Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Baada ya kupata mtoto mawazo yote yalikuwa Kwa mtoto, mtu akiniudhi namshika mwanangu najisemea siwezi kujidhuru nikuache peke yakoNi kweli kabisa introvert imejaa suicide thought, wewe hufanyaje kuweza kuAct extro. Kuna muda najifanya mbishi na mkali afu mtu ananiambia acha kujifanyishe sheee.. Yaani matendo na sura tofauti
Pole mkuu, umeona sasa everyone need to belong to someone. Mtu ambae unamjali na kumpenda. Maisha yanalet maana sana ukiwa na mtu huyo etii? Haijalishi ni nani kwako.Baada ya kupata mtoto mawazo yote yalikuwa Kwa mtoto, mtu akiniudhi namshika mwanangu najisemea siwezi kujidhuru nikuache peke yako
Of cz inatupa confidenc kwa kias fln,tofaut na hivyo kwel tunapitia wkt mgum sanaaTogether brother,
Intoverted, anxiety.. Its killing me, I started drinking too, for the first time in my life, Mungu anajua tunayoyapitia
Kwa introvents mnaweza jaribu shrooms.zinasaidia kuondoa anxiety na kukufanya kuwa na good mood na kuongeza cofidence though utumie kwa uangalifu
Dah nimesoma huu Uzi, hizi sifa karibu zote ninazoMates;
Binaadamu tumeumbwa kwa matabaka tofauti tofauti sio wa rangi wala jinsia, katika upande wa Personalites binaadamu yupo katika makundi mabalimbali. Kuna Makundi makuu mawili ya personalities,ambazo ni Extroverts na Introverts. Kwa upande wa introverts dunia kwao si kikwazo au haina kikwazo chochote ambacho kinaweza kuwafanya wasisonge mbele au kupata yale wanayoyahitaji.
Upande wa Introverts mambo ni tofauti sana sana, wao dunia si mahali salama kwa muono wao na inakua ni ngumu sana kwao kupata yale wanayoyahitaji humu duniani. Introverts wanaamini au wanaiona dunia ist the bed of roses na unaweza kuishi na ku-Earn yale unayoyata bila kutumia nguvu kubwa sana ya mwili ila ya akili.
Bahati mbaya dunia haipo hivyo, dunia imejaa michongoma hii inawafanya introverts kuona hawafit kuishi duniani hapa ila ndio wapo sasa inabidi wakubaliane na matokeo.
Kama tunavyoelewa kua Extroverts ni watu Fulani ambao ni waongeaji wazuri na hawana aibu hata kidogo wakitaka kitu watakueleza mojakwamoja ila Introvert ni watu wasio na uwezo wa kujieleza vizuri na wana aibu sana, mara nyingi hutuia muda mwingi katika kufikiri na kutafakari vitu vipya!
Aliyeumba hizi aina kinzani za watu hakua mjinga, alikua na maana kubwa sana kuwaweka pamoja hapa duniani, katika hizi pande mbili kinzani zimeunganishwa na kitu kimoja ambacho ni Kutegemeana katika mazingira. Pande zote mbili zinategemeana mno kwa kiasi kikubwa kwakua introvert wanatumia muda mwingi kufikiria na kutafakari vitu basi hawa walijaliwa Creative and Genius mind!
Ukiangalia maandeleo katika Nyanja ya dunia hii yameletwa na watu ambao ni Introverts. Lakini Introvert person akiungana na extrovert person basi hua wanatengeneza the best duo, Introvert hua anamtumia huyo extrovert kama mdumo wake au nguvu yake huku yeye akitumia akili yake zaidi katika mambo japo maranyingi sana hua extroverts wanawatapeli introverts baada ya muda.
NB, sio kwamba extrovert hua hawana uwezo wa akili no, ila siku zote mtu anayeanza kutafakari maneno wakati wewe uko unaongea muheshimu sana, lakini pia usichanganye introvert na kibuli.
Wapo watu wengi walikua ni introvert wakaungana na extrovert wakatenda mambo makubwa hapa duniani Nitatoa baadhi ya mifano
Mussa
Huyu jamaa alikua nae ni introvert, hana uwezo mzuri sana wa kujieleza ndio maana alipoitwa na Mungu alimuuliza atawezaje kuzungumza nao wakati hawezi kuongea vizuri? Mungu akampatia msaidizi wake amabae ni Aaron, walitengeneza moja ya kolabo bomba hapa duniani nadhani mambo waliyofanya tunayajua na yataendelea kuwepo daima
Tesla
Tesla alikua ni introvert aliyepitiliza, alijua duniani kila mtu ni mwema kama yeye. Alikutana na bwana Thomas Eddison wakafanya kazi pamoja mpaka leo umoja wao ndio unatufanya tunaweza kuchati hapa, bahati mbaya Thomas alimdhurumu tesla ila hakujali kufa maskini alishukuru tu kua akaili yake imeweza kuleta maendeleo duniani.
Mark Zuckenburg
Binafsi hua nikiamuangalia tu mark namuonea huruma tu kwa munekano wake, ni moja kati ya watu amabao wana Innocent face, ukimuangalia tu unamuhurumia. Ni watu wachache sana wenye hiyo haiba yay a kuonekana wanatia huruma. Mark ni introvert maisha yake chuoni alikua sio muongeaji hata ukimuudhi vipi hua anabaki kimya.
Kuna kipindi kama miaka 2 imepita ilitokea mgogoro kwamba mark kaiga ile technology ya kuangalia game in vitual reality. Ikatakiwa alipe pesa, ilimuuma mno ila hakuongea alibaki nalo rohoni. Rafiki yake mkubwa amabae amemsaidia sana kufanikisha facebook kufika hapa ilipo ni Eduardo Sevarin. Eddu alikua muongeaji tu na mtafuta masoko na investors mpaka leo umoja wao huo ndio umeawafikisha hapa mark ni billionea.
David Benioff
Huyu jamaa ni moja kati ya watengenezaji wa tamthiria ya game of thrones, nayeye sio muongeaji kama walivyo introverts wote pia ana aibu mno. Anar rafiki yake waliyekutana nae chuoni anaitwa Daniel Brett Weiss (D.B.Weiss) naye huyu ni moja ya watengenezaji wa tamthiria hii. Ila huyu DB Weiss hana aibu hata kidogo na nimuongeaji sana.
Hata wakiwa kwenye interview maswali yanayomuhu David benioff hua anayjibu yeye the funny thing ni kwamba walipokua wanafanya casting ya actors labda kama kuna actor Fulani ambaye the next season alitakiwa afe David Benioff alikua hawezi kuwaambia eti anaogopa! So aliyekua anafanya kazi hiyo alikua ni DB Weiss tena kwake ilikua rahisi mno.
View attachment 1526082
Issack Newton
Kama kawaida ya introverts wote basi Newton pia hakua na marafiki kabisa alipenda kujifungia ndani ya maabara yake kufanyia tafiti fikra zake na kujipa nafasi ya kufikiri zaidi. Alikua anamsemo wake anasema kwamba “ Plato is my friend, Aristotle is my friend, but my best friend is truth” Lakini naye alikua na rafiki yake ambae alikua ni muongeaji mzuri/Extrovert aliitwa John Locke. Huyu ndio alikua rafiki pekee wa Newton na yeye ndio aliweza kumuelezea vizuri tabia zake za upweke japo baadae walishindwana urafiki wao. Maana Muda mwingi Newton alikua bize.
Albert Eintein
Albert alipohamia Switzerland akaanza kufanya kazi kwenye ofisi za Patent right (haki miliki) ndipo alipoanza kufanyia kazi Hobby yake pendwa ya Kufikiria. Ofisini kwake kulimwezesha kufikiria maana hakua na kazi ngumu, kupitia dirisha lililokua ofisini mwake aliweza kuformulate theory of relativy maana alikua anautafakari mwanga uliokua unaingia ofisini mwake kupitia dirishani….Japo alikua ni mtu mmoja mkimya sana na alikua anaongea kila baaada ya kutafakari sana anachotaka kuongea pia alikua na rafiki yake wa karibu toka zamani ambae wamesaidiana mengi si mwingine ni Michelle Besso. Beso ndio alikua rafiki yake mkubwa na kumuwezesha Albert kufanya mengi makubwa.
Mifano ni mingi sana ya urafiki wa introverts na extrovert, watu maarufu ambao ni Introverts..na wametenda mengi makubwa duniani mfano:
Albert Einstein,Rosa Parks,Bill Gates,Steven Spielberg,Sir Isaac Newton,Eleanor Roosevelt, Mark Zuckerberg,Larry Page,Al Gore,Marissa Mayer, Abraham Lincoln,JK Rowling,Warren Buffett, Mahatma Gandhi,Hillary Clinton, Michael Jordan,Meryl Streep,Elon Musk,Dr. Seuss,Frederic Chopin
Introverts kwakua wao hawawezi kuingiliana vizuri na jamii waliyomo hivyo basi muda wao mwingi hua wanautumia kwenye mitandao ya kijamii. Huku kwenye jamii hawana attention kwa watu so wanachofanya ni kutafuta attention mitandaoni at any cost. Introvertism,Geniusity,Lonelness na Ugonjwa wa akili ni vitu vinavyoenda sambamba. Ukikuta mtu anaandika mapost marefu,anatukana au kuudhi watu mitandaoni usimchukie.
Muhurumie sana maana anakua muhanga wa matatizo niliyoyaainisha hapo juu. Wanafanya kuudhi watu ili nao waonekane kama wanaweza kufanya kitu, wanajitahid kufit in ila bahati mbaya wanatumia approach mbaya ya kuudhi watu.. Introverts ni watu poa sana, wana mioyo mizuri sana na wana akili zenye uwezo mkubwa.
-Vinci
Hivi watu wa tabia moja wakikaa pamoja wataelewana kweli?INTROVERT WOTE KESHO NINAKIKAO NANYI NYOTE. SAA KUMI JIONI
na wewe ni introvert [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]Halafu kwenye mitandao tunajifanya wachangamfu kwa vile hatuonekani nadhani
sababu nini?Mnadhani sifa kuna mwenzenu huku amejinyonga alikuwa mtu wa ndani ndani ndani.
una demu?Huu utafiti had leo naupongeza sana maana binafsi nilikuwa maarufu sana skul kuanzia primary, o-level had a-level ila bado ni mtu mwenye rafiki wachache yaan contacts zangu tu ziko kama 70 na
Nakaa ndani sana ,nasoma sana na sipendi mikusanyiko kama vile graduation, napenda sana kutumia simu naweza nkaitumia almost all the time nkiwa macho
Kwa upande wa haya dah ndo kabisa marafiki karibu wote nilionao wao ndo walitengeza urafiki
Nilijaribu kujichanganga ila naona nashindwa dah. Huwa nafikiria sana hata kitu kidogo tu mpaka marafiki wakawa wananiona ni mr complicator
dah hapana hata wanajilengesha nawaogopa sometimes hadi najiogopa mwenyeweuna demu?
ni kweli ila jaribu kujichanganya hata na ndugu tu tatizo tunategemea watu wawe loyal sana kwetu kama tulivyo kwaoDah, so sad I fall in this category. Hii haifai kwangu maana hata nashindwa kuomba msaada ninapokabiliwa na matatizo makubwa pengine nikafa najiona. Sijui niwaanzaje watu
Duuh nini kinapendeza mkuu watu wanamasikitiko
Kabisa japo nimeitwa sana majina kama maskini jeuri ila kiukweli imenisaidia sana watu kuniheshimu hata wale wenye pesa za kumwagapia hatujui kumnyenyekea mtu hata kama tuna shida
Nilijua niko peke yangu katika hili...Kabisa japo nimeitwa sana majina kama maskini jeuri ila kiukweli imenisaidia sana watu kuniheshimu hata wale wenye pesa za kumwaga
Sent from my TECNO CF7 using JamiiForums mobile app