Je, Rais Samia Suluhu Hassan ni Rais wa Awamu ya Tano au ya Sita kwa mujibu wa Katiba ya nchi?

Je, Rais Samia Suluhu Hassan ni Rais wa Awamu ya Tano au ya Sita kwa mujibu wa Katiba ya nchi?

Kama Mama Samia hana awamu yake inayojitegemea basi hana mamlaka kamili ya Rais.
 
Ila pia kwa common sense, serikali inaundwa na baraza la mawaziri pia. Baraza la mawaziri ni lile lile. Halijavunjwa na kuwekwa jipya...
Hilo baraza linavunjwa soon subiri tu. 1984 Mwinyi alipopokea kijiti kwa JK alitulia kwanza halafu akapiga kitu.
 
Hilo baraza linavunjwa soon subiri tu. 1984 Mwinyi alipopokea kijiti kwa JK alitulia kwanza halafu akapiga kitu.
Litakapovunjwa na kuundwa tena sasa hapo ndio tutasema serikali ya awamu ya sita...
Hapo tutakua sawa ila mpaka sasa hii ni serikali ya awamu ya tano, muendelezo wake baada ya aliyekua madarakani kufariki, ni rais wa sita ila awamunya tano bado.
 
Alipokufa Dr Omar Juma, aliyekuwa makamu wa awamu ya tatu, je yule Dr. Shein aliyemfuata alikuwa ni makamu wa wamu ya nne?
Makamu ana awamu? Wewe mbona unakwenda kabisa nje ya mada? Ulishaona Idara gani msaidizi anaandikwa kwenye leadership chart ya kampuni.
 
awamu inaisabiwa kwa ukaaji madarakan kwa Rais mfano mzee Mwinyi Zenj ametawala miaka.mingapi na anahesabika
Alipotoka na kuingia mwingine aliendelea na baraza la mawaziri la mwinyi au lilivunjwa?
 
Ninadhani awamu inaanza na uchaguzi! Samia karithi awamu ya tano na ataimalizia kabla hajaanza awamu ya sita iwapo atashinda uchaguzi ujao.
Msimhafifishe Mama kwa kumweka kwenye kivuli cha mtu. Rais wa awamu ya Pili mzee Alli Hassan Mwinyi alitawala nchi hii miaka 11 na alipochukua kijiti kwa Mwalimu akaitwa Rais wa awamu ya 2.
 
Samia sio interim president. Hajashika kiti kusubiri uchaguzi ufanyike apatikane rais 'halali'. Yeye ni full rais as per the contitution.
Ndiyo ni full Rais! Rais wa mpito ni Rais kamili kikatiba. Hakuna alichopungukiwa! Ni wa mpito kea maana ya kwamba ataongoza mpaka uchaguzi mwingine 2025 ambapo atagombea kitu hicho! Bado ni wazo tu, I may be wrong!
 
Ndiyo ni full Rais! Rais wa mpito ni Rais kamili kikatiba. Hakuna alichopungukiwa! Ni wa mpito kea maana ya kwamba ataongoza mpaka uchaguzi mwingine 2025 ambapo atagombea kitu hicho! Bado ni wazo tu, I may be wrong!
Katiba yetu ndio imesema kuwa ni rais wa mpito?
 
Hilo baraza linavunjwa soon subiri tu. 1984 Mwinyi alipopokea kijiti kwa JK alitulia kwanza halafu akapiga kitu.
Mwinyi alichaguliwa mwaka 1985, na hivyo kuanza awamu mpya; hakurithi utawala wa Nyerere!
 
Mzee hukukisoma vizuri hicho kipengele ulichokinukuu. Hakuna mahali kwenye kipengele hicho panapotaja neno awamu. Habari za awamu zilikuja tu toka kwa wanasiasa kwa sababu ya utashi wao tu. Hivyo awamu hii ingeweza kuwa awamu ya tano au ya sita kulingana na anavyoamua mwenye sauti kubwa.

Hili jambo umeliweka kama vile raisi anayeingia madarakani ni lazima awe na vipindi 2. Nafikiria ingeitwa awamu ya ngapi kama kwa bahati mbaya fulani hivi marehemu angeangushwa katika uchaguzi. Ungeendelea kuuita utawala mpya awamu ya tano sababu tu miaka 10 haijakamilika
Angekuwa wa term moja tu!
 
Alipokufa Dr Omar Juma, aliyekuwa makamu wa awamu ya tatu, je yule Dr. Shein aliyemfuata alikuwa ni makamu wa wamu ya nne?
Umakamu hauna awamu kwani makamu hana mamlaka yo yote ya kidola. Hivyo makamu hata wakibadilishwa 10 hawaathiri mamlaka ya dola.
 
Katiba haina lugha ya "awamu". Hii ni lugha ya siasa au wanahabari. Je unaiona wapi kwenye sheria?
 
Back
Top Bottom