Je, wajua kwamba Katiba hii mbovu inamruhusu Rais kuteua Watu wa familia yake kushika vyeo mbalimbali?

Je, wajua kwamba Katiba hii mbovu inamruhusu Rais kuteua Watu wa familia yake kushika vyeo mbalimbali?

Tunataka katiba ambayo wateuliwa katika nafasi nyeti watahojiwa na kamati za bunge, weledi wao kutathiminiwa na wathibitishwe na bunge. Kama hizo kamati za bunge zikiridhia hao wapwa na watoto wa rais kushika hizo nafasi baada ya kuteuliwa na baba yao sawa tu.
Mkuu unatakiwa utulie kwenye mada moja moja,kule kwa majaliwa umeondoka umekuja kuanzisha uzi huku anyway acha na hapa tuwe pamoja.

Naomba uniambie ni katiba ya nchi gani hairuhusu mtu kumchagua ndugu yake au mtu wake wa karibu kuwa katika nafasi husika pale endapo tu atakidhi vigezo husika ?

Hapo kwenye vigezo ndio point ya msingi.

Kwa sababu raisi hana uwezo wa kumchukua kaka yake ambaye yupo mtaani akamchagua akawa IGP lazima IGP awe askari wa cheo fulani.

Hiko kitendo cha kuwa askari wa cheo fulani ndio kigezo chenyewe.

Sasa kama amekidhi vigezo vya kuwa IGP yaani ni askari wa cheo fulani alafu ni ndugu yake naomba uniambie ni katiba ya Nchi gani hapa duniani inakataza jambo hilo ?


Lakini pili ukitaka katiba ambayo raisi hatoruhusiwa kumchagua ndugu yake ama mtu wake wa karibu katika nafasi fulani basi naomba UNIPE SABABU MBILI TU KWA NINI HII ISIWE KATIKA INAYOMBAGUA RAISI KATIKA KUTEUA ?

kwa nini isiwe katiba baguzi dhidi ya raisi ?
 
Kwa katiba tuliyo nayo mhe Samia anaweza kuteua familia yake yote na kuipa vyeo tofauti tofauti. Anaweza kumpa mtu yeyote cheo cha aina yeyote muda wowote. Uwe unataka ama hutaki.

Kwa mfano anaweza kuamua kumteua:-
- Mumewe kuwa waziri wa fedha.

- Mwanawe kuwa mhazini mkuu wa serikali

- Mjukuu wake kuwa gavana wa BoT

- Jirani yake kuwa IGP

Usisahau pia ana uwezo wa kuamuru achotewe kiasi chochote cha fedha afanyie kazi zake binafsi.

Katiba gani hii? No! No! No! Not at all!.

Tunahitaji katiba mpya.
Ingefaa zaidi unukuu na vifungu vya katiba unavyovizungumzia.

Nashangaa mnalishwa matango Pori na ninyi mnayakariri.

Katiba mpya unataka ibague Watanzania? Maana hao wote unaosema ni ndugu zake Rai's ni watanzania na baadhi ya nafasi ulizotaja mtu kuteuliwa kuzishika lazima awe atimize vigezo fulani
 
Tunataka katiba ambayo wateuliwa katika nafasi nyeti watahojiwa na kamati za bunge, weledi wao kutathiminiwa na wathibitishwe na bunge. Kama hizo kamati za bunge zikiridhia hao wapwa na watoto wa rais kushika hizo nafasi baada ya kuteuliwa na baba yao sawa tu.
Ni nchi gani ilikuwa na katiba hiyo alafu watu wakahojiwa ikaonekana hawafai ?

Kama walihojiwa ikaonekana hawafai ina maana hao wanaohojiwa ni ndugu zake tu watu wengine wasiokuwa ndugu zake haifai kuhojiwa ?
 
US mara nyingi sana wateuliwa wa Rais wamewahi kukataliwa na Seneti au Rais kubadilisha wateuliwa baada ya kugundua Seneti haitawapitisa.
Unataka mifano hapa au unaweza Google mwenyewe?
Ni nchi gani ilikuwa na katiba hiyo alafu watu wakahojiwa ikaonekana hawafai ?

Kama walihojiwa ikaonekana hawafai ina maana hao wanaohojiwa ni ndugu zake tu watu wengine wasiokuwa ndugu zake haifai kuhojiwa ?
 
US mara nyingi sana wateuliwa wa Rais wamewahi kukataliwa na Seneti au Rais kubadilisha wateuliwa baada ya kugundua Seneti haitawapitisa.
Unataka mifano hapa au unaweza Google mwenyewe?
Kwa maana wanaohojiwa sio ndugu tu
bali ni yeyote anayechaguliwa na raisi katika nafasi hizo si ndio ?
 
Kwa kweli tunahitaji katiba mpya ili tufunge marais wezi na viongozi wasiowajibika.....tusipofanya hivi tutaendlea kuwa wapumbavu tu
 
Duniani kote hakuna katiba inamnyima Rais kufanya hivyo.
 
Hii ya kwetu mpya tunayoitaka iharamishe Rais kuteua ndugu zake ili wengine waje kujifunza kwetu kama walivyokuja kujifunza nyungu wakati wa Corona.
Duniani kote hakuna katiba inamnyima Rais kufanya hivyo.
 
Ambacho haujui ni kuwa katiba hii inamruhusu hata Jaji Kaijage kujitangaza kuwa ameshinda uchaguzi na kuwa Rais hata bila kugombea. Katiba inasema Kaijage akishatangaza tu hakuna wa kupinga.
Kwa katiba tuliyo nayo mhe Samia anaweza kuteua familia yake yote na kuipa vyeo tofauti tofauti. Anaweza kumpa mtu yeyote cheo cha aina yeyote muda wowote. Uwe unataka ama hutaki.

Kwa mfano anaweza kuamua kumteua:-
- Mumewe kuwa waziri wa fedha.

- Mwanawe kuwa mhazini mkuu wa serikali

- Mjukuu wake kuwa gavana wa BoT

- Jirani yake kuwa IGP

Usisahau pia ana uwezo wa kuamuru achotewe kiasi chochote cha fedha afanyie kazi zake binafsi.

Katiba gani hii? No! No! No! Not at all!.

Tunahitaji katiba mpya.
 
Katiba mpya iwekewe kipengele cha kuwafunga kifungo cha maisha wale wote ambao jinsi yao haijulikani. Mfano Sexless mara anajifanya dume mara jike.
Wewe ndiwe unayekosea. Ni wapi inapoeleza "sexless" ni kujigeuza mara kuwa jike au dume?

Sexless, ni hivyo hivyo ilivyo, haina dume wala jike.
 
We kilaza hao hawakuwa watumishi wa umma wa Marekani, ni wapambe na wabeba mikoba tu wa Rais. Watumishi wa umma wote US wenye kushika nafasi zenye maslahi ya taifa lazima wathibitishwe na Seneti.
Yaani wamtumikie kiongozi mkuu wa nchi, halafu unasema siyo watumishi wa umma? Wee unafikiri hakuna vetting iliyofanyika mpaka wakakubalika na kuruhusiwa kuwa karibu sana na rais?
 
Duniani kote hakuna usawa mnaotaka... hata USA wanachagua/kuteuana wale wanaojuana. Acheni ujinga.
Badilisha jina jiite careless badala ya cardless. Nyie ndo mna justify ujinga kwa sababu dunia inafanya. Hauna tofauti na mtu anaekunya sebuleni. Akaulizwa na mzazi wake kwa nn unakunya akaanza kusema mbona hata rafiki yangu nyumba ya jirani huwa anakunya
 
Ambacho haujui ni kuwa katiba hii inamruhusu hata Jaji Kaijage kujitangaza kuwa ameshinda uchaguzi na kuwa Rais hata bila kugombea. Katiba inasema Kaijage akishatangaza tu hakuna wa kupinga.
Sijui kwa nini alishindwa kujitangaza.
Watu wengine wanapewa fursa na hawajui namna ya kuzitumia.

Vijakazi ni vijakazi tu hawana uthubutu.

Mtu kama Magufuli ungemweka kwenye nafasi hiyo angejitangaza!
 
Ambacho haujui ni kuwa katiba hii inamruhusu hata Jaji Kaijage kujitangaza kuwa ameshinda uchaguzi na kuwa Rais hata bila kugombea. Katiba inasema Kaijage akishatangaza tu hakuna wa kupinga.

Ibara ya ngapi hiyo?
 
Wewe ndiwe unayekosea. Ni wapi inapoeleza "sexless" ni kujigeuza mara kuwa jike au dume?

Sexless, ni hivyo hivyo ilivyo, haina dume wala jike.
Siongelei jina, mchimbe utaona mara anasema sisi wanaume mara sie wanawake
 
Nini hiyo raisi ana mamlaka ya kuagiza hata Mlima Kilimanjaro uvunjwe ili mawe yakajenge SGR!
Tunaweza kupiga kelele hata kuanzisha vurugu kupinga lakini kwa mamlaka aliyoanayo kwa mujibu wa katiba hii anayo power hii!
 
Vetting ni utopolo gani?? Nafasi zote nyeti US lazima watu wake wathibitishwe na kamati husika za bunge la Seneti. Hadi bodi ya posta inathibitishwa na seneti. Washauri wa Rais Marekani sio watumishi Rasmi wa umma.
Yaani wamtumikie kiongozi mkuu wa nchi, halafu unasema siyo watumishi wa umma? Wee unafikiri hakuna vetting iliyofanyika mpaka wakakubalika na kuruhusiwa kuwa karibu sana na rais?
 
Back
Top Bottom