Ahsante Sana kwa mada yako. Ndiyo Iko x usiku kucha jana na inaendelea.
Naongezea; tuna wazee wengi hawatunzwi na watoto wao waliowachapq Sana kwa madai ya kuwatengeneza. Je hii siyo MOJAWAPO ya athari ya mpasuko wa mahusiano ya watoto na Wazee ? Kwamba nguvu kubwa ilitumika kuumiza mwili badala ya ku transform akili ya ndani ya mtoto? Sasa mtoto kawa mkubwa, Tabia zake zilizokandamizwa kwa hofu ya kipigo, sasa zinaanza kushamiri na kumea maana hakuna wa kumpiga tena?
Nini maoni yenu?
Napingana nawewe mh. Tofautisha uonevu kwa mtoto na adhabu kama amekosea!
sisi tumekua ukikosea wewe mwenyewe kabisa unajutia kuwa hapa nimekosea na unastahili adhabu!
hivyo mzazi anapokuja kutoa hiyo adhabu moja kwa moja unathibitisha kabisa kweli hili ni kosa na nilistahili
adhabu.
Point yako ya kusema wazazi wanatelekezwa kisa walitoa adhabu/kipigo kwa watoto wao haina mashiko.
Naweza kusema huo ni moyo wa mtu tu kwanza mtoto anatabia ya kusahau kama unatoa adhabu kwa haki
wapo wengi tu watoto wao walisomesha kwa shida wakiuza ardhi na mifugo nk ili mtoto asome matokeo yake
wazazi hao wametelekezwa na mtoto hana sababu yoyote ya maana.
Point yako yako ya pili mtoto akiwa mkubwa anafanya yale aliyokandamizwa asifanye kwa hofu ya kipigo na sasa anafanya. Hii nayo umeingia chaka vibaya mno.Hakika umelelewa vizuri huwezi kuja kukengeuka ukubwani
mtu anaye kuja kukengeuka ukubwani bado malezi yake yana uwalakini mkubwa kipindi cha makuzi yake.
{Mtoto umuleavyo ndivyo akuavyo}
Mimi nimeanza kutembea sehemu mbalimbali kusiko na ndg isipokuwa rafiki tu anakupa connection
lakini ukifika hiyo circle ina watu wenye tabia ovu kama kuvuta bangi na kutumia madawa ya kulevya.
lakini kwa sababu ya maonyo na vipigo kila tulipoonyesha viashiria vya kihuni mzee alitoa kipigo kitakatifu.
hadi leo hii mzee huwa namwambia bila kipigo nisingekuwa hapa nilipo.
Nina uhakika hata wewe madame umepokea mkong'oto wa kutosha kutoka kwa wazazi na waalimu wako ndio maana upo hapo.
kuzarau mapigo leo hii kutokuwa na shukrani hata kidogo kwa juhudi zilifanyika hadi ukafika hapa ulipo
Ulipaswa utuambia kuwa kwa hakika mapigo kiasi yana mchango kwenye maadili. Lakini leo hii ninyi
ambao wazazi wenu hawakuwa maprofesa waliwalea ninyi mmekuwa ma professor cha ajabu wewe professor katika uzao wako unaweza ukakoswa kabisa professor!
Ukiangalia kila kitu unacho elimu ya kutosha unayo maisha mazuri unayo
mtoto ada sio ya kuuliza bima ya afya mtoto anayo. cha ajabu anaweza kujitahidi sana na kufoji mno akapata
phd. Haya siyasemi kwa bahati mbaya kama wewe hufanyi wenzio wanafanya.
NI MAONI YANGU BINAFISI. ahsante.