Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,743
- 25,564
Naanza na hawa hapa:God is good all the time, All the time....(don moen).
Humu ndani kuna vijana wanatupiga za uso nyingi sana. Mpaka sasa nimeshawakariri members 21 (kwa Id zao), hawa watu ni waongo, ninaposema ni waongo ujue ni waongo kweli kweli (standard gauge). Ni kweli mnafurahisha na kuchangamsha lakini mnazidisha!
Kuna mtu anakuja na stori yake ya kujitungia tungia tu, halafu anavaa uhusika yeye mwenyewe, mwisho wa siku (tena siyo mwisho wa siku, kesho yake) utoana analeta mada nyingine ambayo ukilinganisha na ile ya kwanza, hazileta picha kabisaa!
Kama unajijua unakuja hapa kufurahisha (uongo) na huwezi kukumbuka ulisema/utasema nini kwenye nyuzi zako, basi tumia nafsi ya mtu mwingine ~yeye, ali, wao n.k, siyo "Mimi" nikawasha gari langu nikaondoka (mfano lakini) halafu mwisho wa siku unakuja hapa kulalamikia "ajira".
Kwani hilo gari ni la mkopo? Ok ngoja ninyamaze ili kuepuka shambulio na mkija kivingine, naanza kuwataja mmoja baada ya mwingne, si nawajua!
Mbao za Mawe
mpwayungu village
Zero IQ
BIL lugano