Jifunze mapishi na namna mbalimbali za kupika mkate

Jifunze mapishi na namna mbalimbali za kupika mkate

Afadhali umenitia moyo best....
mimi nimejaribu vitumbua mara kadhaa....
mara wananiambia vile vikaangio havijazoea mata sijui nini. kwa kifupi huwa naishia kuchemsha uji kwenye mafuta.....
nikaamua kujiachia zangu

Hahahahahaha usinichekeshe mi🙂🙂🙂🙂🙂🙂🙂🙂🙂
Eti kupika uji kwenye mafuta lol...
 
Usivunjike moyo shosti endelea kujaribu tu!mapishi mengine mpaka uyajaribu mara kadhaa ndo yanakubali...na ukikosea aina ya mchele tu au kuchujua huo unga haviwi!

Yeah...mkate wa kumimina pendelea kutumia mchele mkavu maana mengine kama ina mafuta mafuta....inakua haiji vizuri
 
Yeah...mkate wa kumimina pendelea kutumia mchele mkavu maana mengine kama ina mafuta mafuta....inakua haiji vizuri

Aisee! naomba uwe unatoa copy na kwa wife wangu pia..anapenda sana kujifunza mambo mapya
 
Mahitaji
1)unga wa ngano 3 mugs
2)tui la nazi au maziwa 2-2.5 mugs
3)hamira 1teaspoon..
4)yai 1
5)chumvi kiasi.
6)samli au mafuta
7)ufuta


Namna ya kutaarisha...
1)changanya unga,hamira,tui la nazi,yai na chumvi...uchangane hadi uwe laini kama wa kaimati ila huu uwe mzito kidogo..
2)wacha hadi uumuke...

Namna ya kuchoma....
1)hakikisha chuma cha kuchomea kinagandisha vizuri na sio kinachopikiwa mafuta.....vizuri ukiroweke kwa maji ya chumvi
2)weka chuma kwenye moto then nyunyizia maji ya chumvi alafu chukua mchanganyiko wako kiganja kimoja na utandandaze...nyunyiza ufuta juu yake...
3)ukikaanza mkate kukauka geuza chuma na ukifudikize kwenye moto hadi mkate uwe dark brown
4)toa mkate kwa kutumia kisu.then pakaa juu samli/mafuta...fanya hivo kwa iliyobakia

5)mikate ya ufuta tayari kwa kuliwa...
 

Attachments

  • 1385454680642.jpg
    1385454680642.jpg
    56.3 KB · Views: 239
  • 1385454774195.jpg
    1385454774195.jpg
    105.7 KB · Views: 232
asante kwa pishi la mkate sijawahi onja mkate wa ufuta........ sipendi mkate jamani labda unitengeneze naweze kupenda huu lol
 
Yani baada ya kusoma hii post, ghafla nimeskia harufu ya mkate wa ufuta.... LOL.
farkhina apo mbona naona kama jiko la gas? Ina maana twaweza kutumia jiko la gas au? Mana mm nshazoea jiko la seredani.
 
Last edited by a moderator:
Toobah! Kuna mkate wa tambi? Manake hii kazi ya kupika nihakikishe paw haibwi imeshanichosha. Haya darasa jipya farkhina.

@fized point, mchanganyiko unatia maji mengi. Na kwenye kikaango haujaweka mafuta ya kutosha. Tia kijiko kizima cha kulia chakula kikaangoni na moto uwe mkali kiasi.
Wanadai kikaango ukikiunguzia machicha ya nazi kinakuwa sawa,sijui pana ukweli hapo?
farkhina naomba ya mkate wa ufuta na mkate wa tambi.
 
Last edited by a moderator:
Yani baada ya kusoma hii post, ghafla nimeskia harufu ya mkate wa ufuta.... LOL.
farkhina apo mbona naona kama jiko la gas? Ina maana twaweza kutumia jiko la gas au? Mana mm nshazoea jiko la seredani.

Mie nachomea kwa cooker...
 
Last edited by a moderator:
Mahitaji

Mchele kikombe 1
Tui la nazi kikombe 3/4- 1
Hamira 1 teaspoon
Hiliki kiasi
Ute wa yai 1
Sukari 3/4 kikombe

Namna ya kutaarisha

1)Roweka mchele usiku 1
2)Saga kwenye blenda mchele,hamira,tui la nazi,hiliki hadi viwe laini..
3)weka sehemu ya joto ili uimuke..
4)washa oven moto kiasi 300-350°..mimina sukari na ute wa yai kwenye mchanganyiko wako then changanya vizuri...
5)weka sufuria jikoni mafuta kidogo yakipata moto mimina mchanganyiko wako
6)baada ya dakika 5-10 mkate ukishaanza kushikana funika kwa ufuniko then weka kwenye oven hadi uwive na kuwa rangi ya brown
7)subiria mkate upoe ndipo uukate vipande vipande
8)mkate wa kuminina tayari kwa kuliwa..

hii kitu unaipika lini ili nije unionjeshe kabla cjaanza kuipika?
 
Back
Top Bottom