Jinamizi la Udini Tanzania: Utabiri wa Sheikh Suleiman Takadir

Tunajua mna mkakati wa kusilimisha NCHI,Hamtaweza.Tangu huyu mzee apewe AZIMIO LA ABUJA.Kaleta MAJANGA.

Abu Jahal,
Kuna mahali nilionya hapa kuwa "Azimio la Abuja," si document ya kutegemea
kwa sababu chanzo chake (source) ni kitabu cha Walokole wa Kimarekani:
"The Two Headed Dragon" ambaho kilisambazwa kwa wingi Nigeria.

Si kitabu cha maana.
 
Kila nikiona malalamiko ya waislamu juu ya Nyerere najiuliza kama mikakati yakuipatia uhuru taifa hili liliratibiwa na waislamu je
1.Ilikuwaje Nyerere akawazidi ujanja?
2.Je walitaka taifa hili liwe la kiislamu?
3.Nyerere kusema taifa hili halina dini wao wameathirika na nini
NB:matokeo yametoka mwanzo walilalamika kuwa ndelichako nikikwazo sasa kaondoka matokeo yametoka kumi bora hampo kumi za mwisho mpo je tatizo nini
 
Babuwaloliondo,
Angalia nimeanza lini kuandika.

Soma kwanza ndipo useme.
 
Mazoko,
Hayo mengine watajibu wengine.

Naomba nikuulize hili moja.
Katoka Ndalichako kaingia nani?
Mazoko,
Hayo mengine watajibu wengine.

Naomba nikuulize hili moja.
Katoka Ndalichako kaingia nani?

Mohamed
Nijibu maana nategemea kuelimishwa nasio kulumbana
Pia aliyeleta mada hii nadhani katoa kwenye gazeti la RAIA MWEMA wiki hii nimesoma hekaya za mwandishi chaajabu nilichoshidwa kuelewa na hasa ndiyo chuki aliyoisema mwandishi nikuwa Nyerere aliwaleta wakristo wagombee uongozi na mwandishi anakiri kuwa wakoloni waliweka sheria ya wagombea wawe wewna elimu ambayo kwa bahati mbaya shekhe na wenzake hawakuwa nayo
Nikajiuliza swali je tulitaka tusipate uhuru mpaka waislamu wasome? Tena anakiri ushindi ulipatikana mkubwa sana kwa mtu mweusi je huyu mkristo alichaguliwa na nani sina dini zote tena akaendelea kusema baada ya ushindi Nyerere akampinga sasa huyu mweshimiwa kwakutaka kuleta udini je kosa la Nyerere nilipi?
 

Mazoko,
Nimekupa swali ili nikugutue na utazame lile ambalo mimi nimeona
limekupita.

Kingine ambacho napenda uzingatie ni kuwa hayo ambayo umeandika
ya TANU kupata ushindi mkubwa kwa kuchaguliwa na watu ndiyo
niliyoandika mimi.

Si wengi walikuwa wanaijua historia hii na mimi nimeileta hapa na
sasa inafahamika.

Katika hali kama hii ni juu ya msomaji mwenyewe kufanya uchambuzi
wake mwenyewe kama ulivyofanya wewe.

Hii ndiyo kazi kubwa ya mwandishi yoyote.
Kuiletea jamii kile ambacho hakikuwa kinafahamika.

Mimi sikulazimishi kuiona historia hii katika jicho langu.

Una uhuru wa kuchambua mambo kama akili yako inavyokuelekeza.

Ila umenisikitisha kusema kuwa historia hii ya TANU hasa kipande
hiki kuelekea uhuru kuanzia 1958 ni "hekaya."

Naelewa moyo unakuuma kwa kuwa kwako historia hii imekuletea
mshtuko wa moyo.

Hauko peke yako.

Watu wengi wameumizwa na hizi taarifa mpya katika historia ya
nchi nchi yetu zaidi kwa kugundua kuwa historia waliyoizoea
haikuwa imekamilika.

Mazoko,
Mimi siandiki hekaya.
Usiwe na haraka katika kunihukumu.

Soma kazi zangu na baadhi zimechapwa na wachapaji wenye sifa
ulimwenguni kama Oxford Univeristy Press.

Soma mada zangu nilizowasilisha katika vyuo tofauti ndani na nje
ya nchi yetu.

Baada ya hapo ndiyo unaweza ukanihukumu ikiwa unao uwezo huo.
 

Cc watanzania cku zote ni bendera fuata upepo. Tunakurupuka na kufanya maamuzi mapema pasi na kufikiria consequence, alafu baadae watu wa majuto na kulalama. Rest in peace Takadir.oo
 

mzee wangu usiishie kutonyesha vidonda, nimekua nikifuatilia haya mambo naona umejitoa kutetea ulichokiona kimepindishwa. endelea kutafuta historia na ushahidi wa kutosha endelea kuandika vitabu ambavyo vitakua urithi kwa watakao endeleza harakati zako mwisho kabisa ni vyema ukawapelekea malalamiko yako vyombo husika.
 
Mohamed Said nasikitika kwanini unakwepa maswali nijibu kwa manufaa ya wengine maana yawezekana unajambo zuri kuliko nijuwavyo mimi maana wakati wakugombea uhuru nilikuwa na miaka19 na kila mmoja wetu tulikuwa tunapigania kupata uhuru nasio kutawaliwa na dini ipi sasa nijibu maswali yangu nadhani unaweza kuyaona nyuma
Nijuavyo mimi nikuwa umeleta mada hii ili kutuelimisha sasa mbona unaleta hadithi badala ya majibu
Ingawa yawezekana ukawa unaniweka kwenye kundi fulani ila siku huko nijibu kwa faida yangu na wengine
 
Kama shekhe takadir alitengwa na wengi ambao ni waislamu kama simulizi inavyosema,maana ake waislamu wenzie waliona umuhimu wakuwa wamoja katika kuikomboa tanganyika na siyo fikra za takadir kuwa anaikomboa dini ya kiislamu,..
 
Kama shekhe takadir alitengwa na wengi ambao ni waislamu kama simulizi inavyosema,maana ake waislamu wenzie waliona umuhimu wakuwa wamoja katika kuikomboa tanganyika na siyo fikra za takadir kuwa anaikomboa dini ya kiislamu,..

Very true hakuna sababu ya sisi Watanganyika kumkumbuka hata kidogo
 

Mazoko,
Swali gani unataka nikujibu.
Nifahamishe.

Makala ya Sheikh Suleiman Takadir imewagusa watu wengi sana.

Toka ilipotoka katika gazeti la Raia Mwema nimepongezwa na pia
kulaumiwa na wengi.

Wengi sana walikuwa hawakijui kisa hiki na kimewasisimua sana.

Nadhani wasomaji wangu wengi watataka kujua nini nitakujanacho
toleo lijalo In Sha Allah.

Sikutii katika kundi lolote.

Mimi nifanyapo utafiti kisha nikaa kitako kuandika huwa nazungumza
na dunia nzima.

Mtu mmoja au kundi la watu lina manufaa au tija gani?

Ndiyo maana naandika na Oxford University Press kisha kwa
Kiingereza ili niufikie ulimwengu.

Kuhusu kuleta, "hadithi."
Allah hakunijaalia kipaji hicho ingawa mie ni mpenzi wa riwaya.

Ujanani nikiwasoma James Hadley Chase, Irving Wallace, Peter
Cheyney
nk.
 

Inaonekana umejitoa ufahamu maswali unayajuwa na unakwepa kwepa

Naona unajivunia kuchapicha Oxford University press mimi nimefanyanao kazi ila kwa sasa ninakampuni yangu mimi nimejikita zaidi kwenye UCHUMI na Upatanishi kuliko dini nawengi wamefaidika na mimi pia nimetembea bara la Ulaya kwenye nchi zaidi 15 Afrika zaidi ya nchi 20 America asia na kwingineko
Huko kote nimealikwa kwenye midahalo yakuikomboa Dunia hasa mwafrika kutoka kwenye utumwa wakimawazo nakujenga uchumi imara

Dunia yaleo sio kuzungumzia dini fulani au utawala wa dini fulani maana hauna tija
Kunachi zinaongozwa kwa imani za kidini kama
Misri,Irak,Iran,Libya nanyinginezo hakuna utulivu zaidi ya ugomvi

Nadhani ifike sehemu dini zibaki misikitini na makanisa huku tuubiri upendo amani basi
 

Great thinker
 

Mazoko,
Sijui kwa nini hii makala ya Sheikh Suleiman Takadir imekukasirisha.

Hapa tulipofika panatosha.
 
Nashukuru kwa kutupa taarifa nani hasa alianzisha chokochoko za kidini Tanzania/Tanganyika. Yalikuwa makosa makubwa sana kutokujua chanzo hasa cha mambo haya ya kidini hapa nchini. Kujua chanzo cha tatizo ni mwanzo wa kupata ufumbuzi wa tatizo hilo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…