Jeshi la Polisi: Madai ya Makonda kuuawa, kama yupo ‘siriasi’ aende Polisi

Jeshi la Polisi: Madai ya Makonda kuuawa, kama yupo ‘siriasi’ aende Polisi

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Muda mfupi baada ya RC wa zamani wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuandika mtandaoni kuwa kuna makundi matano yanamuwinda ili kumuua, Jeshi la Polisi limesema kama kweli ana hofu anatakiwa aende kutoa taarifa Kituo cha Polisi.

Akizungumza na Kipindi cha Jahazi cha Clouds FM, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema: “Raia yeyote wa nchi hii ana haki ya kutoa taarifa Polisi kama ni kweli na ni jambo ‘serious’.

“Mimi sijaliona hilo tamko lake, najua watu ambao wapo serious wanaenda Polisi. Siwezi kushauri kuhusu hilo, watu unaowaongelewa wana weledi, wanajua taratibu, na ninajua wanajua, kwanza siamini, wana maarifa ya kutosha.

“Hao watu unaowazungumzia wana maarifa ya kutosha kujua wafanye nini, kama hana imani basi ofisi za Serikali zingefungwa, kama watu wanakwenda afu wewe unasema huna imani, mtu mmoja akisema hana imani lakini robo tatu wakienda na kupata huduma nani tumfuate hapo,” Muliro.


Source: CLOUDS FM

Pia soma:

Paul Makonda: Kuna makundi matano yanataka kuniua, likiwemo wanaotafuta kulipa kisasi kwa Wasaidizi wa Magufuli
 
yale madarubini yameishia wapi? unaambiwa muombee adui yako aishi siku nyingi

unammaliza adui yako ili unufaike zaidi kumbe ndo anguko lako linapoanzia aianze sasa hiyo safari ya kukesha kujitetea inst si atukumbuki hata kitu kimoja alichofanya kwasababu alifanya kwakutafuta kujionesha kwa umma ila ndani ni chui.
 
Muda mfupi baada ya RC wa zamani wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuandika mtandaoni kuwa kuna makundi matano yanamuwinda ili kumuua, Jeshi la Polisi limesema kama kweli ana hofu anatakiwa aende kutoa taarifa Kituo cha Polis...
Majuzi tu hapa kawasagia kunguni police wachunguzwe, leo hawezi kuwaendea. Keshanyea kambi 😀😀😀😀👐👐
 
Muosha huoshwa🤣
images - 2022-04-12T113355.281.jpeg

20220128_221738.jpg
 
Muda mfupi baada ya RC wa zamani wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuandika mtandaoni kuwa kuna makundi matano yanamuwinda ili kumuua, Jeshi la Polisi limesema kama kweli ana hofu anatakiwa aende kutoa taarifa Kituo cha Polisi.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema: “Raia yeyote wa nchi hii ana haki ya kutoa taarifa Polisi kama ni kweli na ni jambo ‘serious’.

“Mimi sijaliona hilo tamko lake, najua watu ambao wapo serious wanaenda Polisi. Siwezi kushauri kuhusu hilo, watu unaowaongelewa wana weledi, wanajua taratibu, na ninajua wanajua, kwanza siamini, wana maarifa ya kutosha.

“Hao watu unaowazungumzia wana maarifa ya kutosha kujua wafanye nini, kama hana imani basi ofisi za Serikali zingefungwa, kama watu wanakwenda afu wewe unasema huna imani, mtu mmoja akisema hana imani lakini robo tatu wakienda na kupata huduma nani tumfuate hapo,” Muliro.


Source: CLOUDS FM

Pia soma:

Paul Makonda: Kuna makundi matano yanataka kuniua, likiwemo wanaotafuta kulipa kisasi kwa Wasaidizi wa Magufuli
Safi sana Jeshi la Polisi halifanyii kazi habari za mitandaoni
 
RC Dar toa amri Makonda aende kituo chochote cha Polisi akareport shida zake asitusumbue....
 
Back
Top Bottom