Je, Shekilango na Urafiki ndio Stendi mpya za Mabasi yaendayo mikoani?

Je, Shekilango na Urafiki ndio Stendi mpya za Mabasi yaendayo mikoani?

Stand ya Magufuli Mbezi ulikuwa ubunifu usiokuwa na tija. Kwenda kurundika mabasi zaidi ya 300 yanayotakiwa kuondoka kwenda mikoani kwa wakati mmoja ni kituko. Dsm inahitaji stendi nyingi kulingana na eneo ambako magari yanaelekea.

Hapo Mbezi kwenyewe kutafuta gari linalohusika upande ni vurugu na mbinde.

Watu hawasemi lakini Stendi ya Mbezi haina tija kwa wananchi. Labda makusanyo ya serikali tu. Ndio maana mwanzishaji three hii kaona eneo moja tu la ukusanyaji mapato.
 
Ahlan wa sahlan

Naiomba serikali ifunge hizi ofisi uchwara zilizopo hapa maeneo ya shekilango na Urafiki. Mabasi ya mikoani yamekuwa hayaendi tena kupaki stendi ya Magufuli pale Mbezi badala yake yamekuwa yakijazana maeneo ya shekilango na Urafiki nyakati za Alfajiri na Mchana. Najiuliza ile stendi ya mabilioni pale Mbezi imejengwa kwa ajili ya kina nani?

Wahusika mpo na mnalifumbia mamcho jambo hili.Stendi imekuwa ikikosa mapato ya getini kwa abiria wanaoingia ndani ya stendi kutokana na watu sasa kumiminika kwenda maeneo ya Urafiki na Shekilango.

Wito wangu kwa serikali ni kuhakikisha mnazifunga mara moja ofisi hizi uchwara za haya mabasi hapa Shekilango na urafiki kwani hawa jamaa wameshageuza eneo hili kuwa ni terminal
Asante mpiga debe umesikia, kaanga ksranga na choma mihogo uuze utapata hela nzuri kuliko kupiga debe.
 
Nadhani OFISI na STENDI ni vitu viwili tofauti.

"Ofisi zetu zinapatikana stendi ya Magufuli, chumba namba 37".

Kitu kibaya ni pale "ofisi" zinapoifanya kampuni ya mabasi isitumie huduma za "stendi".

Kwa ufahamu wangu najua mabasi yote yanatumia huduma za stendi bila kujali wana ofisi Shekilango, Magomeni, Manzese au eneo lolote lile.

Mimi sioni ubaya maana lengo kusudiwa la kujengwa kwa stendi bado linatimizwa.

Labda tu uwe umeamua kuwafanyia UKATILI hawa watu wa usafirishaji.

Alichoandika mleta mada kina mantiki...

Kuna mabasi yanayoanza na kumalizia safari hapo Shekilango/Urafiki na hayafiki kabisa kwenye hiyo stendi mpya...

Abiria akihitajika kupanda basi, analazimika kwenda hapo Shekilango/Urafiki...

Ilianza kama utani hivi kwa New Force, Dar Lux na Kilimanjaro, lakini sasa hivi kuna makampuni si chini ya 15...
 
Stand ya Magufuli Mbezi ulikuwa ubunifu usiokuwa na tija. Kwenda kurundika mabasi zaidi ya 300 yanayotakiwa kuondoka kwenda mikoani kwa wakati mmoja ni kituko. Dsm inahitaji stendi nyingi kulingana na eneo ambako magari yanaelekea.
Hapo Mbezi kwenyewe kutafuta gari linalohusika upande ni vurugu na mbinde.
Watu hawasemi lakini Stendi ya Mbezi haina tija kwa wananchi. Labda makusanyo ya serikali tu. Ndio maana mwanzishaji three hii kaona eneo moja tu la ukusanyaji mapato.

Idea nzuri sana mkuu, hapa ndipo linapokuja suala la exposure kwa viongozi wetu...

Miji mingi mikuu huko duniani huwa na stendi kuu zaidi ya moja, na stendi hizo hujengwa maeneo fulani kulingana na wapi magari yataelekwa kutokea hapo au pia kurahisisha wananchi kutotembea umbali mrefu kuifuata stendi...
 
Alichoandika mleta mada kina mantiki...

Kuna mabasi yanayoanza na kumalizia safari hapo Shekilango/Urafiki na hayafiki kabisa kwenye hiyo stendi mpya...

Abiria akihitajika kupanda basi, analazimika kwenda hapo Shekilango/Urafiki...

Ilianza kama utani hivi kwa New Force, Dar Lux na Kilimanjaro, lakini sasa hivi kuna makampuni si chini ya 15...
Kwan lazima upande Dar lux...panda mengine yanayoenda unakoenda...acha ghiliba!
 
Ahlan wa sahlan

Naiomba serikali ifunge hizi ofisi uchwara zilizopo hapa maeneo ya shekilango na Urafiki. Mabasi ya mikoani yamekuwa hayaendi tena kupaki stendi ya Magufuli pale Mbezi badala yake yamekuwa yakijazana maeneo ya shekilango na Urafiki nyakati za Alfajiri na Mchana. Najiuliza ile stendi ya mabilioni pale Mbezi imejengwa kwa ajili ya kina nani?

Wahusika mpo na mnalifumbia mamcho jambo hili.Stendi imekuwa ikikosa mapato ya getini kwa abiria wanaoingia ndani ya stendi kutokana na watu sasa kumiminika kwenda maeneo ya Urafiki na Shekilango.

Wito wangu kwa serikali ni kuhakikisha mnazifunga mara moja ofisi hizi uchwara za haya mabasi hapa Shekilango na urafiki kwani hawa jamaa wameshageuza eneo hili kuwa ni terminal

Ujumbe mzuri sana hata Ubungo mama yake ni mnazi mmoja serikali ikiwa na mautopolo mengi watavuna utopolo.
 
Ahlan wa sahlan

Naiomba serikali ifunge hizi ofisi uchwara zilizopo hapa maeneo ya shekilango na Urafiki. Mabasi ya mikoani yamekuwa hayaendi tena kupaki stendi ya Magufuli pale Mbezi badala yake yamekuwa yakijazana maeneo ya shekilango na Urafiki nyakati za Alfajiri na Mchana. Najiuliza ile stendi ya mabilioni pale Mbezi imejengwa kwa ajili ya kina nani?

Wahusika mpo na mnalifumbia mamcho jambo hili.Stendi imekuwa ikikosa mapato ya getini kwa abiria wanaoingia ndani ya stendi kutokana na watu sasa kumiminika kwenda maeneo ya Urafiki na Shekilango.

Wito wangu kwa serikali ni kuhakikisha mnazifunga mara moja ofisi hizi uchwara za haya mabasi hapa Shekilango na urafiki kwani hawa jamaa wameshageuza eneo hili kuwa ni terminal
Acha uchochezi fazaaa
 
Kama alivyosema mdau mmoja hapo juu Viongozi wetu wengi hawajatembea au hawana maono ya mbali. Ni ushamba wa hali ya juu kuweka stendi moja kwa mji mkubwa kama Dar. Tulishindwa nini kujenge stendi kubwa kule Mbagala kwa ajili ya magari yanayoenda mikoa ya kusini??

Tulishindwa nini pale Mnazi mmoja pakachimbwa chini(undeground) kabisa pakawa na bus terminal kwa ajil ya watu wanaotoka katikat ya mji kuanza safar yao pale wakitaka kusafiri?? Tulishindwa kitu gani kuweka terminal kubwa huku upande wa Bagamoyo kisha tukajumlisha na hiyo ya Mbezi zikawa terminal 4. Yaani tuna wasomi wa mipango miji wa hovyo mno nchi hii na wana mawazo mgando
 
Alichoandika mleta mada kina mantiki...

Kuna mabasi yanayoanza na kumalizia safari hapo Shekilango/Urafiki na hayafiki kabisa kwenye hiyo stendi mpya...

Abiria akihitajika kupanda basi, analazimika kwenda hapo Shekilango/Urafiki...

Ilianza kama utani hivi kwa New Force, Dar Lux na Kilimanjaro, lakini sasa hivi kuna makampuni si chini ya 15...
Sijui kwa hayo uliyotaja.. Ila Njombe express yetu inaingia Mbezi kisha inaenda urafiki
 
Sijui kwa hayo uliyotaja..ila Njombe express yetu inaingia mbezi kisha inaenda urafiki

Sawa, hao watakuwa wanafanya vyema...

Kuna mabasi yanayotokea pale Urafiki (sina haja ya kuyataja), breki ya kwanza huwa Kibanda cha Mkaa ambapo ndio itapakia abiria waliopaswa kupandia Mbezi Terminal, baada ya hapo ni safari kwenda mkoa...

Hiyo stendi bubu ya Urafiki/Shekilango iliasisiwa na makampuni machache wakati ule stendi kuu ikiwa Ubungo, na lengo lao lilikuwa ni kusaidia abiria wao kwa kuwapa huduma na mazingira mazuri wakiiga mifano ya wakongwe kama Scandinavia, Fresh ya Shamba...
 
Mleta uzi acha wivu, mabasi yote yanayoanzia safari Shekilango hasa yanayopita Morogoro road lazima yapite stendi ya Mbezi wakati wa kwenda na kurudi, na kuna baadhi yanayopita njia ya bagamoyo hulazimika tena kupitia mbezi. Kila basi linaloingia stendi linatoa ushuru, sasa sijui umefanya utafiti wako kwa muda gani au umekurupuka tu na kuandika.

Tukienda kwenye swala la kupeleka huduma karibu na mteja, sidhani kuna mfanyabiashara yeyote anayeweza kuamua kuweka huduma yake mahali ambapo hakuna uhitaji mkubwa, pale shekilango ni center nzuri kwa wasafiri na inafikika kwa urahisi na inapunguza adhabu kubwa ya kuamka saa 8 kuwahi mbezi na kuanza kupambana na wapiga debe tangu unashuka stendi ya daladala hadi kufika stendi ya Magufuli.
 
Ahlan wa sahlan

Naiomba serikali ifunge hizi ofisi uchwara zilizopo hapa maeneo ya shekilango na Urafiki. Mabasi ya mikoani yamekuwa hayaendi tena kupaki stendi ya Magufuli pale Mbezi badala yake yamekuwa yakijazana maeneo ya shekilango na Urafiki nyakati za Alfajiri na Mchana. Najiuliza ile stendi ya mabilioni pale Mbezi imejengwa kwa ajili ya kina nani?

Wahusika mpo na mnalifumbia mamcho jambo hili.Stendi imekuwa ikikosa mapato ya getini kwa abiria wanaoingia ndani ya stendi kutokana na watu sasa kumiminika kwenda maeneo ya Urafiki na Shekilango.

Wito wangu kwa serikali ni kuhakikisha mnazifunga mara moja ofisi hizi uchwara za haya mabasi hapa Shekilango na urafiki kwani hawa jamaa wameshageuza eneo hili kuwa ni terminal
Una expose upumbavu wako na kwa jinsi gani ulivyo na wivu na roho mbaya
 
Ahlan wa sahlan

Naiomba serikali ifunge hizi ofisi uchwara zilizopo hapa maeneo ya shekilango na Urafiki. Mabasi ya mikoani yamekuwa hayaendi tena kupaki stendi ya Magufuli pale Mbezi badala yake yamekuwa yakijazana maeneo ya shekilango na Urafiki nyakati za Alfajiri na Mchana. Najiuliza ile stendi ya mabilioni pale Mbezi imejengwa kwa ajili ya kina nani?

Wahusika mpo na mnalifumbia mamcho jambo hili.Stendi imekuwa ikikosa mapato ya getini kwa abiria wanaoingia ndani ya stendi kutokana na watu sasa kumiminika kwenda maeneo ya Urafiki na Shekilango.

Wito wangu kwa serikali ni kuhakikisha mnazifunga mara moja ofisi hizi uchwara za haya mabasi hapa Shekilango na urafiki kwani hawa jamaa wameshageuza eneo hili kuwa ni terminal
Mtu atoke Kigamboni akapandie gari Mbezi acha uzwazwa
 
Hoja yako ya stendi kukosa mapato naona kama haina nguvu kwa sababu abiria mwenye tiketi halipi hicho kiingilio.
Na pia ofisi za kukatia tiketi pale stendi ya Magufuli zipo sehemu ambayo unaenda bure bila kulipa hicho kiingilio.

Mkuu, au wewe ni "mpiga debe" (wale wa 'usafiri wa leo blaza') pale stendi ? Samahani lakini.
Umeshaenda pale Magufuli stand siku za karibuni au umeambiwa tu?

Whether una tiketi au huna, hiyo 300 getting utalipa tu.

Unawajua Suma JKT?
 
Back
Top Bottom