Je, utamkumbuka Hayati Ali Hassan Mwinyi kwa mambo gani?

Je, utamkumbuka Hayati Ali Hassan Mwinyi kwa mambo gani?

Mimi nitakumbuka kupanda Magari ya Ikulu maana Moja ya watu wake wa karibu alikuwa class mate wangu. Kila weekend tunaletewa lunch boxes na kufuliwa nguo zetu huko Ikulu.

Udumu rafiki yangu kipenzi wa enzi
 
Ukweli uswemwe bila Kujali

OBC Ni kampuni kutoka uarabuni inayo fanya shughuli za uwindaji Loliondo kwa muda mrefu kwa mkataba mrefu

Ni Kweli Kuna mazuri ya mwinyi ila Hili la kuletea OBC, Otello business cooperation ya uarabuni na kuwapa kitalu cha uwindaji cha miaka 99 Ni hasara kubwa Sana Leo tunapata kwa uwepo wa likampunj Hilo linalo iba wanyam wetu

Sent from my German technology
 
Pale Mzee aliteleza,Ila mpiga Kofi naye akili Hana,ule ushauri ni sawa na polisi kushauri wezi njia nzuri na salama ya kuiba,Nina Imani mzee alifanya toba
Mzee hakuteleza alituambia sisi Wananchi tutumie kinga ili kuepuka ugonjwa wa UKIMWI hata Makka na Saudia Arebia sasa wanatumia Condom.
 
20240301_002905.jpg
 
1- nchi ilikuwa Haina hela ila raia ndio Wana hela. Kipindi hiko watumishi wengi waliacha kazi kwa kukosa mishara. Serikali haikuwa na hela. Alisusa na kutaka kujiuzulu uraisi. Nchi iliingia katika madeni mengi hadi ikawa haikopesheki. Mihadhara ilitamalaki sana. Either way kila nafsi itaonja umauti.
 
Eeeeh jaman kumbe sio mama tena………..mbona mlisema mama ndio amewaleta yani bongo ukifa tabu ukiwa hai tabu ukipanda ndege shida ukishuka shida
 
1. Kupenda Dini na Kusali sana.

2. Kupenda Utani na Ucheshi.

3. Kukitukuza Kiswahili na Kujivunia Kukiongea Kiufasaha.

4. Kuridhika na Maisha aliyonayo huku akipenda sana Kula Vyakula vya Kiasili na vya kuutunza Mwili kwa muda mrefu.

5. Kupenda mno Mazoezi hasa ya Kutembea kwa Miguu kwa Umbali mrefu.

6. Huruma,, Kusamehe na kutokiwa na Kinyongo na Mtu hasa hasa Adui.

7. Kutopenda Kujitukuza kama Kiongozi na kupenda Ushirikiano na Watu na kuwa mwepesi Kushaurika na Kujifunza.

Pumzika Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Alhaji Ali Hassan Mwinyi hakika Mwendo Umeumaliza na huna baya hata kama lipo Watanzania tulishakusamehe Kitambo na Uhai wako huu mrefu ulikuwa ni Zawadi na Faraja kwetu.

Ulale mahala pema. Peponi AHM.
👆👍👌👏🤝🙏
 
Namba 7 ni sifa yake kubwa

ni Mwinyi pekee ndie hakujaribu kupandisha mabega akiwa Amiri jeshi , marais wote watano wengine kuna nyakati walikuwa wanajisahau na kujiona kama vile hawajaumbwa kwa udongo
Hata kikwete nae alipandisha mabega?
 
Back
Top Bottom