Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Naomba muendelezo kuna kitu najifunza hapa mkuu....

Nina kesi ila Dah

Nilimlamba beki3. Kwa sasa ana mtoto hatujui mimba ni ya nani.

Katika kupelelewlza wakti namla bikira kuna mjanja aliishaitoa, huyo ni kijana wa mtaani, muuza duka. ..katika kumbana akamtaja, ila mimi nilikula vile vile..... kuuza duka alkubali baadae akasepa...


Hii kitu inaniuma kwa sababu mtoto hana hatia..

Nawaza nikubali au nikatae

Pembeni kuna wapambe kibao wanasubiri Saudi ya nimekubali




Mtoto ana miaka mitatu..inaniuma isije akawa damu yangu...

Hata kama sio bali mtoto hana hatia.

Mytake..sitakuja kumpa mimba mtu asiye au nisiye mipango naye
 
Wakati mwingine unajichanganya mpaka inafika sehemu unakua huna namna ya kufanya uamuzi. Sasa una mchepuko, ana mimba, unatembea na mfanyakazi wake.
Hapo tayari una mke, mtoto na huwezi muomba mama ushauri au Mzee wako, na kwao yeye ndo wa kiume mkubwa. Lazima uwe limited na option unazokua nazo kuhusu kuomba ushauri. Simcheki sana maana labda ninachomzidi ni kwamba huwa narudi tu Kwa Yesu na kumwambia tu Bwana Mkubwa Yesu nimefika mwisho wa kufikiria niongoze.
😃😃😃 Bwana mkubwa Yesu
 
SEASON 02:
EPISODE 24

“A TRUE STORY BY INSIDER MAN.”

CONTINUE:

Kipindi tuko kwenye flight kwa pembeni yangu dirishani alikuwa amekaa mzee wa makamo kwa kumkadiria umri wake kama miaka 60, kwa pembeni yetu opposite walikaa dada wawili, ambao walionekana kuwa busy sana wakijisnap.

Mzee alikuwa anawaangalia sana wale warembo huku akitabasamu, ilibidi nianze kuongea na mzee;

Mzee nakuona unawaangalia bint zako kwa makini sana vipi kuna tatizo?”

“Najaribu kufikiria kizazi chetu enzi hizo tunakua na kizazi hiki kipya, naona mabadiliko makubwa sana.”

“Upo sahihi mzee, sahivi technologia ni kubwa sana.”

“Sahivi unaweza kuwa na mtu pembeni yako na mnaelekea safari moja na hata msijuane wala kusalimiana sababu ya simu, unakuta mtu muda wote yuko busy na simu.“

“Ni kweli kabisa sahivi mtu anacheka na simu kama binadamu mwenzie.”

“Wazungu wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa sana kututeka na kucontrol akili zetu, ule ubinadamu naona unakufa kila siku, mtu anathamini simu kuliko binadamu mwenzie.”

“Mzee upo sahihi, hiki kizazi cha sasa Mungu atusaidie, simu zimetukamata akili kiasi kwamba hata ukiishiwa bando unaona kama maisha hayaendi.”

“Kila generation inapita na sifa zake, sijui hii ndo ile tuliyotabiriwa?. Anyway, wewe ni Mtanzania kama mimi, sina haja ya kukuuliza hili, unakwenda Zambia kwaajili ya nini?”

“Nakwenda kumsalimia mzee wangu pamoja na kuangalia fursa za biashara.”

“Safi sana hii ndo akili na umri wako?”

“Miaka 27.”

“Wewe ni kama kijana wangu wa mwisho kwa huu umri wako, bado ni kijana mdogo sana.”

“Hahahaa nashukuru mzee, vipi na wewe Zambia unaharakati gani?”

“Mimi nina deal na biashara za copper, kwahiyo nakwenda kwaajili ya masuala ya kibiashara.”

“Nimekuwa interested na biashara ya Copper unaweza kunipa ABC hata hapo baadae nikitaka kuifanya niwe na idea?.”


Mzee alinipa elimu kuhusu biashara ya Copa na namna ya kuanza pamoja na mtaji, Ila sasa changamoto kubwa niliyoiona ni namna ya kuingia sokoni maana wazee wa system wameshateka soko tayari la Copper.

Nilipiga story nyingi sana na mzee mpaka tunawasili Lusaka Airport, nakumbuka tulifika saa 3 za usiku na tulibadilishana namba za simu, alisema anakwenda hotelini.

Kwa upande mwingine, mzee wangu alikuwa amenisubiri pale uwanja wa ndege, kwani alifika mapema sana kwa ajili ya kunipokea. Alikuwa akisubiri kwenye sehemu ya mapokezi, na nilipotoka nje, alikuwa wa kwanza kuniona.

Baada ya kuonana tulisalimia na tulianza safari ya kwenda home, lakini tulianza kwanza kupitia kwenye moja ya mgahawa mzuri kwaajili ya kupata chakula cha usiku.

Mazingira ya Zambia pamoja na hali ya hewa yalikuwa ni ya tofauti sana, baridi ilikuwa ni kali kwa wakati huu wa usiku. Muda huu tukipata dinna mzee alianza kuniuliza kuhusu maendeleo yangu kwa ujumla, nami nikamuuliza jinsi maisha yalivyo nchini Zambia. Mzee aliishia kusifia maisha ya Zambia, akisema kuwa ni mazuri na sehemu salama ya kuishi.

Tulitumia kama dakika 45 kisha tukaondoka kwenda nyumbani kwake, anakoishi Lusaka, sehemu inayoitwa Roma. Alikuwa anakaa huko, na sehemu anayokaa ni kota nyingi ambazo zimepangiliwa vizuri sana.

Baada ya kuingia ndani hakukuwa na mtu yoyote nami sikutaka kuuliza maswali sana ukizingatia ndo ninafika hapa kwa mara ya kwanza. Tulifanya mazungumzo kidogo sana mambo mengi tulikuwa tumeshaongea njiani, na mzee aliishia kunionesha chumba changu, akasema nilale na mambo mengine tutaongea kesho.

Niliamka kwa kuchelewa ile asubuhi nikihisi njaa, nikajisemea, 'wacha niende jikoni nione kama kuna chochote cha kula.' Nilikuwa na uhakika nisingekosa kitu. Lakini nilipotoka chumbani, nikakutana na dada aliyekuwa amekaa sebuleni akipanga nguo. Sikuwa na wazo la kwamba kuna mtu mwingine ndani, kwa hiyo nilishtuka kidogo.

Hata dada naye alishtuka kuniona, maana hakutegemea kama kuna mgeni humu ndani. Alianza kupoteza ujasiri kwa sababu alikuwa amejiachia sana, mnavyojua jinsi wanawake wanavyovaa wakiwa peke yao. Nilimchunguza haraka na nikaanza kuwaza, ‘Huyu ndiye mamdogo nini?’ Nikamsalimia, na kwa bahati nzuri, dada alikuwa anaongea Kiingereza vizuri kabisa.

MIMI: “My name is Insider. Yesterday, I arrived here late but didn’t see you”

DADA: “Oh, really? What time did you get here?.”

MIMI: “I got here around 10 PM. Were you already gone by then?”

DADA: “Yes, I left around 7:30 PM. I don’t sleep here, I just come to work and then leave. Also, I don’t have any information about your presence here."

MIMI: “Mr. William is my father. I thought he told you everything about my presence."

DADA: “Oh, I didn't know that, maybe he forgot to tell me, and how long will you be here?"

MIMI: “I'm planning to stay for a while.”

DADA: “Nice, do you want to explore the area?"

MIMI: “Yeah! I'm looking forward to it. Do you have any recommendations?"

DADA: “Definitely, there's a great park nearby and some wonderful cafes, I can show you around if you would like."

MIMI: “That sounds great, thank you! I would love to.”

DADA: “Great, let's arrange for this weekend. It should be a lot of fun."

MIMI: “Have been loving our conversation but realize I don't even know your name lol.”

DADA: “Well my name is Sandra.”

Ndani ya muda mfupi nilikuwa nimeshazoena na dada huku tunapiga story na alikwenda kuniandalia chai, muda huu nilikuwa nimekaa sebleni nikishangaa TV.

Niliendelea kuwaza kuhusu dada pale, “ina maana mzee amemuajiri huyu dada awe anafanya usafi wa nyumba, anamfulia nguo na kumpikia afu anaondoka, na anamlipa mshahara kila mwezi?, ni vizuri lakini.

Baada ya kupata breakfast nilirudi chumbani kuendelea na mambo mengine, niliwasha laptop yangu ya Macbook niliyopewa na Iryn kama zawadi na nikaanza kupanga mipango yangu.

Mipango yangu ilikuwa niwekeze kwenye real estate na kufungua biashara kubwa kwa kule Dodoma, hivyo nilipanga nikitoka huku, nitakwenda Dodoma. Nilipata wazo la kuwasaliana na madalali wa kule ili waanze kunichekia fremu za biashara.

Baada ya kumaliza mipango yangu niliishia kulala pale kitandani maana sikuwa na kitu cha kufanya. Mchana nilitoka kupata lunch, nikarudi tena kulala na jioni dada alinigongea mlango, kisha akaniaga anaondoka na tutaonana kesho.

Saa 2 usiku mzee alirudi home na tulianza maongezi, kwa upande wangu nilimwambia sababu nyingine ya kuja Zambia ni kuangalia fursa za kufanya kama zipo.

MZEE: “Fursa nyingi sana kwa huku Zambia zipo ukanda wa Copper belt wanakochimba Copper, kule kuna fursa nyingi na vijana wengi wameaniriwa kule migodini.”

MIMI: “Vipi kuhusu biashara za nguo na mavazi maana naona wazambia wengi wanakuja Kariakoo kununua nguo.”

MZEE: “Biashara ya nguo ukisema ufungue huku itakusumbua ufuatiliaji, labda nikushauri uwe unauza kwa jumla, uwe na mtu wa kushirikiana nae huku, mimi baba yako niko busy sana, muda mwingi nakuwa site.”

MIMI: “Kuna dada nimeshinda nae siku nzima hapa home, umemuajiri awe anakufanyia kazi za humu ndani?”

MZEE: “Hapana, ameajiriwa na kampuni kwaajili ya hili, humu ndani sisi tunaishi wawili tu! mimi na ndugu yangu mmoja amesafiri.”

MIMI: “Na ofisi yako ipo wapi?”

MZEE: “Ipo Lusaka mjini kabisa itabidi kesho twende wote ukaijue.”

MIMI: “Sawa haina shida, jambo jingine naomba msaada wa Wi-fi tangu jana siko online.”

MZEE: “Wifi ilipata hitilafu kidogo, kesho tukienda ofisini tutachukua nyingine.”

Tuliendelea kuongea masuala mengine na nilitamani nimwambie kuhusu suala la Iryn, lakini Roho yangu ilikuwa inagoma katakata kumshirikisha hili suala, nilimuaga nikaenda zangu kulala.

Asubuhi na mapema tuliondoka kwenda kazini kwake, baada ya kuwasili pale ofisini alianza kunitambulisha kwa wafanyakazi wenzake na wao waliishia kumsifia mzee kuwa na kijana mkubwa na walionesha kunifurahia sana.

Kuna mama mmoja alitokea kunionyesha ukarimu na upendo wa hali ya juu sana, mpaka nikaanza kuwa na wasiwasi huenda akawa mchepuko wa mzee maana alikuwa akinijali sana.

Mzee wangu anafanyia kazi kwenye moja ya kampuni kubwa sana ya construction kwa kule Zambia na anafanya kama quantity surveyor, kazi zake nyingi asilimia kubwa ni kwenda site sehemu mbalimbali, ni mara chache sana kuwa ofisini.

Nilishinda na mzee ofisini siku nzima na jioni wakati tunarudi home alisema kesho anasafari ya kwenda kusini mwa Zambia sehemu inaitwa ‘Livingstone’ na angetamani twende wote. Niliona wazo la mzee ni zuri ukizingatia sababu kubwa ya kuja huku ni kutembea na kutuliza akili, kuondoka na mzee niliona ni heri kuliko kulala ndani tu.

Baada ya kurudi home niliingia online kuangalia watu walionicheki maana tangu nije Zambia sikuwasha data kabisa, nilikuta Hilda, Allen, Jane, Lucy, Mary, Wife, Dullah bila kumsahau Asmah walikuwa wamenicheki na wengine wengi.

Nilianza kwa kumpigia simu mke wangu ili kujua maendeleo ya familia, kisha nikajaribu kumpigia Asmah, lakini hakuwa online, hivyo nikamtumia ujumbe kumjulisha kuwa nimefika salama. Baadaye, nikampigia Dullah, ambaye alikuwa anatarajia kufunga ndoa Jumamosi hii. Ilibidi nimpe udhuru wa kutokuweza kushiriki, ingawa alilalamika sana, hatimaye alikubali kwa shingo upande.

Nilituma ujumbe mfupi kwa Hilda, kisha nikampigia simu Lucy, na ndani ya sekunde chache, Lucy alijibu simu yangu;

LUCY: “Wewe Insider kwanini hupatikani kwa simu? unanipa mashaka sana.”

MIMI: “Nimesafiri niko Zambia one time ndomana unaona hunipati kwa simu.”

LUCY: “Zambia? Una mishe gani huko?”

MIMI: “Nimekuja kutembea na kumsalimia mzee wangu.”

LUCY: “Ohh! Sawa, nimekupigia simu sana leo, hupatikani.”

MIMI: “Nambie kuna jambo gani unataka kushare mummy.”

LUCY: “Ni kuhusu Iryn maana hapatikani kwa simu since niongee nae ijumaa.”

MIMI: “Unajua hili suala linaniumiza sana akili ndomana nimekuja huku, nataka nitulize akili yangu kwanza, huenda nitapata solution.”

LUCY: “Solution ni kwenda South kuoanana naye myamalize, Iryn bado anahasira juu yako kwa kitendo cha kumpiga kule hotelini na bado anataarifa zako kuhusu kutembea na Asmah, na hili suala la mimba ndo linampa mawazo sana.”

MIMI: “Mimi niko tayari kufanya hayo yote ila sasa hapatikani, mpaka kaka yake Jimmy nae hapatikani nafanyaje?.”

LUCY: “Jaribu kumtafuta kaka yake kwa mara nyingine tena, huenda utampata.”

MIMI: “Sawa nitamcheki tena.”

Niliagana na Lucy pale, kwa upande mwingine alikuwa kashanikumbusha kuhusu Iryn maana nilikuwa nimeshamsahau tangu nije huku Zambia, nilijikuta naanza tena kufikiri upya kuhusu mambo yote yanayoendelea.

Muda huu simu ya Hilda iliingia na nilipokea tukaanza mazungumzo na kubwa nilitaka kujua maendeleo ya ofisi kwa ujumla, alisema kila kitu kinakwenda vizuri na niliendelea kumtia moyo kwamba awe ananitafuta pindi apatapo changamoto.

Baada ya kuagana na Hilda nilimpigia simu Iryn, hakuwa online, nilimcheki na Jimmy tena hakuwa online, bhasi nikalala zangu kwaajili ya safari ya kesho asubuhi.

Asubuhi na mapema dereva wa ofisi alikuja kutuchukua kwaajili ya safari ya kwenda Livingstone kusini mwa Zambia. Ilikuwa ni safari ya kukaa siku mbili na tungerudi jumapili, hivyo nilitembea na nguo za kubadilisha.

Saa 2 asubuhi ndo tulianza safari yetu, na umbali wa kutoka Lusaka mpaka Livingstone ni kama 450km, barabarani dereva alikuwa anatembea balaa, gari ilikuwa ni Hilux, na jumla ya watu tuliokuwa kwenye gari ni watano.

Saa 6 mchana tuliwasili Livingstone mjini, kingine kilichonishangaza ni vile eneo kuwa busy sana na asilimia kubwa ya watu wanaopatikana huku ni foreigners, wazungu ndo walikuwa wengi sana.

Mzee alinambia huku wazungu ni wengi sababu ya utalii kama unavyoona vile Arusha, na alisema hatupo mbali sana na Victoria falls, mbuga za wanyama, na watalii wengine wanavuka boda kwenda Zambezi National Park ya Zimbabwe.

Tulipofika ofisini kwao, ambapo wana tawi katika eneo hili, walianza kupanga mipango na kisha wakaondoka kwenda kukagua mradi. Kulikuwa na sheli mpya ambayo ilikuwa inaanza kujengwa, na hiyo ndiyo kazi iliyowaleta huku.

Mzee alinambia niende hotelini kupumzika wakati yeye anaendelea na majukumu ya ofisi, na kwamba baadaye tutakutana. Aliagiza dereva anipeleke hotelini, ambapo dereva alinipeleka New Fairmount Hotel. Booking ilikuwa tayari imefanywa, na mara tu nilipofika na kuoneshwa chumba changu, niliishia kulala kutokana na uchovu.

Mnamo saa 1 usiku, mzee alinicheki ili kupata chakula cha usiku pamoja na rafiki zake wawili, ambao tulikuwa wote safarini na tulifika katika hoteli hiyo. Kwa upande mwingine, walionekana watu kutoka mataifa mbalimbali ambao walikuwa wamekuja kwa ajili ya utalii, hotel za huku Livingstone zote ni za kitalii.

*****
Jumapili kabla ya kurudi Lusaka, mzee alinipeleka Victoria falls kushuhudia maajabu yake na alinambia bila kwenda kuona, sitakuwa nimefika Zambia kwa kweli, kwani ndoto ya kila mgeni ni kuona Victoria falls.

Saa 6 mchana tulitoka hotelini kuelekea Victoria Falls, na ilikuwa ni mwendo wa takriban dakika 10. Tulipofika, tulishuka kutoka kwa gari na kuanza kutembea kwa miguu hadi kwenye eneo la maajabu. Kwa mara ya kwanza, macho yangu yaliona maporomoko haya ya maji, na ilikuwa ni jambo la kushangaza kweli. Eneo lile linavutia sana, jinsi maji yanavyoshuka na mvuke unaopanda juu ni jambo la ajabu kabisa.

Tulisogea karibu na maporomoko ya maji kwa sababu kuna njia maalum zilizotengenezwa kwa ajili ya kutembea kwa miguu, ili uweze kushuhudia maporomoko haya moja kwa moja kwenye mto Zambezi. Upande huu tulikutana na watalii wengi sana.

Maajabu mengine Victoria falls imegawanyika kati ya Zambia na Zimbabwe na ndo mpaka unaotenganisha kati hizi nchi mbili. Pia, kuna daraja ambalo linatumika kama mpaka ‘Victoria falls bridge’, mbele kidogo kuna border ya Zimbabwe, ukienda mbele tena 12km unakutana na Zambezi National park, sisi tuliishia palepale border.

Jambo lingine ukifika huku utasikia kuna sehemu inaitwa ‘Devil pool’ ambayo inapatikana juu kabisa kwenye edge za mto Zambezi (Sehemu ambayo maji yanaanza kuanguka chini ndo hii pool inapatikana). Watu au watalii wengi huwa wanapenda sana kuogelea kwenye hio pool, nilijisemea ‘hawa jamaa hawako serious na lazima wana Roho ngumu’.

Tulimia kama masaa 4 kutalii maeneo haya na ndani ya muda mfupi nilitokea kulipenda sana hili eneo maana lilinavutia na mazingira yake ni mazuri, kwa upande mwingine nilikuwa nimeona kitu kipya kwenye mboni zangu, niliishia kupiga picha nyingi sana hii siku.

Saa 1 usiku tulianza safari ya kurudi Lusaka, kazi iliyokuwa imewaleta huku ilikuwa imekwisha tayari. Nakumbuka tuliingia Lusaka saa 6 za usiku maana kuna sehemu tulitumia masaa 2 kwaajili ya kupumzika na kupata dinna.

Kesho yake nilichelewa sana kuamka sababu ya uchovu wa safari na nilikuwa nikihisi njaa sana, niliamka ili nicheki chochote kitu nile. Nilikwenda dining na nilikuta chai ipo kwenye chupa imeandaliwa tayari, na muda huu nilimuona dada akitokea jikoni, baada ya kuniona alitabasamu na tukasalimiana.

SANDRA: “Nimekugongea sana leo, ulichoka sana na safari?”

MIMI: “Umejuaje? Jana tumeingia saa 7 za usiku na kule nilikuwa silali kabisa.”

SANDRA: “Kaka ameniambia mlikuwa Livingstone, hope ulienjoy.”

MIMI: “Nimeenjoy kawaida, nimepapenda pale Victoria falls, wish tungekuwa wote.”

SANDRA: “Hahahaa kaka ataniua akijua niko na kijana wake.”

MIMI: “Mzee hawezi kuharibu furaha yangu, labda wewe ukatae lakini hio sio sababu.”

SANDRA: “Unaondoka lini kwanza?”

MIMI: “Ijumaa nafikiri nitaondoka. Kesho tukatembee mjini bhasi, niyaone na mazingira na fursa za kuwekeza.”

SANDRA: “Sawa.”

Baada ya kupata chai nilimshukuru na nikarudi room kuendelea na mambo yangu, na ile kuwasha data nakutana na message kutoka kwa Mary, alikuwa akilalamika nimeondoka bila kumpa taarifa.

Nilimpigia simu ili tuongee na iliita kwa sekunde kadhaa akapokea;

MIMI: “Mambo Mummy.”

MARY: “Safi, nimekutafuta juzi na hujataka kunitafuta, na kwanini umesafiri bila kunipa taarifa?”

MIMI: “Sorry sana, nilikuwa na haraka mpaka nikasahau, I’m really sorry.”

MARY: “Insider sio kweli, kama uliweza kwenda kumuaga dada Jane?, ulishindwaje kunitumia ujumbe?”

MIMI: “Ndomana nimekuomba msamaha, kichwa changu kwasasa kimevurugwa kina vitu vingi sana, huwezi kunielewa kwasasa.”

MARY: “Not true, it’s just a matter of priorities, have a good day.” Na akakata simu.

Ukweli nilikuwa nimezingua sana kuondoka bila kumpa taarifa na sio kwamba nilifanya kusudi ila nilisahau sababu ya mambo yanayoendelea. Niliwaza ni busara nimtafute pindi kitakavyo rudi Dar ili tuongee, ila kwasasa nimuache atulie maana alionesha kuchukia waziwazi. Nilimpigia simu Jane kumjulia hali pamoja na mtoto na alisema anaendelea vizuri kabisa, na aliuliza nitarudi lini? maana amenimiss tayari.

Kwa upande mwingine wife alikuwa kanitumia ujumbe kwamba kuna plot nzuri ya kununua na tunaweza kulipa kwa awamu, alisema ni connection ambayo kapewa na mzee wake na ameshauri tuichukue maana ni potential sana na ipo Mapinga. Niliwaza pale nikaona wacha nirudi Dar kwanza ili nikaione, baada ya hapo ndo nitakwenda Dodoma kuendelea na mipango yangu.

Nilimpigia simu Iryn kwa mara nyingine tena, lakini hakuwa online na hapa sasa nilianza kupatwa na wasiwasi, nilijiuliza kwanini hapatikani? Kuna shida gani? Ni nini kinaendelea?, Au Iryn katoa mimba kwahiyo hataki usumbufu?.

Nilimpigia simu kaka Allen kumpa taarifa ya kinachoendelea kuhusu Iryn, lakini nae alinipa jibu jepesi sana, ‘eti nisiwe na wasiwasi atanitafuta tu’. Niliona bro! anazingua na sikutaka kumjibu chochote zaidi ningemvunjia heshima, nikamyamaza na kukata simu. Niliona kuendelea kumsikiliza ataniingiza shimoni, wacha nirudi Dar mapema, kisha nionane na Lucy, huenda tukapata solution.

Kuendelea kubaki huku Zambia na wakati sijui afya yake na mtoto, nitakuwa sifanyi jambo la busara, nikirudi Dar nitafanya maamuzi magumu hata ya kwenda huko Ethiopia.”

Niliplan kuongea na mzee badae akirudi ili nimpe taarifa ya kuondoka jumatano, kwa bahati mbaya hii siku alichelewa sana kurudi na kesho yake asubuhi aliwahi sana kuondoka. Niliwaza kumpa taarifa kwa simu, lakini niliona sio heshima, hivyo nilimtumia ujumbe kumpa taarifa kuwa nina maongezi na yeye baadae.

Saa 4 asubuhi tulindoka na Sandra kwenda mjini, nilitembea mfukoni na dolla 200 kwaajili ya kutusaidia njiani, tulipitia moja ya bureau de change nikampa afanye exchange na tulipata kwacha 4,000 na point.

Tulikwenda East Park Mall ambayo ipo Lusaka, kipindi tupo pale nilimpa offa ya shopping ya nguo mpaka viatu, na aliishia kufurahi sana maana hakutegemea hii surprise. Nilienjoy sana kuwa maeneo haya, kisha tulikwenda Manda Hill Mall ipo Lusaka pia, tuliingia moja ya mgahawa jina lake unaitwa Nando’s kwaajili ya kupata lunch.

Kipindi tunapata lunch tuliendelea kupiga story za hapa na pale kuhusu Zambia, kwa upande wangu nilikuwa namdodosa ili nimjue kiundani zaidi. Kupitia story nilibaini ni mkubwa kwangu kwa miaka 2, pia ana degree ya sociology na ameajiriwa na kampuni ambayo ilimpangia kazi pale home, lakini alisema amejishikiza bado anaendelea kutafuta ajira sehemu zingine.

Sandra alinitembeza maeneo mengi sana ya Lusaka na kwa upande wangu nilienjoy sana kampani yake na tulirudi home jioni sana, kwa lengo la kuwahi kupika chakula cha usiku. Baada ya kurudi home tulikuwa wote jikoni nikimsaidia kupika na nilimpa taarifa za kuondoka, lakini bado sijaongea na mzee.

Kwa upande wake alizipokea taarifa vibaya sana maana hakutegemea kuona nikiwahi kuondoka, alitamani sana niendelee kubaki Zambia, kwa kipindi kifupi tumetengeneza mahusiano na ukaribu.

Usiku tukipata chakula cha usiku, niliongea na mzee na kumpa taarifa ya kurudi Dar, ilikuwa ni taarifa ya kushtukiza, lakini nilimwambia ni mambo ya office ndo yanafanya nirudi mapema, pia, nina safari nyingine ya kwenda Dodoma.

Mzee kwa upande wake hakukubali mimi kuondoka kesho na alisema niondoke alhamis maana nimemshtukiza, sababu alijua nitaondoka weekend. Sikuweza kupinga, hivyo ilibidi nikubaliane na mzee niondoke siku ya alhamis, alinambia kesho kuna sehemu tutakwenda wote na tutaanzia kwanza ofisini.

Kesho yake saa 3 asubuhi tuliondoka pamoja kwenda ofisini kwake kuna vitu alisema anakwenda kuviweka sawa, baada ya hapo ndo tutaondoka kwenda hio sehemu.

Baada ya kuwasili ofisini kama kawaida mama alifurahi sana kuniona na aliishia kunikaribisha ofisini kwake kwaajili ya maongezi, yeye yuko department ya marketing.

Mama alikuwa akinijali sana, alinitengeneza kahawa akaniletea, kwa kumkadiria ni mama wa miaka 45 hivi mwenye asili ya Rwanda, alionekana kujipenda kuanzia uvaaji kwa ufupi ni mashallah!.

Tulikuwa tunapiga stori nyingi sana, maana alitokea kunikubali sana. Alisema huwa anakuja sana Dar es Salaam, hivyo atakuwa ananitafuta tuonane. Wakati wa mazungumzo, nilimgusia kuhusu familia yake, na akaniambia ana watoto wawili.

Nilianza kuwaza mbali sana, huenda mzee amejiweka hapa, kukaa Zambia kwa miaka 8 bila mchepuko haikumake sense kichwani, na kile kitendo cha mama kunijali nilikuwa nazidi kupata ukakasi.

Mchana tulitoka kupata lunch tukiwa wote watatu pamoja na mama, tulikwenda moja ya mgahawa wa karibu na ofisi;

MAMA: “Kijana wako ni mstaarabu sana anajitambua.”

MZEE: “Dume langu la kwanza nalitegemea hili, limenipa na mjukuu mkubwa.”

MAMA: “Ulinambia hili, amewahi majukumu maana vijana wengi wa age yake bado wanakaa kwao na wengine hawana direction.”

MZEE: “Kwahili kama baba najivunia sana.”

MAMA: “Insider embu nioneshe picha za mjukuu wangu nimuone.”

Nilitoa simu nikampa azione picha za Junior na aliishia kufurahi pale,

MAMA: “Anaonekana mjanja sana, nikija Dar nitakuja kuwasalimia.”

MIMI: “Karibu sana.”

Baada ya kupata lunch tuliagana pale, mama alikuwa anarudi kazini, alinitakia safari njema, tukapeana namba za simu. Kwa upande wake alitamani sana niende kwake nikapajue, lakini kutokana na muda isingewezekana.

Mimi na mzee tulikwenda moja kwa moja mpaka sehemu inaitwa Leopard hill, ulikuwa ni mwendo wa nusu saa hivi, njiani nilikuwa nashauku ya kujua mzee anataka kunionesha nini?.

Baada ya kufika eneo la tukio mzee alipark gari yake chini ya mti mkubwa, nilikuwa wakwanza kushuka kwa gari, nikaanza kushangaa mazingira. Eneo lilionekana kuwa na utulivu wa hali ya juu sana, nyumba zake zilionekana kuwa ni mpya na nyingine ujenzi ulikuwa ukiendelea.

Mijengo ilikuwa imesimama sana mazingira yake ni mazuri sana, kwa Dar es Salaam tunaweza kufananisha na Mbweni/ Kigamboni, jinsi ambavyo watu wanajenga majumba ya kifahari.

MZEE: “Nimekuleta hapa ili uone kiwanja nilichonunua, nina mpango wa kuanza ujenzi mwezi wa 6 na familia yote itakuja huku.”

MIMI: “What? Unataka umtoe mama kule mkoani aje huku?”

MZEE: “Ni mke wangu yule, hata kukaa nae mbali haitakiwi ndomana nikapata wazo nimalize ujenzi ili nimchukue tuishi huku na wadogo zako wale wadogo.”

MIMI: “Na nyumba ya kule mkoani itakuwaje?”

MZEE: “Tutapangisha au wewe ukitaka ukakae ni sawa, kwasasa wewe sikuhesabii maana unafamilia tayari.”

MIMI: “Ni kweli mzee.”

Tuliendelea kuangalia kiwanja pale na ukubwa wake ulikuwa ni ekari moja na kimezungushiwa senyenge.

“Bei za viwanja huku zikoje? Kwa haya mazingira nahisi bei zitakuwa juu sana.”

MZEE: “Kwa maeneo ya huku viwanja viko juu sana hasa miaka ya hivi karibuni, asilimia kubwa wageni na matajiri ndo wanajenga sana huku. Mimi nilinunua hiki kiwanja toka 2018, huku kulikuwa bado porini, kipindi kile viwanja vilikuwa ni cheap sana, na aliyenisaidia mpaka napata hiki kiwanja ni Manager wetu ila hayupo, amekwenda likizo.”

MIMI: “Ni kizuri sana, kwahiyo maisha yako yote utamalizia huku Zambia?.”

MZEE: “Nimeshakaa miaka 8 huku, tayari ni nyumbani, sioni sababu ya kurudi Tanzania.”

Tulishinda pale mpaka jioni maana mzee alikuwa anafanya vipimo vyake, mimi haya mambo sijui kwakweli, nilikuwa namsaidia tu pale huku tunapiga story za hapa na pale.

Baada ya kumaliza tulikwenda moja ya bar tukatulia kwaajili ya kupata dinna na kupata moja mbili tatu, story na mzee ziliendelea;

MZEE: “Ninafurahi kuona umekua mtu mzima sasa na una akili ya maisha, na ushukuru sana Mungu umepata mke mzuri na anayejitambua. Sikuzote familia bora inaanzia kwenu nyinyi wawili, mkishindwa kuelewana na kuishi vizuri, mtatengeneza kizazi cha hovyo sana.”

MIMI: “Ni kweli mzee kwa hili upo sahihi kabisa.”

MZEE: “Kuwa makini sana na wanawake wa nje, watakuharibia familia yako usipokuwa makini.”

Nikajisemea mzee anaongea nini sasa;

MIMI: “Siwezi kufanya mistake kwenye hili jambo, ahsante kwa ushauri.”

MZEE: “Wewe ushakuwa mtu mzima tayari na unaonesha njia nzuri kwa wadogo zako, naomba muendelee kupendana na kushikamana kama ndugu, hata pindi sisi hatupo duniani, bhasi familia inakuwa ipo sehemu salama.”

MIMI: “Sawa mzee kwa hili ondoa wasiwasi, lazima nihakikishe madogo nao wanatoboa.”

MZEE: “Violet ni dada yenu msimtupe pia, hata kama kaolewa, ni binti yangu, muendelee kuwa pamoja. Nina mpango Pasaka hii au ikishindika Christmas tukutane pamoja kwaajili ya kusherehekea.”

MIMI: “Ni wazo zuri, sisi hatuna shida tunakusikiliza wewe, nina ratiba ya kwenda home na familia Pasaka hii.”

MZEE: “Nitaangalia ratiba zangu, kisha tutawasiliana.”

MIMI: “Ahsante sana mzee mimi nimefurahi sana kukuona na kukaa hivi pamoja, ni muda mrefu sana umepita.”

MZEE: “Huku tumekuwa na muda wa kukaa sana pamoja, kipindi kile Dar nilikuwa nina haraka sana.”

MIMI: “Inshort nime enjoy sana, niwe mkweli na nimetokea kukupenda sana huku.”

MZEE: “Suala la mipango ya kufanya biashara huku, subiri kwanza mama yako aje ili iwe rahisi kukuangalizia project zako na zangu pia.”

MIMI: “Hili wazo zuri sana, tuendelee kuomba uzima naamini penye nia pana njia.”

MZEE: “Nikuombe sana ukawe baba mzuri kwenye familia yako, hakikisha Junior anakua katika misingi yako, malezi ya sasa yanachangamoto sana, ukifananisha na zamani. Heshima ya mwanaume ni familia na watoto ndo baraka, kama mimi navyojivunia sasa kuwa na wewe, badae iwe wewe kwa Junior.”

Tuliongea mambo mengi sana na mzee, kwa upande wangu nilikuwa nimepata kitu kikubwa sana kutoka kwake, na sikujutia kuja Zambia. Mzee alinishauri mambo mengi sana muhimu na ya msingi na tuliishia kuondoka kurudi home ili nikajiandae kwaajili ya safari.

Kesho yake niliwahi kuamka kwaajili ya kujiandaa na safari maana nilikuwa nategemea kuondoka na flight ya saa 8 mchana. Asubuhi Hilda anilipigia simu kunipa taarifa kuwa anaona kampuni inamuelemea sana, kwani anaona ofisi haina muelekeo. Habari nyingine mbaya aliyonipa ni kuhusu stock, ilikuwa inaishia afu hajui kama mzigo umeagizwa au laah, niliona ni changamoto sana, hivyo nilimwambia najiandaa kurudi Dar, na pindi nitakavyo land, nitamtafuta ili tuongee.

Nilimuachia ofisi Hilda katika kipindi kigumu sana ukizingatia hana experience ya kutosha, mbaya zaidi maboss wote mpaka mimi hatuko katika maelewano mazuri. Nilifikiri sana nikaona kuna haja ya kufanya something ili kuinusuru kampuni katika kipindi hiki kigumu.

Mzee aliondoka mapema kwenda kazini, alisema atarudi mapema kunichukua kunipeleka airport, hivyo niendelee kujiandaa. Kwa upande mwingine Sandra alikuwa amefika home na nilianza kupiga nae story za mwishomwisho huku namsubiri mzee.

Sandra kwa upande wake alikuwa haamini kama kweli naondoka leo, ukizingatia ndani ya muda mfupi tuliokuwa pamoja tulishakuwa na mahusiano mazuri sana. Nilimwambia siku aje Dar kutembea na apajue home, aliishia kukubali na alisema atafanya hivo, alisisitiza sana nisimdanganye kwa hili maana hajawahi fika Dar.

Saa 6 mchana mzee alirudi kunichukua, kabla ya kuondoka nilimuaga Sandra kwa kumkumbatia, tukabadilishana namba za simu na nikaondoka. (Sandra ni moja ya marafiki zangu wakubwa sana mpaka sasa, ameshaniconnect na rafiki zake wengi sana ambao wanakuja Dar).

Tuliondoka kwenda airport baada ya kuwasili, mzee aliomba nimpe akaunti yangu ya bank ili aniwekee pesa za matumizi ya mjukuu wake. Nilimpa akaunti ya Junior ili aziweke pesa huko maana zilimlenga yeye hivyo, sikuona sababu ya kuziweka kwangu.

Mzee aliniaga maana alikuwa anawahi kurudi kazini na mimi nikaenda kucheck in, lakini sasa niliambiwa ndege itachelewa kuondoka na itabidi tusubiri kwa masaa 2. Sikuwa na jinsi zaidi ya kuendelea kushangaa pale airport, baada ya masaa 2 na nusu ndo tulianza safari ya kurudi Dar, tuliwasili JNIA saa 2 za usiku, nikarequest bolt na kuanza safari ya kurudi home.

Baada ya kurudi home jambo la kwanza kufanya, nilimpigia simu Hilda kumpa taarifa kuwa nimerudi na kesho tutaonana kwaajili ya maongezi.
*****
hii 'story' ya zambia ni mimi peke yangu au na nyie wenzangu mmegundua ni 'kamba'?
 
Thanks God result imetoka vizuri mpaka sasa nina 1st class imenyooka, still hata research ikija vibaya nina uhakika wa 1st class.

Mwakani sikosi cheti cha Best student 🙏

Kwa kusherehekea results, kesho tutaendelea na mwendelezo.
Nasubiri Mtanange wa Sister v Iryn sijui nani alishinda🤦🏻‍♂️
 
hii 'story' ya zambia ni mimi peke yangu au na nyie wenzangu mmegundua ni 'kamba'?
Ni wewe peke yako, maeneo yote nayajua hakuna alikokosea hata moja, kujichanganya kupo kwa mgeni, but yuko sahihi. Nandos restaurant nimeshapata dinna pale, maeneo karibu yote nayajua. Victoria falls amekwenda mlemle,
 
Habari wakuu!....
Tusubiriapo next ep., waweza pitia huu uzi...... full of lessons

View attachment 3067815
Link:
Hii simulizi ni noma sana
 
Hapa mtakula pesa yangu tu, anyway naweka vocha ya 5k kama vocha kwa watu wa2 wa mwanzo kupatia.
Utabiri wangu next episode baada ya kufika south ilikuwa usiku hivyo kesho yake ndio mlianza kumtafuta mtamkutia irene hospital akitaka kufanya abortion ndio wewe utaomba msamaha pia sista ako atachangia kwa irene kubadili maamuzi ya kufanya abortion

Done!!!!
 
Back
Top Bottom