Kuna siku nilikuwa na wife nikakutana na Comando mmoja ambaye ni mshkaji wangu niliwahi soma nae miaka hiyo
Nikamtambulisha kuwa huyu ni comnando
Wife akamtania akamwambia vipi na yeye anaweza kuingia u commando??
Comando akasema ni haiwezekani na kwamba Duniani hakuna Comando mwanamke
Kwa maana Special forces
Na sababu ni maumbile yao hayaruhusu mazoezi ya commando
Kwamba yapo mafunzo ambayo yakifanyika mwanamke anaingia kwenye siku zake automatically so ni ngumu sana kwa wanawake
Na hata Duniani huwezi kuta Navy Seals, Great barrett, Spetsnaz mwanamke
ILA kinachofanyika kwa wanawake ni hupitia mafunzo ya kawaida tu ya kijeshi etc ila sio mafunzo ambayo wanapitia ni ya kikomando
So mtu akikwambia kuna mwanamke Comando ujue ni Fix ya kiwango cha juu