Jinamizi la Udini Tanzania: Utabiri wa Sheikh Suleiman Takadir


Maliedo,
Huna haja ya kuandika kwa ghadhabu,

Ukiandika hivyo unaweza ukanipoteza hata mimi unaetaka kufanya
mjadala nami nikakupuuza.

Kwanza ni kuwa unazungumza jambo usilolijua na hili ni tatizo kubwa.
Kambona hakuacha chuo Uingereza kwa ajili ya TANU.

Soma, tafiti, utajua ukweli kipi kilimfanya akaacha masomo.
Pili hayyo machafuko hayakuwa mwaka wa 1962.

Soma, tafiti, utajua ni mwaka gani yalikuwa machafuko.
Mimi siandiki topiki za dini kama unavyodai.

Nimeshaeleza hili katika post za nyuma tena kwa urefu na ushahidi
wa maktaba kubwa duniani zinazochambua maandiko na maudhui
kisha wakazipanga katika masomo stahiki.

Mwisho nataka nikueleze.

Mimi nilikuwa Mtafiti Msaidizi katika utafiti wa historia ya mapinduzi
Zanzibar nikifanya kazi chini ya mwandishi na mtafiti Dr. Harith
Ghassany
ambae kutokana na utafiti ule aliandika kitabu, "Kwaheri
Ukoloni Kwaheri Uhuru," (2010).

Katika kitabu kile hayo yote uliyouliza hapa kuhusu Oscar Kambona
yameandikwa na zaidi yake.

Unataka kufanya majadiliano na mimi kuwa na staha na adabu
tutajadiliana na sote tutafaidika.

Mwisho ni kuwa Mkwawa hakuhusika katika mkasa ule.
Tafiti, soma utakuwa mwerevu.

Usikurupuke ukaanza kutupa shutuma huku na huko.

Sasa rudi kwa adabu na niulize kwa uungwana nini unataka kujua
kuhusu Kambona nitakueleza toka alipokuja Makao Makuu ya TANU
1956.
 

Pasco,
Fumbo mfumbie mjinga...
 
Hizi historia zenu za kuungaunga uwa zinawadanganya sana angilia ulichoandika.

Kambona lina aliacha chuo na kuja kujiunga na TANU, wakati TANU inaanzishwa Kambona yupo Dodoma anafundisha.

Hayo mapinduzi ya mwaka 1962 ambayo Kambona aliyazimisha ni yapi?

Nakushauri tulizana na uliza maswali kiungwana utajifunza mengi.
 
Pasco,
Fumbo mfumbie mjinga...

Asante kwa kunielewa, na hii ndio inayoitwa communication ya one to one, kwa vile humu tunaandikia kwa ajili ya wengi, ukimaga mtama wenye punje wa dhahabu kwenye kuku wengi, kisha ukasimama kuwaangalia wanavyogombea mtama huo, huku jicho lako likikodolea ile punje ya dhahabu ili tuu kujua ni kuku gani ataimeza!, utafurahi ukishuhudia anayemeza punje ya dhahabu ni kuku wako!,
Maalim Al Alama Mohamed Said, asante kwa kuimeza punje yangu ya dhahabu katika bandiko langu!.

Thank God!, sifa na utukufu ni kwa Aliye Juu!.

Mission imposible!, the'll burn to hell, with their evil motives behind!.

Mungu ni Mkuu na muweza wa yote!.

Sisi sote ni waja wake tuu!.

God Bless You!.

Pasco.
 

Hizo porojo na kubwabwaja kwako ndiyo unaziita punje ya dhahabu? Amma kwa hakika mfa maji haishi kutapatapa.
 
Udini ungefifiisha jitihada za kupata uhuru.

Na kura ziliamua.

uamuzi wa kudemokrasia.
 

Duh,Respect mkuu...sikusifii kiunafiki Mzee Mohamed,Hongera unavyojitahidi kujibu bila hasira,panic na jazba.

Nimefurahia pia uwezo wako katika uandishi wa vitabu katika vyuo maarufu.
 

Umeongea point ya msingi sana kuhusu hizi dini tulizoletewa na wageni halafu tunazigombania. HAHAHAHAHA....DUH,HEBU TUTUMIE AKILI ZETU WAAFRIKA.
 
Pasco,


Hapa naona maneno matupu mie nadhani punje ya dhahabu kwenye huu mnakasha ni kuja na historia ya Tanganyika ili watu tupate faida.
 
Hizo porojo na kubwabwaja kwako ndiyo unaziita punje ya dhahabu? Amma kwa hakika mfa maji haishi kutapatapa.
FF alikuwa ni zamani!, huyu FF wa sasa wa kila siku porojo, kuhororoja na kubwabwaja bila mpango, huyu siye!.

Nadhani FF unaingia anga za miaka 45!, wengine hata umri huo bado, huanza kuonyesha dalili mapema ya zile PM disorders!. Hata hivyo kwa vile mimi ni muelewa, nimekuelewa, naomba na wale wengine wasiokuelewa tatizo ni nini, wakuvumilie tuu kama mimi ninavyokuvumilia kwa sababu naelewa mabadiliko yenu ya baada ya kuvuka miaka 45!.

Pole!, ndio ukubwa huu!, wengine huja vizuri, na wengine huja vibaya!, nilikuwa najiuliza yu wapi yule FF mwenye full mabusara?!. Sasa nimeelewa!.

Hata hivyo hongera kuutua mzigo wa ule usumbufu wa ile hali!.

Pasco.
 
Pasco,


Hapa naona maneno matupu mie nadhani punje ya dhahabu kwenye huu mnakasha ni kuja na historia ya Tanganyika ili watu tupate faida.
Historia ya Tanganyika au taasisi kubwa kama TANU inaandikwa na jopo la watu wasio na DINI wala KABILA mioyoni na vichwani mwao wakati wa kuiandika. Vinginevyo tutaandika kama alivyoandika Mzee huyu.
 

Mkuu ni mzigo upi alioutua mwana mama huyu FF?
 
Historia ya Tanganyika au taasisi kubwa kama TANU inaandikwa na jopo la watu wasio na DINI wala KABILA mioyoni na vichwani mwao wakati wa kuiandika. Vinginevyo tutaandika kama alivyoandika Mzee huyu.
Kwa hiyo historia ya Tanganyika bado haijaandikwa na ile ya Kivukoni iliandikwa na jopo gani?
 
Pasco,

Faiza ni mama mtu mzima sana pengine kuliko hata Mzee Mohamed. Kwenye mjadala kama huu huwa anaamua kujilipua tu. Anajua mzee huyu ni MDINI sana na ndio utambulisho wake. Anamsaidia ili apumue kidogo na makombora ya ndani ya JF.
 
Kwa hiyo historia ya Tanganyika bado haijaandikwa na ile ya Kivukoni iliandikwa na jopo gani?
Ya Kivukoni ambayo ndio tumesoma sote iliandikwa na wanazuoni wa taasisi hiyo. Inayo mapungufu kama yalivyo kwenye Biblia na Q'uran pia.
 

Al Akhiy Mohammad Said,

Kwa hishma kubwa tulikuwa na KIU kubwa ya kupata darsa hili la KUONDOSHWA KWA SHEIKH HASSAN bin AMEIR Na kuundwa kwa BAKWATA.

Tafadhwar Al Akhiy tunaomba Utudarsishe hapo ili tufyonze ilmu.

 
Umeongea point ya msingi sana kuhusu hizi dini tulizoletewa na wageni halafu tunazigombania. HAHAHAHAHA....DUH,HEBU TUTUMIE AKILI ZETU WAAFRIKA.

If you did not use them during the colonial times The Scramble for Africa hey days and you did not use them 50 years ago you will never use them again you will continue to pass the relay to you children and grand children generation by generation because your masters in reality never set you free.
For your clue just Search in Facebook for "Bring Back The Empire" teh teh teh.
https://m.facebook.com/profile.php?id=234069788705
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…