Jengo Maarufu Zanzibar kwa utalii, Beit Al Ajaib laporomoka

Jengo Maarufu Zanzibar kwa utalii, Beit Al Ajaib laporomoka

hebu nitajie umri wa hili jengo kesha tuone kama limekuwa historia au ni la miaka mi2 kama unavohisi majengo ya warabu sio imara🐸🐸
1883.Ukienda Rome kuna majengo ya 14.....na yapo imara. Sema hufanyiwa renovation pia.
 
Lilikuwa likifanyiwa ukarabati.

Nilikuwa naenda kuangalia movies Zanzibar International Film Festival hapo.

Inasemekana Sultani alivyolijenga, kuna nguzo fulani katikati aliweka maiti za watumwa.
Sasa ni wakati muafaka wachimbue hizo maati zilizo daiwa kufukiwa chini ya nguzo ikiwa zimesimama paoja na nguzo hizo.
Waletwe wataalamu wa mabaki ya binadau ili wachunguze tuhuma hizo, na zikithibiti basi Jamshi,aliyekuwa mtawala wa Mwishowa Zanzibar kama sultani bado yuko hai Oman awajibike.
 
Jengo hili lilikua ndio sura ya mji Mkongwe Zanzibar na kivutio Kiki kikubwa cha utaliii, lakini serekali imeshindwa kulitunza.

Serekali ya Oman [emoji1190] ilikua tayari kulikarabati lakini inaonekana wamefanyiwa urasimu na watendaji wenye tamaa.

===

Jengo la Beit al Ajaib lilijengwa na sultan wa pili wa Zanzibar, Barghash bin Said mwaka 1883 likilengwa kuwa jengo la kasri la sherehe na sehemu maalum ya mapokezi kwa wageni

Liliitwa Jumba la Ajabu, kwa kiarabu Beit Al Ajaib kwa kuwa lilikuwa ni jengo la kwanza kuwa na umeme Zanzibar, la kwanza Afrika Mashariki kwa kuwa na 'elevator'

Jengo hilo limeonekana kuporomoka, Leo Desemba 25, Mtu mmoja ameokolewa katika tukio hiloView attachment 1658939View attachment 1658933View attachment 1658934View attachment 1658935View attachment 1658936View attachment 1658937
Ivi hilo limeporomoka lenyewe au limebomolewa ? Huo uzio Wa mabati ni wa nini ? Wakati hua hua kuna fence ya kwaida tu
 
Sasa ni wakati muafaka wachimbue hizo maati zilizo daiwa kufukiwa chini ya nguzo ikiwa zimesimama paoja na nguzo hizo.
Waletwe wataalamu wa mabaki ya binadau ili wachunguze tuhuma hizo, na zikithibiti basi Jamshi,aliyekuwa mtawala wa Mwishowa Zanzibar kama sultani bado yuko hai Oman awajibike.
Awajibike kwa jengo lililojengwa kabla hajazaliwa?
 
Tabu ya waswahili.Sultan wa Oman atatuma watu waje kujenga kumbukumbu ya babu zake.
Kwani wewe babu zako wana kumbu kumbu gani zaidi ya vyungu vya udongo na vibanda vya msonge?
sasa wenzio angalau walijenga Ghorofa ya Miti ,udongo na mawe kwa kuitelekeza juu ya Nguzo za Vyuma .Takriban miaka 150 iliyopita ,lazima wajipongeze na kutunza utaalamu wao kwa zama hizo.
 
Sasa ni wakati muafaka wachimbue hizo maati zilizo daiwa kufukiwa chini ya nguzo ikiwa zimesimama paoja na nguzo hizo.
Waletwe wataalamu wa mabaki ya binadau ili wachunguze tuhuma hizo, na zikithibiti basi Jamshi,aliyekuwa mtawala wa Mwishowa Zanzibar kama sultani bado yuko hai Oman awajibike.
Hizo zilikuwa ni mbinu za kuwaaminisha watu kuwa waarab ni wabaya.
Jemshid ana miaka zaidi ya 90 na ni mzima wa afya na anatembea kwa miguu yake miwili tena bila mkongojo.
IMG_20201225_162747.jpg
 
Ubaya wa hao watu wanaoitwa Waarabu hauhitaji concept hii.

Biashara ya utumwa tu inatosha kuuonesha ubaya wao.
Mmiliki wa soko la watumwa alikuwa ni mwingereza mwenyewe. Nenda Kanisa la Mkunazini kasome historia.
 
Kwa hivyo Muarabu hajafanya biashara ya watumwa Zanzibar?

Biashara ya watumwa Africa Mashariki kwenda Arabuni ilianza lini? Muingereza alifika lini? Muarabu alifika lini?

Nani aliipiga marufuku?
Umembana kila kona hawezi chomoka hapo....
 
Ila kwa huo uzio wa mabati inamaanisha lilikuwa likifanyiwa ukarabati?
Ulikuwa babaisha toto tu huo uzio. tangu 2012 hadi leo hii ukarabati gani wanaofanya? Nikipita hayo maeneo sikuwa nikiona shughuli zozote za ukarabati zikiendelea. Baniani mbaya kiatu chake dawa, wamiliki halali wa hilo naskia wametoa pesa nyingi wametoa ili jengo walikarabati kwa faida ya SMZ wenyewe kuvutia watalii lakini waaapi!!! Kwenye safu ya uongozi akiwepo mtu anaitwa Balozi Seif Ali Iddi lazima hela zisionekane zimeenda wap 😀

Wanajenga mahakama mpya, tangu kiwanja kitupu mpaka jengo lishakuwa na sura tena, hili la foro hata nguzo moja wameshindwa kuimaliza. Na hio mahakama mpya imeanza kujengwa mwaka huu tu. Serikali ilioacha kiti kwa Mwinyi wamejua kuifisidi nchi!

Nasubiri nione kama kuna mafuvu ya watu kwenye zile nguzo, maana wanamapinduzi walisema nguzo za lile jengo zilijengwa kwa mafuvu ya watumwa 😀
 
Sasa ni wakati muafaka wachimbue hizo maati zilizo daiwa kufukiwa chini ya nguzo ikiwa zimesimama paoja na nguzo hizo.
Waletwe wataalamu wa mabaki ya binadau ili wachunguze tuhuma hizo, na zikithibiti basi Jamshi,aliyekuwa mtawala wa Mwishowa Zanzibar kama sultani bado yuko hai Oman awajibike.
Wanamapinduzi nilisikia wanasema kila nguzo ina mafuvu ya watumwa. Ni muda muafaka sasa yatafutwe, wataalamu waje wafanye utafiti wanaweza kutwambia walikuwa watu gani/wa wapi n.k

Hata Bungi miembe mingi walisema kila kwenye muembe kuna mafuvu ya watumwa.... miembe inakatika lakini bado fuvu halijapatikana.
 
Back
Top Bottom