Je, Tundu Lissu ashitukia biashara za Freeman Mbowe? Ahoji biashara gani haina TIN Number?

Je, Tundu Lissu ashitukia biashara za Freeman Mbowe? Ahoji biashara gani haina TIN Number?

Lissu ni muwazi sana sana.
Hapa amepuyanga kuhusu habar za biashara. Lissu kwa sasa anatapa tapa, atapoteza kuaminika na watu makini.

Nasisitiza auchunge mdomo wake. Naona hajawaelewa watanzania, ataonekana ana nongwa tu.

Yeye amekuwa anatuhumu kila kitu, si apeleke ushahidi TRA, Financial crime, pccb ili mbowe akamatwe yeye apite kirahisi tu.

Binafsi naanza kupata mashaka sana na Lissu hasa kwa namna anayoropoka ropoka. Mbona wagombea wengine hatuwasikii isipokuwa yeye tu na mambo ambayo yanasemwa kama sio mwanasheria.

Ni heri hata Msukuma ama yule jamaa wa mtera 😂
 
Kumbe Mbowe Hotels hazina TIN number? Yale mashamba aliyoharibu Byakanwa na zile biashara lissu alizowahi kiri Magufuli alimharibia Mbowe kumbe ilikua uongo?
Kwani Lisu kataja wapi jina la Mbowe?
Mbona mnaweweseka sana?
 
Wakuu, Tundu Lissu alipofika Uwanja wa ndege, amehoji chanzo cha fedha kwa baadhi ya watu.
View attachment 3194290
Tundu Lissu amesema, "Ni muhimu tukajua, katika Mazingira ya Tanzania halisi hii, haya Mamilioni haya yanatokea wapi na ni salama kiasi gani? Kama mtu ana biashara Nchini au Nje ya Nchi, kuna biashara ambayo huwa haijulikani? Kuna Biashara isiyokuwa na TIN number, isiyokuwa na Leseni, isiyokuwa na jina isiyokuwa na Ofisi Mahali, isiyokuwa na Bank account? Ipo? Niambieni." Mwisho wa kumnukuu.

Je, haya maneno yanalenga Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman Mbowe?

Sababu ndo huwa anasema ana biashara zake.

Kuna Kipindi Paul Makonda alishindwa kujua Mbowe anafanyabiasha gani hadi akahisi anafanya biashara za madawa ya kulevya.

Pia, soma:

Vita dhidi ya Dawa za Kulevya awamu ya Pili: RC Makonda awataja Mbowe, Manji, Gwajima, Idd Azzan...

Dawa za Kulevya: Freeman Mbowe akamatwa na Polisi; ahojiwa na kuachiwa
Mbowe angesoma alama za nyakati.
Angestaafu kama mwami.
 
Lissu akikuchukia anakupakazia na kukuzushia kitu chochote.

Akishindwa uchaguzi wa Jan 21 game yake inaishia hapo.

Atakuwa na wakati mgumu sana kwenye siasa za upinzani, mara elf aende CCM kuliko ku deal na wapinzani wawili wawili.

Shida yakr ni njaa, hana chochote na hawez biashara yeyote
Mbowe mjasiliamali wa siasa tu. Anaitumia cdm kujinufaisha na kujilipa ruzuku ndio maana hataki kuachia.
Awamu hii atatoka tu, chama sio mali yake binafsi
 
Wenje na mbowe onyesheni haraka TIN nambazenu lasivyo kimbilieni ugaibuni huko
 
Mbowe mjasiliamali wa siasa tu. Anaitumia cdm kujinufaisha na kujilipa ruzuku ndio maana hataki kuachia.
Awamu hii atatoka tu, chama sio mali yake binafsi
Maria Sarungi kawapa kazi ngumu sana
 
Kwa hili Lissu ni mshamba sana,

Zipo Bislashara kibao wamiliki ni ghosts for a reason.

Mazingira yeyote ya kuweka biashara zako wazi ukiwa kwenye siasa ni kitafuta kujimaliza.

Wapo wengi sana duniani hawaonekani kwenye list yeyote ya legal business lakini ni matycoon.

Yeye hajawahi fanya biashara and he knows nothing about it.....

Atulie aombe michango achangiwe aache bla bla za kishamba.

Hashangai ni yeye tu anazungusha bakuli kuomba mia mia wenzake daily Dubai, Nairobi, Dar, US etc..

Wewe unaish kwa free meal ya special political asylum card bwana wacha kujilinganisha na kila mtu.
Ila mkuu we Mshamba na Mjuaji sana!
 
Mbowe safari hii kayakanyaga. Alijua lissu ni sawa na zitto kabwe
Mkuu LISu huyu warthog wa mjini Mr kasongo, Marais watatu walishamfanyi fitina wote walichemka
1)mkapa , juu ya migodi nyamongo huko ,ikabidi amfungulie KESI ya uhaini ,kotini serikali ikadondokea pua

2)kikwete , huyu alienda hadi kwao akawambia wananchi msimchague LISu kuwa mbunge ,akashindwa

3) magufuli akaona isiwe SHIDA ,akampigisha risasi nyingi mwamba kachomoa Yuko hai

Samia ,silaha yake ilikuwa mbowe ,ngoja tuone sasa
 
Ila mkuu we Mshamba na Mjuaji sana!
Ndio I know things..

Niulize maswali.

Nasema nipo hapa kuweka rekodi na kuzuia vishoka wa kuchangisha mpaka chakula cha mchana kwa jina la harakati.

Tafuteni kaz zinazowaingizia vipato mumchangie huyo bwana Mil 30 ya uchaguzi mkuu.

La Ushamba ni kweli mimi mshamba maana nimezaliwa Shamba and i have gone places and i know people
 
Back
Top Bottom