bategereza
JF-Expert Member
- Dec 26, 2013
- 3,314
- 1,071
Nimemkumbuka kalikuwa kanaitwa afande Msagati... Sikonge!!
Katika sehemu umenikumbusha ni Lwamkoma dah nakumbuka kipindi cha palizi nilipewa mstari mmoja na nusu! Dah nikapalilia ila nilikoma stasahau chakula kile maana hata nguruwe mpenda kula hakiwezi chakula ugali mbaya na dagaa zinamawe, nyasi wameloweka na kuchemsha wakatuletea shamba dah hapana op Kizota!! My force no W73.....Wazalendo;
Moja ya shemu ya maisha yangu ambayo kamwe sitasahu ni kupitia JKT.
Nilijiunga na JKT Ruvu na baadaye nikaenda Service Buhemba Lwamkoma.
Sitosahau kamwe mafunzo ya ukakamavu, kwata, mchaka mchaka, disko na vitimbi mbalimbali kati ya Makuruta na Maafande. Nilikuwa Combania E.
Moja ya vituko vya kukumbuka ni simulizi kutoka- Operation OKOA, kulikuwa na huyu jamaa alikuwa ni mweusi sana anaitwa afande Lucas, badala ya kuwaaamsha kuruta kwa filimbi, alikuwa anaingia na kuvuta Sigara. Kuruta inatakiwa ukisikia harufu ya Sigara uamke na kufoleni nje. Usipotoka in time unakula mijeledi.
Basi siku moja Kuruta wakapanga wamfanyizie na wakatoka mapema nje na kujificha huku ndani kwenye Bweni wakiyaviringisha mablanketi mithili ya mtu amelala. Afande alipomaliza sigara hakuna aliyetoka akajua siku hiyo kuruta wamegoma kuamka na kuanza kuchapa viboko yale mablanketi yaliyovingirishwa. Alishtukia kaanza kushambuliwa yeye na kuruta toka nje ambao walikuwa na fimbo kibao mpaka akakoma. Kisha kuruta wakafoleni nje. Nakumbuka Mkuu wa Kombania alipata habari na kulikuwa na drill si kawaida na mpaka push ups za kunusa mkojo katika nyasi walizokuwa wanakojoa kuruta usiku. Hata hivyo yule afande naye alikoma kwani hakurudia mchezo wa kuwaamsha watu kwa sigara.
Kwa waliokuwa Ruvu Operation Okoa:
Na miss - Ugali na korosho mnapojongo kambini
Namiss Mihogo ya Vibwende kwa Babu
Wali na Maembe
Uji wa Mestin ya Jeshi
Bukta na Green Vest
Kuokota kuni
Bustani
Michezo
Disco . . . Ama Johnnnnn ambaaaa ambaaa John, amba Johnnn wa Tanzania . .
. . . . Arusha Mbali, Arusha Mbali, tukumbukane kwa Barua nk.
Nakumbuka pia siku moja sikuimbisha disco vizuri na kipindi kile 1985 bado kulikuwa kuna ubaguzi wa rangi Africa Kusini, basi afande akanipiga mkwala na kuniambia . . . .
"Kuruta nitakutemea mate yenye sumu usoni upofuke macho, na sijui utatibiwa wapi kwani mipaka yote Afrika Kusini imefungwa . . . (Kana kwamba hakukuwa na hospitali ya kutibu mate ya sumu hapa bongo"
Jamani mliokosa JKT, mlikosa mengi, japo tulipata tabu lakini tulijifunza mengi katika maisha.
Je, wewe unakumbuka nini?
Katika sehemu umenikumbusha ni Lwamkoma dah nakumbuka kipindi cha palizi nilipewa mstari mmoja na nusu! Dah nikapalilia ila nilikoma stasahau chakula kile maana hata nguruwe mpenda kula hakiwezi chakula ugali mbaya na dagaa zinamawe, nyasi wameloweka na kuchemsha wakatuletea shamba dah hapana op Kizota!! My force no W73.....
Ingawa binafsi sijapitia JKT lakini katika story zote za JKT nilizozisikia sijawahi kusikia waungwana wakizungumzia maluteni kanali.
Ambacho sitasahau ni siku moja afande alijisaidia kwenye mlango wa hanga akatusingizia. Tukapewa adhabu ya kuchukua kila mtu kidogo kidogo. Akajitolea mmjo kuzoa lakini wakakataa. Kila mtu alishika mpaka ikaisha.
kunyanyua mikono juu wanapima nn kwenye kifua?
mkakati wa watarajiwa wa jwtz kupitishwa jkt ni ugoro wa watawala kutafuta kuingiza watu wao ndani ya jwtz. Jkt ni jeshi la kujenga taifa, liliwekwa kwa ajili ya wasio na ajira wakajiunge na kujifunza kujiajiri pamoja na kuwa wanajesi wa akiba wanaoweza kuitwa wakati wa dharura kutoa huduma za mwelekeo wa kijeshi. Waliokuwa wakilazimishwa kujiunga ni school leavers (x-formvi na x-university) kabla hawajaiingia katika ajira. Madhumuni ilikuwa kujenga nidhamu yao, na kweli walikuwa na nidhamu hata kazi zao zilionekana hivyo. Mafisadi walikuwepo wachache sana.
Hawa wajanja wanaopeleka watoto wao jkt miezi 4 halafu wanawafanya ndio wenye sifa ya kujiunga na jwtz ni waharibifu na matokeo yake mtayaona karibuni. Kuna "shamsi vuai nahodha" mwingine atajiuzulu tu kwa ugoro wa wanajeshi hao.
Halafu mnasema mnashangaa mawaziri sasa wanashindwa kuongoza wizara zao huku mkipeleka nyenzo zenyewe za kuwafanya washindwe kufanya kazi. Mama sitta alipeleka walimu bambuccha sasa masahibu yanamkuta kawambwa. Na kwa nini kawambwa na si majaliwa hapo pia unabaki kinywa wazi. Heri yake jakaya maana yeye wakijiuzulu anateua wengine, yeye aaaaaaaah!!!!!! Walioshindwa ni wao siyo yeye, yeye yuka amerika.
mmeshindikana uraiani ndio mmekuja hapa kushindanana ! ................. hapa hafukuzwi mtu !
Hii ilikuwa mitaa ya afande Mlimba,Maduma, Masabo,Tyetyetye,Bahati,Bandeke.Mirudy,Chilumba aka Chiluba n.k..Kule kwenye shamba la dunia tumekula sana bisi kabla hujaja usawa wa gudulia.Week end mnachomokea Mirongo Inne kula konyagi mwitu na kuku wa kienyeji.Raha ajabu.
Matangazo ya kujiunga yanatoka lini?nilifuatilia kweli mwaka jana wakati nimemaliza chuo lakini sikufanikiwa napigiwa tu simu na wenzangu kuwa wameshapata kwa njia ya wakubwa,je kwa wale wa kufuata haki unapataje hiyo nafasi ya kujiunga JKT(taarifa nitapata wapi)?na pili ukiwa na target ya kwenda jwtz au intelligence inakuaje?Swala la JKT limekua compulsory kwa wale wote tunaosubiri nafasi za professionals za jeshi kwani ni lazima kwanza tu serve jkt for four months then ndio miezi sita ya officer cadet. Mimi naomba kwa wale ambao mmepitia huko (hususan walioapa juzi juzi) mtu habarishe nini cha ku expect huko, na since day 1 mlivowasili kambini ilikuaje etc. Hii itasaidia wengi kujiandaa psychologically and physically kwaajili ya mafunzo. Kwani huku mtaani speculations ni nyingi sana, wengine wanasema wiki sita za kwanza hamna kuvua mabuti wala kulala na rumours nyingine kama hizo hivyo kwa ambaye hatojali basi tungefurahi kama ata share na sisi hapa.
Regards,
Don Lucchese cc xir jyerphy
matangazo ya kujiunga yanatoka lini?nilifuatilia kweli mwaka jana wakati nimemaliza chuo lakini sikufanikiwa napigiwa tu simu na wenzangu kuwa wameshapata kwa njia ya wakubwa,je kwa wale wa kufuata haki unapataje hiyo nafasi ya kujiunga jkt(taarifa nitapata wapi)?na pili ukiwa na target ya kwenda jwtz au intelligence inakuaje?
1984 Mlale JKT sitasahau afande 'Nguvu ya Nyani, wa Chale Coy! Hii ni operation NGUVU KAZI wakuu!!! Meja Mandwa alivyotutesa silaha ilipoibiwa! Afande Ngunduguru watu walivyokuwa wakimdhihaki kwa kumwita Mku....nduguru!!!! Namisi Chipole kwa masista na mihogo ya Embakasi na kule kijijini kwenye Ulanzi na kitimotoz! Namisi Disco la kuimba huku mmekaa na kupiga makofi, namisi Mustini wangu kiunoni, na misi Kujongo kwenda magagula! Bustani ya tomato, Cabbage nk! Kweli duniani maisha ni historia!!!