Jinamizi la kuchelewa kuzaa na kuolewa linavyotesa wanawake

Mama mchungaji Hivi hii mizimu inakuaje kuaje???

Nakumbuka niliambiwaga mizimu yetu Ina nguvu sana hakuna mchawi ataeweza kunidhuru na hata waliojaribu kunidhuru walishindwa..

Hapo nilikua kanisani!
Donatila
Mizimu ni wafu yaani watu waliokufa...

Roho zao zinakuwa zinaishi Bado zinatumikishwa kufanya matukio mabaya.

Matukio hayo ni kama kuua, kuharibu mimba, kufunga uzao, pesa nk..

Mizimu ni uchawi uliotukuka yaani mizimu ni zaidi ya uchawi ..

Wazee wa zamani waliitumia kwa kuiomba kama Mungu, pia walitoa sadaka..
 
Ndo nilichomwambia sio issue ya pesa tu.
Kweli upo sahihi sasa wanaume wa hivi wapo wachache Sana

Unaweza kuzaliwa na kufa hujakutana naye na mbaya wengi wao hupendelea kukaa single na kuchelewa kuoa na nikwasababu hawapo sex driven because they know their potential ni watu wakuchagua Sana .


Hao ndo huitwa Mme mwema Kama mwamposa disciples wasemavyo
 
Umeniomba, nakupa ukichokiomba.

Uchawi hakuna, Mungu hayupo, mizimu hakuna.

Na ujinga kama huu wa kulazimishana kuolewa na kuzaa unatokana moja kwa moja na imani ya Mungu.

Inawezekana watu hawaoni hilo au kulijua.

Kuna vitabu vya dini vinasema Mungu kaagiza zaeni muongezeke mkaijaze dunia.

Hivyo watu wanaona kuzaa ni amri ya Mungu, usipozaa hautimizi amri ya Mungu.

Kwa hivyo, na wewe kama unaamini Mungu, ili usiwe na contradiction, ilitakiwa ukubaliane na hii hoja ya kulazimisha watu kuolewa na kuzaa.

Ukiipinga, unaonesha contradiction katika fikra zako.
 


1 - Wanachelewa kuolewa sababu wanachagua sana wanaume. wanasema hawataki ku settle for less

2 - wanapata shida ya kupata mimba ama kuzaa sababu wanatafuta mimba wakiwa na umri mkubwa.

ki sayansi inashauriwa mwanamke aanze kuzaa mapema. quality eggs za uzazi zina decline age inavyoenda.

hata wanaume pia sperm quality inapungua kutokana na age inavyoongezeka.

ndoa za kisasa zinasababisha mimba zisipatikane kwa urahisi imagine mwanaume wa miaka 35 anafunga ndoa na mwanamke wa miaka 30, hapo mwanamke mayai yamepungua quality na hapo hapo huyo mwanaume sperm zimepungua quality. uzazi lazima usumbue tu
 
Mimi nitachukulia kama hallucinations...

Mind tricks...

Je huo moto unakuunguza au basi tu umewaka...

Nimeishi miji na majiji kibao ila sijawahi kukutana na hivyo vitu...
 
Smart911 naimagine utavokimbia na Mlango usiuone ujikojolee😁😁😁😂😂😂😂🤣
 
Ungejua wanavyoteseka wenyewe usiamini wanavyokuaminisha nje
Kwanza kabisa, wanawake wote hawako sawa.

Wanatofautiana sana, kielimu, kifamilia, kihistoria, kiuchumi, kibaiolojia.

Naona hapa kuna tatizo kubwa la ku generalize "wanawake wako hivi.. wako hivi...". Wakati wanawake wanatofautiana sana.

Kwa hivyo, inawezekana huko uliko, kwa sababu fulani za kiutamaduni, kielimu, kihistoria, kiuchumi etc, wanateseka kweli.

Lakini, hilo halimaanishi kuwa wanawake wote wanateseka.

Pia, kuna wanawake wameolewa na wamezaa ila wanajuta kuolewa na kuzaa, na wengi wao hawa hawasemi tu ukweli kwa sababu maoni haya jamii haiyapendi sana.

Kuna wanawake kibao wapo katika anti-natalist movement. Wanasema si maadili mazuri kuzaa watoto na kuwaleta kwenye dunia hii yenye matatizo mengi bila ya kupata idhini ya hao watoto. Wengine wapo katika hii movement na hawataki kuolewa, wanapata fulfillment kwenye kazi zao. Na hata wasipopata fulfillment, ni uamuzi wao.

 
Uzao wa kiume umepigwa....
Jamii iliwekeza sn Kwa mtt wa kike,wakasahau kabisa kuwa mtt wa kiume ndo 'mbegu" ndo mbeba uzao wa kizazi kimoja kwenda kingine..
Matokeo ndo haya ss ,wanawake wanaojiweza wengi, wanaume wachache sn!
Sio kweli kwamba wanawake wanaojiweza wengi kuliko wanaume
 
Mimi nitachukulia kama hallucinations...

Mind tricks...

Je huo moto unakuunguza au basi tu umewaka...

Nimeishi miji na majiji kibao ila sijawahi kukutana na hivyo vitu...
Haukuunguzi yani unawaka unazima unawaka unazima kama mara tatu then kunakua kawaida!
Hapo unavokua unawaka na chumba kinavibtare mtoto mdogo kachanga analia huku anajinyonga nyonga kama mtu anaetolewa mapepo!

Wachawi sio watuu smart!
 
Smart911 naimagine utavokimbia na Mlango usiuone ujikojolee😁😁😁😂😂😂😂🤣
Hata siku moja...
Kuna Jiji nimewahi ishi...

Hali ya hewa yake hua inapenda kutengeneza vimbunga vidogo vidogo au sometimes vikubwa kiasi...

Wengine wakiona hivyo wanakimbia ati wachawi wanakuja, mimi nilikua naenda kuingia katikati ili nione kitatokea nini...
 
Haukuunguzi yani unawaka unazima unawaka unazima kama mara tatu then kunakua kawaida!
Hapo unavokua unawaka na chumba kinavibtare mtoto mdogo kachanga analia huku anajinyonga nyonga kama mtu anaetolewa mapepo!

Wachawi sio watuu smart!
Ila yale mambo na Ile hali ulijitakia mwenyewe Kwa ubishi wako...

Anyways Cha muhimu umeponyeka...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…