Jeshi la wananchi laonywa lisivunje katiba ya nchi kwa kufanya majukumu yasiyo yake kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi

Sheria zetu zinasema je?
Kama tumejiwekea sheria kufuata mnapata taabu ya nini
kifungu gani kinamtaka lieutenant aingie kwa mtogole kusaka magwanda ya jeshi?
 
jamaa zangu wa chadema kama mna sare zirudisheni tuh
Hakuna sare ama kesi hapo.

Ukiona nguo inayofanana na nguo ya jeshi usiseme ni "nguo ya jeshi" bali sema "nguo zinazofanana na nguo za...".

Je kitu kufanana ndiyo kuwa ni kitu halisi?

Je mtu anaweza kutiwa hatiani kwa kosa la kufanana, kufananishwa ama kutumia bidhaa zinazofanana na bidhaa zenye "marufuku"?

Tangia day1 yule mwanajeshi alipotoa tangazo hilo kwa waandishi wa habari, tuliosikiliza tuliona ni la vioja!

Tulisema wazi kuwa majeshi ya Tz hayana haki miliki ya nguo wanazovaa, bali huagiza kwa kutumia wazabuni kwa gharama wanazokubaliana.

Na mzabuni huagiza kokote, ndani ama nje ya nchi kwa bei anayoiona itamletea faida.

Pia nguo zinazofanana na za jeshi ni karibu rangi zote za vitambaa vya suti madukani vinashonwa sare za jeshi.

Na tulisema pia maswali muhimu aliyoulizwa afisa huyo hakuweza kuyajibu kwa ufasaha, aliyakwepa au alijiuma uma.

Nilimsikia mwandishi mmoja akiuliza kuhusu wasanii wanaovaa mavazi majukwaani yenye kufanana na "kombati", swali hilo alishindwa kulijibu nadhani hakulitegemea kuulizwa, maana majibu aliyotoa si ya kisheria!

Tuliuliza pia kama kutakuwa na gharama za fidia watakazopewa wafanya biashara wa nguo watakaosalimisha hiyo mitumba na majora ya nguo zenye rangi zinazofanana na rangi wanazotumia wanajeshi.

Wapi walipoandaa centre ama base "afficial"
kusalimishia mabelo hayo?

Suala hili linagusa mpaka uchumi wa nchi likichukuliwa seriously!

Kwa jicho la tatu, tuliona ni tamko la kisiasa kwa sababu lilianza kutolewa pindi Mbowe alipoonekana akihutubia kwenye mkutano kuupiga madongo "mkataba wa bandari", huku nyuma yake kukiwa na mpambe kavaa nguo zinazofanana na za jeshi.

Sasa wanajeshi wameanza fitina na figisu za kisiasa?

Kwa kauli hii jeshi limejidhalilisha sana kwa sababu zifuatazo kama alivyosema wakili:

Hawana mandet ya kufanya wanayotaka kuyafanya bali ni Polisi.

Pia rangi zote za nguo wanazovaa hawana haki miliki zake, iwe za baka baka, ama rangi moja, bali wana haki ya kuvaa nguo hizo kwa kununua kama walivyo na haki raia.

Kama wanahaki hiyo wasimame hadharani waoneshe hakimiliki hiyo ya kumiliki rangi hizo kisheria ili kila raia ama wafanya biashara waelewe namna ya kuepuka kutumia ama kununua rangi ambazo zina hakimiliki ya taasisi za majeshi ya Taifa ama Polisi, Magereza, Zimamoto, Uhamiaji na Migambo.
 
UMEULIZWA JESHI LINA HAKI YA KUPEKUA RAIA MITAANI AU KUKAMATA?
 
Huyo mpuuzi jeshi halifanyi ujinga ukiona hivyo ujue kuna tishio kubwa sana la usalama, na toka matukio ya kibiti Police haiaminiki tena kwenye mambo nyeti, undercover police wasaliti walikuwa wengi sana
Umeambiwa taratibu za kisheria, wewe unaleta porojo
 
Yes umenisanua kitu aiseeh
 
Umeandika kilichomo kichwani kwako , hujajibu hoja
 
Rejesheni nguo zao , kama mnazo.
Sheria zenu zitawaponza
 
Mnaleta utani kwenye ulinzi wa Taifa, acheni upumbavu tutawafuata majumbani uniform za jeshi ni haramu kutumiwa na raia
Hakuna anepinga kua Uniform za Jeshi ni haramu kutumiwa na Raia. Ila kufuata hizo uniform kwa Raia bila kufuata sharia ni haramu pia.

Kila mtu afuate sharia za nchi hii katika kutekeleza majukumu yake ya kila siku.

Hongera sana Mwabukisi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…