Je, Watoto wanaolelewa bila vipigo hawana maadili?

Mie kamkono kwangu kepesi mno!
 
No mkuu nmetolea mfano tu , mmonyoko wa maadili ni mkubwa sana kwa wenzetu tofauti kabisa na kwetu , pia hata wao wanapenda sana jinsi sisi tulivyo naongea kitu ninachokijua na sio nilichosikia mkuu .
Mimi mjomba wangu alikuwa ananikanda, watoto wake hakuwakanda yamekuwa ya ovyo!Anawaambia muwe kama huyu binamu yanu,hayana Adabu kabisa,namuuliza kwa Nini hukuwakanda,anabaki Kutoa macho tuu
 
Walimu pia ni walezi, wanakaana watoto muda mwingi shuleni

Je adhabu za viboko mashuleni ni sawa ?
 
Mimi mjomba wangu alikuwa ananikanda, watoto wake hakuwakanda yamekuwa ya ovyo!Anawaambia muwe kama huyu binamu yanu,hayana Adabu kabisa,namuuliza kwa Nini hukuwakanda,anabaki Kutoa macho tuu
Kina junia hawachapwi ,hawachewi kutoka kavaa nguo ya ndani ya mama yake kichwani , mbele ya wageni sebuleni 😁😁
 
Min

Ulisema hivi “Hata hawa watoto wa miaka ya 2000 wengi wao hawakupitia viboko , je umeona tofauti yoyote kimaadili?”

rejea sasa swali nililokuuliza.
Zaman zetu tulikua tunachapwa hata na jirani ukikosea , hilo wewe kwa kipindi cha sasa umeliona? Na vip kuhusu maadili ya sasa ?
 
Hapo kwenye kuvunja vyombo ni kweli tushapigwa sn.
Mie kwangu marufuku kutumia vyombo vya plastic kwa wtt kulia chakula eti kisa vya kigae watavunja. Kuna mtu aliniambia kuwa vyombo navyo vina roho vikifika siku yake vinakufa. Napia kutumia vyombo vya kigae kwa wtt vinawafundisha Kuwa na tahadhari wkt wa kuvitumia.
Mie mtt wangu wa miaka 6 anaosha chombo chake bila waswas
 
Yaani hapo umesema kweli kabisa
Niweke plastic na maradhi yake kisa naogope vyombo kuvunijika? Hapana kwa kweli
Kama unavyosema kila kiumbe ni kufundishwa tu
Kwanza wanakuwa waangalifu zaidi kwa vyombo vizito
Hayo ya plastic mara yanafanywa silaha mara mpira hapana 😄

Kuna kipindi cha tv uk huwa naangalia kinaitwa dogs behaving very bad
Sasa kama mbwa anaweza kubadilishwa tabia bila kupigwa itakuwa binadamu anaekusikia maneno yote?
Watch that one
 
Usiseme vipigo sema kuadhibu..

Kuna tofauti kubwa kati ya kumuadhibu mtu kwa Nia la kuinstill discipline na kumshushia kipigo... Sasa wewe kitendo Cha kushindwa kutofautisha hivyo viwili umeonesha una tatizo kubwa sana kwenye ufahamu wako wa malezi.

Naamini kabisa kwa hii thread yako wewe utakuwa ni mzazi wa kisasa na watoto wako hawana adabu hata kidogo.
 
Mimi binafsi kuna vipigo nilivyowahi kuchezea kutoka kwa maza na mshua siwezi sahau hadi leo.. na sikuwahi kurudia yale makosa niliyoadhibiwa nayo.
 
Jiulize, wewe ukikosea, ni nani huwa anakupiga?
Hii Wala sio hoja yenye nguvu ya kupinga matumizi ya viboko, japo wewe unaweza ukawa unajiona umewaza sana.

Huwezi ukalinganisha utovu wa nidhamu/ukosefu wa mtu mzima ambaye anajua kabisa anachofanya na wa mtoto ambaye mara nyingi kama sio mara zote anakuwa hajui kama anachofanya ni sahihi au si sahihi.

Yaani hapo ni sawa sawa na wewe umemkamata mwizi ndani mwako halafu unaanza kusema kwa vile Mimi mwenyewe nimewahai kuiba na hakuna aliyenipiga Wala kunipeleka polisi, basi hata huyu mwizi nilyemkamata acha tu nimwache aende zake.

Kwa ufupi tu hii ni uliyotoa counterargument dhaifu sana
 
Neno pekee ambalo waafrica wamelielewa kwenye biblia, na wanalitendea kazi ni " usimnyime mtoto mapigo"
 
Neno pekee ambalo waafrica wamelielewa kwenye biblia, na wanalitendea kazi ni " usimnyime mtoto mapigo"
Mithal 22:15, asili ya malezi ya kiafrika yaheshimiwe, traditional education kabla ya kuja kwa wazungu ilizalisha jamii yenye maadili, productive na ya kizalendo, mambo yamekuja kubadilika baada ya kudharau taratibu zetu na kukumbatia mila na desturi za wazungu.
 
Eti wazungu wakikosea mtu hachapwi wakati huo huo kuna majimbo Marekani mpka mwaka huu bado mtu akikosa ANANYONGWA… kwanini ananyongwa sasa? Si aitwe aelekezwe taratiiibu?
Hawa wabongo wanaokopi malezi ya wazungu ni kama wendowazimu.

Hii comment yako ukiifungua utapata mjadala mpana sana ambao naamini Hawa wabongo wanaojiona wazungu hawawezi kuujadili......

Leo hii tuna mahakama na vyombo lukuki vya dola ikiwemo police ambavyo vipo kwa ajili ya kudili na watovu wa nidhamu au wakosefu na Tena vikitumia nguvu kutimiza majukumu yake, Sasa kama binadamu haitaji matumiz ya nguvu hili aweze kuwa ni mtu Bora na mwem, vyombo hivi vya dola vipo kwa ajili gani Sasa???

Tukiachana na Hilo, huko marekani wamehalalisha umiliki na matumiz ya silaha za moto kama bunduki, mara kadhaa tumeona watoto wadogo wakiiba silaha kutoka kwa wazazi wao na kisha kwenda kuwashambulia watoto wenzao mashuleni(school mass shootings)..... Sasa kama aina ya malezi waliyonayo ya kutokuchapa ni bora kivip tunaona matukio kama haya yalitokea? Inakuwaje wanakuwa na watoto ambao ni psychopaths Wana uwa wenzao kikatili namna ile???
 
Jina lako tu ni mnyenzi ina maana ni mshenzi nyinyi ndio wapotoshaji wakubwa wa maadili shenzi kama jina lako
😄 🤣
Hii sasa vita.

Mbona makasiriko ndugu yangu.

Usipige mtoto ndugu unamuonea tu, kama ni kukosea hata wewe unakoseaga, kama ni kupiga basi mpige mtu alie size yako mf; bosi wako, konda wa daladala ili upate matokeo sawa.

Halafu unapokua unapiga mtoto mara nyingi huwa unakua kwenye hali ya hasira, hivyo hata mapigo utakayompa yatakua ni makali ili umalize hasira na sio kufundisha..

Kaa chini zungumza na mtoto, mwambie wazi alipokosea na umpe maelekezo/usaidizi, yaani mtoto mwenyewe atakua mwelewa sana mpaka utashangaa(hasa kama ulianza nae tangu utoto)


View: https://youtu.be/CejhQC9hUO8?si=x2lpn6tgnNu_Qocp
Angalia hiyo video halafu jiulize lingekua dingi la kibongo hapo, huyo mtoto angekula mambata tu, kumbe ni ishu ndogo mtoto unaongea nae anakuelewa


View: https://youtu.be/2vs0A56HSHU?si=B5cI3lQhodANcfG9
Wenzako wanaanzaga tangu umri huu.
Mtoto anaongea mambo hata hayaeleweki lakini dingi anasapoti
 
Katika malezi tunatakiwa tukumbuke hao Watoto tunaolea ndio wakubwa wa baadae, sio sanamu wala robot.

Tuwape uhuru wa kuamua Maisha yao ya baadae wanapofikia umri lakini wakiwa chini ya hapo miongozo na adhabu za kibinaadam zenye funzo Kama kulima bustani, kusafisha msalani, kusafisha kuta za nyumba na mengine Kama hayo ndio stahiki .

Kwa maana mtoto sio ng’ombe ni Mtu, anahitimu Utu wake Kwa hatua, Kama wewe ilivyokua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…