Je, wajua? - Special Thread

Je, wajua? - Special Thread

Kweli aisee na population Africa ipo kwa nchi 6
Nigeria 179M
Ethiopia 108 M
Egypt 99M
DRC. 80 M
Tanzania 58M
South Africa 51 M

Kwingine mapori tuu
 
India unaiacha wapi ambayo inaipiku china muda si mrefu,
JUA HILI
Idadi ya raia wa China ni 1,437,268,056 na idadi ya bara lote la Afrika ni 1,340,598,140
Kwahyo utofauti wake na China inazidi bara lote la Afrika watu takribani 96,668,961
Hii inamanisha watu wote wa Afrika wanaweza ishi China na Watu wa China wakiishi wote Africa watakua wengi zaidi.
 
JUA HILI
Idadi ya raia wa China ni 1,437,268,056 na idadi ya bara lote la Afrika ni 1,340,598,140
Kwahyo utofauti wake na China inazidi bara lote la Afrika watu takribani 96,668,961
Hii inamanisha watu wote wa Afrika wanaweza ishi China na Watu wa China wakiishi wote Africa watakua wengi zaidi.
Humo wachina diaspora wapo?
 
Mende ni mdudu anayeweza kuishi zaidi ya mwezi bila ya kula chakula chochote.

Ni mdudu anayeweza kuishi wiki mbili bila ya kunywa maji.

Wakati moyo wa mwanadamu ni mmoja wenye chemba nne mende ana moyo mmoja wenye chemba kumi na tatu.

Baadhi ya mende wa kike hawaitaji wanaume kuweza kuzalisha mayai hupandana wao kwa wao na kutaga mayai katika kipindi chote cha maisha yao.

Mende ana uwezo wa kukaa kwa zaidi ya dakika 40 bila ya kupumua.

Mende ana uwezo wa kuishi zaidi ya wiki mbili akiwa amekatwa kichwa.

Ana uwezo wa zaidi ya mara 15 ya binadamu wa kuzuia miale mikali ya nuklia isimdhuru na kubaki hai

Mende ni mdudu asiye na mapafu.

Ana uwezo wa kuruka maili 3 kwa saa

Mende ni mdudu asiyeweza kuamla akilalia mgongo

Paka ni mnyama asiyeweza kuangukia mgongo

Sijui sisi binadamu tuna nini cha kushangaza ... labda siasa chafu!!! 😂 🤣
 
Je wajua kuwa ndege jamii ya Cuckoo hutaga mayai yao kwenye viota vya ndege wengine?

Ndege jamii ya Cuckoo hutaga mayai yao kwenye viota vya ndege wengine (hasa jamii ya dunnocks, meadow pipits & reed warbles) na kuacha mayai yao yaanguliwe na ndege wengine na vifaranga kulishwa na ndege wamiliki wa viota.
 
Je wajua kuwa ndege jamii ya Cuckoo hutaga mayai yao kwenye viota vya ndege wengine?

Ndege jamii ya Cuckoo hutaga mayai yao kwenye viota vya ndege wengine (hasa jamii ya dunnocks, meadow pipits & reed warbles) na kuacha mayai yao yaanguliwe na ndege wengine na vifaranga kulishwa na ndege wamiliki wa viota.
Aisee!
 
Je wajua mnyama aina ya Kenge mvua ikinyesha akiwa nchi kavu haraka huikimbia mvua na kukimbilia majini kama maji yako karibu kama hayako karibu anajificha mvua isimpate? kwanini?
Sababu alivyoumbwa maji ya mvua yanabadilisha haraka sana mfumo wake wa pressure ya mwili osmotic pressure kwasababu maji ya mvua hayana madini yeyote hivyo anakimbilia haraka majini maana angalau majini kuna madini yanayoweza kuweka mfumo wake wa osmotic pressure sawa au angalau akijificha hiyo shida haijitokezi.
Sio kwamba watu wanadhani ni ujinga wake kukimbia maji ya mvua na kukimbilia kwenye dimbwi kuna sayansi ndani yake.
 
Jewajua..

→✏ Nyanya ndo tunda Maarufu zaidi Duniani. Ndizi sio tunda ni mtishamba{Herbs}.
→✏ Kila Bara linaishia na Herufi iliyoanza nayo mwanzo, mfano: Africa, Europe, Asia.. [Kwa Kingereza lakini]
→✏ Maji huwa hayaexpire, expire date ni ya Chupa.
→✏ Asali ndo Chakula Pekee Kisichoharibika.
→✏ Unaweza kupunguza Uchachu wa embe kwa Kuliloweka dakika 10 kwenye Maji ya Uvuguvugu.
→✏ 96% ya Mishumaa hununuliwa na Wanawake.
→✏ Uking’oa kucha zote za vidole vya mkono, itakuchukua miezi 6 Mpaka ziote na Zikomae tena.
→✏ Kuna Radi takribani 2,000 kwa kila dakika Duniani.
→✏ Gesi haina Harufu, bali harufu huwekwa ili Kutaarifu kama Gesi ikivuja.
→✏ Katika Alfabeti zote, herufi ‘e’ ndo hutumika Zaidi.
→✏ Mabegi ya kuburuta Matairi yalianza Kutumika tangu 1971.
→✏ Watoto wadogo chini ya miezi 3, hawawezi kutetemeka kwa baridi.
→✏ Duniani kuna wastani wa Watu 6 ambao Unafanana nao kila Kitu kasoro Jina tu, na una 9% ya Kukutana nao!
→✏ Mahusiano mengi Duniani huzaliwa siku ya Jumatano.
→✏ 97%ya watu wakipewa Kalamu Mpya, basi wataijaribu ubora wake kwa kuandika Majina yao ama kuweka alama ya Sahihi.
→✏ Ukiwa unaandika namba zako za Siri, ukahisi Umekosea hata moja huwa Unafuta Zote na kuanza Upya.
→✏ 3% ya watu wote Duniani ni Mapacha. *Mapacha wanaweza Kuwa na Baba tofauti.
→✏ Watoto 255 huzaliwa kila dakika, taarifa: UNICEF.
→✏ Kama Umezaliwa 1999, Basi jua Umeishi ndani ya Miongo 3, Karne 2 na Millennium 2.
→✏ Kujinyonga India, kumeua Watu wengi Kuliko Ukijumulisha ajari na magonjwa kwa Pamoja
→✏ Pweza ana Bongo 9, Mioyo 3 na damu ya bluu. Maziwa ya Kiboko ni ya Pink.
→✏ Huwezi kupiga Chafya bila kufumba Macho.
→✏ Ukidownload file “PDF” inayoishia na ‘exe’ ifute io ni Virus.
→✏ 74% ya Watumiaji wa facebook huiangalia Kila siku, Mtu mmoja hutumia angalau dk 35 kwa Siku.
→✏ Video Billion 8 Hutazamwa fb kila Siku. Marekani ina idadi kubwa ya watumiaji fb. fb profile feki Duniani zinakadiliwa Kufika Million 270.
→✏ Account Million 391 za twitter hazina follower. Watu million 500 hutembelea Twitter kila mwezi bila kulog in.
→✏ Kombe la Dunia lilianzishwa rasmi 1930,Uruguay akiwa Mdhamini, na ndo aliyechukua Kombe kwa Mara ya kwanza.
→✏ Sehemu nyeupe ya Kucha yako inaitwa ‘lunula’.
→✏ Kama jicho lingekua Camera lingekua na MegaPixel [576MP].
→✏ Mende ana Uwezo wa Kuishi kwa Wiki kadhaa akiwa hana Kichwa.
→✏ Ukihesabu kwa Maneno ya kingereza 1-1,000 hutopata herufi ‘a’. Mpaka ufike 0ne thous‘a’nd ndo utaipata.
→✏ Kwa Siku, ni Bora Ukulala Mara mbili kwa Masaa 4, kuliko Kulala Masaa 8 kwa Pamoja.🙏

Wako Emmanuel Kasomi
 
Back
Top Bottom