Jeshi la Polisi lapewa siku 90 kuhakikisha mitambo ya LUGUMI inafanya kazi vituo vyote

Jeshi la Polisi lapewa siku 90 kuhakikisha mitambo ya LUGUMI inafanya kazi vituo vyote

Ni kitu cha kustaajabisha sana Mkuu. Ilikuwa ni ufisadi tu hivyo wakatunga vituo 14 kati ya 108. Wakaingia mitini kwenda kutafuna mabilioni yao. Baada ya ripoti ya CAG ndiyo wakaenda kununua mashine nyingine mwaka huu ili kuchakachua ripoti ya CAG. Magufuli ni janga kubwa la Taifa.
Lugumi kafanya ufisadi kwanini analindwa na serikali/bunge? katuibia fedha zetu hiyo kampuni.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mkuu bila shaka hii hela aliyopiga aligawa mpaka Ikulu na ndani ya chama cha mafisadi hivyo ni lazima wamlinde na kuwalinda wahusika wote kwa gharama yoyote ile.

Imefikia mahali ripoti ya CAG hawa wahuni wa MACCM wanaichakachua ili tu kulinda ufisadi wao. Bilioni 37 zilizofisadiwa na Lugumi na mafisadi ndani ya Serikali na MACCM ni juu kidogo ya bajeti ya mwaka mzima waliyompa CAG 2016/2017 ya bilioni 32.

Lugumi kafanya ufisadi kwanini analindwa na serikali/bunge? katuibia fedha zetu hiyo kampuni.
 
Bilioni 37 kununua computers/machine 114 Za kutambua alama za vidole? Hizo hela zinazidi thamani ya kazi yenyewe
 
eti tuchangie madawati, wakati akina lugumi wanapeta, hii haikubaliki duniani mpaka mbinguni, kuanzia Leo nafunga na kuomba ili mungu wetu aliye hai. aidhibu hii serikali dhalimu, fisadi,
 
"Wazee wangu msijali,nitawalinda kwa nguvu zangu zote" Angeguswa Lugumi, tungewaona wahusika wenyewe wa huo mradi.
 
Ni baada ya Kamati ya Bunge iliyopewa kazi ya kufuatilia Sakata la Lugumi kuthibitisha kuwa vifaa mashine hizo zimefungwa katika vituo vyote.

Agizo hilo limetolewa na Bunge kupitia kwa Naibu Spika, Dr. Tulia Ackson wakati akiahirisha Bunge la 11 leo mjini Dodoma
==========



Habari wakuu,

Leo akihitimisha bunge, naibu spika ametolea ufafanuzi utekelezaji wa mfumo wa kielektroniki wa utambuzi wa alama za vidole(AFIS), hoja iliyojengwa kutokana na mkaguzi wa hesabu za serikali(CAG) kwa kutokamilika kwa mradi huo.

Agizo la bunge lilimtaka afisa masuhuli wa jeshi la polisi kuhakikisha mfumo wa AFIS unafanya kazi ndani ya kipindi cha miezi sita. Ripoti ilieleza mfumo wa AFIS ulikuwa unafanya kazi katika vituo 14 pekee kati ya vituo 108 hivyo agizo la kamati halikuwa limetekelezwa kikamilifu.

Spika ametoa agizo kwa serikali kuhakikisha mfumo huo unafanya kazi ndani ya miezi mitatu ili kuboresha uwezo wa jeshi la polisi kuwa na utambuzi wa haraka wa wahusika wa matukio ya kihalifu katika vituo vyote nchini. Pili masuala yote yaliyobainika kuwa na dosari za kiutendaji yapatiwe ufumbuzi haraka.

Spika anatarajia sasa suala hilo litafikia mwisho na mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali atafunga hoja yake baada ya kujiridhisha na utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa.

Mtoa mada lete mada nyingine hii mkuru alisema atawalinda tu kwanza anashangaa watu wanaongea hovyo mkwere na familia yke washitakiwe
 
Lugumi

Name: Said Hamad Lugumi



DoB: 1972

Place of birth: Magu, Tanzania

Nationality: Tanzanian

Company: MESSRS Lugumi


Key business associates:

1. Ridhiwani Kikwete (Tanzanian lawyer, Member of Parliament in the Tanzania’s national parliament and son to the 4th President of Tanzania)

2. Said Mwema (former Tanzania’s Inspector General of Police who is also Said Lugumi‘s father in-law)


Business channels:

1. Forensics
2. ICT
3. Corporate Printing
4. Drug trafficking (unconfirmed)


Background

Said Lugumi was born in Magu, Mwanza Tanzania in 1972. He was born from Christian parents but later converted to Islam. He was never educated beyond Tanzania’s Primary School System which is a 7 years elementary education. As a young man he grew up as a shoeshiner in Mwanza and later made his way to Dar es Salaam (Tanzania’s main commercial capital) in early 1990s. In Dar es Salaam, Said Lugumi lived in a couple of third class suburbs including Mwananyala area going on with his earlier “profession” (shoe shinning).

A lucky man

Through lucky, Said Lugumi met Said Mwema’s daughter and the two fell in love and eventually married. With influential inlaws Said Lugumi was led to establish Lugumi Enterprises initially dealing with corporate printing and fumigation and later diversified to forensics and ICT. Pictured, Air Tanzania House Dar es Salaam city centre where MESSRS Lugumi offices are located.



Lugumi Enterprises

Is a forensics and ict company famous for huge annd shoddy deals in Tanzania and now crossing to other East African countries. The key clients are government institutions including the Tanzania Police Force which until recently was under Said Lugumi‘s father inlaw – Said Mwema.

Unlike other suppliers to the government, Lugumi Enterprises payments aren’t delayed and are cleared within days or few weeks of any business. This has been a controversial issue and widely discussed within Tanzania’s most famous political forum, The Jamii Forums. Pictured, KZ Security, a new MESSRS Lugumi subsidiary.


Key shareholders in this firm are Said Lugumi, Said Mwema and Ridhiwani Kikwete.
The company has been one of the key symbols of corruption in Tanzania’s government under President Kikwete and a symbol of law enforcement willingness from the Tanzania’s government. (A list of businesses between the company and government institutions like the Police Force shows a clear violations of Public Procurement Procedures)


Said Lugumi has also been rumoured to take part in drug trafficking allegations that are putting him in close scrutiny by the US Department of State and other international law enforcement agencies. In Dar es Salaam he’s known for his lavish lifestyle, sexual scandals with hundreds of women among other controversies. Pictured, company officials donating equipment to schools in their struggle in CSR. A new strategy by another MESSRS Lugumi subsidiary RAN IT to harness new markets.


International affiliations

Where Lugumi Enterprises stands today brings a lot of “fear” on it’s future in business within and outside Tanzania. It’s shaky reputation will soon chase away international partners and it’s illegal patronage from the current Tanzania government is coming to an end as President Kikwete’s second term ends in November 2015.
Some of it’s international partners are Jino Motors, Foster & Freeman and Bio Metrica. It’s now in the hands of these reputable international firms and other players in forensics and ict who are interested on investing in Tanzania and East Africa to rethink if this is a company that they would like to partner with.
 
Siku zote husema na ninaamini kuwa serikali yetu ipo juu ya sheria, issue ya sugu, sijui anatrophia haraka haraka majibu wametoa hii ya lugumi tukaambiwa bunge lijalo leo naibu speaker anakuja na mpya, huu utumbuaji naona ni isidingo, hapo issue hii ya lugumi ndo ishapotezewa na atakayehoji kama kawaida pigwa lock up, duu aisee
 
13592253_523763481167402_2098519877267425107_n.jpg
 
Kwa maana Nyingine Ufisadi Unafagiliwa Uvunguni, Na serikali ya Magufuli, ambayo Ufuatiliaji wa Uhalifu, Ni kwa wale wanaomkosoa Magufuli, Lakini Wanaoiba Mabilioni, Wanaambiwa Wekeni Mambo sawa! Magufuli aliyemdhalilisha Maya wa Jiji Kuwa ati anapenda Ujambazi, kwa Kukosa Kuwepo kwenye ghafla ambayo hakualikwa, Magufuli huyu akimtumia stooge wake Tulia Ackson wanataka Kufagilia Kashfa ya Lugumi Uvunguni, (Sweep under the bed) Magufuli Huyu aliyempa Uwaziri Pr. Muhongo, Nikuulize Magufuli Kama Ulivyouliza Swali la Kebehi kwa Maya wa Dar. Je wewe Magufuli Unapenda Ufisadi?
 
Double standards ya kimataifa, hongera Lugumi, wewe Ni don, mtoto wa mjini.
Acha wavimba macho tuendelee kutoka mapovu.
Hapa kazi Tu.......
Tanzania, like nowhere in the world
 
Mkuu usitegemee jipya kutoka Bunge Haramu la MACCM.

Alaf hao wanaopewa miezi mitatu vifaa vifanye kazi ndio wanaotakiwa wasimamie sheria zitekelezwe na wananchi, watoa maamuzi ndio hao wanaokimbizana na vikesi mara sijui majipu kwa vitu hata vizivyo na msingi. Kwa hili la Lugumi...nimeishiwa maneno mkuu.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Ni uozo wa hali juu. Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali anafanya kazi yake ya kukagua hesabu mbali mbali za taasisi za Serikali na kugundua ufisadi mkubwa sana wa shilingi bilioni 37. Halafu huyu jipu Tulia akishirikiana na Serikali dhalimu wanachakachua kazi ya CAG na kudai mashine zimefungwa katika vituo vyote 108 wakati CAG aligundua ni vituo 14 tu.

Ufisadi hautaisha Tanzania.
BAK soma hii

Utetezi wa Polisi sakata la Lugumi huu hapa

CAG ajiuzulu maana inaonekana kasema 'uongo'
Tenda ilitangazwa lini? Mzabuni alipataikanaje?

Miaka 3 mzabuni kalipwa 99%.
Kazi haijafanyika kwa mujibu wa Naibu Spika

a) Hao waliozemebea ni akina nani na wamechukuliwa hatua gani?

b)Pesa za kukamilisha zitatoka fungu gani,mzabuni keshamaliza kazi na kulipwa 99%

c)Kulikuwa na haja gani ya kuunda kamati kuchunguza kazi ambazo zipo chini ya wizara?

d)Kwanini taarifa haikujadiliwa na bunge?

e) Kulikuwa na sababu gani za kutupiana mpira ikiwa vituo vilikamilika?

f)Gazeti la Nipashe 22 April lilitoa taarifa ya Polisi ikisema vilivyofungwa ni 14 kati ya 108.
Gazeti kama lilisema uongo kwanini halichukuliwi hatua?

g) Kazi ya miaka 3 inakwishaje kwa miezi 3 na nini kilikwamisha

Tuliwambia danadana ilikuwa na mambo, mkadhani sisi ni wendawazimu

Hii ni kawaida ya CCM, na CCM ni ile ile. Huwezi kuzaa mtoto akakua na kubalehe kwa mila za Kingoni ukidhani siku moja atakuwa na mila za kibondei.

Lugumi kwisha, tuendelee kutumbua majipu na sasa mahakama ya mafisadi

Taarifa ya CAG inasema jambo moja

Taarifa ya Polisi (kwa mujibu wa gazeti hapo juu) inasema jingine

Taarifa ya Naibu Spika inazungumzia tukio tofauti kabisa

Hoja ni moja Lugumi, taarifa zinakinzana

CAG ajiuzulu maana katika hili sijui kama ana la kusema tena

''Yaliyopita si ndwele tugange yajayo''

Taratibu watatuelewa

The Boss Mag3 Nyani Ngabu BAK MsemajiUkweli Ngongo
 
Bunge uchwara +Serikali Uchwra= uchwara uchwara uchwara tu.😡😡😡
 
wakuu ninaomba tuwe na mjadala mpana kwenye jambo hili kwa maslahi ya taifa letu.

Nimesikiliza Video ya Naibu spika kwa Umakini mkubwa akihitimisha Sakata la Lugumi kuhusu mkataba wake tata na jeshi la polisi.

pamoja na mambo mengine niliyoyabaini kwenye mradi huo, lakini vile vile taarifa aliyoisoma spika bungeni inaonyesha kuipelekea lawama serikali na jeshi la polisi kwa kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo ilhali LUGUMI kwa upande wake tayari amekamilisha ufungwaji wa vifaa alivyoagizwa na mkataba.

nimeichambua kwa kifupi kama alivyokuwa anaisoma mheshimiwa Tulia Mwansasu naibu spika wa bunge hapo jana tarehe 30.06.2016.
hii hapa
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------

SAKATA LA LUGUMI

TAARIFA YA SPIKA KWA UFUPI.


- 23 April 2016, PAC iliomba Kuunda kamati ndogo kwa mujibu wa Kanuni ya 117 fasili 18 ili kufuatilia utekelezaji wa Agizo la PAC la bunge la 10 lililotolewa tarehe 23.10.2014 kwa Jeshi la Polisi Kuhusu utekelezaji wa Mradi wa kielektroniki wa utambuzi wa alama za vidole AFPIS


- Msingi wa Agizo ni Ripoti ya CAG 2012/2013 kutokana na kutokukamilika na kutokufanya kazi ipasavyo kwa mradi huo.


- Kazi ya Mradi huo ilikuwa ni kati ya Jeshi la Polisi na Kampuni ya LUGUMI ENTERPRISES LIMITED.

- Polisi waliagizwa Mitambo ifanye kazi ndani ya miezi sita.

--CAG aliripoti tena utekelezaji kuwa AFPIS inafanya kazi katika vituo 14 tu kati ya vituo 108

- Kamati ilimtaka katibu mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani alete taarifa ya utekelezaji. Katibu mkuu taarifa yake ikaonyesha mitambo imefungwa vituo 153 pamoja na makao makuu ya polisi tofauti na taarifa ya CAG ilivyosema.



- Kamati ikaomba kuhakiki kujiridhisha na kujionea, na kamati ndogo ikaundwa kuhakiki.


HADIDU REJEAkamati ifanye uhakiki iwapo Vifaa vilinunuliwa na kufungwa

- kamati imemaliza kazi yake, Imeiwasilisha PAC na PAC imeijadili na kuikabidhi kwa Spika kama Kanuni zinavyotaka.


MATOKEO YA TAARIFA YA KAMATI

i. Kamati imejiridhisha kwamba VIFAA VIPO Vituo vyote 153 na makao makuu ukiacha kasoro zilizojitokeza.



ii. Kilichobaki ni vifaa hivyo kufanya kazi


v Nimekabidhi matokeo (maoni, Ushauri na mapendekezo) yote ya kamati kwa serikali

AGIZO

i. Serikali ihakikishe mfumo huu unafanya kazi ndani ya Miezi mitatu kutoka leo hii ili kuboresha uwezo wa jeshi la polisi.


ii. Maswala yote yaliyobainika kuwa na dosari za kiutendaji yapatiwe ufumbuzi haraka.



iii. PAC ihakikimaelekezo niliyoyatoa na baada ya uhakikikamati itoe taarifa bungeni wakati wa uwasilishaji wa taarifa yake ya mwaka.


iv. Ninatarajia sasa swala hili litafika mwisho na CAG atafunga hoja yake baada ya kujiridhisha utekelezaji wa maagizo niliyoyatoa.
 
Back
Top Bottom