Jenerali Mabeyo amuaga Rais Mwinyi. Ajiandaa kustaafu June 2022

Jenerali Mabeyo amuaga Rais Mwinyi. Ajiandaa kustaafu June 2022

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Venance Salvatory Mabeyo leo amefika Ikulu ya Zanzibar kwaajili ya kumuaga Rais wa Zanzibar Hussein Mwinyi ikiwa ni maandalizi ya kustaafu mwishoni mwa mwezi huu.

Jenerali Mabeyo 65, amelitumikia jeshi kwa miaka 42 sasa na muda wake wa utumishi unaenda ukingoni mwezi huu.

Jenerali Mabeyo amehudumu nafasi ya Mkuu wa Majeshi kwa miaka 6 sasa baada ya kuteuliwa mwaka 2016 na aliyekuwa Rais wa awamu ya tano, hayati John Pombe Magufuli.

Katika uongozi wake kama CDF, alishuhudia kukabidhiwa kwa madaraka kwa Rais wa kwanza mwanamke, Samia Suluhu Hassan baada ya kifo cha mtangulizi wake.

Daima utumishi wake uliotukuka utaendelea kukumbukwa ndani ya JWTZ na Nchi kwa ujumla. Nikutakie maandalizi mema ya kustaafu Jenerali Mabeyo

View attachment 2252170u
Alipaswa awe amestaafu mwaka 2017!! Hakukuwa na ulazima wa yeye kuendelea na kazi baada ya kufikisha miaka 60 hapo june 2017.
 
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Venance Salvatory Mabeyo leo amefika Ikulu ya Zanzibar kwaajili ya kumuaga Rais wa Zanzibar Hussein Mwinyi ikiwa ni maandalizi ya kustaafu mwishoni mwa mwezi huu.

Jenerali Mabeyo 65, amelitumikia jeshi kwa miaka 42 sasa na muda wake wa utumishi unaenda ukingoni mwezi huu.

Jenerali Mabeyo amehudumu nafasi ya Mkuu wa Majeshi kwa miaka 6 sasa baada ya kuteuliwa mwaka 2016 na aliyekuwa Rais wa awamu ya tano, hayati John Pombe Magufuli.

Katika uongozi wake kama CDF, alishuhudia kukabidhiwa kwa madaraka kwa Rais wa kwanza mwanamke, Samia Suluhu Hassan baada ya kifo cha mtangulizi wake.

Daima utumishi wake uliotukuka utaendelea kukumbukwa ndani ya JWTZ na Nchi kwa ujumla. Nikutakie maandalizi mema ya kustaafu Jenerali Mabeyo

View attachment 2252170



---
Jenerali Venance Mabeyo ni Mkuu wa Majeshi wa nane kuliongoza Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania tangu alipoteuliwa Februari 6, 2017 na aliyekuwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa awamu ya tano, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli.
Alizaliwa Julai 1, 1956 wilayani Magu mkoani Mwanza na kupata elimu ya msingi katika shule ya Namibu mkoani Mara kuanzia 1965 hadi 1971.
Alianza elimu ya Sekondari katika Seminari ya Nyegezi kuanzia 1972 hadi 1975, kisha akaendelea na kidato cha tano na sita Mzumbe Sekondari kuanzia 1976 hadi 1977.
Jenerali Venance Mabeyo alijiunga na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania Januari 1, 1979 na kuhudhuria kozi ya afisa mwanafunzi na kupata kamisheni mwaka 1980 kuwa Luteni Usu.
Safari ya Jenerali Venance Mabeyo JWTZ
Julai 1980: Luteni Usu
Agosti 1981: Luteni
Januari 1987: Kapteni
Oktoba 1991: Meja
Juni 1998: Luteni Kanali
Mei 2006: Kanali
Septemba 2010: Brigedia Jenerali
Septemba 2014: Meja Jenerali
Juni 2016: Luteni Jenerali
Februari 2017: Jenerali
Jenerali Venance Mabeyo alihudhuria kozi mbalimbali ndani na nje ya nchi, baadhi ya nchi hizo ni Kenya, India, Canada na Marekani
Jenerali Venance Mabeyo katika kulitumikia Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania alishika nyadhifa mbalimbali ikiwemo Mwambata Jeshi nchini Rwanda, Msaidizi wa Mkuu wa Majeshi , Mkuu wa Tawi la Usalama na Utambuzi na Mnadhimu Mkuu wa JWTZ.
Jenerali Venance Mabeyo ametunukiwa medali mbalimbali;
Miaka 20 ya JWTZ
Medali ya utumishi mrefu.
Medali ya miaka 40 ya JWTZ.
Medali ya utumishi uliotukuka.
Medali ya Comoro na Anjouan.
Medali ya miaka 50 ya uhuru
Medali ya miaka 50 ya Muungano
Miaka 50 ya JWTZ
Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara
Ana mabinti huyu mzee? Nataka nipate hiyo mbegu. Muungwana sana huyu jamaa.
 
Anakaa ofisini miaka sita anatunzwa hadi afe, halafu nesI aliyetumika miaka 45 anaambulia kiko kotoo
Maisha ni uchaguzi, Nesi angechagua kuwa Mjeda labda naye bahati ingempata
 
..magaidi wameingia eneo la serikali wakajaribu kuua mbunge. Na wameondoka bila kuguswa.

..magaidi wamelipua ofisi za mwanasheria karibu na makao makuu ya jeshi. Na hawakukabiliwa na askari yeyote.

..tungekuwa na jeshi imara hayo yasingetokea.

..nchi hii inalindwa na MUNGU.
Umenena vyema kabisa, nchi hii tunalindwa na Mungu tu..sidhani kama dhana na malengo ya kuanzishwa JWTZ yanatekelezwa kikamilifu, ni kama JWTZ imeungana na wanasiasa kuweka matabaka kwenye Jamii ya watz..sabab hata jina tu kuitwa JWTZ ilikuwa na maana JW kuwa watetezi wa wananchi bila kujali adui anatoka nje ya mipaka ya nchi au ndani ya mipaka ya nchi, ni Bahati mbaya sana hapa kwetu..kwa sasa maadui wa wananchi wamo humu humu ndani, lkn hatujawahi kusikia JW wanatutetea dhidi ya ukandamizwaji haki na uhuru wa wananchi, demokrasia nk, JW nao wamekuwa wanafanya kazi km ya polisi..kulinda watawala, nidhamu pia imeshuka..mimi ningependa kuona JW wanasimama na wananchi 100% wasikubali hongo ya vyeo baada ya kustaafu au hata nyongeza ya mishahara kwao tofauti na watumishi wengine, ningependa kuona JW wakiweka kambi za muda sehemu zote karibu na boarder post zetu..namanga, tunduma, sirari nk hii habari ya kukamata wahabeshi na wasomali katikati ya nchi isingekuwepo tena sasa ndio imezidi..ningependa kuona JW wanakuwa na program za kuweka kambi za kutembea, mobile camping vijijini na kushiriki kazi za maendeleo kuonyesha kwa vitendo wao ni jeshi la wananchi kweli..
Ndio maana tunataka katiba mpya ili JW irudi kwa wananchi kwa vitendo..Mungu yupo ipo siku!
 
..tukiweza kubadilisha Maraisi bila vurugu.

..tukiweza kubadilisha majority bungeni bila vurugu.

..kwangu mimi hizo ndizo "LITMUS TEST" za demokrasia yetu kuwa imekomaa.

Kuwa na mapenzi na chama fulani cha kisiasa ni kitu kimoja na kuwa na mpango wa baadaye wa kugombea nafasi ya kisiasa kwa ticket ya chama hicho ni kitu kingine.

Kumzuia retired soldier au judge/magistrate kugombea nafasi ya kisiasa hakusaidii chochote. Wapo wenye mapenzi na chama fulani cha kisiasa na wako tayari kukipendelea ingawa hawana mpango wowote wa baadaye wao kugombea nafasi za kisiasa kwa ticket ya chama hicho. Kama ni shida hao bado wataendelea kuwa shida, kwa sababu ya mapenzi waliyonayo kwa chama!
 
kweli umehudumia taifa kwa kiwango Cha kutukuka nenda tu kajipumzikie huko mashambani ukalime na kufuga mifugo Ila nikikuangalia usoni nabaki natoa machozi.
images (1).jpeg
 
Mkuu hata ingekuwa wewe lazima hali hiyo ikukute, unapaswa kuelewa mzazi na mlezi ni watu wawili tofauti kabisa!.
 
Back
Top Bottom