Jeshi la polisi limebariki huu wizi Kariakoo?

Jeshi la polisi limebariki huu wizi Kariakoo?

Habari wana JF,

Kuna huu wizi sijui niite utapeli ambao binafsi nimeanza kuushuhudia tangu mwaka 2022 kwa maeneo ya Kariakoo na kila mara nikipita eneo hilo nakuta huo wizi unaendelea utapeli wenyewe unafanywa na jamaa wauza juice ya miwa mitaa ya karume mbele ya TBL (Tanzania Breweries Limited)

Wizi unafanyika kama ifuatavyo:
Muuza juice atakuita na kujifanya amekufananisha kisha atakuuliza ''Vipi mzee daah kitambo sana mwanangu, vipi siku hizi wapi?''

Wewe utajibu labda nipo Magomeni siku hizi.

Muuza juice: Anhaa ndiyo maana kule kitaa sikuoni siku hizi.

Wewe: Wapi? Kule kitunda au?

Basi hapo ndo utakuwa umeyavagaa jamaa atajifanya kukujua sana atakuuliza kuhusu story za vipi wale jamaa wanaopiga matizi uwanjani pale bado wapo?

Actually hakuna sehemu ambayo haina uwanja wa mpira so yote kwa yote jamaa atakuwa amekuteka akili kwa kujifanya anakujua sema ni vile tu umemsahau

Kinachofuatia jamaa atakumiminia juice " karibu juice kaka".

Ukimaliza kunywa tu hiyo juice jamaa anakubadilikia na kuanza kukudai hela ya Juice.

ukishindwa kulipa atakukaba, atakupiga hata kukuumiza.

Wahanga wakubwa wa haya matukio ni wale wa kuja lakini hata kama born town unaweza kujikuta umeingia mkenge vile vile

Kinachonifikirisha ni kuwa Kituo cha polisi Gerezani hakipo mbali na hapo Karume na pia maeneo ya China Plaza, hawa jamaa hawajanusa taarifa za huu ushenzi kweli? Au kuna mgawo, maana hawa jamaa wanafanya hii michezo kuanzia asubuhi hadi jioni tangu 2022 nimewaona hadi leo 2024 wapo.

Picha mojawapo ya mhuhusika wa hiyo michezo ni hiyo hapo huyo muuza juice na hapo alikuwa anamuingiza mkenge jamaa.

Niliwahi kusimamishwa na jamaa hapo Karume akafanya kunipigisha stori kama ulivyosema. Hadi leo nilichokuwa najua ni kwamba alikuwa anatafuta namna ya kumpa sapoti katika biashara yake na nilijua wazi hanifahamu wala simfahamu ila ni mbinu tu ya kutafuta mteja. Hilo la kukaba ndio nalijua sasa hivi, na sikuwahi kuwaza kama kuna element za utapeli
 
mnaomaindi mimi kuleta hii hoja kwahiyo mnaona hili suala ni sawa au?yaan hamuoni kama ni tatizo?
 
Marehemu Zacharia na utajiri wake wote lakini alikuwa kila siku kabla hajaingia msikitini anakunywa juice ya kwenye madeli pale msikitini kitumbini nendeni mkaulize hata leo hii hayupo lakini mtaambiwa , sembuse watu wengine wa kawaida ??
huku mitandaoni bhana kila mtu anakunywa Juice Mac juice tu na misosi ya samaki samaki mlimani city,safi sana wakuu
 
Mwendo wangu nikiwa natembea aisee mpka awaze kunisimamisha tyr nishamaliza kilometer 3.
 
usisimame barabarani kwa kuitwa na mtu usiemjua, akikuita itikia ongea nae huku unatembea usimpe nafasi ya kusimama hata kama ni mlemavu
 
Habari wana JF,

Kuna huu wizi sijui niite utapeli ambao binafsi nimeanza kuushuhudia tangu mwaka 2022 kwa maeneo ya Kariakoo na kila mara nikipita eneo hilo nakuta huo wizi unaendelea utapeli wenyewe unafanywa na jamaa wauza juice ya miwa mitaa ya karume mbele ya TBL (Tanzania Breweries Limited)

Wizi unafanyika kama ifuatavyo:
Muuza juice atakuita na kujifanya amekufananisha kisha atakuuliza ''Vipi mzee daah kitambo sana mwanangu, vipi siku hizi wapi?''

Wewe utajibu labda nipo Magomeni siku hizi.

Muuza juice: Anhaa ndiyo maana kule kitaa sikuoni siku hizi.

Wewe: Wapi? Kule kitunda au?

Basi hapo ndo utakuwa umeyavagaa jamaa atajifanya kukujua sana atakuuliza kuhusu story za vipi wale jamaa wanaopiga matizi uwanjani pale bado wapo?

Actually hakuna sehemu ambayo haina uwanja wa mpira so yote kwa yote jamaa atakuwa amekuteka akili kwa kujifanya anakujua sema ni vile tu umemsahau

Kinachofuatia jamaa atakumiminia juice " karibu juice kaka".

Ukimaliza kunywa tu hiyo juice jamaa anakubadilikia na kuanza kukudai hela ya Juice.

ukishindwa kulipa atakukaba, atakupiga hata kukuumiza.

Wahanga wakubwa wa haya matukio ni wale wa kuja lakini hata kama born town unaweza kujikuta umeingia mkenge vile vile

Kinachonifikirisha ni kuwa Kituo cha polisi Gerezani hakipo mbali na hapo Karume na pia maeneo ya China Plaza, hawa jamaa hawajanusa taarifa za huu ushenzi kweli? Au kuna mgawo, maana hawa jamaa wanafanya hii michezo kuanzia asubuhi hadi jioni tangu 2022 nimewaona hadi leo 2024 wapo.

Picha mojawapo ya mhuhusika wa hiyo michezo ni hiyo hapo huyo muuza juice na hapo alikuwa anamuingiza mkenge jamaa.

Hapo polisi asilaumiwe kama wewe unajua kabisa huyu kiumbe sijawahi kuonana naye ananizuga ilistory ziende wewe nawe unaenda hvyohvyo kwanini unywe juice yake? hyo nitamaa yako imekuponza, yupo kazini anatafuta pesa nahyo ndio ameona njia yake yake ya haraka kuuza juice. Huyo jamaa ataakipelekwa mahakamani hakuna sheria yakumtia hatiani. Ni ufala wako na tamaa zako ndio zitakuwa imekuponza.
 
Hapo polisi asilaumiwe kama wewe unajua kabisa huyu kiumbe sijawahi kuonana naye ananizuga ilistory ziende wewe nawe unaenda hvyohvyo kwanini unywe juice yake? hyo nitamaa yako imekuponza, yupo kazini anatafuta pesa nahyo ndio ameona njia yake yake ya haraka kuuza juice. Huyo jamaa ataakipelekwa mahakamani hakuna sheria yakumtia hatiani. Ni ufala wako na tamaa zako ndio zitakuwa imekuponza.
kwa hiyo hawa jamaa hawana kosa au vipi
 
Kila jambo mnataka mamlaka ziwasaidie like B.O.T wakat pesa ulienda kopa mwenyewe,sijui polisi wakat ulisimama mwenyewe na kuongea na mtu usijemjua na juice unapokea...nk kichwan humo hamna ubongo wa kupambanua mambo white ni ipi na black ni ipi...

Endeleeni subiria wengine watatue matatizo yenu wakat na wao Wana matatizo Yao.
 
Back
Top Bottom