Je, unakumbuka nini enzi zako za JKT? Ni mambo gani yalikufurahisha au kukukwaza?

Je, unakumbuka nini enzi zako za JKT? Ni mambo gani yalikufurahisha au kukukwaza?

Baada ya kuuona uzi huu, ghafla nimemkumbuka Yesu!

Sio Yesu wa Nazareth, hapana. Ni kijana mmoja tu wa kichaga aliefanya muujiza akazawadiwa hilo jina!

832 KJ Danger Coy, OP miaka 50 ya jkt.

Tuliharibu kazi tukaanza kupewa doso mpaka mida ya saa nane usiku.

Ndipo huyu mshkaji wetu wa kichaga akaamua kutoka nduki kuelekea kusikojulikana.

Makamanda walikuepo arround wakamuunganishia, na wakamkamata.

Kilichofuatia ni kwamba wengine wote tuliruhusiwa kwenda kulala, jamaa ndo akala kazi mpaka asubuhi. Ikabidi apewe jina la Yesu kwa kujitoa mhanga kuokoa kombania nzima!

Pale Muhuga mess, afande aliweka simu juu ya TV then akakaa kuangalia mpira mbele kabisa ya TV. Kuruti waliiba simu na hakumuona mwizi. Afande alibaki anacheka!

Nakumbuka tulivyokua tunatoroka saa kumi za usiku kuja dar, na kurudi kambini usiku muda wa kuhesabiwa tumetimia.

Yes, nakumbuka totoz za kiskazini zilivyokua za moto.

Namkumbuka msabato aliegoma kufanya kazi siku ya sabato. Adhabu zote zilifeli kwa huyu jamaa, hadi getini kofia nyekundu walimshindwa. Good thing ni kwamba siku nyingine alikua anapiga kazi kweli kweli, shambani anabeba ndoo mbili kwa mpigo.

Nakumbuka mshkaji wangu alivyoibiwa simu akiwa anaichaji na ameishikilia. Alisinzia, kushtuka akajikuta ameshikilia chaja pekee!

Naikumbuka route match kilomita 30 kuitafuta Bagamoyo, achilia mbali mbio za kilomita 16 kila siku kwenda shamba na kutafuta kuponi.

Namkumbuka mshkaji kibonge aliekuja na mwili kama wa Le mutuzi akarudi na mwili kama wa joti.

Na mkumbuka kamanda Bafeni, baba hansi na service man maneno!

Mwisho nakumbuka nilivyopiga kwata kikakamavu mbele ya mkuu wa majeshi wa kipindi hicho General Mwamunyange.

Jeshi ni noma wakuu!
Hahaaa hayo matukio nimebaki nacheka tu, jeshi bana mchana kumetulia kazikazi tu za hapa na pale ila ikifika jioni duuh hilo doso lake + maovyoovyo hatari mpk midnight huhuuu
 
Magera namkumbuka mkuu.Kama sikosei OP yetu alikuwa Danger au Eagle Coy ..

Kuna koplo alikuwa anaitwa MAYAI.Huyu jamaa ukikutana nae tu ujue umeisha(hata kama huna kosa).

Kuna kamanda mwingine anaitwa KABEYA na BABU WA LOLIONDO..
Sir Major Mayai alikuwa Danger Coy kwa intake yetu, nikiwa chini ya usimamizi wake.

Kwa kifupi vipi unakumbuka yule mwanadada aliyekwenda kutangaza uwanja wa damu kuwa ametongozwa na afande halafu akamkataa?
 
Sir Major Mayai alikuwa Danger Coy kwa intake yetu, nikiwa chini ya usimamizi wake.

Kwa kifupi vipi unakumbuka yule mwanadada aliyekwenda kutangaza uwanja wa damu kuwa ametongozwa na afande halafu akamkataa?
Namkumbuka mkuu.Ni yule bonge sana akawa anasimulia mbele ya CO Kanole na watu wote tulikuwa kimya.Afande akampigia magoti yule dada na jamaa akaenda jera.Kwa kifupi yule jamaa alikosea ila pia jamaa alikuwa bonge la afande yani full amani tu.Ilikuwa ukikutana nae atakuita "Kurutu njoo haya shika pua,shika mdomo,shika kiuno" hahaha yani wkati anasema shika kiuno kabla mkono haujafika kiunoni anasema sheka pua...

Alikuwa akija kombania ataulia cheichei yuko wa kombania yuko wapi..

Je unamkumbuka yule dogo wa kike alitoroka jeshi halafu akarudishwa na baba yake? Unakumbuka tulikunja ngumi wakati anasimulia? Ilikuwa noma siku ile maana anahadirhia kama mtoto yani hatua moja moja kutoka kambini mpaka kwao.
 
Namkumbuka mkuu.Ni yule bonge sana akawa anasimulia mbele ya CO Kanole na watu wote tulikuwa kimya.Afande akampigia magoti yule dada na jamaa akaenda jera.Kwa kifupi yule jamaa alikosea ila pia jamaa alikuwa bonge la afande yani full amani tu.Ilikuwa ukikutana nae atakuita "Kurutu njoo haya shika pua,shika mdomo,shika kiuno" hahaha yani wkati anasema shika kiuno kabla mkono haujafika kiunoni anasema sheka pua...

Alikuwa akija kombania ataulia cheichei yuko wa kombania yuko wapi..

Je unamkumbuka yule dogo wa kike alitoroka jeshi halafu akarudishwa na baba yake? Unakumbuka tulikunja ngumi wakati anasimulia? Ilikuwa noma siku ile maana anahadirhia kama mtoto yani hatua moja moja kutoka kambini mpaka kwao.
Hahaaa mjinga sana yule alituumiza kweli kweli anasimulia polepole wakati watu tunaumia.

Kama ulikuwa danger coy unanifahamu Katika list ya madoja tatu bora nilikuwa sikosi!
 
Hahaaa mjinga sana yule alituumiza kweli kweli anasimulia polepole wakati watu tunaumia.

Kama ulikuwa danger coy unanifahamu Katika list ya madoja tatu bora nilikuwa sikosi!
Mimi nilikuwa BRAVO mkuu.Ila yule jamaa yenu sijui mnamwita CHACHA akiwahi nidaka na simu .

Ilikuwa ni shida mkuu.

Ile nyie Danger mlikuwa mnakula sana kazi.

Me nilikuwa Doja pale nyuma ya kombania yenu kwenye kuchoma takataka kila asubuhi sana .Kama kijiwe kile uliwahi kuja basi utanikumbuka maana ndio nilikuwa main talker .

MP Chaula jamaa alikuwa mwepesi kama mchina .
 
Mimi nilikuwa BRAVO mkuu.Ila yule jamaa yenu sijui mnamwita CHACHA akiwahi nidaka na simu .

Ilikuwa ni shida mkuu.

Ile nyie Danger mlikuwa mnakula sana kazi.

Me nilikuwa Doja pale nyuma ya kombania yenu kwenye kuchoma takataka kila asubuhi sana .Kama kijiwe kile uliwahi kuja basi utanikumbuka maana ndio nilikuwa main talker .

MP Chaula jamaa alikuwa mwepesi kama mchina .
Hahaa kijiwe cha taka nimekikumbuka tumelala sana pale mkuu [emoji1].

Yule chacha hafai kabisa kuna kipindi alinipiga stick za mgongo acha kabisa yule jamaa mpaka kesho simpendi kabisa.
 
Rwamkoma jkt OP kikwete nilikua c coy chini ya Marwa! nawakumbuka sana marafiki zangu tuliokutana Rwamkoma kama kuna mtu kapita pale basi tukumbushane
Mzee bangu ukila mihogo Shamba dunia .anazingua kinomaa...
Bila kusahau kina jeneza...kenge... Walinishikilia kutoka resort nkaokolewa na sir mang'ombe
 
Mambo ya jeshini jamani hapana ,nakumbuka nilivyokua naambiwa kwenye mazoezi ya kwata 'Nanga huyu wa Demo kwa mwendo wa haraka mbele tembea basi nikianza kutembea watu wote hoi kwa kicheko sijui kwanini hahaaaa'
Kibangala hiki cha mananga mguuuuuu pandeee
 
Vijana Wa Matanga Mbushi na Ghadafi tunapaki magari yetu wapi humu.... Charlie Coy ya Demo CCP. Platoon 11. Nyambizi moja....
 
Mambo ya jeshini jamani hapana ,nakumbuka nilivyokua naambiwa kwenye mazoezi ya kwata 'Nanga huyu wa Demo kwa mwendo wa haraka mbele tembea basi nikianza kutembea watu wote hoi kwa kicheko sijui kwanini hahaaaa'
Wee inaonyesha ulikuwa unaanza kutanguliza mguu wa kulia ndo maana u nanga ulikuwa hauishi
 
OP ni moja tu,inayoitwa OP MKAPA ilikuwa ruvu na makutopora dodoma hiyo mingine ni mifano tu2001/02
 
Back
Top Bottom