antimatter
JF-Expert Member
- Feb 26, 2017
- 47,274
- 126,778
Inaelekea mleta mada anachukulia waajiriwa walio nje ya mfumo wa ajira ya serikali kama wageni au watu duni. Hili siyo sahihi. Na wao ni watanzania, na ni walipa Kodi. Kama wakiwa na vigezo stahiki wakaajiriwa tatizo nini?Thread hii, inatokana na baadhi ya teuzi za wakurugenzi wa TANESCO na MSD kutoka nje ya mfumo. Nina declare interest kwamba sina shida na teuzi ya MSD. Ni mmoja wa colleagues tuliyekuwa tukifanya naye kazi nje ya mfumo. Ninaamini anastahili, na ataweza.
Tatizo linatokea hapa.
1. Hivi inakuwaje nchi yenye watumishi wa serikali zaidi ya 500,000 ikose mtu mmoja wa kuongoza taasisi kama MSD au TANESCO? Je, viongozi wa taasisi ndogo ambao wanaweza pata promotion ya kupewa nafasi kama hizo hawajiwezi? Kama hawajiwezi kuchukua nafasi kama hizo kwanini wasiwapishe watanzania wengine ili kuwaandaa watu wapya kwa nafasi kama hizo?
2. Katika hao watanzania 500,000 walioajiriwa na serikali, hakuna watu ambao mpaka sasa hawajapata nafasi za uongozi na bado wanaweza fanya vizuri? Kwani ili upewe nafasi ya uongozi lazima uoneshe uzoefu wa kuongoza? Watumishi hawa uzoefu waoneshee wapi? Kwani hakuna traits ambazo zinaweza tumika kuibua kiongozi mzuri?
3. Kama huu mfumo wa kuchukua watu toka nje ya mfumo unafaa na vyombo vyetu vya vetting vinaona ni mzuri kwanini huu huu mfumo tusiutumie na kwenye vyombo kama Majeshi ya Ulinzi na Usalama, TISS na PCCB? Kwani huko kuna kitu gani special wanachofanya hadi nafasi zao zilindwe ndani ya mfumo? Mtu akiwa vizuri apate nafasi na kumwingiza kwenye mfumo husika.
Sina shida na wateuliwa, wanastahili, ila ninahisi kuna shida mahala hasa katika kutafuta watumishi wa serikali wenye sifa na kuwafanyia vetting.
Kwanini hawa jamaa wa vetting wasiwe wanaadhibiwa kwa kutofanya vetting nzuri? Yaani katika watumishi laki tano ukose mtu wa kuongoza MSD au TANESCO?
HII NI AJABU.
Kufanya 'recycling' ya waajiriwa hao hao ambao kimsingi ni 'deadwoods' hakuwezi kufikisha nchi popote.
Afterall, mifumo ya utendaji kazi ya serikali, haiwapi fursa waajiriwa wake kujifunza, kupata uzoefu na kuwa mahiri ktk maeneo ya ushindani, uendeshaji na uongozi wa biashara wa kisasa. Hii ni kwa sabb ya ukiritimba unaotokana na utitiri wa kanuni, taratibu, urasimu, miongozo, maagizo, makatazo, nk vinavyosababisha waajiriwa kukosa ubunifu!!!
Chukulia mfano wa MD wa TPDC ambaye kimsingi ni zao la private sector.. Ukiangalia background yake kutokana na maelezo yake mwenyewe (hapo chini), siyo rahisi kupata mtu wa viwango vyake kutoka kwenye manispaa, halmashauri, Tamisemi, nk..
Interview: Dr. James Mataragio, Tanzania Petroleum Development Corporation
The TPDC's Managing Director discusses the restructuring of the Tanzanian O&G market, long-term plans, and exploring Tanzania's enormous potential.