unauleta leo wakati mama yupo madarakani? Wewe na wenzio wote wanafiki wakubwa akiwemo Humphrey polepole! Mna ndimi mbili kama nyoka. Acheni ujinga na kuleta chokochoko. Sisi wote ni waTz ujinga wenu pelekeni kwa wake zenu acheni mama atawale Nchi kwa raha na afanye lolote atakaloona linawapa faida Raia wake
 
Watanganyika ndio wanautaka wala sio wazanzibar
Bora hata wangejitawala wenyewe. Kama wangeamua kutawalia na Sultan wao wa Oman, wangejua wenyewe. Huu Muungano hauna tija wala faida yoyote ile kwa Tanganyika!

Kama hofu ilikuwa ni Vita Baridi, kwa sasa havipo tena! Kwma vipi wakabidhiwe tu Visiwa vyao, na sisi tuendelee na nchi yetu.
 
Watanganyika ndio wanautaka wala sio wazanzibar
Huu Muungano naona unawanufaisha tu CCM. Sidhani kama hiyo idadi ya Watanganyika ni kubwa kihivyo! Ni wale wachache tu wanao fanya kazi huko Zanzibar, wafanyabiashara na pia wale walio jenga undugu kwa kuoana/kuoleana!

Kinyume na hapo, hakuna.
 
Yaan mzanzibari aongoze bara kwa mambo hata yasiyo ya muungano ila Mbara asiingilie mambo yasiyo ya muungano Zanzibari! asee Nyerere alikosa hekima katika hili.
Hii shida yote hii wakumlaumu ni nyerere, muungano wenyewe umekata kimtego mtego tuu, nguvu zinatunika kuulinda,sisi watanganyika ndiyo tunaulazimisha sijui tunaumwa nini?
 
Niliweka andiko humu juu ya umuhimu wa TAMISEMI kuwa chini ya Waziri Mkuu ambaye ndio mtendaji wa bara.
 
Mkuu kwa nini Mh. Samia Suluhu Hassan amekuwa Rais? Tuanzie hapo kwanza.

Ukishajibu hilo hapo juu, sasa zile nguvu ambazo wewe na wanakikundi wenzakolikuwa mnasema mnahitaji Magufuli 2025 basi sasa hivi hamishieni kwa Madam President! Si umesikia juzi kasema yeye na Magufuli ni Kitu Kimoja? Kwa hiyo hakuna mtachopoteza wewe na wanakikundi wenzako.
Rejea uzi wako wa Feb 16, 2021.

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
Hayupo anayepinga uwepo wa Samia, yeye yupo kwa mujibu wa Katiba iliyopo, Ila madhaifu ya hii Katiba na aina ya muungano tulionao unaonekana zaidi kipindi hiki. Muungano mzuri wa serikali moja tuu na sio vinginevyo
 
Nakushairi uachane na kutaka kujua mimi ni nani, acha kunijadili mimi na jadili hoja.

Mbona jambo ni rahisi sana, tumeungana katika mambo 22, kwa upande wa Zanzibar wana chombo kinacho deal na mambo yasiyo na muungano, kwa upande wa Bara hakuna chombo kama cha Zanzibar pindi rais wa Jamhuri anapotoka Zanzibar.

Tujadiliane kwa hoja na kwa kujenga sio kuitana majina
Mkuu mambo ya Tanganyika yasiyo ya muungano yanasimamiwa na TAMISEMI ambapo hapo awali TAMISEMI ilikuwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu.
 
Yaan mzanzibari aongoze bara kwa mambo hata yasiyo ya muungano ila Mbara asiingilie mambo yasiyo ya muungano Zanzibari! asee Nyerere alikosa hekima katika hili.
Mkuu, ktk vitu Vya kisheria, huwa vina tabu yake, Sheria unaweza itengeneza leo na ukaiona inakidhi matakwa ya hiyo, lkn kadri siku zibavyokwenda, sheria hiyo huwa inaenda inapitwa Wakati, na ndiyo maana kuna kipindi cha marekebisho ya sheria

Tafadhali, usimlaumu mtu, zungumzia hizo sheria, bado zinahitajika ama zimepitwa Wakati??
 
Tuelewe kwamba Zanzibar ilipata Uhuru wake kutoka kwa Waingereza 1963 lakini wazalendo walitaka kumuondoa Sultan na walifanikiwa kufanya hivyo mwaka1964.

Sultan alikimbilia Uingereza lakini nchi yake ya asili yaani Oman ilikua tayari kumpa msaada wa kijeshi arudi Zanzibar. Wazalendo waliomba msaada Bara na huu muungano kuzaliwa.
Tumeshachanganya sana damu ni vigumu kukwepa kuwa kitu kimoja.
 
Serikali moja ya majimbo mawili
Hayupo anayepinga uwepo wa Samia, yeye yupo kwa mujibu wa Katiba iliyopo, Ila madhaifu ya hii Katiba na aina ya muungano tulionao unaonekana zaidi kipindi hiki. Muungano mzuri wa serikali moja tuu na sio vinginevyo
 
Muundo wa muungano uliopo ni kaburi kwa Tanganyika
(Umeifanya Tanganyika kuwa ya kunyonywa na kutawaliwa na Zanzibar)
  • Zanzibar haichangii gharama za uwekezaji na uendeshaji ila mgao wa mapato, faida, bakaa inapata
  • Kule Zanzibar hakuna mtanganyika anayeruhusiwa kumiliki ardhi ila bara wazanzibari wanajitwalia tuu
  • Kule Zanzibar hakuna mtanganyika anayeruhusiwa kuajiliwa SMZ lakini wazanzibari wanaajiliwa mpaka ualimu na ajira za kada ya afya
  • Kule Zanzibar hakuna mtanganyika anayeruhusiwa kugombea uwakilishi ila bara wanagombea tuu
  • Kule Zanzibar hakuna mtanganyika anaeteuliwa kushika nafasi za uongozi kwenye serikali ya Zanzibar ila bara wanateuliwa kuwa ma DAS, DED, DC, RAS, nakadhalika
Aisee hili la kupata Raisi anayetokea Zenji, halikuja bule, limekuja ili lituonyeshe jinsi katiba Yetu ilivyombovu na mapengo mengi yanayohusu muungano wetu

Ni Wakati muafaka sasa Katiba irekebishwe ama mambo yanayozungumzwa yakihusisha kero za muungano, na hili liongezwe kwenye kero la muungano
 
A. UTANGULIZI
Napenda kuweka wazi kwamba nimeanzisha mjadala huu, ili kuondoa mkanganyiko na mkwamo ninao uona wazi wazi katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania. Kwa mara nyingine katiba yetu imejaribiwa (imekuwa tested), hivyo ni busara kuwepo kwa mjadala wa kuondoa shaka na hoja gonganishi katika katiba yetu kwa ustawi bora na imara wa Taifa letu Pendwa.

B. HISTORIA KIDOGO
Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania iliundwa Tar.26 April 1964, ikiwa ni muungano wa maTaifa huru ya Jamhuri ya Tanganyika (1962) na Jamhuri ya watu wa Zanzibar (1964). Jamhuri hizi mbili ziliingia mkataba wa pamoja 1964 na kuanzisha dola la Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania.
Kwa mujibu wa Katiba ya J.M.T ya mwaka 1977, ibara ya 4(3) imeorodhesha mambo 22 ya muungano baina ya pande mbili zilizo-ungana.
Kwa upande wa Tanzania bara (Tanganyika) mambo yasiyo ya muungano yanasimamiwa na serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, na Kwa upande wa Zanzibar, mambo yasiyo ya muungano yanasimamiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.


Kwa Lugha rahisi, Muungano wetu ni wa serikali Mbili, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika ilifutwa na haipo.

C. MAMBO YA MUUNGANO
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (1977), ibara ya 4, ibara ndogo ya 3, imetoa mwongozo kuhusu mambo ya muungano. Na, yameorodheshwa katika nyongeza ya kwanza ya katiba yetu.
Yafuatayo ni mambo 22 ya muungano kwa mujibu wa Katiba yetu.
1. Katiba ya Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
2. Mambo ya Nchi za Nje.
3. Ulinzi na Usalama.
4. Polisi.
5. Mamlaka juu ya mambo yanayohusika na hali ya hatari.
6. Uraia.
7. Uhamiaji.
8. Mikopo na baiashara ya Nchi za Nje.
9. Utumishi katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
10.Kodi ya Mapato inayolipwa na watu binafsi na mashirika, ushuru wa forodha na ushuru wa bidhaa zinazotengenezwa nchini Tanzania unaosimamiwa na Idara ya Forodha.
11.Bandari, mambo yanayohusika na usafiri wa anga, posta na simu.
12.Mambo yote yanayohusika na sarafu na fedha kwa ajili ya malipo yote halali (pamoja na noti); mabenki (pamoja mabenki ya kuweka akiba) na shughuli zote za mabenki; fedha za kigeni na usimamizi juu ya mambo yanayohusika na fedha za kigeni.
13.Leseni ya viwanda na takwimu.
14.Elimu ya juu.
15.Maliasili ya mafuta, pamoja na mafuta yasiyochujwa ya motokaa na mafuata ya aina ya petroli na aina nyinginezo za mafuta au bidhaa, na gesi asilia.
16.Baraza la Taifa la Mitihani la Tanzania na mambo yote yanayohusika na kazi za Baraza hilo.
17.Usafiri na usafirishaji wa anga.
18.Utafiti.
19.Utafiti wa hali ya hewa.
20.Takwimu.
21.Mahakama ya Rufani ya Jamhuri ya Muungano.
22.Uandikishaji wa Vyama vya siasa na Mambo mengine yanayohusiana navyo.

Angalau kwa mujibu wa katiba yetu, haya yaliyo orodheshwa ndiyo mambo ya muungano.


D. HOJA MEZANI (HOJA KINZANI)

Kwa kuwa Rais aliyeko madarakani ni asili ya Zanzibar, hivyo ni mZanzibari, na anaongoza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na yeye ni zao la muungano wetu. Na, kwa kuwa Katiba yetu imebainisha dhahiri mambo ya muungano, Je? Ni sahihi kwa Rais wa sasa kuongoza Tanzania Bara (Tanganyika) hata kwa mambo yasiyo ya muungano?

1.Kama ni sahihi, anaongozaje mambo yasiyo ya muungano ilhali yeye ni mZanzibari na ni zao la muungano na ana uishi muungano pamoja na mambo ya muungano, tukumbuke kwamba , tumeungana lakini hatujaungana katika mambo yoye, tumechagua mambo ya kuungana.
2.Kama sio sahihi nini kifanyike?

E. HITIMISHO
Kuna watu mtaacha kujibu hoja na kuleta vioja, kuna watu mtauliza kwa nini hoja hii inaletwa sasa. Majibu yake ni kwamba, Jana(26.04.2021) ilikua siku ya kukumbuka Muungano wetu, hivyo ni busara kuujadili kipindi hiki, na jana kuna kongamano lilifunguliwa ,kuendeshwa na makamu wa Rais Dkt.P.Mpango. Lakini, kwa maya nyingine tumepata Rais Mzanzibar kwa mujibu wa Katiba, hivyo nimeona ni vyema tujadili jambo hili ili kutoa/kuondoa hoja hizi kinzani.

Kwa maoni yangu, Kuna haja ya kuangalia maslahi ya Tanzania bara(Tanganyika) katika muungano wetu. Sioni maana ya Mzanzibari kuwaongoza waTanganyika katika mambo yasiyo ya muungano, unless tukubali kuungana kwa kila jambo. Pia, kuna haja ya kuwalinda waTanganyika kama ambavyo katiba inawalinda waZanzibari, Mathalani;
-Mtanganyika hawezi kumiliki ardhi Zanzibar kwa hoja mufilisi kwamba Zanzibar ni ndogo, lakini kwenye mgawanyo wa pesa za Maadhimisho ya Muungano watataka equal share.
-Wakati anahutubia Bunge, Rais Samia alitoa ahadi ya kununua Meli za uvuvi nne, huku mbili zikielekezwa Zanzibar na mbili Bara. Kwanza hii sio haki, kwani Uvuvi, na Usafirishaji wa majini siyo mambo ya muungano, sioni matiki kwa nini Rais wa Muungano aanze kuhangaika na mambo yasiyo ya muungano kwa Zanzibar kwa kutumia pesa za Watanganyika.

Niko Tayari kurekebishwa na kusahihishwa katika mjadala huu, ili tujenge Muungano utakao kidhi matakwa ya pande zote za Muungano.
Ni vigezo gani vilitumika rais wa Tanganyika kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na rais wa Zanzibar kuwa Makamo. Kifo Cha Abed Aman Karume kiliacha maswali mengi ya Muungano yasiyokuwa na majibu.Kama angekuwepo mwaka 1977 katiba isingekuwa kama ilivyo sasa.Kwa maoni yangu yeye Karume hakutaka rais wa Muungano atoke Zenj.Lengo lake lilikuwa ni ulinzi wa serikari ya Mapinduzi Zanzibar.Ndio maana bado inaendelea kuwepo.Wewe utakuwa rais na mimi makamo.Mtazamo was hayati Karume na unapaswa kuwa endelevu
 
Back
Top Bottom