Jeshi la wananchi laonywa lisivunje katiba ya nchi kwa kufanya majukumu yasiyo yake kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi

Jeshi la wananchi laonywa lisivunje katiba ya nchi kwa kufanya majukumu yasiyo yake kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi

Watanzania uzuzu wetu umeanzia kuonekana hapa hapa kwenye huu uzi. Yaani kabisa kuna watu wanamdhihaki na kumwona Mwambukusi kama amekosea. Watu kama hao unatarajia kuna siku watakomboka na kuwa huru kifikra???
[emoji2956][emoji2956]
 
Mwambulukusi Hoyeeee. Itisha mkutano na mdudu na slaa kama kawaida yenu, na yule askofu wenu. Mlianzishe na wanajeshi. Hili ndiyo dili. Tutawaunga mkono sisi wote.

Tena mwanzishe na maandamano yao haraka sana.
 
Ni vizuri upitie sheria za jeshi ujue military polisi ana wajibu gani na wakati gani anaweza fanya majukumu yake. Na majukumu yake nipamoja na nini. Natumai uwezi niuliza tena hilo swali!

Jeshi (JWTZ) lipo kwa ajili ya raia. Halipo kwa ajili yake binafsi. Lipo kulinda amani ya nchi na mipaka ya nchi. Sasa ikitokea uniform za jeshi zimeenea mtaani unadhani nini kinafuata?

Nimeishi Ethiopia, uniform za polisi ilitokea zikaenea sana kwa raia. kuna muda ilikuwa ngumu kutambuia polisi halali ni yupi kwa kuangalia. Hii ilileta madhara makubwa ktk amani ya nchi.

Walichelewa kuchukua hatua hivyo ilibidi wabadili mavazi ya jeshi la polisi nchi zima. japo madhara yalikuwa tayari yameisha tokea.

Kazi ya polisi ni maswala ya jinai na si vinginevyo.

Ebu nitajie kifungu cha sheria za jinai kinachoeleza kukutwa na mavazi ya jeshi la wananchi. Hapo ndo utajua kuwa unapokutwa na magwanda ya jeshi ufikishwi mahakamani. Bali magandwa ya JWTZ ni mali yao wanachofanya ni kuyachukua na kurejesha kwao.

Kwa maswala ya amani ya nchi ebu tuache siasa na ushabiki. Waacheni jeshi wafanye zoezi la kurejesha magwanda yao. Na uzuri wameomba watu warejeshe wao wenyewe.

Ila wale wabishi ndo wao jeshi watawafuata majumbani au kokote waliko kuyarejesha. Shida hiko wapi?
Punguza ujinga huko Ethiopia ulikwenda kichunga ng'ombe na huna unachojua! Hata JKT hujaenda utajua vipi kazi za military police!
 
Huyo mpuuzi jeshi halifanyi ujinga ukiona hivyo ujue kuna tishio kubwa sana la usalama, na toka matukio ya kibiti Police haiaminiki tena kwenye mambo nyeti, undercover police wasaliti walikuwa wengi sana
Ya Kibiti yalishadhibitiwa vyema na jeshi letu adhimu....ile ilikuwa ni kazi yao sahihi na kutukuka....

Hili la sare ni kazi ya PT....ni kazi yao kiraia....unaongea kihisia sana kinyume na UHALISIA [emoji1787][emoji1787]
 
Kwa mara ya kwanza naunga mkono Mwabukusu.Hii tabia ya Baadhi ya taarifa kujifanya ziko Juu ya sheria ikome mara Moja.

Kila taasisi itekeleze wajibu wake kwa.mujibu wa sheria ,hakuna raia aloye Juu ya mwingine Kwa kisingizio Cha mwanajeshi sijui Tiss na blaa blaa kama hizo.
Naunga mkono HOJA yako [emoji120][emoji120]
 
Jeshi linapaswa kuzagaa mtaani pale ambapo wanaona kuna external threat au wenyewe wameamua kuchukua nchi. Sasa kweli unakatiza mitaa ya mbagala kusaka sare za jeshi?
Fact...

Aibu kubwa hiyo....

PT wanatosha kuifanya hiyo kazi...kuruhusu hilo ni kulidharau PT.....

JWTZ iheshimu katiba....
 
Wakili MWABUKUSI yuko sahihi....

PT wanatosha kuhangaika na hizo sare.....

PENDEKEZO

Wizara zinashirikiana....hebu Wizara ya ulinzi ikae mezani na wizara ya mambo ya ndani "iwezeshane fungu" ili PT wetu waweze kuifanya hiyo kazi ya "kusanya sare za JWTZ"....

Kwani ni lazima kila siku tufanye yaleyale tuliyoyazoea?!! [emoji15][emoji15][emoji1787][emoji1787]

Dunia inabadilika na UBUNIFU unahitajika katika mambo mengi....

#SiempreJMT[emoji120]

#Karibuni Komoni[emoji120]
 
WAKILI MWABUKUSI ANATAKA MKUU WA MAJESHI AZUIE UVUNJIFU WA KATIBA.

"Nchi inaongozwa kwa mujibu wa sheria na katiba. Kazi ya kukamata wa halifu ni ya Jeshi la Polisi. Jeshi la wananchi halina mamlaka kisheria na kikatiba kuingia kufanya msako mitaani kwa kisingizio cha kutafuta sare zao. Jukumu lao ni kulinda mipaka ya nchi. Cha ajabu hawajatuambia walizipeleka lini huko mitaani au zilichukuliwa na nani au waliibiwa lini? This is more than a comic [Huu ni usanii]!

Mwanajeshi hana mamlaka ya kupekua mtu katika makazi yake au maungo ya raia. Hii ni kazi ya Polisi wetu. Isipokuwa pale kunapokuwa na hali ya hatari au tishio dhahiri la mapinduzi.

Sheria inaruhusu kukataa ukamataji haramu na iwapo jeshi litaingia kwa namna hii ni haki ya wananchi kukataa ukamataji au upekuzi haramu usiofuata sheria ikiwemo kumshtaki Mwanasheria mkuu na Mkuu wa Majeshi ili kulinda sheria na Katiba ya Nchi na kudai fidia ya usumbufu.

Kama jeshi limeibiwa sare zake likaripoti Polisi. Polisi wafanye uchunguzi na wakibaini kosa Polisi ndiyo wenye utaalamu wa kupeleleza uhalifu wa wizi. Jeshi au wanajeshi hawako juu ya sheria [hivyo] wapunguze mihemko.

Kumekuwa na ujasiri wa uvunjaji katiba na sheria na kuwatisha wananchi katika taifa letu katika uongozi huu wa sasa na kwa hili hatutakubali na tutalitolea tamko rasmi kupinga vurugu hizi katika utumishi wa umma.

Mkuu wa Majeshi awajibike haraka kuzuia ukora huu wanaotaka au kupanga kuufanya!

Najisikia aibu sana kuishi na kushuhudia viroja hivi. Mungu bariki Watanganyika! Mungu ibariki Tanzania! Mungu waadhibu na kuwakemea madhalimu wote.

Boniface Kajunjumele Mwabukusi!
Kwani wote sini wapo kitengo jmn 🤣 hizi kelele zinatoka wap
 
Wewe ndo hutumii akili kwa sababu hujui majukumu ya jeshi. Mmekariri vita tu. Ha ha ha! Ingekuwa jeshi linasubiri vita kwanini mabalozi wengi duniani ni wanajeshi.

Kwa nini maofisa wengi balozini ni wanajeshi. Si wangekaa kambini kusubiri vita kama unavyomaanisha.

Kwanini kamati za usalama za nchi nyingi hata hapa Tanzania kamati za usalama zinajumuisha wanajeshi, anzia wilayani, mkoa hadi Taifa. Unajua vikao vya ulinzi na usalama vinajadili maswala gani?

Ati serikali! Unajua hiyo serikali inavyoendeshwa? Unajua mambo yote unayoyaona kuanzia kijinini kwenu, wilayani, mkoani hadi Taifa jeshi wanahusikaje?

Kwa taarifa yako humu duniani serikali zote zinategemea jeshi. Si maswala tu ya vita hata na mengineyo.

Kagame, na ethiopia wanaongoza kwa kuwa na wanajeshi wengi nje hawako kivita wapo kwa kazi maalum. Marekani, Uingereza, Ufaransa, na nchi zinginezo wanajeshi ndo maintellijensia wa uchumi. Jeshi linakazi zaidi ya vita.

Tafakari ndugu yangu. Unajua mambo unayoyaona nje ni tofauti na inavyokuwa ndani.
Mfano tu wakati Rais Magufuli amefariki kulitokea matafaruku nani ashike nchi, kuna baadhi ya viongozi waliosema Makamu wakati huo Samia hawezi. Ili liko wazi. Mama Samia alilisema na Mkuu wa Majeshi wakati huo aligusia kidogo.
Ni Mkuu wa majeshi ndo alie toa msimamo kuwa katiba ifuate wote wakaufyata! Kwanini Mkuu wa jeshi aliingia katika kikao cha serikali si angekuwa kambini kwa msemo wako.

Narudia jeshi si vita tu!
Acha kuendelea kujidhalilisha! Mwanajeshi kupewa kazi nyingine inawezekana kuwa demotion au kimkakati na pia kustaafishwa kwa lazima lakini hahusiki na raia!
 
Back
Top Bottom