Kuishi kwa ndugu
Hichi ndio kipengele pekee nimelipenda , nimekumbuka kipindi nimemaliza form six nilienda kwa ndugu (baba yangu mdogo) mkoa fulani nyanda za juu kusini
Sasa kulikuwa na dogo mwingine ambaye si mwanae ni mtoto wa dada yake alikuwa akilalamika kuhusu mke wa jamaa kuwa anakauli za kibaguzi na ni kweli nilikuwa naona the way anawatreat wanae na huyo mwingine ni tofauti hivyo ilikuwa mumewe akiwepo ndio tunakuwa na ahueni ,
Kauli yake moja ilinifanya nipange safari ya kuondoka pale , alimwagiza mwanae majani ya chai dukani akampa elfu5 sasa watoto wakawa wanagombania kila mmoja anataka aende , huyu aliyepewa hela akakimbia nayo kufika getini kajikwaa kaanguka nakuanza kulia
Mama mtu kufika akasema kuna mijitu mikubwa imekaa tu haina kazi imerelax ,mtoto anaenda dukani akirudishwa chenji tsh 200 atajua?
Sikumaliza week 2 nikaondoka[emoji23]