Je, Rais Samia Suluhu Hassan ni Rais wa Awamu ya Tano au ya Sita kwa mujibu wa Katiba ya nchi?

Je, Rais Samia Suluhu Hassan ni Rais wa Awamu ya Tano au ya Sita kwa mujibu wa Katiba ya nchi?

Kwa namna yoyote mama SSH ni rais halali kabisa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mujibu wa katiba ya JMT mwenye madaraka ya kutekeleza shughuli za wadhifa wake bila kulazimika kunukuu chochote kutoka kwa mtangulizi wake. Anaweza kunukuu ya mtangulizi wake pale tu atakapoona vyema hivyo. Hivyo sio sahihi hata kidogo kunasibisha chochote anachotakiwa kufanya na vya mtangulizi wake. Narudia tena halazimiki kurefer chochote toka kwa mtangulizi wake.
 
Ni nini kinasababisha neno awamu litokee?.Bila shaka ni kiongozi, kwa maana ni hesabu ya kawaida ya kuhesabu marais.

Kumbuka pamoja na Mwalimu Nyerere kupiga 20+ Bado ni awamu moja.
 
Jibu la swali lako linajibiwa Zanzibar Hussein Mwinyi ni rais wa awamu ya nane kwa kuwa ni rais wa nane kuna marais kama karume alikufa akiwa madatakani kuna abou jumbe alijiuzuru kuna mwinyi Hassan alimalizia mwaka moja baada ya jumbe na kuna Abdulwakil alidumu kipindi kimoja tu
 
Ni nini kinasababisha neno awamu litokee?.Bila shaka ni kiongozi,kwa maana ni hesabu ya kawaida ya kuhesabu marais.

Kumbuka pamoja na Mwalimu Nyerere kupiga 20+ Bado ni awamu moja.
Ila kwa katiba ya sasa, yaweza kuwa miaka kumi (ibara ya 40 (1) na (2)).
 
Katiba haina lugha ya "awamu". Hii ni lugha ya siasa au wanahabari. Je unaiona wapi kwenye sheria?
Inawezekana maneno 'awamu' na 'kipindi' yanazaliwa au ni tafsiri ya ibara ya 40 (1) na (2).
 
Kuna awamu ya Rais wa Kwanza

Kuna awamu ya Rais wa pili ..... Awamu ya Rais wa tano.


Sasa tunaye Rais wa awamu ya Sita Mama Samia Suluhu Hassani.

Hii no awamu ingine na atafanya teuzi zote kwa mujibu wa Sheria kuanzia Waziri Mkuu na Baraza lake na wengine kwa jinsi itakavyompendeza.
 
Litakapovunjwa na kuundwa tena sasa hapo ndio tutasema serikali ya awamu ya sita...
Hapo tutakua sawa ila mpaka sasa hii ni serikali ya awamu ya tano, muendelezo wake baada ya aliyekua madarakani kufariki, ni rais wa sita ila awamunya tano bado.
Uko sahihi kabisa ni rais wa sita ndani ya serikali ya awamu ya tano
 
Hivyo awamu ya tano (phase 5) imekuwa na Marais wawili. Mmoja ameshika kipindi cha kwanza (1st term) na mwingine karibu kipindi cha pili (2nd term) kwa sababu yule wa kwanza amefariki dunia.
Hebu nisaidie: Rais wa Awamu ya Tatu Zanzibar anaitwa nani?!
 
Mbona wewe hujauliwa ?
Awamu ya tano imetuua imetupiga imetupoteza na kutubambikia uhujumu awamu ya tano imetuzulumu imetusababishia maradhi
Ninahamu tuisahau awamu hio yenye laana
 
Hebu nisaidie: Rais wa Awamu ya Tatu Zanzibar anaitwa nani?!
Kwa mujibu wa Ibara ya 40 (4) ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais wa sasa amefungua awamu ya sita. Hayo ya Z'bar sina information ya kutosha kwa sasa.
 
Ni nini kinasababisha neno awamu litokee?.Bila shaka ni kiongozi,kwa maana ni hesabu ya kawaida ya kuhesabu marais.

Kumbuka pamoja na Mwalimu Nyerere kupiga 20+ Bado ni awamu moja.
Jibu sahihi linapatikana katika ibara ya 40 (4) ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania!
 
Awamu wanapeana CCM wenyewe.. Hakuna kampeni,hakuna ilani aliyokabidhiwa Mama SS kuinadi,hakuteuliwa na tume ya uchaguzi kugombea urais...anatumia ilani aliyopewa JPM, kura alizopata JPM...anatimiza ahadi za JPM,hana kitu alichotuahidi Mh Madame SS.. Huu ni udhaifu wa katiba.
 
Kama Mama Samia hana awamu yake inayojitegemea basi hana mamlaka kamili ya Rais.
Kwa mujibu wa Ibara ya 40 (4) ana awamu yake, lakini Rais anaweza hasiwe na awamu na akabaki kuwa na mamlaka kamili kwa mujibu wa ibara hiyo hiyo ya 40 (4)!
 
Mbona wewe hujauliwa ?
Kweni nimeandika kuuwawa peke yake Mimi nilipigwa hadi kupoteza fahamu kwa kosa la kumpelekea chakula msimamizi wangu wa Chadema wakati wa Uchaguzi mkuu uliovurugwa
 
Awamu wanapeana CCM wenyewe.. Hakuna kampeni,hakuna ilani aliyokabidhiwa Mama SS kuinadi,hakuteuliwa na tume ya uchaguzi kugombea urais...anatumia ilani aliyopewa JPM, kura alizopata JPM...anatimiza ahadi za JPM,hana kitu alichotuahidi Mh Madame SS.. Huu ni udhaifu wa katiba.
Lakini si alikuwa mgombea mwenza? Labda udhaifu wa katiba unatokea kwenye makamu wa Rais, lakini Bunge linawakilisha wananchi?
 
Mwinyi alichaguliwa mwaka 1985, na hivyo kuanza awamu mpya; hakurithi utawala wa Nyerere!
Kwa mujibu wa ibara ya 40 (4) ya katiba, hii imeshakuwa awamu mpya ya sita!
 
Back
Top Bottom