Je Wajua Japo Baba ni Kichwa cha Nyumba, Mama Anaweza Kugeuka Kichwa Akawa Baba?. Wajua Rais Samia ni Mwanamke , ni Mama, Kwa TZ ni Kichwa ni Baba?.

Je Wajua Japo Baba ni Kichwa cha Nyumba, Mama Anaweza Kugeuka Kichwa Akawa Baba?. Wajua Rais Samia ni Mwanamke , ni Mama, Kwa TZ ni Kichwa ni Baba?.

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,

Nawasalimu kwa jina la JF.
Angalizo la uchangiaji, hili ni moja ya mabandiko yangu ya kuwaanda Watanzani kisaikolojia kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka huu, nakushauri, ukiusoma uzi huu, ukijiona kama huuelewi elewi, jipitie zako tuu kwa amani, usiparamie kuchangia, ila kwa vile jf ni ukumbi wa wote, simple, mind, ordinary mind na great mind, kwa simple mind, wataliona bandiko hili kama bandiko la kichawa, kwa great mind watajikita na the motive behind!. Hivyo kwa wale mtakao niona nimekuwa chawa, niko ok, nioneni chawa, ila ma GT, tunaelewana!, karibuni.

Kila mtu anayesema chochote, au kuandika chochote, anakuwa na kitu kinachotwa drive, msukumo wa kusema ua kuandika, msukumo huo unaitwa causative agent, inaweza kuwa umeulizwa swali hivyo unasema kwa kujibu, au mtu ameandika kitu ukaguswa ukajibu, au kuchangia, ila katika hicho ulichokisema au ulichoandika, unakuwa na kitu kinachoitwa the motive behind, yaani unayasema hayo au unaandika hayo ili iweje?.

Huu ni mwaka wa uchaguzi, mwaka huu, mimi na PPR yangu tumeamua kujikita katika utoaji elimu kwa umma kuhusu siasa, uchumi na jamii, kuwaelimisha Watanzania, elimu ya demokrasia, katiba, sheria, haki na wajibu, ili wakati wa kufanya maamuzi, Watanzania wafanye informed decisions.

Naomba kukiri, nimehamasika kulizungumzia hili jambo, la mtu ambaye ni mwanamke, ni mama , na anaitwa mama, kumbe, sii mama tuu, ni mamababa!, kwa kuhamasishwa na kauli ya Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu, wakati akiitolea ufafanuzi, kauli yake ya "no reforms, no election", na kusema huo ndio msimamo wa Chadema, na kuufafanua kwa wale wana Chadema wanaotaka kugombea uongozi, kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu, wajiulize "unagombea uongozi, ili iweje?", jibu la hilo swali la ili iweje, ndio the motives behind. Bandiko hili pia lina the motives behind, ila hiyo motives behind, naomba nisiiweke kwenye bandiko hili, tutakuja kukumbushana huko mbele ya safari, muda muafaka ukiwadia!.

JF ilianzishwa mwaka 2006, mwakani tunasherehekea miaka 20 ya JF, kuna sisi baadhi yenu tulijiunga na jf tukiwa vijana, tumeoa tukiwa jf, sasa tunazeeka tukiwa jf, mfano mwana jf yoyote under 20, ajijue tangu anazaliwa watu tuko humu jf, lazima wajifunze kuwa na heshima.

Kufuatia long experience ya uzoefu wa muda mrefu, mara moja moja, nitakuwa napandisha makala elimishi za mambo yoyote ya busara, kwa jina la Busara za Mzee P.
na kwa vile mimi ni story teller, mabandiko haya yatakuwa ni marefu na story story kibao!.

Busara ya leo ni kuhusu majukumu ya kifamilia kwa mujibu wa dini kuu mbili, Ukristo na Uislamu, na mila nyingi za Kiafrika, zinazo fuata mfumo dume, patriarch, zimelelewa kwa malezi ya ubaguzi wa mfumo dume kuwa Baba ndio kichwa cha nyumba na mama ni kiwiliili. Kiwiliwili bila kichwa, ni hakuna kitu, lakini kichwa bila kiwiliwili, kinaweza kuchukua kiwiwili kingine chochote, maisha yakaendelea, ndio maana dini na mila za Kiafrika, zimeruhusu mwanamume kuwa na mke zaidi ya mmoja, lakini kwa mwanamke ni mume mmoja tuu, ukiondoa uongo wa mke mmoja kwa Wakristu, na mila za baadhi ya makabila ya matriarch, ya makabila machache ya Afrika, Asia na Latin America, mke ndie anaoa hivyo kuwa huru kuoa zaidi ya mume mmoja!

Ubaguzi huu huanzia kwenye ngazi ya familia na malezi kuwa mwanamke ni kiumbe dhaifu, dhalili, hivyo mtoto wa kike analelewa kiulaini laini na mtoto wa kiume analelewa kiugumu ugumu. Mtoto wa kike anafunzwa kuegemea na kumtegemea mwanaume, ni mtu wa kubembelezwa kuletewa na kupokea, na mtoto wa kiume anafunzwa kugangamala, ni mtu wa kutafuta, kutoa na kukomaa.

Hali hii huanzia tangu katika ujenzi wa familia, mtoto wa kike, anafundishwa kusubiri kuchaguliwa, kutongozwa, kuhongwa, kupendwa, kuchumbiwa, na kulipiwa mahari, ndipo apende, na ndani ya nyumba, mwanaume ndie kichwa cha nyumba, ndiye mtafutaji, anayepambana kutafuta, mke akiwa golikipa, akisubiri kuletewa.

Hata process ya uumbaji, procreation, kwa binadamu na viumbe wote, ukiondoa nyuki, ni mwanaume hukaa juu, mwanamke chini, ni mwanaume ndie anatoa mbegu, mwanamke anapokea, na kubeba, na kwa hapa Tanzania Bara, ni kosa la mwanaume kumpa mwanafunzi ujauzito, lakini kwa Zanzibar kosa ni la mwanamke kupokea ujauzito, kwasababu ni mwanamke ndie anayeruhusu!.

Na hata kukitokea msiba wa familia, akifa mama, japo baba huitwa mgane, lakini hakuna ajabu kwa baba kuoa tena, ndio maana ni aghlabu sana kusikia matatizo ya wagane, akifa mama, familia haitetereki, kwasababu baba ni the breadwinner, lakini akifa baba, mke huitwa mjane na familia nyingi hutetereka, kidini na kiafrika mjane hutakiwa kurithiwa, na familia kutegemezwa.

Lakini japo baba ndie kichwa cha nyumba, si wengi wanajua kuwa kunapotokea mazingira kama kufiwa na baba ambaye ni kichwa cha nyumba, mama akiamua kusimama na nyumba yake, hahitaji kurithiwa, huyu mama anakuwa amegeuka kichwa!, hivyo anageuka baba, hivyo kuna wanawake wengi tuu, japo ni wanawake na wanaitwa mama, lakini ni actual fact, wanawake hawa ni Baba!. Nyumba ikifiwa na mama, baba hawezi kugeuka mama, bali anatafuta mama mwingine, maisha yanaendekea, lakini nyumba ikifiwa na baba, mama anaweza kukomaa na kugeuka baba na maisha yakaendelea!.

Huu mfumo dume tumeurithi kwa wakoloni na kwenye mila zetu, kuna majina ya posts fulani fulani, ni majina ya kiume, mfano gavana ni post ya kiume, mwanamke anaitwa governess. Amiri Jeshi ni posti ya kiume, mwanamke ni Amirati. Chairman ni post ya kiume, mwanamke ni Chairwoman, hata president ni post ya kiume. Mwanamke anaposhika nafasi ya mwenyekiti wa chama, yaani Chairmanship, japo ni mwanamke, anageuka mwanaume na ataitwa Chairman , na sio chairwoman, hata mwanamke anapokuwa Amiri jeshi mkuu, anageuka mwanaume, anaendelea kuitwa amiri jeshi na sio amirati!, hivyo hata mwanamke akiwa ni president wa nchi, japo ni mwanamlke na wengi wanamuita mama, lakini in actual fact huyu ni baba!.

Kila awamu, rais wa nchi ndie baba wa taifa husika, na mke wake japo huitwa first lady, lakini sio mama wa taifa, bali mke wa rais, vivyo hivyo rais wa nchi anapokuwa ni mwanamke, rais huyo ni bado ni baba wa taifa hilo ambaye ni mama, na mume wake sio baba wa taifa, ni mume wa rais.

Leo nimeone niwafundishe hili somo, kuwa japo Rais Samia ni Mwanamke, na wengi humuita Mama Samia, ila ki nchi, kitaifa, ki madaraka na ki mamlaka na ki utawala, Rais Samia ndie kichwa cha nchi yetu, ndie Baba wa Tanzania ya leo kwa sasa, yeye ndiye kichwa cha nyumba yetu, ni Baba!.

Naomba kumalizia kwa ahadi nilowaomba kwa leo, mjifunze kuweka akiba ya mabandiko kama unavyoweka akiba ya fedha, mliweke akiba bandiko hili la Samia ni Baba, siku ya siku ikifika, nitalirejelea kwanini nimesema Rais Samia, japo ni mwanamke, ni mama, lakini sii mama tuu, ni ... ni MamaBaba!.

Mzee Pasco.
 
ila kumpa cheo Cha u baba ni kupima kina Cha bahari Kwa miguu, wote tuna jua uwezo wa kufikiria wa mwanaume ni level kubwa.

Hata maamuzi yake yana kuwa haya tetereshwi na uwepo wa kiumbe yoyote, huyu mama yenu ana endekeza uswahili wa kipwani zaidi kuliko kazi.
 
Una lazimisha mambo Paschal.

You are forcing things instead of letting nature flow in it's natural-course.

Iwe ni kimaumbile au kiuongozi,nature inakataa.

Kimaumbile au kiuongozi,samia hawezi kuwa Baba.
 
Tunaweza kumuita baba ukitaka. Hivi hamna vitu vya maana vya kuzungumza kuhusu nchi yetu? Kila kitu samia. Sasa akiitwa mama au baba nini kitabadirika! Andiko reeefu limejaa ujinga ujinga tu. Unajisikiaje kuzeekea JF halafu unaandika maandiko yasiyo na tija namna hii?! Jamani, hata mnapomuongelea Samia hebu jaribuni kuongea sanse.
 
Wanabodi,

Nawasalimu kwa jina la JF.
Angalizo la uchangiaji, hili ni moja ya mabandiko yangu ya kuwaanda Watanzani kisaikolojia kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka huu, nakushauri, ukiusoma uzi huu, ukijiona kama huuelewi elewi, jipitie zako tuu kwa amani, usiparamie kuchangia, ila kwa vile jf ni ukumbi wa wote, simple, mind, ordinary mind na great mind, kwa simple mind, wataliona bandiko hili kama bandiko la kichawa, kwa great mind watajikita na the motive behind!. Hivyo kwa wale mtakao niona nimekuwa chawa, niko ok, nioneni chawa, ila ma GT, tunaelewana!, karibuni.

Kila mtu anayesema chochote, au kuandika chochote, anakuwa na kitu kinachotwa drive, msukumo wa kusema ua kuandika, msukumo huo unaitwa causative agent, inaweza kuwa umeulizwa swali hivyo unasema kwa kujibu, au mtu ameandika kitu ukaguswa ukajibu, au kuchangia, ila katika hicho ulichokisema au ulichoandika, unakuwa na kitu kinachoitwa the motive behind, yaani unayasema hayo au unaandika hayo ili iweje?.

Huu ni mwaka wa uchaguzi, mwaka huu, mimi na PPR yangu tumeamua kujikita katika utoaji elimu kwa umma kuhusu siasa, uchumi na jamii, kuwaelimisha Watanzania, elimu ya demokrasia, katiba, sheria, haki na wajibu, ili wakati wa kufanya maamuzi, Watanzania wafanye informed decisions.

Naomba kukiri, nimehamasika kulizungumzia hili jambo, la mtu ambaye ni mwanamke, ni mama , na anaitwa mama, kumbe, sii mama tuu, ni mamababa!, kwa kuhamasishwa na kauli ya Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu, wakati akiitolea ufafanuzi, kauli yake ya "no reforms, no election", na kusema huo ndio msimamo wa Chadema, na kuufafanua kwa wale wana Chadema wanaotaka kugombea uongozi, kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu, wajiulize "unagombea uongozi, ili iweje?", jibu la hilo swali la ili iweje, ndio the motives behind. Bandiko hili pia lina the motives behind, ila hiyo motives behind, naomba nisiiweke kwenye bandiko hili, tutakuja kukumbushana huko mbele ya safari, muda muafaka ukiwadia!.

JF ilianzishwa mwaka 2006, mwakani tunasherehekea miaka 20 ya JF, kuna sisi baadhi yenu tulijiunga na jf tukiwa vijana, tumeoa tukiwa jf, sasa tunazeeka tukiwa jf, mfano mwana jf yoyote under 20, ajijue tangu anazaliwa watu tuko humu jf, lazima wajifunze kuwa na heshima.

Kufuatia long experience ya uzoefu wa muda mrefu, mara moja moja, nitakuwa napandisha makala elimishi za mambo yoyote ya busara, kwa jina la Busara za Mzee P.
na kwa vile mimi ni story teller, mabandiko haya yatakuwa ni marefu na story story kibao!.

Busara ya leo ni kuhusu majukumu ya kifamilia kwa mujibu wa dini kuu mbili, Ukristo na Uislamu, na mila nyingi za Kiafrika, zinazo fuata mfumo dume, patriarch, zimelelewa kwa malezi ya ubaguzi wa mfumo dume kuwa Baba ndio kichwa cha nyumba na mama ni kiwiliili. Kiwiliwili bila kichwa, ni hakuna kitu, lakini kichwa bila kiwiliwili, kinaweza kuchukua kiwiwili kingine chochote, maisha yakaendelea, ndio maana dini na mila za Kiafrika, zimeruhusu mwanamume kuwa na mke zaidi ya mmoja, lakini kwa mwanamke ni mume mmoja tuu, ukiondoa uongo wa mke mmoja kwa Wakristu, na mila za baadhi ya makabila ya matriarch, ya makabila machache ya Afrika, Asia na Latin America, mke ndie anaoa hivyo kuwa huru kuoa zaidi ya mume mmoja!

Ubaguzi huu huanzia kwenye ngazi ya familia na malezi kuwa mwanamke ni kiumbe dhaifu, dhalili, hivyo mtoto wa kike analelewa kiulaini laini na mtoto wa kiume analelewa kiugumu ugumu. Mtoto wa kike anafunzwa kuegemea na kumtegemea mwanaume, ni mtu wa kubembelezwa kuletewa na kupokea, na mtoto wa kiume anafunzwa kugangamala, ni mtu wa kutafuta, kutoa na kukomaa.

Hali hii huanzia tangu katika ujenzi wa familia, mtoto wa kike, anafundishwa kusubiri kuchaguliwa, kutongozwa, kuhongwa, kupendwa, kuchumbiwa, na kulipiwa mahari, ndipo apende, na ndani ya nyumba, mwanaume ndie kichwa cha nyumba, ndiye mtafutaji, anayepambana kutafuta, mke akiwa golikipa, akisubiri kuletewa.

Hata process ya uumbaji, procreation, kwa binadamu na viumbe wote, ukiondoa nyuki, ni mwanaume hukaa juu, mwanamke chini, ni mwanaume ndie anatoa mbegu, mwanamke anapokea, na kubeba, na kwa hapa Tanzania Bara, ni kosa la mwanaume kumpa mwanafunzi ujauzito, lakini kwa Zanzibar kosa ni la mwanamke kupokea ujauzito, kwasababu ni mwanamke ndie anayeruhusu!.

Na hata kukitokea msiba wa familia, akifa mama, japo baba huitwa mgane, lakini hakuna ajabu kwa baba kuoa tena, ndio maana ni aghlabu sana kusikia matatizo ya wagane, akifa baba familia haiterereki, kwasababu baba ni the breadwinner, lakini akifa baba, mke huitwa mjane na familia nyingi huterereka, kidini na kiafrika mjane hutakiwa kurithiwa, na familia kutegemezwa.

Lakini japo baba ndie kichwa cha nyumba, si wengi wanajua kuwa kunapotokea mazingira kama kufiwa na baba ambaye ni kichwa cha nyumba, mama akiamua kusimama na nyumba yake, hahitaji kurithiwa, huyu mama anakuwa amegeuka kichwa!, hivyo anageuka baba, hivyo kuna wanawake wengi tuu, japo ni wanawake na wanaitwa mama, lakini ni actual fact, wanawake hawa ni Baba!. Nyumba ikifiwa na mama, baba hawezi kugeuka mama, bali anatafuta mama mwingine, maisha yanaendekea, lakini nyumba ikifiwa na baba, mama anaweza kukomaa na kugeuka baba na maisha yakaendelea!.

Huu mfumo dume tumeurithi kwa wakoloni na kwenye mila zetu, kuna majina ya posts fulani fulani, ni majina ya kiume, mfano gavana ni post ya kiume, mwanamke anaitwa governess. Amiri Jeshi ni posti ya kiume, mwanamke ni Amirati. Chairman ni post ya kiume, mwanamke ni Chairwoman, hata president ni post ya kiume. Mwanamke anaposhika nafasi ya mwenyekiti wa chama, yaani Chairmanship, japo ni mwanamke, anageuka mwanaume na ataitwa Chairman , na sio chairwoman, hata mwanamke anapokuwa Amiri jeshi mkuu, anageuka mwanaume, anaendelea kuitwa amiri jeshi na sio amirati!, hivyo hata mwanamke akiwa ni president wa nchi, japo ni mwanamlke na wengi wanamuita mama, lakini in actual fact huyu ni baba!.

Kila awamu, rais wa nchi ndie baba wa taifa husika, na mke wake japo huitwa first lady, lakini sio mama wa taifa, bali mke wa rais, vivyo hivyo rais wa nchi anapokuwa ni mwanamke, rais huyo ni bado ni baba wa taifa hilo ambaye ni mama, na mume wake sio baba wa taifa, ni mume wa rais.

Leo nimeone niwafundishe hili somo, kuwa japo Rais Samia ni Mwanamke, na wengi humuita Mama Samia, ila ki nchi, kitaifa, ki madaraka na ki mamlaka na ki utawala, Rais Samia ndie kichwa cha nchi yetu, ndie Baba wa Tanzania ya leo kwa sasa, yeye ndiye kichwa cha nyumba yetu, ni Baba!.

Naomba kumalizia kwa ahadi nilowaomba kwa leo, mjifunze kuweka akiba ya mabandiko kama unavyoweka akiba ya fedha, mliweke akiba bandiko hili la Samia ni Baba, siku ya siku ikifika, nitalirejelea kwanini nimesema Rais Samia, japo ni mwanamke, ni mama, lakini sii mama tuu, ni ... ni MamaBaba!.

Mzee Pasco.
Ww unatakiwa ukamatwe namana juzi Uliwatukana wanaomshauri mama kuwa wanamzunguka hawampi ushauri wa maana Leo unamsifu inamana ww ni mtu KIGEU GEU PASCHAL MAYARA ACHANA NA HAYA MAMBO itakutokea puani acha kabisa h
 
Mkuu rekebisha Kuna sehemu ume chapia kidogo.

haiterereki - haitetereki
akifa baba, akifa baba, Ume yarudia sehemu ya kuweka mama.
Mkuu Intelligent businessman , wewe kweli intelligent, you have eye fr details, sio nimechapia, bali nimekosea, kuchapia ni kuweka uongo wa makusudi. Asante sana!, ungekuwa journalist, ungekuwa editor!.
P
 
Paragraph za kwanza tu kujihami sijui great mind Ndio wataelewa Nikawaza Fuvu nijue leo kaja na kitu gani.

Aaah kusoma ndani bwana ushuzi mtupu. Kumbe ile paragraph ilikua difensive tu,Ndani ushuzi wa Haja.

We Unazeeka vibaya.
 
Mhm huyu "baba" huyu.. Let me reserve my comment! But seriously speaking kumpa cheo cha ubaba ni in any way ni kuidhalilisha hii jinsia.. Pascal sijui umewaza nini
Mkuu Mshana Jr , kwanza naomba kuendelea kukuhakikishia, I have very highly respect to you, or for you.
Kinachofanya baba awe kichwa cha familia, sio ile jinsia yake bali ni responsibilities to be the provider, bada anapokuwa amekufa, kidini na kimila, mama anatakiwa kurithiwa na baba mwingine!, lakini kuna wanawake wa shoka, anafiwa na mume, anasimama imara na ku assume the responsibility kuongoza familia, anakuwa kichwa, anakuwa baba!.

The same applies to nchi, baada ya lile tukio (lilitokea tarehe 12 March) na kutangazwa 17 March, for 5 good days watu walihaha wamtafute mrithi!, alipoipokea nchi, japo yeye ni mwanamke na ni mama, lakini ki nchi, huyu ni baba!, sijaidhalilisha jinsia ya kike, kwasababu, ule ukichwa cha familia, au ubaba wa nyumba au nchi, sio ile jinsia, bali the responsibilities, hivyo nimeipandisha hadhi sana jinsia ya kike!. Wanawake Wana Akili Kuliko Wanaume? Hata kwenye Siasa na Uongozi, Wanawake Wameonyesha Uwezo Kuliko Wanaume

P
 
Mamlaka iliyo kuu imewekwa na Mungu. Uwepo na Mama umeruhusiwa na Mungu. Tutaendelea kuwa nae kama Mama yetu na kiongozi wetu, hawezi badilika akawa Baba. Na kila kitu kitaenda kama Mungu alivyokusudia.
 
Kifalsafa upo Sahihi.
Nafikiri Mada hii umezungumzia kifalsafa zaidi.

Kwenye falsafa kuna kipera cha Logic (Mantiki) ambapo kwenye Lugha hasa isimu kuna kitu inaitwa Semantic.

Baba maana yake ni enye nguvu, chanzo, mtoaji(mhudumiaji), Mamlaka, hodari n.k.

Kwa Mantiki hiyo mtu yeyote mwenye nguvu, chanzo,au mtoaji na mwenye Mamlaka, mwenye nguvu huyo ni Baba.

Kibaolojia, Baba ni Maumbile
 
Back
Top Bottom