JF Hard Talk "FaizaFoxy"

JF Hard Talk "FaizaFoxy"

Hilo ni kweli kabisa. Ilifikia mpaka Waislam kupunguziwa points zao wakati Ndalichako alipokuwa mkuu wa mitihani. Waislam mpaka wakaingia mitaani kuandamana mpaka Ndalichako akaachia ngazi.

Magufuli alipoingia madarakani akatuzaba Waislam kofi la kikelb kwa kumrudisha wizara hiyohiyo na kumfanya Ndalichako awe waziri wa elimu. Hatari.
Je unauhakika kuwa, mnaferishwa, au ni system ya kiislam ambayo ina base zaidi katika, mafunzo ya kiislam na kuzembea katika masomo ya shule, mfano mtoto anakazania zaidi madrasa kuliko shule, unawezaje kufanananisha na mtoto anaye shinda shule fulltime?
 
Nina swali kwako mkuu
Sasa huo upunguani. Nimekwepa nini na nimekujibu kwa muono wangu? Au kuna majibu ulishayapanga ujibiwe? Si ungenambia tu, swali hili nataka jibu hili.

Sharia haimkatazi mtu kupata elimu yeyote ile. Nadhani hafahamu kuwa hakuna dini iliyosisitiza kusoma kama Uislam. Aya ya kwanza ya Qur'an kushushwa ni "Soma".

Hivi " madrasa" unaoisikia unafikiri nini zaidi? Unajuwa kuwa neno "madarasa" la Kiswahili limetokana na hilo "madrasa"? Limit ya masomo ya madrasa ni Mwalimu au waalimu tu wanaofundishwa. Hakuna somo lisilofundishwa madrasa. Kumbuka hilo.

Neno "shule" ukienda Somalia hawalifahamu hilo, labda huyo Msomali ajuwe Kiswahili au Kijerumani kwani neno hilo limetokana na Kijerumani.

Nnaamini mtu ukiwa mjinga ndiyo unakubali kila unaloambiwa bila hata ya kufikiri au kuuliza.

Nakupongeza sana wewe kwa kuuliza kwani unaonesha unayosikia hayakuingii akilini. Hiyo ni akili nzuri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Je unauhakika kuwa, mnaferishwa, au ni system ya kiislam ambayo ina base zaidi katika, mafunzo ya kiislam na kuzembea katika masomo ya shule, mfano mtoto anakazania zaidi madrasa kuliko shule, unawezaje kufanananisha na mtoto anaye shinda shule fulltime?
mnaferishwa = mmefelishwa

Wakati huo Ndalichako alikiri kuwa "kuna makosa ya IT" ndiyo yalipelekea Waislam pekee wapunguziwe points!

Pitia uzi huu: Dr.Joyce Ndalichako atakiwa kujiuzulu. - JamiiForums
 
Hapa naona kama lugha na maelezo ilivyotimika si sawa navyojua Ke anaolewa na Me anaowa. Au umetohoa kutoka lugha ya yule mama aliyekuwa mtawala wako wakati unazaliwa??
Kiislaam, tunaoana.
 
Hilo ni kweli kabisa. Ilifikia mpaka Waislam kupunguziwa points zao wakati Ndalichako alipokuwa mkuu wa mitihani.i.
Any proof beyond reasonable doubts?...au hizi ni story za karumenge, essopo.. za kwenye vijiwe vya kahawa?
 
Vijiwe vya kahawa vinatofautiana vipo vya Kisiju,kuna vya Posta, vipo vya uwanja wa fisi na pia vya Mikocheni...fafanua
 
Huko juu nimeona sehem inazungumziwa jihad! Na umejibu 'vizuri' kuwa kwa mmoja ni 'ugaid' na mwingine ni 'kuupigania' uhuru

Ikiwa jihad ina taratibu zake na ili iitwe 'jihad' ni lazma taratibu hizo zifuatwe.,

1.Napenda unijuze, uislam umeamrisha kuwa ktk jihad haipaswi kumuua muislam mwenzetu ikiwa hatudhuru, na pia hatupashwi kuharibu uoto i.e miti. Je, 'jihad' hii inayoendelea inazingatia hayo?

2. Ni yupi Amir wa 'jihad' hii inayoendelea?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom