Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

Wakati wajumbe wanakaa kupitisha suala la stori kuwekwa Weekend tu sikuwepo maana nisingeunga hiyo hoja...Hii stori ilipaswa itupiwe humu kila siku jioni mtu unatoka kibaruani unajua kabsa kuna burudani ukifka home
Sisi tulipitisha nikiwa makamu mwenyekiti na kura ilipigwa na ikaonekana wengi wali unga mkono story iletwe ijumaa , jmoss na jpili

Na hili limekuja Muda mfupi baada ya baadhi ya wajumbe kusema hii story Ni chai tupu na Hakuna ukweli wowote ndipo bwana insider akaomba kuahirisha kutoa story yake na ndio baadae sisi tulifika Hadi nyumbani kwake makulu anakojenga kwenda kumuomba agahirishe uamuzi wake ndio akakubali alete every weekend

Hata hili ya kuleta ktk za week Ni kwamba amefunja mkataba tulio wekeana na hili alikubaliki kbsa namuonja atii mkataba wa kuleta story kila weekend
 
Sisi tulipitisha nikiwa makamu mwenyekiti na kura ilipigwa na ikaonekana wengi wali unga mkono story iletwe ijumaa , jmoss na jpili

Na hili limekuja Muda mfupi baada ya baadhi ya wajumbe kusema hii story Ni chai tupu na Hakuna ukweli wowote ndipo bwana insider akaomba kuahirisha kutoa story yake na ndio baadae sisi tulifika Hadi nyumbani kwake makulu anakojenga kwenda kumuomba agahirishe uamuzi wake ndio akakubali alete every weekend

Hata hili ya kuleta ktk za week Ni kwamba amefunja mkataba tulio wekeana na hili alikubaliki kbsa namuonja atii mkataba wa kuleta story kila weekend
Utakuwa unatamani kumuonja.
 
Sisi tulipitisha nikiwa makamu mwenyekiti na kura ilipigwa na ikaonekana wengi wali unga mkono story iletwe ijumaa , jmoss na jpili

Na hili limekuja Muda mfupi baada ya baadhi ya wajumbe kusema hii story Ni chai tupu na Hakuna ukweli wowote ndipo bwana insider akaomba kuahirisha kutoa story yake na ndio baadae sisi tulifika Hadi nyumbani kwake makulu anakojenga kwenda kumuomba agahirishe uamuzi wake ndio akakubali alete every weekend

Hata hili ya kuleta ktk za week Ni kwamba amefunja mkataba tulio wekeana na hili alikubaliki kbsa namuonja atii mkataba wa kuleta story kila weekend
Bora sasa INSIDER MAN amepata mtetezi wa kweli [emoji120]
 
EPISODE 26

“A TRUE STORY BY INSIDER”

Jumatatu ya Pasaka asubuhi nilifanya mawasiliano na yule constructor wa Mzee na nikamwambia baada ya lisaa nitakuwa Mbweni na yeye alisema yuko njiani ndo anaelekea.

Kwa upande mwingine yale materials ya kununua nilimtumia picha Mzee Mollel na alinisaidia kunitajia bei na kunipa connection kwa sehem yanakopatikana, alinitumia namba za baadhi ya masupplier akanambia nikiwapigia simu niwaambie yeye ndo amenikonekti.

Baada ya kufika Mbweni nilikuta kazi zikiendelea na mimi niliwasalimia Mafundi na Jamaa alikuwa amefika tayari.

Sababu alikuwa anajua kinachoendelea pamoja na ujio wangu, hata hakuwa na maswali zaidi alisema nimpe pesa akanunue materials.

“Kwenye kununua materials tutakwenda wote mkuu usiwe na wasiwasi.”

Na muda huu nilifanya kuwasiliana na baadhi ya supplier na tukapata mmoja pale Africana ndo alikuwa na bei nzuri.

Tulikwenda wote na Jamaa mpaka Africana kuna duka kubwa sana pale lipo mataa ya Africana, mkono wa kushoto kama unakwenda Juliana.

Tulifanya manunuzi ya materials mbalimbali na tukarudi Mbweni, vifaa vyote nilisimamimia manunuzi. Jamaa kama alimind hivi kwanza, pia hakuwa akiamini kuona nayajua maduka vile, kumbe nyuma ya Pazia alikuwepo mzee Mollel anayenipa CODE.

Sababu hii siku nilikuwa na miadi na Mama wa2, nilimwaga jamaa na nikaondoka. Nilitoka pale Mbweni kuelekea Mbezi Beach na muda huo ilikuwa saa 6 kasoro za mchana.

Hii siku tulikuwa tunakwenda kumpokea mdogo wake Airport na kuhusu kwenda kuangalia nyumba yake alisema tutakwenda siku nyingine.

Mama wa2 alitumia dakika 30 kutoka ndani na tukaelekea Airport.

“Insider Unaendeleaje.”

“Safi tu, mgeni ataingia sangapi?”

“Saa 8 atakuwa amefika tayari.”

Tuliwasili pale JNIA na tulikwenda moja kwa moja mpaka Terminal 2 ndo tukapark gari. Tuliamua kwenda kukaa kwenye kimgahawa tukimsubiri mgeni.

“Insider leo jioni nataka twende Masaki na wanangu tukatembee.”

“Sawa haina shida mimi nipo free leo.”

“Nilipata taarifa Uber wanasitisha huduma zao vipi kwako utafanyaje?.”

“Kwa wateja wa Card na kampuni bado wanaendelea ila wanaotumia card ni wachache sana, wateja wa cash ndo wengi kwa bongo hapa. Sio mbaya sana lakini maana Bolt bado wapo japo imeniathiri sana.”

“Pole sana ndo changamoto hizo naamini watarudi soon.”

“Ni mambo yanayohusisha serikali acha tuone itakuwaje.”

Suala la Uber kusitisha huduma zao kwa upande wa magari ni kutokana na LATRA kuwataka kupunguza kamisheni zao kutoka 25% mpaka 15%. Madereva wa Tax mtandao wolilamika kwa mamlaka husika kuwa hizi kampuni zinatoza kamisheni kubwa sana. Uber hawakuwa tayari kupunguza kamisheni zao kwani walisema wanatozwa kodi na tozo kibao hivyo wangeendesha biashara kwa hasara.

Tuliendelea kukaa pale na Mama wa2 huku story zikiendelea maana ndege ilichelewa kutoka KIA kwa taarifa ambazo Mama wa2 alizipata.

Saa 9 kasoro ndege iliwasili na na baada ya dakika 15 mamdogo alitoka na wakakumbatiana na dada yake pale. Walionekana kumisiana sana.

Nilimsaidia kubeba bag lake na tulikwenda parking tulikokuwa tumepark gari na tukaanza safari ya kurudi Mbezi Beach.

MAMA WA2: “Insider huyu ndo mdogo wangu wa mwisho anaitwa Joana.

MIMI: “Nimeona pia mmefanana sana, Joana karibu sana Dar es Salaam.”

“Ahsante.”

MAMA WA2: “Huyu anaitwa Insider ni mtu wangu wa karibu sana.”

MIMI: “Mama mkwe hujawai kunambia kuwa una mdogo mzuri hivi.”

Na wote waliishia kucheka muda huu na walikuwa wamekaa siti za nyuma.

Njiani walikiwa busy sana wakiongea mambo yao na tulitumia kama dk40 kufika nyumbani maana hakukuwa na foleni kabisa.

Tuliingia ndani muda ule na mimi nikatoa bag la mgeni nikaingiza ndani.

Baada ya kuingia ndani mamdogo alisalimiana na kina Rachel na Pili na mimi muda huu nilikuwa nawaza msosi maana njaa ilikuwa inanigonga balaa, toka asubuhi nilikuwa sijaingiza chochote tumboni.

Mama wa2 alitukaribisha dining kwaajili ya lunch na mimi ndo nilikuwa wakwanza kufika pale. Nilikuwa nimeshapazoea kwa Mama wa2 ilikuwa kama niko nyumbani tu.

Na wakati tuko dining Mama wa2 aliwaambia bint zake wajiandae kwaajili ya kutoka out. Mama wa2 alikuwa busy sana na mdogo wake hii siku hata nilipomaliza kula nilimshukuru kwa chakula na mimi nikaenda kukaa seblen.

Joana pia alikwenda kujiandaa na wakati huo bint zake walikuwa wako tayari wamejiandaa.

MAMA WA2: “Insider tunakwenda wapi eti?”

PILI: “Mama twende Slip way.”

MIMI: “Kama watoto wanataka kwenda huko tuwapeleke haina shida.”

MAMA WA2: “Bhasi tutakwenda huko.”

Na muda huu akina Pili na Rachel walionekana kufurahia sana kwenda huko.

Baada ya dakika 20 mamdogo alikuwa naye kajiandaa na ametoka hao tukaanza safari na muda huo ilikuwa saa 11 jioni.

Tulitumia dakika 25 kufika eneo lile na hii siku palionekana kuwa busy sana na tulikwenda upande wa chini wa Restaurant.

Tulitafuta sehemu nzuri ya kutosha watu sita na tukakaa, kwenye hii meza mimi pekee ndo nilikuwa mwanaume pale na hii ilikuwa ikinipa ufahari flani hivi.

Kila mtu aliagiza anachotaka kwa upande wangu sikutaka kuagiza chakula maana nilikuwa nimeshiba, niliagiza heineken 3 tu maana sikutaka kulewa hii siku. Kwa upande mwingine mama wawili aliagiza bucket ya Savanna kwaajili yake na mdogo wake.

Story zilikuwa zimetawala meza yetu tukicheka na mimi nilikuwa nimekaa karibu na Pili nampigisha story sana,

Sasa wakati dada analeta vinywaji Pili alishangaa sana kuona dada kaniwekea heineken pale mezani.

PILI: “Uncle Insider na wewe unakunywa kumbe?”

MIMI: “Nakunywa kwaajili yako hapa.”

PILI: “Toka hapa! mimi situmii pombe”

MIMI: “Wewe ni mchaga soon utaanza kutumia, muulize mama yako alianzaje kutumia. Unataka sikuonjeshe kidogo?”

PILI: “Aku sitaki mimi. Kwanza Baba yangu sio Mchagga”

Pili alikuwa kashanizoea kwa muda mfupi hata Mama wa2 alishangaa sana kuona Pili kanizoea haraka vile.

Mida ya saa moja usiku wakati tukiendelea kunywa na kupiga story, Prisca alinipigia simu, nikaamua kutoka eneo lile ili nikaongee naye mbali na pale.

PRISCA: “Hello baby how you doing?”

MIMI: “Niko poa za toka jana.”

PRISCA: “Safi tu, nimekumiss”

MIMI: “Jana ulinambia mnatoka as family nipe ripoti.”

PRISCA: “Insider ungekuwa unanijali ungekuwa ulinipigia simu na ukajua kinachoendelea.”

MIMI: “Aisee, nijue kinachoendelea kwenye mambo ya familia yenu?, naona kama unanikosea.”

PRISCA: “Sasa unataka ripoti ya nini?”

MIMI: “Ripoti niliyotaka mimi nijue ulirudi sangapi, Jana sikutaka kukutafuta maana nilijua utakuwa busy na Familia.”

PRISCA: “Okay we had funny yesterday, inshort we enjoyed.”

MIMI: “Nice na uko wapi kwa sasa?”

PRISCA: “Niko home nimelala on bed. Nimekumiss nataka nikuone.”

MIMI: “Acha uongo unanimisije na upo period?”

PRISCA: “Insider unataka kumaanisha kwasababu niko period siwezi onana na wewe? You only want sex from me that's all you care about.”

MIMI: “Prisca mimi naona hayo ni mawazo yako, ila naomba utambue kitu kimoja. Usifikiri mimi kama napenda sana kumchepuka Mama Junior na ninampenda sana. Unapaswa kunipa vile navyokosa kwa Mama Junior na sio kulalamika, kumbuka ulichagua mwenyewe na hukulazimishwa na kama unaona nakuumiza unaweza kuniacha na maisha yangu.”

PRISCA: “Leo ndo nimeprove upo na mimi kwasababu ya shida zako na huna hata tone la upendo kwangu, Ahsante nashukuru.” Akakata na simu.

Mimi sikutaka kumpigia tena simu niliamua kumpotezea na nikasema hasira zake zitakuwa sababu ya Period.

Wakati nimerudi pale mezani Mama wa2 aliniangalia afu akatabasamu

“Insider naona ulikuwa kujenga matofali”

Na mimi niliishia kucheka tu muda huu.

Tulikaa mpaka saa4 usiku ndo tukatoka pale na muda huu Mama J alikuwa akisumbua sana kwa kupiga simu.

Baada ya kuwashusha akina Mama wa2 alinipa malipo yangu na mimi nikaelekea nyumbani.

Nilimkuta wife yuko seblen anaangalia movie na mimi niliwasalimia na nikaunganisha bafuni kuoga.

Wakati nimetoka bafuni nilimkuta wife yuko kitandani amejilaza kizembe.

MIMI: “Nambie swahiba toka jana hatujaongea kabisa, hujanambia sikukuu ilikwendaje.”

WIFE: “Ilikuwa poa tu, Mama anakusalimia pia amesema uache tabia mbaya. Kwanini hupendi kujumuika na sisi?”

MIMI: “Usijali mwambie nitakwenda msalimia, na vipi kuhusu Mzee ulifanikiwa kuongea naye?”

WIFE: “Ndio alisema mwisho wa mwezi huu atanipa hizo hela.”

MIMI: “Wow nice umetisha sana swahiba, nafanya haya mambo kwaajili yako na hii bajaji tutatumia jina lako.”

WIFE: “Sawa haina shida, twende ukale maana leo nimekupikia vitamu.”

MIMI: “Sawa tangulia nakuja.”

Muda huu nilikaa kitandani maana nilikuwa nafuraha sana kuona jambo limefanikiwa tayari.

**********

Hii week baada ya Pasaka nilikuwa nashinda tu kule kwa Mzee Pama Mbweni. Asubuhi nikishawapeleka wateja wangu Posta naunganisha moja kwa moja mpaka Mbweni. Sikutakaa kaa mbali kabisa na eneo la tukio nilitaka kusimamia kila hatua kwenye ile nyumba.

Kazi ilikuwa inakimbia balaa na kwa upande mwingine mtu wa bustani alikuwa amekuja tukakubaliana bei na nikamwambia miti na maua tutakwenda nunua wote.

Mpaka kufikia jumapili nyumba ilikuwa imekamilika kila kitu kwa ndani na ilibaki vitu vidogo nje vya kumalizia kama kuweka tank na kumalizia pavings. Jumatatu ndo tulimalizia kila kitu na nikatafuta mtu wa kufanya usafi mle ndani, nje na kutengeneza barabara inayokwenda kwenye ile nyumba maana ilikuwa mbovu sana.

Kufikia jumatatu kila kitu kilikuwa kimekamilika vilibaki vitu vichache sana ambavyo sio vya lazima, lakini nyumba ilikuwa tayari kwaajili ya kuhamia.

Katika zile Pesa ambazo alinikabidhi mzee nilibakiwa na kama 3,200,000/= na hapo ndo nikajua jamaa alimpiga mzee japo pia nilipata discount kwenye mizigo ila kulikuwa na balance kubwa sana.

Niliitamani sana hii pesa lakini niliogopa jamaa anaweza kunisnitch kwa Mzee akampa hesabu za vitu na gharama zote afu nikapoteza trust kwa Mzee. Palepale nikachomoa million moja nikasema hii nitaitolea maelezo kwa Mzee ila hii amount inayobaki nitamrudishia.

***********

Kwa upande mwingine Jumapili ndo siku ambayo Pili alikuwa ana rudi shule hivyo Mama wa2 aliomba kampani yangu.

Nilitoka Mbweni kuelekea Mbezi Beach kwa Mama wa2 na saa 7 mchana nilikuwa pale.

Saa 8 mchana ndo tulitoka kuelekea Bagamoyo shuleni. Tulitumia saa moja na nusu kufika Bagamoyo shuleni na Mama wa2 alikwenda kumkabidhi.

Na hii siku walionekana Wazazi wengi wakiwarudisha watoto wao shule.

Baada ya kumuandikisha kuna sehemu tulikaa tukiwa tunaongea na mimi nilimshauri sana Pili asome kwa bidii na akae mbali na wanaume. Ilibidi nimchane ukweli ajitunze Mafisi “wazee wa kula kimasihara” sio watu wazuri Kabisa awe makini.

Pili alionekana kuwa makini sana akisikiliza ushauri wangu na nilitoa laki moja nikampa itamsaidia kama pocket money.

Niliona aibu kumwacha bila kitu afu mama yake alikuwa kanisaidia mkopo wa Pesa nyingi, niliamua kurudisha shukrani kwa njia hiyo.

Pili alishukuru na alifurahi sana, akasema next time nikamchukue na Mama yake pia alimpa Matron namba yangu incase kama kuna lolote wanaweza kunipigia na mimi. Na mama wa2 alininiandikisha mimi kama Uncle wa Pili.

Tuliondoka pale shuleni na kuanza safari ya kurudi Dar na njiani tulikuwa tukiongea mambo mengi sana na Mama wa2.

MAMA WA2: “Insider mwanangu Pili amekuzoea haraka sana, the way ambavyo unaongea naye nilikuwa najiskia faraja sana. Baba yake hajawai hata siku moja kumpa ushauri binti yake nashukuru sana kwa leo.”

MIMI: “Pili ni kama mdogo wangu lazima nihakikishe anafikia malengo yake na kama unajambo lolote usisite kunambia.”

MAMA WA2: “Next time utamfata wakifunga shule.”

Tulitumia lisaa kufika Mbezi Beach nikamwacha kwake na mimi nikarudi zangu home mapema sana.

Usiku mzee alinicheki akanambia kesho nikamchukue Airport ndo anarudi na anatarijia kuingia saa 7 mchana na alinisisitiza sana kuwa ontime, maana tungeenda na kukagua nyumba kule Mbweni.

Asubuhi nilimka mapema na nikafanya usafi wa gari mwenyewe na baada ya kumaliza nilirudi ndani ili nipate kifungua kinywa.

*********

Tarehe 26 ndo siku ambayo mzee alirudi kutoka safari na ilikuwa ni siku ya Muungano. Na mimi mapema sana nilikuwa pale Terminal 3 nikimsubiri.

Nilimcheki dada Tyna akanambia yuko busy atanichek mida kidogo, na muda huu nilikuwa nikipiga story na yule jamaa yangu mlinzi.

Saa 8 kasoro ndo muda ambao mzee Pama aliwasili pale JNIA na nilimpokea na baada ya dakika chache tuliondoka maeneo yale.

Safari yetu ilikuwa ni kwenda moja kwa moja mpaka Mbweni ili afanye ukaguzi wa nyumba. Na tulitumia saa moja na nusu kufika pale

Mzee alifanya ukaguzi wa nyumba na aliridhika kuona jinsi ujenzi ulivyokuwa umekamilika vizuri tena kwa viwango vya hali ya juu. Pia alishangaa kuona nimetengeneza ile Barabara na imekaa vizuri, alishangaa kuona nimetengeneza bustani mpaka nje ya geti na palikuwa pamejengwa vizuri. Mzee pia alinisifu kwa kufanya usafi wa nyumba nje na ndani.

Mzee alimjengea mchepuko wake mjengo mkali sana tena wa kisasa, nyumba ilikuwa kubwa ya vyumba vinne.

MIMI: “Mzee naona unataka kuwa na Familia kubwa vyumba ni vingi sana.”

MZEE: “Nataka anizalie watoto wa3 hata pale tayari ni mjamzito.”

MIMI: “Hongera sana Mzee ni jambo la neema hilo.”

MZEE: “Kabisa, Kijana niseme Ahsante kwa kazi nzuri uliyofanya umenifurahisha sana, materials ni zenyewe hakuna ulichokosea.”

MIMI: “Mzee nilikuwa namsimamia Fundi mwanzo mwisho nilikuwa nakuja asubuhi nashinda na Mafundi jioni narudi nyumbani. Ndomana unaona kila kitu kimeenda vizuri na kwa wakati sahihi.”

MZEE: “Hii nyumba nimejenga kwa siri sana hakuna anayejua kabisa hili suala.”

MIMI: “Sasa suala la watoto vipi hutaki wajuane?”

MZEE: “Hao hakuna shida watajuana tu ila sitaki ifahamike kama mke mdogo anakaa huku italeta shida.”

MIMI: “Sawa mzee hapo nimekuelewa”

Mzee Pama alikuwa ni mzee wa umri wa miaka 60-65 alikuwa anacheza humu ila alikuwa ni dizaini ya wale wazee wajanja au wahuni.

Tulitoka pale Mbweni saa 11 jioni na Mzee alinambia nimpeleke kwake Ununio.

Wakati tumeingia kwenye gari nilifungua drow na nikatoa invoices za manunuzi na nikamkabidhi, na alianza kuzitizama muda ule.

MIMI: “Mzee na hii Pesa ndo ilibakia kwenye manunuzi.”

MZEE: “Kijana kama pesa imebaki ni yako, umefanya kazi kubwa sana. Bila kumsimamia Fundi vizuri angenipiga yule mshenzi.”

Nilimshukuru Mzee na nikawasha gari ili tuondoke eneo lile. Nilimpeleka Mzee kwake ununio na akaniahidi kunitafuta kwani kuna vitu vya kununua vingi anataka nimsaidie kusimamia.

Muda huu nilijikuta nam-miss sana Iryn kwakweli, kwani ndo ilikuwaga mida ya kwenda kwa Iryn kumchukua. Licha ya yote Iryn alikuwa ni moja ya watu wangu wa karibu sana na ilitokea kuelewana sana.

Tulikuwa tunakwenda karibu mwezi bila mawasiliano yoyote na nilikuwa sijui maendeleo yake, kipindi hiki.

Kwasababu mwisho wa mwezi ulikuwa umekaribia nikawaza muda ule niende kwake Kijitonyama. Na lengo langu ilikuwa nijishushe nimwombe msamaha kama kuna sehemu nilimkwaza.

Niliona sometimes ni bora kuwa mjinga ili mambo yako yaende ila kwa upande mwingine niliwaza hivi nikijishusha sana si ataniona mimi bwege? Yaani bila yeye maisha yangu hayaendi? Niliwaza pale ataweza kunisumbua sana huko mbeleni. Pia nilikuwa nawaza ni jambo gani ambalo limemkera mpaka kuchukua maamuzi yale?. Iryn ni mwanamke ambaye ni hatabiriki “UNPREDICTABLE”.

Saa 12 jion nilikuwa pale kwa Iryn Kijitonyama na hata sikumpigia simu niliamua kwenda bila kutoa taarifa, nilitaka iwe saprize.

Nilipark gari nje ya geti na nikafungua geti maana nilikuwa tayari mwenyeji kwenye zile apartments. Niligonga mlango wake na baada ya dakika kadhaa alitoka kufungua.

IRYN: “Ooh Insider karibu na nilikuwa nawaza nikupigie simu toka jana ili uje tumalizane maana namzigo wako.”

MIMI: “Ooh sawa ila mimi sijaja kwaajili ya hilo, nimekuja kukuona na kukujulia hali maana ni muda kidogo toka unitumie ile text ya kuterminate mkataba, pia nilitaka kujua sababu ni nini mpaka ukaamua vile.”

IRYN: “Insider hakuna sababu yoyote na hakuna jambo lolote baya ambalo umefanya, ila nataka kufocus na masuala ya mama kwa sasa.”

MIMI: “Kama hakuna jambo nililokukosea ungenipigia simu na tungekaa chini tukaongea. Iryn mimi ni binadamu sijakamilika kwa asilimia mia, kama kuna sehemu nilikukosea nisamehe. Iryn naomba utambue mimi ni Mwanaume ambaye nakuheshimu sana na bado utaendelea kuwa mtu muhimu sana kwenye moyo wangu.”

IRYN: “Insider hakuna shida mimi naona wewe ndo una wasiwasi.”

MIMI: “Hapana mimi nimekuja kukuomba msamaha pale ambapo sikuwa sawa na nimekukosea. Sijaja hapa kuomba unirudishe kazini, masuala ya kazi ni yako na ni maamuzi yako wewe.”

Na muda huu Iryn hakuongea kitu bali alifunga laptop yake na kuingia chumbani na mimi nilikaa pembeni ya coach. Na baada ya dakika 3 Iryn alitoka akiwa ameshika bahasha ndogo ya kaki

IRYN: “Insider pesa zako hizi nimeweka na fine ya kuvunja mkataba na wewe.”

Na muda huu alinikabidhi ile bahasha na mimi nikasimama nikaipokea ile bahasha pale na nikaiweka mfuko wa nyuma.

MIMI: “Ahsante but nishaelewa tatizo ni nini.”

IRYN: “What do you mean?”

Na muda uleule nikamshika mikono yake miwili na nikapandisha mikono yangu kuzunguka kiuno chake na nikamvuta upande wangu kwa nguvu, kilikuwa kitendo cha ghafla sana. Nikampa ulimi wangu na yeye akanipa wake haraka bila kizuizi na tulichezeshana pale kwa sekunde kadhaa na palepale tulishtuka tukaacha ule mchezo.

MIMI: “I mean hiki ndo ulichokuwa unakitaka, Iryn thank you for everything, I have missed you so much. Mimi naondoka nikutakie maisha mema ila kama utahitaji msaada wangu never hesitate to call me. Byee.!

Nilimwacha pale Iryn katika sintofahamu kwani hakuweza kuongea neno lolote muda ule na alikuwa akiniona nikipotea machoni mwake live.

Na wakati niko kwa gari nilikuwa mtu mwenye furaha sana na kama nilikuwa nimepata Nguvu mpya na nikajisemea pale “When one door closes another opens.”

TO BE CONTINUED
Biashara ya Uber pia imeniachia kumbukumbu mbaya sana ambayo sitokuja kuisahau kwenye Maisha yangu.

“MEMORIES NEVER DIE.”
Imekuachia kumbukumbu gan mbaya
 
EPISODE 36

“A TRUE STORY BY INSIDER”

Muda huu nilianza kujilaumu kwa kutotilia maanani hili suala, niliwaza pale hata Police wangeniona mimi ni mzembe sana. Nilivuta pumzi ndefu sana na nilijikuta macho yangu yakiwa yamejaa machozi na mapigo ya Moyo yalianza kuongezeka spidi.

CONTINUE….

Mtoto wa kiume nilitokwa na machozi muda huu na mawazo yalikuwa yananiambia Iryn atakuwa ametekwa. Nilitafakari pale, Muajemi ameondoka jumanne kwenda Iran na alisema kaongea na Iryn Jumatatu. Niliwaza huenda Muajemi kafanya jambo, haiwezekani iwe harakaharaka hivi, na muda huu Rose alitoka ndani akiwa amevaa skin jeans.

ROSE: “Jiran niko tayari tunaweza kuondoka.”

MIMI: “Sidhani kama Police ni muhimu kwa sasa nafikiri tuendelee ku-buy time kwanza, I have a plan.”

ROSE: “Jiran hivi hujui kwamba utajiweka kwenye matatizo? Maana mpaka sasa wewe ndo first suspect.”

MIMI: “I know, Iryn ana mama yake mlezi nadhani utakuwa unamjua, nafikiri tuwasiliane naye kwanza.”

ROSE: “Sijakuelewa Jiran unamaanisha nini?”

MIMI: “Kuna Mama Mzungu anakujaga hapa mwenye hizi apartments.”

ROSE: “Yule mama Mzungu ambaye anaongea kiswahili vizuri ni ndugu na Iryn?”

MIMI: “Exactly yule ni Mama mlezi wa Iryn na alikuwa rafiki wa mama yake kipenzi.”

Ilibidi nimpe historia kidogo kuhusu maisha ya Iryn mpaka kifo cha mama yake na mpaka Mama Janeth kuwa mama mlezi wake.

ROSE: “Jiran mimi sijawai kufaham kama yule Mama mzungu (Mama Janeth) ana undugu na Iryn, ila nilishawai kumwona mara 2 lakini sikujua kama ndo mwenye nyumba.”

MIMI: “Plan yangu kabla hatujakwenda Police ni bora niwasiliane naye kwanza huenda anajua kinachoendelea.”

ROSE: “Umewaza jambo zuri.”

Nilitoa simu yangu kwenye gari na nilitafuta namba za mama Janeth ambazo Iryn alinitumiaga kipindi kile napeleka mzigo kwake na nikazipata. Nilipiga ile namba lakini ilikuwa haipatikani na nilirudia kama mara 5 lakini ilikuwa haipatikani.

MIMI: “Jiran hapatikani acha niende Masaki kwake.”

ROSE: “Unajua anakoishi? Twende wote.”

Tuliondoka pale Kijitonyama na tulikwenda Masaki moja kwa moja mpaka kwa Mama Janeth. Baada ya kufika pale kwake nilipiga honi na baada ya dakika kadhaa alitoka mlinzi ambaye ndo nilikuwa namwona kwa mara ya kwanza na alikuja upande wangu, na mimi nikashusha kioo.

MLINZI: “Bro habari nikusaidie nini?”

MIMI: “Kaka nashida na Mama Janeth sijui nimemkuta?”

MLINZI: “Mama Janeth ni nani? Usije ukawa umekosea nyumba.”

MIMI: “Bro anaishi hapa hata week iliyoisha nilikuwa hapa, unaonekana ni mgeni hapa ndomana humjui, ana watoto wa2 wa kizungu wakiume na kike.”

MLINZI: “Kaka sasa nimekuelewa kama ulikuja week iliyopita huyo sijui mama Janeth atakuwa amehama, maana sisi tumehamia hapa Ijumaa na tunaweek tayari tuko hapa na huyu Tajiri nimeanza naye kazi muda mrefu sana.”

ROSE: “Kaka tusaidie kama yupo maana tumekuja kuonana naye kuna jambo muhimu sana tafadhali.”

MLINZI: “Hata mimi nawaona mmekuja kwa mazuri nayowambia nikweli kabisa, sisi tuna week hapa toka tuhamie.”

Ukweli nilikosa cha kusema na sikuielewa hii movie kabisa inavyokwenda, kitendo cha Iryn kupotea kimaajabu na kutopatikana na bado mama Janeth hapatikani na ninaambiwa amehama kilinipa maswali sana muda huu.

MIMI: “Jiran hii movie siielewi naona kama sina maamuzi kwa sasa.”

ROSE: “Hauna Plan B ya kumpata Mama Janeth?”

MIMI: “Ipo twende saloon huenda dada wa pale atakuwa na mawasiliano naye.”

ROSE: “Let’s go.”

Tulindoka maeneo yale na tulikwenda saloon yao ya kulekule Masaki na baada ya kufika pale nilikwenda moja kwa moja ndani.

Baada ya kuingia ndani niliwakuta wafanyakazi wakiwa busy sana na niliwasalimia pale.

“Sumaiya nimemkuta?”

“Yupo alikuwa around hapa ngoja nimpigie simu.”

Dada alitoa simu yake mfukoni akapiga simu na wakaanza kuongea pale,

“Anakuja unaweza msubiri pale kwenye coach.”

“Dada mimi niko nje parking namsubiri.”

Nilitoka ndani na nikaenda parking nilikokuwa nimepark gari.

ROSE: “Jiran what is going on?”

Na muda huu Rose alishuka kwenye gari na akasogea karibu yangu. Rose alionesha kuguswa sana na hili jambo na alionesha kunionea huruma sana.

ROSE: “Jirani pole sana najua unapitia wakati mgumu sana kwasasa ila tutampata akiwa mzima kabisa, hata mimi hili jambo limenigusa sana, kwa kipindi tulichoishi na Iryn, nimetokea kumpenda sana.”

MIMI: “Ahsante sana Jiran ngoja huyu dada aje tuone atakuwa na jambo gani.”

Baada ya dakika 10 Sumaiya alitoka na alikuja moja kwa moja mpaka Parking nilikokuwa nimepark gari. Sumaiya alikuwa ni msimamizi wa Saloon kwa upande wa Masaki kama alikvyokuwa Lucy msimamizi wa Mikocheni na Sinza.

SUMAIYA: “Hi Insider za wewe? Dada mambo?”

ROSE: “Safi za kwako?”

MIMI: “Umetuweka sana hapa ujue.”

SUMAIYA: “Sorry nilikuwa nina mteja nisingeweza kumwacha katika mazingira yale.”

MIMI: “I know usijali, nimekuja hapa kwa jambo moja tu.”

SUMAIYA: “Jambo gani Insider?”

MIMI: “Mama Janeth simpati kwa simu na nimekwenda kwake naambiwa amehama.”

SUMAIYA: “Mara ya mwisho tumeongea Jumapili na sijampigia tena maana sahivi hatuja pungukiwa na kitu na tukitaka kutoa mzigo si tunakucheki wewe?. Kidogo kumpigia simu kumepungua afu mauzo tunatuma report kwa Queen (Iryn).”

ROSE: “Na alikohamia unakujua?”

SUMAIYA: “Hapana hata alikokuwa anaishi before sikujui na sijawahi fika, mara nyingi mazungumzo yetu yanafanyika hapahapa ofisini. Si uwasiliane na Queen akupe namba zake?”

MIMI: “Mpaka nimekuja kwako kutafuta namba za Mama Janeth ni kwamba Iryn hajulikani aliko toka jumatatu, Mama Janeth ndo mtu pekee aliyebaki wa kuokoa hili jahazi maana tunataka kureport Police.”

SUMAIYA: “Insider acha kupoteza muda wako, unahangaika kumbe amejifungia Hotelini na Bwana wake. Acha kupoteza muda amini maneno yangu hata uko Police usiende kabisa.”

Na muda huu Rose alimkata jicho kali sana Sumaiya.

ROSE: “Naona unaleta masikhara kwenye vitu serious mtu zaidi ya week asipatikane? haimake sense.”

SUMAIYA: “Nachoongea ni kweli, Insider jaribu kumpigia Bossy au mtext kwenye whatsapp.”

MIMI: “Sawa Ahsante miss.”

SUMAIYA: “Insider trust maneno yangu, ukimpata Queen nijulishe.”

Sumaiya hakuonesha kujali kabisa na alikuwa akileta matani sana muda huu. Na sisi tuliondoka eneo hili kurudi Mikocheni na muda huu Lucy alinipigia simu na tukakubaliana tukutane palepale kwa Iryn.

ROSE: “Jirani usipompata Mama Janeth Whatsapp tunafanyaje?.”

MIMI: “Nafikiri turudi home pale tuonane na jirani mwingine na pia kuna dada atakuja anasimamia saloon za Sinza na Mikocheni tutapata majibu.”

ROSE: “Sawa, zote ni saloon zake?”

MIMI: “Yeah zake.”

ROSE: “Yuko vizuri sana nilikuwa namchukulia poa sana.”

Tuliwasili pale Kijitonyama na tulimkuta Lucy kafika tayari anatusubiri sisi, na muda huu giza lilikuwa lishaanza kuingia.

LUCY: “Insider vipi umefanikiwa kuonana na huyo Mama Janeth?”. Lucy alikuwa hamfaham Mama Janeth.

MIMI: “Hapana kwakweli Mama Janeth hapatikani na pale kwake kahama.”

LUCY: “Amehama toka lini?”

MIMI: “Hata mimi sielewi kwakweli maana last week jumanne nilikuwa pale kwake, leo tunaambiwa amehama.”

ROSE: “Mimi nahisi mlinzi hajataka tu uonane na Mama Janeth.”

LUCY: “Hata mimi nahisi hivyo.”

Na muda huu tulisikia geti likifunguliwa na alikuwa ni yule jamaa Jirani. Baada ya kuingia ndani na kupark gari alishuka na alivyotuona tumesimama pale kwa Iryn ilibidi asogee.

JAMAA: “Habari zenu Majirani, vipi kuna usalama hapa leo?.”

Na wote tuliipokea salamu yake

ROSE: “Jirani hapa hakuna usalama, ndugu yetu Iryn hajulikani aliko na mara ya mwisho kupatikana kwenye simu ilikuwa jumatatu.”

MIMI: “Labda Jirani mara ya mwisho ulimwona Iryn lini?”

JAMAA: “Nilimwona jumatatu jioni wakati narudi kazini na alikuwa amesimama hapo kibarazani, tulipungiana mikono na mimi nikaingia ndani.”

Na muda huu Jamaa alikwenda kusimaa eneo alilokuwa Iryn.

MIMI: “Mpaka sasa tuna uhakika Iryn Jumatatu alikuwa maeneo haya, sasa nini kimetokea asipatikane kwa simu na bila kuwa na taarifa yoyote?”.

JAMAA: “Bro! Wanawake wana siri nyingi sana labda nikuulize toka mkutane na shem mna muda gani?”

MIMI: “Tuna miez mi-nne sasa.”

ROSE: “Mimi nafikiri tu ripoti Police hili jambo mapema, naona hili suala linazidi kuwa gumu sana.”

JAMAA: “Unakuta huyu mtu amekufa huko ndani au alitekwa kwa maelezo yanayotolewa hapa mimi nafikiri hivyo.”

ROSE: “Guys twendeni Police jamani!”

LUCY: “Police hapana mimi Roho inaniambia Iryn yupo somewhere, Insider huwezi kutafuta means ya kumpata mama Janeth kama whatsapp hapatikaniki?”

MIMI: “Itabidi Jumatatu sasa niende ofisini kwake.”

JAMAA: “Bro mara ya mwisho ulikuwa na shem lini?”

MIMI: “Tuliondoka Ijumaa kwenda Zanzibar na tukarudi Jumapili usiku.”

JAMAA: “Mlitoka wawili tu?”

MIMI: “Hapana tulikuwa watatu afu Iryn sio mpenzi wangu kama mnavyofikiri ni mtu wangu wa karibu.”

Ilibidi niwape mkanda mzima wa kule Zanzibar tangu tunakwenda na kurudi na sikutaka kuficha suala la Muajemi.

JAMAA: “Kwa maelezo yako inaonesha huyo Muajemi anamtaka Iryn kwa njia yoyote ile na hatuwezi jua mpaka Iryn anakubali offa yake kwenda Zanzibar alipewa nini. Bro hawa wanawake sometimes wanasiri nyingi sana huenda amekula Pesa za jamaa nyingi sana. Kama dada alikuwa anamkazia huenda jamaa kaamua kumfanyia kitu mbaya wanasema usishindane na tajiri. Swali langu lingine kwanini akuage haraka anakwenda Iran?, something crazy is going on, kama alimwekea sumu huko Zanzibar ambayo itamwuua taratibu utajuaje?”

Maneno ya Jamaa yalituingia vizuri kila mmoja alikuwa anaguna tu muda huu, jamaa aliongea point sana.

ROSE: “So what’s next?”

JAMAA: “Tufungue mlango tuangalie ndani kwanza kwa suala la Police inaweza kuwa msala zaidi, Bro wewe ndo utakuwa kikaangoni na msala wote utabaki kwako ujue, sisi wengine tutakuwa mashahidi tu.”

ROSE: “Una maanisha tuvunje geti na mlango?”

JAMAA: “Yeah atleast tutapata picha nzuri ya kuanzia.”

ROSE: “Huoni kama tutasababisha majanga zaidi kama Police wakitambua kuwa mlango umevunjwa?”

JAMAA: “Vitasa vinarudishika vizuri hili lisikupe shida kabisa, idea ya kwenda Police mimi sikubaliani nayo.”

LUCY: “Hata mimi naunga mkono huko Police tutaenda kukuza mambo tu.”

Lucy alikuwa hataki kabisa kusikia masula ya Police na alikuwa akipinga waziwazi.

Muda huu wote tuliunga wazo la Jamaa kuhusu kubomoa geti ili tujue ndani kuna nini. Na muda huu jamaa alifanya mawasiliano ili kumpata mtaalamu wa kufungua pale na baada ya nusu saa fundi alikuwa amefika na mashine ya kazi.

Ilimchukua fundi dakika 30 kuweza kufungua lile geti pamoja na ule mlango wa kuingilia sebleni na alifungua kitaalamu sana.

Baada ya jamaa kumaliza kazi yake tulifanya malipo na tukamwambia aende ila kesho tutampigia kwaajili ya kufunga vitasa. Lengo letu asijue kinachoendelea pale.

Muda huu milango ilikuwa wazi ikitusubiri sisi kuingia ndani ili tujihakikishie kama Iryn yuko ndani ama laah. Kila mmoja alionekana kuwa na wasiwasi sana na hofu ilitawala mahali hapa, Rose alikuwa anatetemeka na alianza kusali muda huu. Mimi ndo niliyekuwa wakwanza kufungua mlango na kuingia ndani.

TO BE CONTINUED
Sijui kwa nini nahisi kwamba Irene atakuwa kafia huko ndani kwake? Japo naombea isiwe kweli

Ndugu zangu tusipende sana kuishi peke yetu kwa vyovyote vile tujitahidi angalau kuwa hata na ndugu mmoja au dada wa kazi hata kama unaona hauhitaji dada wa kazi but for security reasons better to have one.

Wakati mwingine unaweza hata ukaumwa ghafla au ukafia ndani peke yako tu hakuna atakayejua ukiwa unaishi mwenyewe.

Sasa hapo kama Irene angekuwa na dada wa kazi angalau zisingepita siku zote hizo bila kutafutwa!! Dada wa kazi angeshirikisha majirani kama mama mwenye nyumba haamki au hajarudi kama alitoka.

Huu uzi una mengi ya kujifunza.
 
Sijui kwa nini nahisi kwamba Irene atakuwa kafia huko ndani kwake? Japo naombea isiwe kweli

Ndugu zangu tusipende sana kuishi peke yetu kwa vyovyote vile tujitahidi angalau kuwa hata na ndugu mmoja au dada wa kazi hata kama unaona hauhitaji dada wa kazi but for security reasons better to have one.

Wakati mwingine unaweza hata ukaumwa ghafla au ukafia ndani peke yako tu hakuna atakayejua ukiwa unaishi mwenyewe.

Sasa hapo kama Irene angekuwa na dada wa kazi angalau zisingepita siku zote hizo bila kutafutwa!! Dada wa kazi angeshirikisha majirani kama mama mwenye nyumba haamki au hajarudi kama alitoka.

Huu uzi una mengi ya kujifunza.
Ungelijua raha tunazopata watu tunaoishi home alone wala usingetoa ushauri huo, kufa mtu atakufa tu Na kuoza ataoza hata apigwe kafru maiti, hofu ya nini sasa, Na tusikariri kifo mungu alivyokuandikia kitokee hata ukaishi mwezini au barabarani utakufa ulipopangiwa mauti yakukute.
 
EPISODE 36

“A TRUE STORY BY INSIDER”

Muda huu nilianza kujilaumu kwa kutotilia maanani hili suala, niliwaza pale hata Police wangeniona mimi ni mzembe sana. Nilivuta pumzi ndefu sana na nilijikuta macho yangu yakiwa yamejaa machozi na mapigo ya Moyo yalianza kuongezeka spidi.

CONTINUE….

Mtoto wa kiume nilitokwa na machozi muda huu na mawazo yalikuwa yananiambia Iryn atakuwa ametekwa. Nilitafakari pale, Muajemi ameondoka jumanne kwenda Iran na alisema kaongea na Iryn Jumatatu. Niliwaza huenda Muajemi kafanya jambo, haiwezekani iwe harakaharaka hivi, na muda huu Rose alitoka ndani akiwa amevaa skin jeans.

ROSE: “Jiran niko tayari tunaweza kuondoka.”

MIMI: “Sidhani kama Police ni muhimu kwa sasa nafikiri tuendelee ku-buy time kwanza, I have a plan.”

ROSE: “Jiran hivi hujui kwamba utajiweka kwenye matatizo? Maana mpaka sasa wewe ndo first suspect.”

MIMI: “I know, Iryn ana mama yake mlezi nadhani utakuwa unamjua, nafikiri tuwasiliane naye kwanza.”

ROSE: “Sijakuelewa Jiran unamaanisha nini?”

MIMI: “Kuna Mama Mzungu anakujaga hapa mwenye hizi apartments.”

ROSE: “Yule mama Mzungu ambaye anaongea kiswahili vizuri ni ndugu na Iryn?”

MIMI: “Exactly yule ni Mama mlezi wa Iryn na alikuwa rafiki wa mama yake kipenzi.”

Ilibidi nimpe historia kidogo kuhusu maisha ya Iryn mpaka kifo cha mama yake na mpaka Mama Janeth kuwa mama mlezi wake.

ROSE: “Jiran mimi sijawai kufaham kama yule Mama mzungu (Mama Janeth) ana undugu na Iryn, ila nilishawai kumwona mara 2 lakini sikujua kama ndo mwenye nyumba.”

MIMI: “Plan yangu kabla hatujakwenda Police ni bora niwasiliane naye kwanza huenda anajua kinachoendelea.”

ROSE: “Umewaza jambo zuri.”

Nilitoa simu yangu kwenye gari na nilitafuta namba za mama Janeth ambazo Iryn alinitumiaga kipindi kile napeleka mzigo kwake na nikazipata. Nilipiga ile namba lakini ilikuwa haipatikani na nilirudia kama mara 5 lakini ilikuwa haipatikani.

MIMI: “Jiran hapatikani acha niende Masaki kwake.”

ROSE: “Unajua anakoishi? Twende wote.”

Tuliondoka pale Kijitonyama na tulikwenda Masaki moja kwa moja mpaka kwa Mama Janeth. Baada ya kufika pale kwake nilipiga honi na baada ya dakika kadhaa alitoka mlinzi ambaye ndo nilikuwa namwona kwa mara ya kwanza na alikuja upande wangu, na mimi nikashusha kioo.

MLINZI: “Bro habari nikusaidie nini?”

MIMI: “Kaka nashida na Mama Janeth sijui nimemkuta?”

MLINZI: “Mama Janeth ni nani? Usije ukawa umekosea nyumba.”

MIMI: “Bro anaishi hapa hata week iliyoisha nilikuwa hapa, unaonekana ni mgeni hapa ndomana humjui, ana watoto wa2 wa kizungu wakiume na kike.”

MLINZI: “Kaka sasa nimekuelewa kama ulikuja week iliyopita huyo sijui mama Janeth atakuwa amehama, maana sisi tumehamia hapa Ijumaa na tunaweek tayari tuko hapa na huyu Tajiri nimeanza naye kazi muda mrefu sana.”

ROSE: “Kaka tusaidie kama yupo maana tumekuja kuonana naye kuna jambo muhimu sana tafadhali.”

MLINZI: “Hata mimi nawaona mmekuja kwa mazuri nayowambia nikweli kabisa, sisi tuna week hapa toka tuhamie.”

Ukweli nilikosa cha kusema na sikuielewa hii movie kabisa inavyokwenda, kitendo cha Iryn kupotea kimaajabu na kutopatikana na bado mama Janeth hapatikani na ninaambiwa amehama kilinipa maswali sana muda huu.

MIMI: “Jiran hii movie siielewi naona kama sina maamuzi kwa sasa.”

ROSE: “Hauna Plan B ya kumpata Mama Janeth?”

MIMI: “Ipo twende saloon huenda dada wa pale atakuwa na mawasiliano naye.”

ROSE: “Let’s go.”

Tulindoka maeneo yale na tulikwenda saloon yao ya kulekule Masaki na baada ya kufika pale nilikwenda moja kwa moja ndani.

Baada ya kuingia ndani niliwakuta wafanyakazi wakiwa busy sana na niliwasalimia pale.

“Sumaiya nimemkuta?”

“Yupo alikuwa around hapa ngoja nimpigie simu.”

Dada alitoa simu yake mfukoni akapiga simu na wakaanza kuongea pale,

“Anakuja unaweza msubiri pale kwenye coach.”

“Dada mimi niko nje parking namsubiri.”

Nilitoka ndani na nikaenda parking nilikokuwa nimepark gari.

ROSE: “Jiran what is going on?”

Na muda huu Rose alishuka kwenye gari na akasogea karibu yangu. Rose alionesha kuguswa sana na hili jambo na alionesha kunionea huruma sana.

ROSE: “Jirani pole sana najua unapitia wakati mgumu sana kwasasa ila tutampata akiwa mzima kabisa, hata mimi hili jambo limenigusa sana, kwa kipindi tulichoishi na Iryn, nimetokea kumpenda sana.”

MIMI: “Ahsante sana Jiran ngoja huyu dada aje tuone atakuwa na jambo gani.”

Baada ya dakika 10 Sumaiya alitoka na alikuja moja kwa moja mpaka Parking nilikokuwa nimepark gari. Sumaiya alikuwa ni msimamizi wa Saloon kwa upande wa Masaki kama alikvyokuwa Lucy msimamizi wa Mikocheni na Sinza.

SUMAIYA: “Hi Insider za wewe? Dada mambo?”

ROSE: “Safi za kwako?”

MIMI: “Umetuweka sana hapa ujue.”

SUMAIYA: “Sorry nilikuwa nina mteja nisingeweza kumwacha katika mazingira yale.”

MIMI: “I know usijali, nimekuja hapa kwa jambo moja tu.”

SUMAIYA: “Jambo gani Insider?”

MIMI: “Mama Janeth simpati kwa simu na nimekwenda kwake naambiwa amehama.”

SUMAIYA: “Mara ya mwisho tumeongea Jumapili na sijampigia tena maana sahivi hatuja pungukiwa na kitu na tukitaka kutoa mzigo si tunakucheki wewe?. Kidogo kumpigia simu kumepungua afu mauzo tunatuma report kwa Queen (Iryn).”

ROSE: “Na alikohamia unakujua?”

SUMAIYA: “Hapana hata alikokuwa anaishi before sikujui na sijawahi fika, mara nyingi mazungumzo yetu yanafanyika hapahapa ofisini. Si uwasiliane na Queen akupe namba zake?”

MIMI: “Mpaka nimekuja kwako kutafuta namba za Mama Janeth ni kwamba Iryn hajulikani aliko toka jumatatu, Mama Janeth ndo mtu pekee aliyebaki wa kuokoa hili jahazi maana tunataka kureport Police.”

SUMAIYA: “Insider acha kupoteza muda wako, unahangaika kumbe amejifungia Hotelini na Bwana wake. Acha kupoteza muda amini maneno yangu hata uko Police usiende kabisa.”

Na muda huu Rose alimkata jicho kali sana Sumaiya.

ROSE: “Naona unaleta masikhara kwenye vitu serious mtu zaidi ya week asipatikane? haimake sense.”

SUMAIYA: “Nachoongea ni kweli, Insider jaribu kumpigia Bossy au mtext kwenye whatsapp.”

MIMI: “Sawa Ahsante miss.”

SUMAIYA: “Insider trust maneno yangu, ukimpata Queen nijulishe.”

Sumaiya hakuonesha kujali kabisa na alikuwa akileta matani sana muda huu. Na sisi tuliondoka eneo hili kurudi Mikocheni na muda huu Lucy alinipigia simu na tukakubaliana tukutane palepale kwa Iryn.

ROSE: “Jirani usipompata Mama Janeth Whatsapp tunafanyaje?.”

MIMI: “Nafikiri turudi home pale tuonane na jirani mwingine na pia kuna dada atakuja anasimamia saloon za Sinza na Mikocheni tutapata majibu.”

ROSE: “Sawa, zote ni saloon zake?”

MIMI: “Yeah zake.”

ROSE: “Yuko vizuri sana nilikuwa namchukulia poa sana.”

Tuliwasili pale Kijitonyama na tulimkuta Lucy kafika tayari anatusubiri sisi, na muda huu giza lilikuwa lishaanza kuingia.

LUCY: “Insider vipi umefanikiwa kuonana na huyo Mama Janeth?”. Lucy alikuwa hamfaham Mama Janeth.

MIMI: “Hapana kwakweli Mama Janeth hapatikani na pale kwake kahama.”

LUCY: “Amehama toka lini?”

MIMI: “Hata mimi sielewi kwakweli maana last week jumanne nilikuwa pale kwake, leo tunaambiwa amehama.”

ROSE: “Mimi nahisi mlinzi hajataka tu uonane na Mama Janeth.”

LUCY: “Hata mimi nahisi hivyo.”

Na muda huu tulisikia geti likifunguliwa na alikuwa ni yule jamaa Jirani. Baada ya kuingia ndani na kupark gari alishuka na alivyotuona tumesimama pale kwa Iryn ilibidi asogee.

JAMAA: “Habari zenu Majirani, vipi kuna usalama hapa leo?.”

Na wote tuliipokea salamu yake

ROSE: “Jirani hapa hakuna usalama, ndugu yetu Iryn hajulikani aliko na mara ya mwisho kupatikana kwenye simu ilikuwa jumatatu.”

MIMI: “Labda Jirani mara ya mwisho ulimwona Iryn lini?”

JAMAA: “Nilimwona jumatatu jioni wakati narudi kazini na alikuwa amesimama hapo kibarazani, tulipungiana mikono na mimi nikaingia ndani.”

Na muda huu Jamaa alikwenda kusimaa eneo alilokuwa Iryn.

MIMI: “Mpaka sasa tuna uhakika Iryn Jumatatu alikuwa maeneo haya, sasa nini kimetokea asipatikane kwa simu na bila kuwa na taarifa yoyote?”.

JAMAA: “Bro! Wanawake wana siri nyingi sana labda nikuulize toka mkutane na shem mna muda gani?”

MIMI: “Tuna miez mi-nne sasa.”

ROSE: “Mimi nafikiri tu ripoti Police hili jambo mapema, naona hili suala linazidi kuwa gumu sana.”

JAMAA: “Unakuta huyu mtu amekufa huko ndani au alitekwa kwa maelezo yanayotolewa hapa mimi nafikiri hivyo.”

ROSE: “Guys twendeni Police jamani!”

LUCY: “Police hapana mimi Roho inaniambia Iryn yupo somewhere, Insider huwezi kutafuta means ya kumpata mama Janeth kama whatsapp hapatikaniki?”

MIMI: “Itabidi Jumatatu sasa niende ofisini kwake.”

JAMAA: “Bro mara ya mwisho ulikuwa na shem lini?”

MIMI: “Tuliondoka Ijumaa kwenda Zanzibar na tukarudi Jumapili usiku.”

JAMAA: “Mlitoka wawili tu?”

MIMI: “Hapana tulikuwa watatu afu Iryn sio mpenzi wangu kama mnavyofikiri ni mtu wangu wa karibu.”

Ilibidi niwape mkanda mzima wa kule Zanzibar tangu tunakwenda na kurudi na sikutaka kuficha suala la Muajemi.

JAMAA: “Kwa maelezo yako inaonesha huyo Muajemi anamtaka Iryn kwa njia yoyote ile na hatuwezi jua mpaka Iryn anakubali offa yake kwenda Zanzibar alipewa nini. Bro hawa wanawake sometimes wanasiri nyingi sana huenda amekula Pesa za jamaa nyingi sana. Kama dada alikuwa anamkazia huenda jamaa kaamua kumfanyia kitu mbaya wanasema usishindane na tajiri. Swali langu lingine kwanini akuage haraka anakwenda Iran?, something crazy is going on, kama alimwekea sumu huko Zanzibar ambayo itamwuua taratibu utajuaje?”

Maneno ya Jamaa yalituingia vizuri kila mmoja alikuwa anaguna tu muda huu, jamaa aliongea point sana.

ROSE: “So what’s next?”

JAMAA: “Tufungue mlango tuangalie ndani kwanza kwa suala la Police inaweza kuwa msala zaidi, Bro wewe ndo utakuwa kikaangoni na msala wote utabaki kwako ujue, sisi wengine tutakuwa mashahidi tu.”

ROSE: “Una maanisha tuvunje geti na mlango?”

JAMAA: “Yeah atleast tutapata picha nzuri ya kuanzia.”

ROSE: “Huoni kama tutasababisha majanga zaidi kama Police wakitambua kuwa mlango umevunjwa?”

JAMAA: “Vitasa vinarudishika vizuri hili lisikupe shida kabisa, idea ya kwenda Police mimi sikubaliani nayo.”

LUCY: “Hata mimi naunga mkono huko Police tutaenda kukuza mambo tu.”

Lucy alikuwa hataki kabisa kusikia masula ya Police na alikuwa akipinga waziwazi.

Muda huu wote tuliunga wazo la Jamaa kuhusu kubomoa geti ili tujue ndani kuna nini. Na muda huu jamaa alifanya mawasiliano ili kumpata mtaalamu wa kufungua pale na baada ya nusu saa fundi alikuwa amefika na mashine ya kazi.

Ilimchukua fundi dakika 30 kuweza kufungua lile geti pamoja na ule mlango wa kuingilia sebleni na alifungua kitaalamu sana.

Baada ya jamaa kumaliza kazi yake tulifanya malipo na tukamwambia aende ila kesho tutampigia kwaajili ya kufunga vitasa. Lengo letu asijue kinachoendelea pale.

Muda huu milango ilikuwa wazi ikitusubiri sisi kuingia ndani ili tujihakikishie kama Iryn yuko ndani ama laah. Kila mmoja alionekana kuwa na wasiwasi sana na hofu ilitawala mahali hapa, Rose alikuwa anatetemeka na alianza kusali muda huu. Mimi ndo niliyekuwa wakwanza kufungua mlango na kuingia ndani.

TO BE CONTINUED

Iyrn alifia ndani kwake baada ya kuwekewa sumu kwenye kinywaji na Muajeni pindi wakiwa Zanzibar, sumu hiyo ilimla pole pole na baada ya kufika nyumbani kwake ndipo alifia ndani.

Wewe Insider baada ya kumpigia Muajemi kumuulizia kuhusu Iyrn nae pia akakujibu hafahamu, na ndipo Muajeni akawa amepata jibu sahihi kuwa sumu aliyomuwekea Iyrn pindi wakiwa Zanzibar imefanya kazi na ametimiza lengo lake la kumuua Irene, ndipo akaamua kufunga safari yake ya ghafra kuondoka,

Na ndio maana tangu akate simu hakumpigia tena Muajemi ili kumuuliza kama amempata Iyrn,

Na kingine ninachoweza kuhisi ni kwamba, Yule Mama mzungu huenda pia amehusika kwa kifo cha Iryn , huenda Muajemi alikua ni mamluki aliekodiwa na mama mzungu ili kumuua Iyrn ili mama huyo aweze kuendelea kumiliki mari zote alizotakiwa kuzimiliki Iyrn na ndio maana mama huyo amehama alipokua akiishi na amezima simu yake.


, Bira shaka baada ya kuvunja mlango na kukuta maiti ya Iyrn ulijaribu kumpigia kwa njia ya WhatsApp Muajemi hakupatina tena.

WAUAJI NI MUAJEMI NA MAMA WA KIZUNGU.🫡
 
Iyrn alifia ndani kwake baada ya kuwekewa sumu kwenye kinywaji na Muajeni pindi wakiwa Zanzibar, sumu hiyo ilimla pole pole na baada ya kufika nyumbani kwake ndipo alifia ndani.

Wewe Insider baada ya kumpigia Muajemi kumuulizia kuhusu Iyrn nae pia akakujibu hafahamu, na ndipo Muajeni akawa amepata jibu sahihi kuwa sumu aliyomuwekea Iyrn pindi wakiwa Zanzibar imefanya kazi na ametimiza lengo lake la kumuua Irene, ndipo akaamua kufunga safari yake ya ghafra kuondoka,

Na ndio maana tangu akate simu hakumpigia tena Muajemi ili kumuuliza kama amempata Iyrn,

Na kingine ninachoweza kuhisi ni kwamba, Yule Mama mzungu huenda pia amehusika kwa kifo cha Iryn , huenda Muajemi alikua ni mamluki aliekodiwa na mama mzungu ili kumuua Iyrn ili mama huyo aweze kuendelea kumiliki mari zote alizotakiwa kuzimiliki Iyrn na ndio maana mama huyo amehama alipokua akiishi na amezima simu yake.


, Bira shaka baada ya kuvunja mlango na kukuta maiti ya Iyrn ulijaribu kumpigia kwa njia ya WhatsApp Muajemi hakupatina tena.

WAUAJI NI MUAJEMI NA MAMA WA KIZUNGU.🫡
Dah nimeogopa
 
Iyrn alifia ndani kwake baada ya kuwekewa sumu kwenye kinywaji na Muajeni pindi wakiwa Zanzibar, sumu hiyo ilimla pole pole na baada ya kufika nyumbani kwake ndipo alifia ndani.

Wewe Insider baada ya kumpigia Muajemi kumuulizia kuhusu Iyrn nae pia akakujibu hafahamu, na ndipo Muajeni akawa amepata jibu sahihi kuwa sumu aliyomuwekea Iyrn pindi wakiwa Zanzibar imefanya kazi na ametimiza lengo lake la kumuua Irene, ndipo akaamua kufunga safari yake ya ghafra kuondoka,

Na ndio maana tangu akate simu hakumpigia tena Muajemi ili kumuuliza kama amempata Iyrn,

Na kingine ninachoweza kuhisi ni kwamba, Yule Mama mzungu huenda pia amehusika kwa kifo cha Iryn , huenda Muajemi alikua ni mamluki aliekodiwa na mama mzungu ili kumuua Iyrn ili mama huyo aweze kuendelea kumiliki mari zote alizotakiwa kuzimiliki Iyrn na ndio maana mama huyo amehama alipokua akiishi na amezima simu yake.


, Bira shaka baada ya kuvunja mlango na kukuta maiti ya Iyrn ulijaribu kumpigia kwa njia ya WhatsApp Muajemi hakupatina tena.

WAUAJI NI MUAJEMI NA MAMA WA KIZUNGU.🫡
Duuuh
 
Sijui kwa nini nahisi kwamba Irene atakuwa kafia huko ndani kwake? Japo naombea isiwe kweli

Ndugu zangu tusipende sana kuishi peke yetu kwa vyovyote vile tujitahidi angalau kuwa hata na ndugu mmoja au dada wa kazi hata kama unaona hauhitaji dada wa kazi but for security reasons better to have one.

Wakati mwingine unaweza hata ukaumwa ghafla au ukafia ndani peke yako tu hakuna atakayejua ukiwa unaishi mwenyewe.

Sasa hapo kama Irene angekuwa na dada wa kazi angalau zisingepita siku zote hizo bila kutafutwa!! Dada wa kazi angeshirikisha majirani kama mama mwenye nyumba haamki au hajarudi kama alitoka.

Huu uzi una mengi ya kujifunza.
Kama umauti ulivyomkuta marehemu Isaac Muyenjwa Gamba huko nchini Ujerumani, so sad yani [emoji17]
 
Back
Top Bottom