Jeshi la Israeli limechukua udhibiti wa kilele cha Mlima Hermoni upande wa Syria bila pingamizi, eneo la kimkakati linalotazama Lebanon na Syria

G Tank

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2023
Posts
2,297
Reaction score
8,760
Ni eneo la kimakati lililowaumiza Israel vichwa kwa muda mrefu, kilele cha mlima Hermon kiliwapa advantage kubwa Syria na Hezbollah kuichunguza na kuishambulia Israel.

Israel imetwaa eneo hili bila pingamizi katika kile kinachodhaniwa "hakuna kitu cha Bure", Israel waliweza kutoa msaada mkubwa wa kudhoofisha majeshi ya Assad kwa kufanya mashambulizi ya anga kwenye kambi za Assad, msaada huu umechangia pakubwa waasi kuitwaa nchi, hivyo wamewapa eneo hili la kimkakati kama "Asante"

Faida kwa Israel kuchukua udhibiti wa kilele cha Mlima Hermon

Kupata udhibiti wa Mlima Hermon kunatoa nafasi ya kutuma mashambulizi kwa urahisi dhidi ya maadui walioko chini, kwani mlima ni sehemu ya kimkakati ya kijeshi.

Kilele cha Mlima Hermon ni mahali pa juu kabisa, kinachowezesha Israeli kufuatilia harakati za kijeshi za Syria na Hezbollah kutoka mbali.

Kuwa juu ya mlima kunatoa faida ya kuzuia mashambulizi kutoka kwa maadui hasa wakati wa usiku na ni vigumu kwa adui kushambulia Israeli moja kwa moja bila kutambuliwa.

Udhibiti wa kilele hiki unaruhusu Israel kufuatilia harakati za maadui na kukusanya taarifa muhimu za kiintelejensia

kilele cha Mlima huu mrefu katika nchi zote tatu ni eneo lenye ufanisi mkubwa wa rada, Israel ina uwezo wa kuchunguza anga ya majirani zao

Milima ya Hermon ni njia muhimu ya usafirishaji wa silaha kati ya Syria na Hezbollah. Udhibiti wa Israel utaifanya kuwa vigumu kwa wapinzani kutumia njia hiyo.


 
na hawatarudisha ng'oooo. imeisha hiyo. MLima hermoni hata hivyo ni mali ya mzayuni tangu enzi, basi tu alikuwa hajachukua chake.
 
Ndiyo umeandikwa kwenye biblia kama eneo la Israel zaidi ya mara kumi.....soma 1 Mambo ya Nyakati 5:23 (KJV) Na wana wa nusu-kabila ya Manase walikaa katika nchi; nao wakaongezeka kutoka Bashani mpaka Baal-hermoni, na Seniri, na mlima Hermoni.
 
 
Ndiyo umeandikwa kwenye biblia kama eneo la Israel zaidi ya mara kumi.....soma 1 Mambo ya Nyakati 5:23 (KJV) Na wana wa nusu-kabila ya Manase walikaa katika nchi; nao wakaongezeka kutoka Bashani mpaka Baal-hermoni, na Seniri, na mlima Hermoni.
Safi sana mkuu barikiwa Sana Kwa reference
 
Ndiyo umeandikwa kwenye biblia kama eneo la Israel zaidi ya mara kumi.....soma 1 Mambo ya Nyakati 5:23 (KJV) Na wana wa nusu-kabila ya Manase walikaa katika nchi; nao wakaongezeka kutoka Bashani mpaka Baal-hermoni, na Seniri, na mlima Hermoni.
Kumbe wamechukua kilicho chao. Safi sana Bani Israili.
 
Huu si ndio ule mlima Isaka mwana wa baba wa imani Ibrahim alitolewa wakfu na ahadi ya milele kati ya Muumba na kizazi cha Baba wa Imani? Ni haki yao kulitwaa.
Kumbe kuna historia ndefu hapo mlimani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…