Jinamizi la Udini Tanzania: Utabiri wa Sheikh Suleiman Takadir

Jinamizi la Udini Tanzania: Utabiri wa Sheikh Suleiman Takadir


Jina la Sheikh Suleiman Takadir halijapatwa kutajwa popote katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika wala katika historia ya TANU. Hatajwi na hakupata kutajwa baada ya uhuru kupatikana mwaka 1961 na sidhani hata kama atakuja kutajwa au kukumbukwa na hawa viongozi walio katika madaraka hivi sasa.

Mkuu Maalim Mohamed Said, kwanza asante kwa kisa hiki cha Mzee wako, Sheikh Suleiman Takadir, ila sio kweli kuwa Mzee huyu hatajatwa popote kwenye historia ya Tanu, kwa sababu mimi nimelisikia jina la Sheikh Suleiman Takadir siku nyingi, kabla sijakusoma wewe, hivyo lazima kuna mahali alitajwa hadi mimi kumjua!, na sio kutajwa tuu, nadhani ia kuna namna alienziwa, sikumbuki vizuri, lakini nahisi niliwahi kulisikia jina la Mtaa fulani ukiitwa Takadiri japo sikumbuki vizuri!.

Mikutano ya kwanza ya TANU ikifanyika pale Mnazi Mmoja na kabla Nyerere hajapanda juu kwenye jukwaa kuzungumza na wananchi alikuwa kwanza anatangulia Sheikh Suleiman Takadir kusawazisha uwanja na kuwaweka wananchi tayari kumsikiliza kiongozi wao. Kama alivyokuwa Nyerere, Sheikh Suleiman Takadiri alikuwa na kipaji cha kuongea. Leo hii huenda baadhi ya wasomaji wangu wasiamini lakini ukweli ni kuwa Sheikh Suleiman Takadir alikuwa kabla hajazungumza lolote alikuwa akipiga fatha, wananchi wakaitika na kwa umoja wao wakasoma, Surat Fatha, sura ya ufunguzi katika Quran Tukufu, kisha Sheikh Takadir akaomba dua na wananchi wakawa wanaitika kwa pamoja, Amin, Amin, Amin. Baada ya hapo ndipo atapanda Nyerere na kuanza kuhutubia.
Kama hii ndio ilikuwa sifa kuu ya Sheikh Takadir, "kuongea sana na kupiga 'fatha' kwenye mikutano ya Tanu!, connotation meaning ya para hii ni kuwa Mkiristo Nyerere, alikuwa hawezi kupanda jukwaani kuwahutubia Waislamu wa Tanu, mpaka kwanza Sheikh Takadir atangulie kuwapooza kwa 'fatha'!, jambo ambalo sii kweli!, ili ukweli ni kuwa Maeneo mengi ya Uswahilini, walijaa Waislamu, hivyo hizo 'fatha' ni kikolezo tuu cha kujengea hamasa, kama alivyoakifanya Salum Tambalizeni kwenye mikutano ya CCM, yaani kazi ya uhamasishaji, hivyo inawezekana kwa sasa, usimsikie Tambalizeni ekienziwa popote!, kama ambavyo alivyotoswa Sheikh Takadir!, msingi wa mtu yeyote kuenziwa ni mchango wake kuthaminiwa kwenye jambo fulani!, kama mchanga wake ni uhamasishaji tuu, then alivyothaminiwa hata kwa kutajwa tuu hadi mimi kumfahamu, ni thamani tosha!. Wako wengi walioisaidia sana Tanu, na wengine hadi kufungwa gerezani kuipigania Tanu kama kina Robert Makange na Kheri Bagdelalah lakini sikumbuki kuwasikia ni wapi walienziwa!. Kuna mamia wengine huko mikoani, wamefanya makubwa kwa Tanu, lakini sikupata kuwasikia mfano Dr. Kyaruzi, mimi ndio nimemsikia juzi juzi tuu baada ya kufariki kimya kimya huko kwao Bukoba!. Hivyo kuna wengi waliofanya makubwa kwa Tanu, hawajatajwa, ila wewe unajenga picha kwa Wazee wako tuu kuwa hawajatajwa kwa Uislamu wao!, kitu ambacho sii kweli, na haitakuwa kweli hata siku moja!.[/QUOTE]

Huyu ndiye Sheikh Suleiman Takadir na huyu ndiye Nyerere kama alivyokuja kutambulishwa kwa watu wa Dar es Salaam na Sheikh Suleiman Takadir kwa mara ya kwanza mwaka wa 1954.Kabla ya hapo Nyerere alikuwa akijulikana na watu wachache katika TAA.
Huu pia ni urongo, hapa unataka kujenga picha kuwa eti ni Sheikh Takadir ndie aliyemtambulisha Nyerere kwa mara ya kwanza kwa watu wa Dar es Salaam!, sii kweli!, kwenye utambulisho wa Nyerere kwa watu wa Dar es Salaam, naamini unaujua vilivyo!, labda ungesema, Sheikh Takadir pia alipiga ile 'fatha' yake maarufu kwenye mkutano wa kwanza wa kumtambulisha Nyerere kwa watu wa Dar es Salaam, ningekukubalia, lakini siye yeye aliyemtambulisha Nyerere kwa watu wa Dar es Salaam!.

Sheikh Takadir alimpenda sana Nyerere kiasi kuwa mwaka 1957 katika hotuba aliyotoa katika tafrija moja ya taarab Mtaa wa Mvita, alimwita Nyerere, Mtume wa Afrika, aliyetumwa na Mungu kuwaokoa Waafrika. Maneno yale ya Sheikh Suleiman Takadir alikuwa kama anamtabiria Nyerere makubwa katika mustabali wa Afrika, kwani miaka mingi baadae Nyerere alikuja kusimama mstari wa mbele katika kuikomboa Afrika kutoka makucha ya wakoloni.
Hili pia ni kujazilizia tuu kile Nyerere alichoandikiwa, kama Sheikh Takadir aliyasema haya 1957, alicopy tuu utabiri uliotangulia na kuja kuwa paste hapo kwenye hiyo tafrija ya Taarab, nyota ya Nyerere iliisha anza kung'aa siku nyingi tangu yuko Tabora School, Makerere, Edinburg hadi St. Francis (Pugu) siku nyingi kabla, hivyo utabiri huu wa Sheikh Takadir ilikuwa ni kujazia tuu yaliomo yamo!, usitaka kudanyanga humu eti aliyemtabiria Nyerere ukuu ni Sheikh Takidir!, is just one of them!.

Lakini usuhuba huu ulikuja kuvunjika na watu wawili hawa wakawa mahasimu wakubwa, Sheikh Suleiman kafa hasemi na Nyerere na Nyerere kwa upande wake hakupata hata siku moja kumtaja Sheikh Takadir popote hadi anaingia kaburini.
Huu utakuwa ni urongo mwingine, unless wewe ulikuwa bennet na Mwalimu, 24/7 hadi anaingia kaburini, ndio uweze kulisema hili kwa hakika!.

Inaaminika Sheikh Takadir alikufa kihoro baada ya kupigwa pande na TANU na wakazi wote wa Dar es Salaam na wanachama wa TANU kwa kosa la kuchanganya dini na siasa.
Sheikh Takadir akatoswa, kwani alikuwa amevunja mwiko mkubwa katika TANU. Mzee Iddi Tulio akachaguliwa kushika nafasi yake. Huku kutoswa na kutengwa na jamii ndiko kulikosababisha kifo cha Sheikh Takadir. Alikuwa hata akitoa salamu hakuna aliyeitika. Akienda sokoni Kariakoo kununua chochote kile hakuna aliyekuwa tayari kupokea hela yake. Haikuchukua muda mrefu Sheikh Takadir akaaga dunia. Kabla Sheikh Takadir hajafa TANU ilifanya mkutano mkubwa sana na Nyerere akamshambulia Sheikh Takadir kwa kutaka kuwagawa Watanganyika katika misingi ya dini. Baada ya mkutano kundi kubwa lilikwenda nyumbani kwa Sheikh Takadir Mtaa wa Msimbazi kuzomea huku wakiimba, Takadir Mtaka Dini. Sheikh Takadir alitoka nje akasimama kizingitini akasema maneno haya, Ndugu zangu In Sha Allah iko siku mtakuja kunikumbuka. Haukupita muda mrefu Sheikh Takadir akatangulia mbele ya haki na kwa kipindi kirefu katika historia ya uhuru wa Tanganyika hakuna aliyemkumbuka Sheikh Suleiman Takadir.
Hapa sasa ndio the Best of Maalim Mohamed Said!, muogope Mola wako!, huwezi kudaid kuwa Sheikh Takadir alikufa kwa kihoro cha kutoswa!, yaani kisababishi cha kifo chake ni kule kutenwa na jamii!. Uhai umeumbwa, na kifo pia kimeumbwa, Sheikh Takadir alijifia natural death siku yake aliyopangiwa na Mungu ilipowadia!. Kwa msio jua!, Malaika mtoa roho, Israel, anampitia kila mmoja wetu mara sabaini fii sabaa kwa siku, ili kuhakikisha muda wake ukifika asizidishe hata sekunde moja!. Hili ni moja ya bandiko jingine la Maalim Mohemed Said lenye kutoa ilmu adimu, but with "ill motive" behind!, ili ilionekane hata kifo cha Shekh Sulemain Takadir, msababishi ni fulani!.

Pamoja na "the ill motive behind", asante kwa simulizi nzuri,
endelea tuu kuipalilia na kuimwagilia na kuitilia mbolea hii "mbegu", soon itamea vilivyo na tutapata mavuno stahiki muda stahiki ukiwadia, wakati huo huo mimi naendelea kufanya research yangu kwenye urais wa Tanzania, rais akiwa ni Mkristo ni kwanini lazima awe ni Mkatoliki?.
Pasco.
 
scan0026.jpg


Kutoka Kushoto: Sheikh Suleiman Takadir, Mbutta Milando, JohnRupia na Julius Nyerere Hao Waliowazunguka na Silaha za Jadi ni Bantu Group Kundi la Vijana wa TANU lililokuwa linatoa Ulinzi kwa Viongozi wa TANU. Picha Hii Ilipigwa Mwaka wa 1955.


Jina la Sheikh Suleiman Takadir halijapatwa kutajwa popote katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika wala katika historia ya TANU. Hatajwi na hakupata kutajwa baada ya uhuru kupatikana mwaka 1961 na sidhani hata kama atakuja kutajwa au kukumbukwa na hawa viongozi walio katika madaraka hivi sasa. Lakini naamini viongozi hawa walio madarakani hivi sasa ambao wakati wa kudai uhuru walikuwa watoto wadogo lazima watakuwa wamesikia jina hili likitajwa na wazee wao. Sheikh Suleiman Takadir hutajwa kila linapotokea jambo ambalo Waislam huonekana wanadhulumiwa na serikali kwani ilikuwa Sheikh Suleiman Takadir ndiye aliyeweka agenda ya hali ya baadae ya Waislam na Uislam katika Tanganyika huru mwaka 1958. Jambo hili alipolileta lilitishia kuigawa TANU katika misingi ya dini katika wakati amabo umoja wa Waafrika ulikuwa unahitajika sana. Mwaka wa 1958 TANU ilikuwa imeenea nchi nzima na tayari iko katika barabara ya kuelekea kuchukua madaraka ya ndani na kisha Tanganyika kupata uhuru wake kamili.

Sheikh Suleiman Takadir alikuwa nani na nini ulikuwa umaarufu wake? Sheikh Suleiman Takadir kwanza alikuwa ‘’alim,” mwanazuoni kisha alikuwa Mwenyekiti muasisi wa Baraza la Wazee wa TANU kuanzia TANU ilipoundwa mwaka 1954 hadi “alipotoswa” mwaka 1958 kwa kosa la “kuchanganya dini na siasa.’’ Sheikh Takadiri alishiriki vilivyo ndani ya Baraza la Wazee wa TANU katika kutayarisha safari ya Nyerere kwenda UNO mwaka 1955. Wapenzi wake katika harakati za kupigania uhuru walimpachika jina la utani wakimwita “Makarios,” wakimlinganisha na Askofu Makarios wa Cyprus na Ugiriki aliyekuwa anapambana na ukoloni wa Waingereza wakati yeye alipokuwa anapambana na Waingereza katika ardhi ya Tanganyika. Sasa kwa kuwa Suleiman Takadir alikuwa sheikh na mpambanaji ndipo walimpa jina hilo la “Makarios” na kwa hakika jina hili lilimkaa, likamwenea vyema na yeye akalipenda.


WAZEE%2BWA%2BTANU.jpg


Baraza la Wazee wa TANU
Sheikh Suleiman Takadir wa Pili Chini Kulia, Wa Pili Waliosimama Dossa Aziz,
Wa Sita Julius Nyerere, Wa Saba John Rupia, Wa Tisa Said Chamwenyewe,
Anaefuatia Jumbe Tambaza, Mshume Kiyate

Mikutano ya mwanzo ya TANU ilikuwa ikifanyika Mnazi Mmoja mbele ya baadae ilipojengwa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima. Wakati ule pale palikuwa hakuna jengo lolote, palikuwa na kiwanja kitupu na ardhi ile ilikuwa mali ya Mzee John Rupia Makamu wa Rais wa TANU. Kiwanja hiki baaadae Mzee Rupia aliwapa TANU na TANU wakaanzisha Chuo Kikuu pale mara baada ya uhuru. Mikutano ya kwanza ya TANU ikifanyika pale Mnazi Mmoja na kabla Nyerere hajapanda juu kwenye jukwaa kuzungumza na wananchi alikuwa kwanza anatangulia Sheikh Suleiman Takadir kusawazisha uwanja na kuwaweka wananchi tayari kumsikiliza kiongozi wao. Kama alivyokuwa Nyerere, Sheikh Suleiman Takadiri alikuwa na kipaji cha kuongea. Leo hii huenda baadhi ya wasomaji wangu wasiamini lakini ukweli ni kuwa Sheikh Suleiman Takadir alikuwa kabla hajazungumza lolote alikuwa akipiga “fatha,” wananchi wakaitika na kwa umoja wao wakasoma, “Surat Fatha,” sura ya ufunguzi katika Qur’an Tukufu, kisha Sheikh Takadir akaomba dua na wananchi wakawa wanaitika kwa pamoja, “Amin,” Amin,” “Amin.” Baada ya hapo ndipo atapanda Nyerere na kuanza kuhutubia. (Picha za mwanzo za mikutano hii zipo na zilipigwa na Mzee Shebe ambae katika miaka ile ya 1950 alikuwa na studio yake Mtaa wa Livingstone na Kipata. Picha hizi baadhi nimepata kuziona. Mzee Shebe ndiye alinipiga picha yangu ya kwaza nikiwa na umri wa mwaka mmoja au miwili hivi na picha hii ninayo hadi hii leo. Inaaminika Mzee Shebe ndiye mpiga picha wa kwanza wa TANU na Nyerere).


002_2.JPG


Mwandishi Akiwa na Mwaka Mmoja Au Miwili Picha Aliyopigwa na Mzee Shebe
1952/53 Kwenye Studio Yake Mtaa wa Livingstone na Kipata


scan0027-1.jpg


Nyerere Akihutubia Mkutano wa TANU Siku za Mwanzo

Huyu ndiye Sheikh Suleiman Takadir na huyu ndiye Nyerere kama alivyokuja kutambulishwa kwa watu wa Dar es Salaam na Sheikh Suleiman Takadir kwa mara ya kwanza mwaka wa 1954.Kabla ya hapo Nyerere alikuwa akijulikana na watu wachache katika TAA. Sheikh Takadir alimpenda sana Nyerere kiasi kuwa mwaka 1957 katika hotuba aliyotoa katika tafrija moja ya taarab Mtaa wa Mvita, alimwita Nyerere, “Mtume wa Afrika,” aliyetumwa na Mungu kuwaokoa Waafrika. Maneno yale ya Sheikh Suleiman Takadir alikuwa kama anamtabiria Nyerere makubwa katika mustabali wa Afrika, kwani miaka mingi baadae Nyerere alikuja kusimama mstari wa mbele katika kuikomboa Afrika kutoka makucha ya wakoloni. Nyerere akawa hapungui nyumbani kwa Sheikh Takadir Mtaa wa Swahili. Nyumba hii iko jirani na kilabu ya mpira ya Pan Africa. Kutembelewa na Nyerere pale nyumbani kwake ikapelekea baba mwenye nyumba, Jumbe bin Jumaa wa Digosi amuhamishe nyumba Sheikh Takadir asije kumponza kwa kwani Nyerere alijulikana kama adui mkubwa wa Waingereza. Hii kwa muhtasari ndiyo historia ya Sheikh Suleiman Takadir na Nyerere. Lakini usuhuba huu ulikuja kuvunjika na watu wawili hawa wakawa mahasimu wakubwa, Sheikh Suleiman kafa hasemi na Nyerere na Nyerere kwa upande wake hakupata hata siku moja kumtaja Sheikh Takadir popote hadi anaingia kaburini. Inaaminika Sheikh Takadir alikufa kihoro baada ya kupigwa pande na TANU na wakazi wote wa Dar es Salaam na wanachama wa TANU kwa kosa la “kuchanganya dini na siasa.” (Ikiwa msomaji wangu ulisoma makala yangu ya juma lililopita utakuwa umeona kuwa TANU ikiongozwa na Mufti Sheikh Hassan bin Amir ilipitisha azimio la kupiga vita hisia zozote na chembechembe za Uislam ndani ya TANU). Hakika Uislam ulikuwa na nguvu ndani ya TANU lakini haukuachiwa uvuke mipaka kuwabagua wengine waliokuwa si Waislam.

Kilitokea nini hadi kupelekea Sheikh Suleiman Takadir agombane na Nyerere? Chanzo cha mtafaruku huu ni Uchaguzi wa Kura Tatu wa mwaka 1958. Waingereza waliweka masharti ambayo kwa hakika yalikuwa ya kibaguzi na yalifanya wananchi wengi wasiweze kukidhi sifa zilizowekwa za kuweza mtu kupiga au kupigiwa kura. Kulikuwa na sifa ya elimu, kipato na kazi ya kukubalika na kupiga kura kwa tabaka za rangi. Mpiga kura Mwafrika alitakiwa ampigie kura Mzungu, Muasia na Mwafrika. Masharti haya yalikuwa kisiki kigumu kwa uongozi wa TANU na wanachama wake kutimiza. TANU na viongozi wake wengi hawakuwa na hiyo elimu iliyokuwa ikitakikana wala kipato cha maana. Ili mtu asimame kama mgombea kuingia katika Baraza la Kutunga Sheria au awe angalau mpiga kura ilibidi azikusanye sifa zote hizo mahali pamoja. Wapiga Kura na wagombea walitakiwa wawe na kisomo cha darasa la 10 au kipato cha pauni 400 kwa mwaka na kuwa na kazi ya maana. Waafrika waliokuwa na sifa hizi hawakuwa wengi katika TANU. Wengi katika TANU kama walivyokuwa wakipenda kujiita wenyewe walikuwa, “Baba Kabwela.” Ikawa sasa ili TANU iweze kuweka wagombea ilibidi iwatafute watu nje ya uongozi wa TANU. Hapa ndipo lilipokuwa tatizo.


scan0023.jpg


[TABLE="class: tr-caption-container, align: center"]
[TR]
[TD="class: tr-caption"]Nyerere Akitia Sahihi Azimio la Tabora[/TD]
[/TR]
[/TABLE]


Ilibidi TANU sasa iwalete watu wenye sifa nje yake na wengi wa watu hawa walikuwa Wakristo waliosomeshwa na wamishionari. Jambo hili lilimkera sana Sheikh Takadir na wanachama wengi wa TANU kwa ujumla wao na kwa hakika TANU nzima hawakutaka kabisa kuingia uchaguzi ule kwa masharti yale waliyoyaona ya kibaguzi. Wanachama wa TANU walikuja na kauli mbiu isemayo, “Kuingia Kura Tatu ni sawa na kujipaka kinyesi.” Ilikuwapo minong’ono kuwa Wakristo wataichukua nchi lakini kwa muda mrefu hofu hii ilizuiwa kwenye vifua hakuna aliyekuwa na ujasiri wa kulisema hilo waziwazi kwani jambo la dini lilikuwa mwiko mkubwa katika TANU. Ikawa tatizo lile la kushiriki kwa TANU katika Uchaguzi wa Kura Tatu lijadiliwe kwenye Mkutano Mkuu wa TANU wa mwaka 1958 uliopangwa kufanyika Tabora. Mpinzani mkubwa wa Kura Tatu alikuwa Zuberi Mtemvu, Katibu Mwenezi wa TANU kwa wakati ule. Ukweli ni kuwa Kura Tatu ilitishia uhai wa TANU na zilikuwapo dalili za chama kumeguka pande mbili. Kulikuwa na uwezekano mkubwa sana kuwa Zuberi Mtemvu na Sheikh Takadir wangelikuwa upande mmoja na wangeweza kuja na chama kingine ingawa agenda zao zilikuwa tofauti. Mtemvu yeye alisimama kwenye Afrika kwa Waafrika na Sheikh Takadir kwenye Uislam. Mkutano wa Tabora ni kisa kirefu In Sha Allah tutakitafutia wakati wake makhsusi tukizungumze. (Nimekiandikia kitabu kizima “Uamuzi wa Busara,” Abantu Publishers 2007, Dar es Salaam) Sheikh Suleiman Takadir na baadhi ya wazee katika Baraza la Wazee wa TANU walikuwa wajumbe katika mkutano wa Tabora. Kufupisha kisa TANU ilipiga kura kukubali kuingia kwenye Uchaguzi wa Kura Tatu na manusruna kura zifungane kati ya wale wanaounga mkono na wale waliokuwa wakipinga. TANU iliingia katika Uchaguzi wa Kura Tatu na ikapata ushindi mkubwa.

Hofu aliyokuwanayo Sheikh Takadir ilikuwa kuwa watu walioingia katika TANU kuchukua uongozi ni Wakristo. Sheikh Takadir alikuwa anajua nguvu ya madaraka waliyokuwa wanakabidhiwa akawa na hofu kama uongozi huu mpya utakuja kutoa haki kwa Waislam uhuru utakapopatikana. Sheikh Takadir alitaka uhakika wa hali ya baadae ya Waislam katika Tanganyika huru. Katika mkutano wa Halmashauri Kuu Makao Makuu ya TANU, New Street Sheikh Takadir alimkabili Nyerere akamshutumu kuwa hakuwa na nia nzuri na Waislam, atakuja wapendelea ndugu zake Wakristo katika Tanganyika huru. Sheikh Takadir akawageukia wenzake katika Baraza la Wazee wa TANU akasema, “Tuzibe ufa tusije tukajenga ukuta.” Jambo lile lilikuwa zito. Nyerere alijiinamia na aliponyanyua uso wake machozi yalikua yanambubujika. Mkutano haukuweza kujadili jambo lile na kikako kile kikavunjika pale pale na wajumbe wakawatawanyika.

Sheikh Takadir ‘’akatoswa,’’ kwani alikuwa amevunja mwiko mkubwa katika TANU. Mzee Iddi Tulio akachaguliwa kushika nafasi yake. Huku ‘’kutoswa’’ na kutengwa na jamii ndiko kulikosababisha kifo cha Sheikh Takadir. Alikuwa hata akitoa salamu hakuna aliyeitika. Akienda sokoni Kariakoo kununua chochote kile hakuna aliyekuwa tayari kupokea hela yake. Haikuchukua muda mrefu Sheikh Takadir akaaga dunia. Kabla Sheikh Takadir hajafa TANU ilifanya mkutano mkubwa sana na Nyerere akamshambulia Sheikh Takadir kwa kutaka kuwagawa Watanganyika katika misingi ya dini. Baada ya mkutano kundi kubwa lilikwenda nyumbani kwa Sheikh Takadir Mtaa wa Msimbazi kuzomea huku wakiimba, “Takadir Mtaka Dini.” Sheikh Takadir alitoka nje akasimama kizingitini akasema maneno haya, “Ndugu zangu In Sha Allah iko siku mtakuja kunikumbuka.” Haukupita muda mrefu Sheikh Takadir akatangulia mbele ya haki na kwa kipindi kirefu katika historia ya uhuru wa Tanganyika hakuna aliyemkumbuka Sheikh Suleiman Takadir, Askofu Makarios wa Tanganyika. Hivi sasa Sheikh Suleiman Takadir anatajwa sana na kizazi cha leo. Utabiri wake kuwa ndugu zake watakuja kumkumbuka umetimia. Swali la kujiuliza ni iweje hii leo baada ya miaka 57 kupita Sheikh Suleiman Takadir anarejeshwa upya katika historia ya kupigani uhuru wa Tanganyika? Hiki ni kitendawili kinachongoja kuteguliwa.


3ngq7mfoNBkDsGoTihZVXo4ZzngGhTG3i5TneJ6bQLk=w409-h207-p-no

nilipoanza kuisoma mwanzo tu nkaelewa serikali inatambaa kwa kutumia mgongo wa waislamu kutimiza malengo yao waislam tunatakiwa kuamka adui sio mkristo
 
Huo ni mtizamo wako binafsi. Usilazimishe mtizamo wako kihistoria uwe ndiyo msimamo "official". Mada zako nyingi zimejikita katika Uislamu na Pwani ya Tanganyika. Nikutaarifu tu kwa mimi niliyetoka "interior" Tanganyika kwa mara ya kwanza nimekutana na waislamu (sisi kule kwetu tunaita "Waswahili") mwaka 1970 ukichukulia maanani nimezaliwa miaka ya 50. Lakini chama cha TANU nimekisikia mwaka wa 1964. Waswahili walikuwa confined to the coastal belt na vision yao kabla ya Nyerere sidhani kwamba ilikuwa kubwa kwa sababu malengo yao yalikuwa ni ya kijamii zaidi kuliko kisiasa. TAA ilibadilika sana Nyerere alivyoingia kwa sababu ailibadilisha vision na mission ya TAA kuwa political rather than social. The very fact kwamba mtu mmoja alileta mabadiliko makubwa kiasi hicho wakati kundi la waswahili hawakuweza kufanya hivyo mpaka Nyerere alipofika, ndicho kinachokukwaza sana na unafikiri labda Nyerere aliwakandamiza. Historia imejaa mifano mingi tu ya namna mtu mmoja anavyoweza kuhamasisha watu kwa lengo fulani. Hivyo mantiki yako ni very narrow na hii haishangazi sana kwa kuwa "Religion has never been the best argument to base on, unless mtu umefilisika kabisa kifikra".
Hakuna anayelazimisha huo ndiyo ukweli wa history ya Tanganyika, kwa faida ya JF tufahamishe wewe history ya Tanganyika.

Cc; FaizaFoxy
 
Last edited by a moderator:
Kweli kabisa...nisichoelewa ni kwanini unashabikia sana udini kwa kigezo cha Nyerere. Udini tuufanye sisi halafu matusi yaende kwa Nyerere. Inamsaidia nani? Jamii yetu inaumwa...inahitaji tiba ya kweli. Tusipofungua macho na kuona hilo tutaadhirika. Nyerere amekuja na kwenda. Leo tupo mimi na wewe na wengine waliopo. Changamoto zetu lazima tuzikabiri wenyewe kwa heshima na maridhiano. Tunao uwezo huo kama hatutasukumwa na egoes zetu.

Sishangai mambo mengi yanakwama sababu nyuma ya kila ajenda tumeficha unafiki wetu

Nadana!
Unapokwenda kwa Daktari kwa sababu una maradhi yanayokusumbua anachofanya Daktari Mzuri sio atakutafutia Tiba tu bali atataka kujua Ulipata vipi Huo Ugonjwa au Hayo maradhi.
Na baadabya kujua Chanzo chake ni lzm akupe Ushauri Ili Usije kuugua Tena.

Sasa anachofanya hapa Mzee Mohamed Said Ni Kutuonyesha Sisi watanzania Tusiojua au tunaojifanya hatujui CHANZO CHA Huu ubaguzi wa Udini. Na shukurani nyingi zimuendee mzee Mohamed Said Tumefahamu Mengi mno yaliofichwa na Kukaliwa na Serikali ya huyo Nyerere muasisi wa Mfumo Kristo.

Na kwa taarifa yako ile SRATANI ya Mfumo Kristo aliotuachia bado Inaendelea Kuota Mizizi kila.Kona Ktk Serikali yetu. Na wewe km Una macho Lzm Utakuwa umeshaliona hilo la km huna Basi Wazee wasomi Km Hawa Watakusaidia Kuyaona hayo kupitia Kwenye Macho yao ya Kalamu.

Tushirikiane ktk kutafuta hio Tiba lkn waache wazee km Mohamed Said aendelee kutukumbusha Chanzo cha haya MARADHI ili Sisi kizazi cha sasa tusijerudia makosa aliyo yafanya yule mzee aliekosa Huruma na Imani Mchonga meno wa butiama.
Kafa katuachia balaa huku nyuma.
Mungu amuongeze Adhabu.

Sema amen!
 
Last edited by a moderator:
ninaichukia dini na siasa ni vitu vyepesi ila imara katika kuvunja ama ni..
Tanzania Si nchi salama waislam wanashindana na wakristo na wakristo vivyohivyo..
hatutaishia pazuri.
 
Ghosryder,
Una ushahidi madhubuti kwa tuhuma hizo?

Kama unao ulete hapa.

Haipendezi mtu kuzua maneno kuwatia watu hofu.
 
Demulikuy,
Umekuja na historia ya Kivukoni.

TAA ilichukua mkondo wa siasa 1950 baada ya mapinduzi ya Dk. Vedasto Kyaruzi na Abdul Sykes na wakaunda TAA Political Subcommittee.

Kamati hii ndiyo iliyoandika katiba waliyoipendekeza TAA kwa Gavana Twinning.

Nyerere hakuwapo wala hakuna mtu aliyekuwa anamjua.

Habari hii nimeieleza kwa kirefu katika kitabu changu.

Masahihisho haya ya historia ya Tanganyika ndiyo yaliyovutia kitabu changu na kusababisha nipate mialiko mingi ya kuzungumza ndani na nje ya nchi.

Hii si dalili ya mtu aliyefilisika.
 
Pasco,
Mtaa wa Takadiri uko Magomeni ila si kwa ajili ya sheikh.

Ilikuwa mwiko Sheikh Takadir kutajwa...

Kusikika nje ya duara jina likisikika kama vile alivyokuwa
akitajwa Abdul Sykes lakini ndani ya TANU hakuwa akitajwa.

Hivi vitu vikinishangaza sana.
 
Huyo Mzee Takadir alikuwa hafai, badala ya kuuliza Mstakabali wa Watanganyika baada ya Tanganyika huru anauliza mstakabali wa Waislamu? Alikuwa na agenda gani kana kwamba Tanganyika ilikuwa na waislamu pekee. Na huu ni Mfuno Baguzi unaofanywa na Waislamu dhidi ya jamii ya watu wengine wasiyokuwa Waislamu.
 
Pasco,
Sikuzuii kusema ulitakalo.

Mimi nimewaeleza wazee wangu kwa kuwa nawajua.

Sikulazimishi kuniamini.

Sasa Mzee Mbona Maandiko yako hayana hitimisho, tuwafanyie nini hawa waislaam ili kuwalipa fadhira za kupigania uhuru. Tuwafanyie nini ili wao waridhike maana mchango wao ni mkubwa
 
Hata hueleweki. Je ni kwa nini unaleta mada hizi kipindi hiki ambacho watu wanaojinasibisha na uislam wakiwa wanashambulia vituo vya polisi na kutaka kuunda dola ya kiislam, tukuchukulieje? uko upande gani?
Nadhani wewe ndio hutaki kumuelewa! Halafu usichanganye mada, Mzee Mohammed Saidi anaongelea historia, huko unakomoeleka hakuhusiani kabisaa na mada zake.
 
Pasco,
Sikuzuii kusema ulitakalo.

Mimi nimewaeleza wazee wangu kwa kuwa nawajua.

Sikulazimishi kuniamini.

tatizo lako lipo kwenye umimi ktk kuwaelezea wazee wako.. then udini
. Bhaaasi nje ya hapo maandishi yako yangekuwa na maana sana.
 
Huyo Mzee Takadir alikuwa hafai, badala ya kuuliza Mstakabali wa Watanganyika baada ya Tanganyika huru anauliza mstakabali wa Waislamu? Alikuwa na agenda gani kana kwamba Tanganyika ilikuwa na waislamu pekee. Na huu ni Mfuno Baguzi unaofanywa na Waislamu dhidi ya jamii ya watu wengine wasiyokuwa Waislamu.

na Nyerere alikuwa hana masihara na wadini.
 
Tunahitaji hitimisho, sio kutoa history. Tunataka tujue waislaam wanataka nini ili waridhike maana haya malaamiko bila kujua tunafika vip tamati ili wenzetu waridhike maana Tanzania ni ya wote
 
Sasa Mzee Mbona Maandiko yako hayana hitimisho, tuwafanyie nini hawa waislaam ili kuwalipa fadhira za kupigania uhuru. Tuwafanyie nini ili wao waridhike maana mchango wao ni mkubwa

hawa jamaa hawaridhiki hata wakisikilizwa hoja zao nyanya.....ipo siku watasema marufuku kula na kunywa hadharani mwezi wa Ramadhan.....ni rahisi kuishi kwa amani na paganism, hindu, au buddha kuliko watu wa dini hii...
 
Tunaokuomba mzee KINGUNGE Na wewe andika historia ya WAPAGANI Waliopigania UHURU.Tumechoka na HEKAYA HIZI za huyu mzee.
 
Tunajua mna mkakati wa kusilimisha NCHI,Hamtaweza.Tangu huyu mzee apewe AZIMIO LA ABUJA.Kaleta MAJANGA.
 
Tanzania hii, inamchango wa watu wengi katika kuleta uhuru. Wakati ule isingelikuwa rahisi kwa namna yoyote ile wazee wa mji fulani kuleta uhuru wa nchi hii peke yao. Maandiko mengi ya Mzee wetu M. Saidi nimeyasoma. Na hitimisho langu ni kuwa ukiayaangalia kwa jicho la kutokuelemea upande ni kuwa historia inayodaiwa kufichwa haipo, bali kinachoelezwa ni jinsi ya kuwatia hamasa watu wa imani nyingine kujiona kuwa walishiriki kikamilifu, ila sasa wamesahauliwa. Hili si la kweli hata kidogo na halikubaliki.

Tatizo lingine la historia nayoidai mwandishi ni historia ya kuvizia. Akishafariki mtu, basi ndipo maandiko yake huibuka. Kwa kuwa marehemu hana lake hivyo basi inakuwa ni wakati wake wa kujenga hoja za chuki. Wakiwa hai hana muda wa kuwahoji, ila wakifa huwatia maneno vichwani mwao na midomoni mwao.

Utetezi wake ni kuwa maandishi yake yamechapishwa na vyuo na majarida maarufu. Lakini kuchapishwa kwake sio hoja ya kusema ni sahihi.

Kama kweli Mzee. M. Saidi unaipenda sana nchi yetu, basi usingechagua watu katika historia yako kwa misingi ya dini zao. Mfano unaaandika wazee wa dar wa dini fulani, baadae unaenda mikoa ya magharibi na kanda ya ziwa, kule unaandika wazee wa imani hiyo hiyo, kisha unaenda mikoa ya kaskazini unafanya hivyo.

Kisha unamalizia kwa kumlaumu nyerere. Nia yako ni ipi hasa kama sio chuki.
 
NYERERE Itakuwa alijuta kufanyia HARAKATI Huku,watu wanataka Fadhila wawe kundi special kuliko wengine.
 
Back
Top Bottom