Je, wabunge 19 wa CHADEMA walijiteua? Je, CC ya CHADEMA ni Kangaroo Court? Je, Baraza Kuu litabariki ukangaroo ule?

Je, wabunge 19 wa CHADEMA walijiteua? Je, CC ya CHADEMA ni Kangaroo Court? Je, Baraza Kuu litabariki ukangaroo ule?

Hivi ni nani mwenye nguvu ya kumtoa mtu aliendani gerezani usiku usiku na kesho yake akaapishwa kua ni mbunge?!! Tena wakaapishiwa garage, sio ndani ya ukumbi wa bunge!!

Yaani CHADEMA ipeleke jina la mtu ambae yuko gerezani zaidi ya miezi miwili na imtoe usiku?!!

Ifike sehemu tuache unafiki na uhuni!!
Kwamba list ya Viti maalum alikua nayo magufuli? Duuuh
 
Mkuu kwa hili nakubaliana na wewe, yaani mtu hatakiwi kuangalia alipojikwaa bali alipoangukia!, yaani tusijali tena chanzo, tujikite tuu kwenye matokeo!. Naamini hakuna mtu yeyote mwenye akili timamu, atakaye thubutu kuishutumu Chadema kwa hatua zitaka chukua katika utekelezaji wa sheria taratibu na kanuni, ila sasa hapa ndipo katiba ya Chadema itakapo kuja kwenye the limelight!, was it constitutional right?!.

Pasco
Alipofukuzwa Zitto Kabwe uliandika hivi. Leo hao hao walioamua kwa ZZK una wa question.
 
Halima Mdee bado mdogo sana,ni mwanasiasa mzuri ila ameteleza tuu, in general ana agenda nzuri za kutetea wananchi na kufichua mafisadi kitu ambacho ni muhimu, i hope atarudi na atakuwa amejifunza, na ukizingatia umafia na changamoto ya siasa za awamu iliyopita ni bora kumsamehe tuu, i hope CDM wana utaratibu wa kumrudishia mtu uwanachama baada ya kufukuzwa
 
Halima Mdee bado mdogo sana,ni mwanasiasa mzuri ila ameteleza tuu, in general ana agenda nzuri za kutetea wananchi na kufichua mafisadi kitu ambacho ni muhimu, i hope atarudi na atakuwa amejifunza, na ukizingatia umafia na changamoto ya siasa za awamu iliyopita ni bora kumsamehe tuu, i hope CDM wana utaratibu wa kumrudishia mtu uwanachama baada ya kufukuzwa
Akiomba kurudishiwa lakini
 
Yaani huwa najiuliza kuwa huyu Pascal alisoma kweli Ilboru sekondari au alikuwa msoma magazeti? Hata Mimi niliyesoma shule ya kayumba najua mbivu na mbichi Sasa huyu mchumia tumbo anakuwaje jinga kiasi hiki.

Pascal ni janga la kitaifa yaani tukiwa na wachumia tumbo Kama hawa hta wakiwa wawili ni hatari kwa usalama wetu.

Pascal anatafuta uteuzi kwa damu za watu na ni mzandiki shetani kuliko hata Ibilisi.
Mayala maana yake njaaa
 
Mkuu Pascal Mayalla

Umekuwa unazunguka sana kuhusu Wabunge 19 kiasi cha kujiuliza kulikoni!

Unaonyesha kuna Kangaroo court, hujaonyesha vifungu gani vimekiukwa

Unaelezea k 'Karma' kama mwongozo wa chama badala ya katiba unayosema inakiukwa

Miwsho unauliza swali, je, ni kangaroo court?
Halafu una conclude kwa ? kabla ya jibu, ''Baraza kuu litabariki'

Kila mtu ana haki ya maoni, kwangu, kusimama na misingi ya chama iwe CCM, CDM etc ni kitu muhimu sana kuliko personality. Nilikataa wakati wa Maalim RIP na kila chama.

Hawa 19 ni Wasaliti,hawana Karma inayowalinda bali inayowawinda.

Watu wamepoteza damu, ni vilema n.k. wakipigania haki zao, hawa wanawasaliti kwa Ubunge wakishirikiana na Ndugai, Bushir etc.

Ni waovu na Wasaliti tu! Hawasafishiki mkuu Pasco

JokaKuu
Kila mtu ana haki ya maoni, kwangu, kusimama na misingi ya chama iwe CCM, CDM etc ni kitu muhimu sana kuliko personality. Nilikataa wakati wa Maalim RIP na kila chama.
,[emoji1545][emoji1545][emoji1545]
 
Bandiko kuu lina maswali ya msingi na ya kufikirisha kwa Wajumbe wa Baraza Kuu la CHADEMA, kutokana na mwenendo, kauli na matendo ya viongozi wakuu wa chama. Naamini, kama Wajumbe watayazingatia kwa undani maswali hayo, na kuyapatia majibu halisi, hakuna shaka chama kitakuwa imara kuelekea chaguzi za kitaifa zijazo
mwengeso kwa kila changamoto CDM inayopitia inazidi kujiimaarisha na kuwa bora zaidi na kuimarika zaidi
Maoni ya Pasco yatabaki kuwa maonj kwakuwa naamini viongozi wa CDM kwa hakika wanajua wanachofanya kuliko mtu mwingine yeyote nje yake

Kuna wale vijana tunaowaita LUMUMBA BUKU7 ambao siku hizi wamepotea na kupoteana kabisa.. Hawa tulikuwa tunajua udhaifu wa hoja zao hasa linapokuja lolote linaloihusu CDM.. Lakini anapotokea mtu wa kaliba ya pasco kufanya hivyo inanitatiza kidogo
 
Kikao cha Baraza Kuu Chadema, kimelazika, limebariki ule Ukangaroo uliofanywa na CC ya Chadema, uamuzi wa Baraza Kuu Chadema ni uamuzi wa mwisho, final and conclusive. Sijasikia popote juhudi zozote za kumtafuta aliyesaini barua ya uteuzi, sijasikia popote Chadema wakisema kuna forgery au kuripoti popote forgery ile, hivyo hoja za bandiko hili zinasimama, wabunge hao 19 wa Chadema, hawakujiteua wenyewe, waliteuliwa na kiongozi wa Chadema aliyesaini barua yao ya uteuzi!. Hakuna forgery yoyote iliyofanywa kwenye uteuzi wao ndio maana Chadema hawajaripoti forgery popote!.

Tena kiukweli, Halima Mdee ni mwanamke wa shoka kweli kweli nilidhani mbele vya kikao cha Baraza Kuu Chadema angesimama na kuyasema ukweli wa barua yao ya uteuzi, wajumbe wangebaki midomo wazi!.

Kama it's a battle, kina Halima have lost the battle, they have nothing more to loose au ni kukubali kufa kikondoo kwa kuisubiria karma iwalipie, au to keep on fighting hadi risasi ya mwisho na tone la mwisho la damu limwagike kwa kuhamishia mpambano kwenye wiwanja vingine vya Kisheria!.

Halima anamjua aliowasainia barua ya uteuzi, ili kumlinda, waliamua kunyamaza kwa imani kuwa atawaombea msamaha, kumbe... kwenye siasa hakuna rafiki wa kudumu wala adui wa kudumu.

Life goes on
P
Mzee unayumba sana sijui kwanini, hivi hata kwa mtoto mdogo wa chekechea anaweza kuongea vitu vya maana kuliko unachofanya hapa Pasco

Sent from my M2103K19G using JamiiForums mobile app
 
Kuna sababu gani kutambulisha kazi yako katika jambo hili? Lakini kwa maandishi yako unaonekana kama umeshavuta mgao tayari.

Labda niachane na hayo, niseme hivi:

1: Kama shida yako kutaka kujua mbona ndani yake umekuwa na majibu na mitazamo ambayo ungependa ifanyiwe kazi? Hii inadhirihisha kutokana na lugha ya maudhi kuwa baraza kuu ni nyumbu. You really slagged off them in a way that wont be acceptable.

2: Kwa muda mrefu Zitto hakuwahi kuwa mpinzani, sijui kama unanielewa kwa kusema hivi.

3: Tumekuelewa lakini hayakuhusu!
 
mwengeso kwa kila changamoto CDM inayopitia inazidi kujiimaarisha na kuwa bora zaidi na kuimarika zaidi
Maoni ya Pasco yatabaki kuwa maonj kwakuwa naamini viongozi wa CDM kwa hakika wanajua wanachofanya kuliko mtu mwingine yeyote nje yake

Kuna wale vijana tunaowaita LUMUMBA BUKU7 ambao siku hizi wamepotea na kupoteana kabisa.. Hawa tulikuwa tunajua udhaifu wa hoja zao hasa linapokuja lolote linaloihusu CDM.. Lakini anapotokea mtu wa kaliba ya pasco kufanya hivyo inanitatiza kidogo
Mkuu Mshana Jr nilitegemea hoja badala ya "personal attack" ya Paskali.

Hakuna ubishi kuwa hao wanaoitwa COVID-19 walisukumwa na uchu wa madaraka kujiteua. Pamoja na kuvuliwa uanachama na Kamati Kuu ya Chama hawakuona busara kuondokana na Ubunge waliojichagua.

Pia hakuna ubishi Kamati Kuu ya Chama haikufuata Katiba yake (Ibara ya 5.4, Toleo la 2016) kuwavua uanachama. Isitoshe Baraza Kuu halikuitishwa, katika muda mwafaka, kubariki uamuzi wa Kamati Kuu kwa suala nyeti kama hilo wakati CHADEMA ni Chama Kikuu cha upinzani chenye nia ya kushika madaraka.
 
nimeskia kumbe mkewe wa kwanza aalimuacha akaoa mwengine angekuwa mvumilivu angebembeleza maisha yende lkn uvumilivu umemshinda sasa leo anashauri chdm iwasmehe mbona yy hakusamehe mkewe wa kwanza
Mkuu MWALLA , usiamini kila unachosikia!. Sisi Wasukuma tunajuaga kuoa tuu, hatujui kuacha!. Tatizo letu ni huwezi kuwa peke yako, lazima msaidiane na wenzio!. Naomba tuheshimu the right to privacy za watu, tujadili mada iliyo mezani.
P
 
Hivyo hili ni bandiko la swali "Je Wabunge 19 wa Chadema Walijiteau?. Je CC-ya Chadema ni Kangaroo Court?. Je Baraza Kuu Litabariki Ukangaroo Ule?. Likibariki, Karma Itawatafuna!"
Nawatakia wana Chadema, kikao chema cha Baraza Kuu.

Paskali
tena ajabu zaidi ipo kule bungeni, ambapo kiongozi wa muhimili wa kutunga sheria anapoamua kuwakumbatia wanawake 19 wasiowakilisha chama chochote kinyume cha katiba, kwa manufaa ya chama na serikali yake.
Mkuu denooJ, mimi kama mwanahabari ni muelimishaji umma, nimeamua kuanzia mwaka huu, nianze kujitahidi kuwasaidia kuwaelimisha wana jf, na kutumia elimu yangu kuelimisha umma na kutumia uwezo wangu kusaidia taifa langu.

  1. Nakuomba sana nikuelimisha kuwa objective kwenye hili, wabunge wale wamepewa uteuzi na NEC, hivyo Bunge lina kosa gani?.
  2. Kwanini hamjishughulishi kabisa kujua barua ya uteuzi ilitoka wapi?, NEC sio vichaa!, Bunge halina kosa kabisa kwenye hili!.
  3. The right thing ni Chadema ilipaswa ifanye a due diligence, ikijiridhisha kuna jinai ya forgery, that is a police case!.
  4. Hata kama ni kweli wamefoji, then Chadema ilipaswa kufuata katiba yake kuwatimua!.
  5. Nashauri, kwa vile hii kesi iko mahakamani, nashauri tusubiri maamuzi ya mahakama ndipo niendelee kukuelimisha na sio maamuzi ya zile kangaroo courts 2!.
p
 
Mkuu denooJ, mimi kama mwanahabari ni muelimishaji umma, nimeamua kuanzia mwaka huu, nianze kujitahidi kuwasaidia kuwaelimisha wana jf, na kutumia elimu yangu kuelimisha umma na kutumia uwezo wangu kusaidia taifa langu.

  1. Nakuomba sana nikuelimisha kuwa objective kwenye hili, wabunge wale wamepewa uteuzi na NEC, hivyo Bunge lina kosa gani?.
  2. Kwanini hamjishughulishi kabisa kujua barua ya uteuzi ilitoka wapi?, NEC sio vichaa!, Bunge halina kosa kabisa kwenye hili!.
  3. The right thing ni Chadema ilipaswa ifanye a due diligence, ikijiridhisha kuna jinai ya forgery, that is a police case!.
  4. Hata kama ni kweli wamefoji, then Chadema ilipaswa kufuata katiba yake kuwatimua!.
  5. Nashauri, kwa vile hii kesi iko mahakamani, nashauri tusubiri maamuzi ya mahakama ndipo niendelee kukuelimisha na sio maamuzi ya zile kangaroo courts 2!.
p
- Sheria inasema ili mtu awe mbunge, lazima awe anawakilisha chama cha siasa, hao wanawake 19 wamefukuzwa na chama chao, sasa hebu tuambie, wanawakilisha chama gani kule bungeni? kama hukijui hicho chama, basi hilo ndio kosa la bunge.

- Barua ya uteuzi ndio issue ya forgery inapoanzia, tatizo kule mahakamani unapopalalamikia kila siku, kumetawaliwa na watu wasioijua/kuijua sheria, lakini wanaofanya kazi kwa interest zao kama ulivyo wewe.

Sasa kama hiyo kesi ya forgery ikienda mahakamani, unadhani haki itakuwepo toka kwa wale majaji waliopewa ulaji na mwenyekiti wa CCM? [ hapa bahati nzuri nawe unaonesha mashaka kwenye uzi wako mwingine kuwa mahakama zetu hazipo huru]

Zaidi, kulazimisha kujua barua ya uteuzi ilipotoka, ni ujanja wako tu wa siku zote, najua unafanya hivyo pia kwa interest zako ili ku divert attention kwa manufaa yenu, au kama wewe una ushahidi wapi hiyo barua ilipotoka, basi tuwekee hapa tuione...
 
Wanabodi.

Utambulisho.

Mimi ni mwandishi wa habari wa kujitegemea, yaani freelance journalist, hatutumwi na mtu yoyote au media yoyote. Sisi waandishi tuko wa aina nyingi na tunafanya kazi za aina nyingi, wengine ni maripota, wengine watangazaji, wengine wahariri, na ndani ya makundi hayo, kuna baadhi yetu, kazi yetu ni kuuliza tuu, hivyo hiki ndicho ninachokifanya kwenye bandiko hili, nauliza tu: Je, Wabunge 19 wa Chadema Walijiteau? Je CC-ya Chadema ni Kangaroo Court?. Je Baraza Kuu Litabariki Ukangaroo Ule? Likibariki, Karma Itawatafuna!
Paskali
Hatimaye Chadema wamejitambua, keshokutwa Jumatano Siku ya Wanawake Duniani , Chadema itatangaza kuwasamehe mashujaa hawa hivyo sasa karma haitawashukia tena Chadema!, sasa ni baraka kwa kwenda mbele.
Update
Hatimaye Chadema wameacha kushupaza shingo na wamekubali matokeo!, kwa kuufuata ushauri wa bandiko hili CHADEMA kubalini matokeo na m-survive, or shupazeni shingo. You go to hell 6ft under Hao Makamanda 19 ni mashujaa, kuendelea Ubunge wao

Nimepokea taarifa, hii kutokea twitwani
Kisha nikasoma na bandiko hili humu JF Tundu Lissu: CHADEMA tumeanza kupokea Ruzuku

Chadema wameufuata ushauri wa bandiko hili, waneacha ujinga wa kujifanya hawayatambui matokeo ya uchaguzi wa 2020!, sasa wameacha kushupaza shingo, wameyatambua matokeo kimya kimya!, wamewasamehe mashujaa hawa kimya kimya msamaha ambao utatangazwa rasmi siku ya Jumatano tarehe 8 Machi na Mwenyekiti wa Chadema, mbele ya Rais Samia!.

Iliwa kusemwa kuwa hakuna mkate mgumu wowote mbele ya chai!, tayari Chadema imeisha anza kupokea ruzuku hivyo sasa ita survive!. Na ile kesi ya kina Halima Mdee na wale 19 iliyopo mahakamani itafutwa!.

Hongera sana Chadema, for doing the right thing!, mtabarikiwa, viongozi wenu watabarikiwa, chama chenu kitabarikiwa na Tanzania Itabarikiwa!.
Mungu ibariki Chadema
Mungu ibariki CCM kwa kukubali reconciliation
Mungu ibariki Tanzania
Paskali
 
Hatimaye Chadema wamejitambua, keshokutwa Jumatano Siku ya Wanawake Duniani , Chadema itatangaza kuwasamehe mashujaa hawa hivyo sasa karma haitawashukia tena Chadema!, sasa ni baraka kwa kwenda mbele.
Update
Hatimaye Chadema wameacha kushupaza shingo na wamekubali matokeo!, kwa kuufuata ushauri wa bandiko hili CHADEMA kubalini matokeo na m-survive, or shupazeni shingo. You go to hell 6ft under Hao Makamanda 19 ni mashujaa, kuendelea Ubunge wao

Nimepokea taarifa, hii kutokea twitwani
Kisha nikasoma na bandiko hili humu JF Tundu Lissu: CHADEMA tumeanza kupokea Ruzuku

Chadema wameufuata ushauri wa bandiko hili, waneacha ujinga wa kujifanya hawayatambui matokeo ya uchaguzi wa 2020!, sasa wameacha kushupaza shingo, wameyatambua matokeo kimya kimya!, wamewasamehe mashujaa hawa kimya kimya msamaha ambao utatangazwa rasmi siku ya Jumatano tarehe 8 Machi na Mwenyekiti wa Chadema, mbele ya Rais Samia!.

Iliwa kusemwa kuwa hakuna mkate mgumu wowote mbele ya chai!, tayari Chadema imeisha anza kupokea ruzuku hivyo sasa ita survive!. Na ile kesi ya kina Halima Mdee na wale 19 iliyopo mahakamani itafutwa!.

Hongera sana Chadema, for doing the right thing!, mtabarikiwa, viongozi wenu watabarikiwa, chama chenu kitabarikiwa na Tanzania Itabarikiwa!.
Mungu ibariki Chadema
Mungu ibariki CCM kwa kukubali reconciliation
Mungu ibariki Tanzania
Paskali
Nakukubari comrade
 
Back
Top Bottom