OLESAIDIMU
JF-Expert Member
- Dec 2, 2011
- 19,139
- 9,562
Upo mwingine wa kero za madereva jijini sijaona mchango wako na amekuita.
Mkuu waweza kuwa na engine nzuri na gari iko njema ila pulley bearing ya compressor yaweza kuwa imechoka
Hapana, haijachoka kihivyo; ndio ina mwaka wa pili barabarani; bado iko njema sana.
Mkuu nitafuatilia, ni kibarua cha kesho hicho majaaliwa.
OLESAIDIMU ni wale ambao amewakosoa na maelezo yake.im good kaka...humu jf tunawezana wenyewe.....
Kwa muda mrefu watu wengi wamekuwa wakiamini ukitumia AC unatumia mafuta mengi kuliko ukiendesha bila AC[vioo wazi].
Kiufundi ili AC ifanye kazi inahitaji nguvu ya ziada kutoka kwenye engine ili compressor izunguke,sitaingia kiundani kwasababu mimi sio mtaalam wa AC. Na kwa kuzingatia hili watu wengi wanaamini ukitumia AC unatumia mafuta mengi kuliko ukiendesha bila AC.
Hili si kweli. Ukitumia AC gari inatumia nguvu zaidi LAKINI ukiacha vioo wazi gari inatumia nguvu zaidi ya ukifunga vioo na kuwasha AC. Vioo vikiwa wazi gari inatengeneza kitu kinaitwa 'DRAG' yaani upepo unajaa ndani ya gari na kuifanya iwe nzito kwahio inatumia nguvu nyingi kutembea kuliko ukifunga vioo na kutumia AC.
Kwenye speed ya 80kph ukifungua vioo unatumia mafuta 20% zaidi ya ukifunga vioo na kuwasha AC. Kwa maelezo haya nahitimisha kuwa UKITUMIA AC GARI INATUMIA MAFUTA KIDOGO KULIKO USIPITUMIA AC NA KUACHA VIOO WAZI.
Hiki nilichoandika hapa ni scientifically proved ya SOCIETY OF AUTOMOBILE ENGINEERS[SAE],sikuweka link ili nichangamshe mada,jisomeeni hapo chini. page 1,2 even 3 mkiweza
http://auto.howstuffworks.com/fuel-efficiency/hybrid-technology/driving-with-windows-down1.htm
CC: OLESAIDIMU MANI Kaizer Kalamzuvendi Titans
Hii uliyousema ni sahihi ukiwa safarini. Lakini AC inaongeza ulaji wa mafuta gari ikiwa sailensa( kiswahili). Fanya majaribio gari hizi mbili: Noah na RAV4( chukua Old model na Medium Model/ Kill time) . Jumamosi saa6 mchana wiki ya kwanza washa RAV4 model yoyote ukiwasha AC ukitokea mfano Magomeni na Mafuta ya elfu20, lengo uende Kigamboni. Ukifika ferry kule foleni utakuta inaanzia fence ya Ikulu. Hadi unavuka na gari kwenye Pantoni angalia mafuta yako. Rudia zoez hilo bila kuwasha AC kwa RAV4 na pia Rudia kwa NOAH utaratibu uleule halafu uje utupe majibu. Kwa magari madogo yenye cc less than 1998(say 2000) unaweza usione ulaji wa mafuta. Ila kwa NOAH, RAV4 AC kwenye foleni usipime, ila ukiwa safarini ni poa tu, adui nkubwa ni foleni yaani gari kuunguruma, mafuta yanaenda sana tena sana!
Hizi mada zina wenyewe bwana...mimi naperuzi tu wala sihitaji kudadisi maana hata gutta sina
OLESAIDIMU, MANI, RRONDO: Thanks very much, uzi haukunilenga lakini nimepata mwanga wa tatizo langu; nitafuatilia na nadhani kitasomeka.
Hii uliyousema ni sahihi ukiwa safarini. Lakini AC inaongeza ulaji wa mafuta gari ikiwa sailensa( kiswahili). Fanya majaribio gari hizi mbili: Noah na RAV4( chukua Old model na Medium Model/ Kill time) . Jumamosi saa6 mchana wiki ya kwanza washa RAV4 model yoyote ukiwasha AC ukitokea mfano Magomeni na Mafuta ya elfu20, lengo uende Kigamboni. Ukifika ferry kule foleni utakuta inaanzia fence ya Ikulu. Hadi unavuka na gari kwenye Pantoni angalia mafuta yako. Rudia zoez hilo bila kuwasha AC kwa RAV4 na pia Rudia kwa NOAH utaratibu uleule halafu uje utupe majibu. Kwa magari madogo yenye cc less than 1998(say 2000) unaweza usione ulaji wa mafuta. Ila kwa NOAH, RAV4 AC kwenye foleni usipime, ila ukiwa safarini ni poa tu, adui nkubwa ni foleni yaani gari kuunguruma, mafuta yanaenda sana tena sana!
Mimi hua sishushi vioo hata kidogo....inakera pale unapompa mtu lift halafu ile kupanda tu anaanza na kupunguza au kuongeza sauti ya redio,akimaliza hapo anabonyeza button ya vioo sasa kwa vile ume-lock button utasikia "bro shusha vioo basi tupate fresh air".
Sent from my iPhone using JamiiForums
Mi nimeona nikiwashs AC wakati wa kupanda milima gari hupungua nguvu, nikizima inakuwa na nguvu kawaida. Sijui hii ni kwa gari yangu tu au wengine nanyi mmeliona hilo? Naomba uzoefu wenu tafadhali.
Kaka vitu vingi tu huna na unavijua na unavitumia!!!!!
Unahitaji mifano???!!!!
Una mke au mpenzi???!!!
Mkuu asante kwa taarifa yako japo na mimi nilishaisoma miaka 4 iliopita kwenye link hiyo hiyo uliotupa. Humu kuna watu wabishi wanaamini walichozoea na stori za mitaani kua AC inakula sana mafuta.
Japo wameshauri kwenye hiyo makala kua kama unaendesha kwenye jam kubwa gari inapokwenda kwa mwendo mdogo sana ni bora ukashusha vioo na kuzima AC kama unataka kusevu mafuta .