Jinsi maombi yanavyoshusha Imani yako kwa Mungu

Jinsi maombi yanavyoshusha Imani yako kwa Mungu

Imani chanzo chake ni kusikia neno la Mungu.
Mungu amesema Usiue. Sasa Imani ni kutoua.

Imani ndio inakutaka uamini kitu unacho hata kama huna. Na sioaneno unaanza kuchukua hatua KATIKA ya Kutokujua. Ukitaka Hadi ujione ndio uamini hiyo sio Imani ni EVENT.

Ibrahim aliamini akaenda asikokujua.
Ibrahim aliamini atarudi na mtoto wake licha ya kujua anakwenda kumchinja.
Musa aliamini bahari itaachia kabla hajaona iachie na hajwahi kuona tangu azaliwe.
Yesu alishukuru kupata mikate ya kulisha watu 5000 wakati haipo.

Imani ni independent na 5 senses ikiwepo kuona. Ndio maana ukiwa na Imani Kali lazima uonekane chizi. Paulo alionekana mpumbavu tu.

Ushahidi kuwa hicho kitu unacho hata kama hakipo sio kuonekana kw hico kitu Bali ni Hilo neno lililosemauna ho au UTAPEWA ndani ya biblia.

Na ushahidi kwamba utapata hata kama ni pesa. Utaondoka Kwa bidii ukiamini kabisa fursa yoyote itakayojitokeza ndio sehemu ya udhihirisho a neno unaloamini. Ndio maana mtu wa Imani ni mtu wa action.faitj without action Is a deadfaith.
Na ni Mungu huyo huyo aliyesema usiseme uongo

Sasa kama wewe ni masikini halafu mnamdanganya kuwa we ni tajiri huoni kwamba hiyo ni dhambi?

Ibrahimu hakuamini atarudi na mtoto wake kwasababu lilikuwa ni agizo LA Mungu na hakujua kama hill no jaribio amepewa

Ukisema aliamini atarudi na Issack maana yake alijua exactly kuwa anaenda kujaribiwa

Na Abraham akishajua kuwa hili ni jaribio maana yake hiyo inakuwa ni cheating amefanya na majibu yanayopatikana hapo hayawezi kuwa sahihi

Na Mungu angejua kuwa huyu Abraham amekwishajua lengo la yeye sio kumuamuru amchinje mwanae basi agizo hilo lisingetumika kama kipimo cha imani
 
Asante Sana mkuu. Kuna mambo kadhaa naomba nifafanue.

1🙂 nazungumzia (Maombi) Kwa maana ya asking or begging kitu ambacho tayari Mungu ameshasema amekupa. Kwa Mujibu wa mstari ulioutoa,
Warumi 10:17 Imani chanzo chake ni kusikia. Sasa kama Mungu ameshasema amekupa afya, na huna afya. Unatakiwa ushukuru sio uombe. Maana tayari umesikia Umepewa afya hata kama katika ulimwengu wa mwili haipo.


2: Command sio sehemu ya maombi. Hii ni mamlaka ya kutamka. Huitaji kucommand kma sehemu ya maombi. Hakuna huo mfano kwenye biblia. Command, announcements, decrees, Declarations HIZI unazitamka katika kauli zako na vitu vinatii huombi hapo. Ndio maana hazimo kwenye package ya Sala ya Kwetu. Ile sio Sala ya Bwana, Maana Bwana Yesu ametupa sisi.


3:Imani haiji Kwa kuomba kitu ambacho umeshapewa.Imani huja Kwa Kushukuru Neno la kristo lililotamka hicho kitu limekupa.utashukuru Hadi kiwe.

Ninakushukuru Sana Bwana mkubwa. Tunaweza kuendelea kupeana maarifa.
Mkuu labda kabla hatujaenda mbali ningependa kujua unasoma biblia gani, ya kiswahili pekee?

Binafsi nasoma ya kiswahili (kidogo sana) na si kwa nia mbaya ila ni kutokana na kuwa kwanza biblia ya kiswahili haikutafsiriwa moja kwa moja toka kwny biblia ya kiebrania(vitabu vinavyoitwa agano la kale) na kigiriki (vitabu vinavyoitwa vya agano jipya). Hii inaifanya inakuwa na baadhi ya maana tata/ambazo hazikukusudiwa kutokana na ufinyu na uhaba wa misamiati wa lugha husika wakati wa tafsiri ilipofanyika.

Pia nasoma ya kiingereza (mainly KJV) na pia nasoma ya kiebrania na kigiriki.

Sasa ukisoma biblia ya lugha moja pekee bila kupitia hizi zingine kuna vitu vingi sana utapishana navyo hasa katika tafsiri.

Kama uko deep kwny hizi nyingine, nijulishe ili tuzame kwny mjadala wako vizuri tukianza na maana ya neno "prayer", kwa nini tunaomba ikiwa Mungu anajua haja zetu, kwa nini maombi ya watu fulani yanajibiwa ila we ukiomba the same prayer hupati jibu? Je ni maombi ndiyo yenye nguvu ama nguvu ni ya muombaji nk nk.
 
Tazama ninawapa amri ya kukanyaga nge na nyoka...

Wala hakuna litakaloshidikaba kwenu. Mathayo 17:20

Kifupi sisi tunaomuamini Mungu tunazo nguvu za Mungu ambazo tunatakiwa tuzitumie kuvuka changamoto maishani.

Hivyo wakati changamoto zijapo wengine tunakosea kuanza tena kuomba Mungu atende vitu fulani..wakati mamlaka hayo amshakupa tayari, ila wewe ndiyo umeshindwa kuzitumia nguvu hizo.

Na sawa uwepo kwenye chumba chenye umeme halafu uanze kulia kuwa kuna giza...unatakuwa kuwasha tu switch ili mwanga utokeze.

Hivyo wakati mwingine tunapitia shida ambazo tulikuwa tunaweza kuzitatua kwa mamlaka tuliyopewa...ila tunapoteza muda kwa kuanza tena kumsihi Mungu atende jambo fulani....yeye naye anasema laiti kama huyu mwanangu angejua kuwa tayari anazo nguvu za suluhisho la tatizo lake, asingepoteza muda kulia kwenye maombi akiniomba.

Speak to your challenges, amuru kwa nguvu za Mungu na milango iliyofungwa itakufungukia. Ukishaomba wewe amini tu, kuhusu utekelezaji wewe muachie Mungu.
 
Kuna kaukweli fulani maana hizi kuombewa na kuomba imekuw fashion kiasi kwamba watu WA Mungu wamebaki kukimbizana kwa wachungaji na manabii waombewe mambo Yao yaende sawa...... By doing that kamwe hawatakaa wawe na Imani thabiti sababu wao hawajiamini kuwa wanaweza kuwa na mahusiano na Mungu straight na Kutatua shida zao zote so wamelemaaa kwenye kuombewa tu but sio kushukuru. Na ndio maana hawapati kile wanachokiomba kila siku ukipita wanapoombea wapate wachumba Leo ukija baada ya MWAKA mmoja unawaona bado wapo vilevile au wamejaa zaidi...... Unajiuliza...... Hupati jibu.... MUNGU tayari anajua huitaji lako..... Jaribu kushukuru Utashangaa kwa yatakayokutembelea
 
Maombi hayana nguvu zozote mnazodanganyana.

Yangekuwa na nguvu basi idadi ya wagonjwa, vita, uonevu, mauwaji na umasikini visingekuwa kwa hali iliyopo hivi leo[emoji16][emoji16].

Kwa jinsi wafia dini mnavyokesha kwenye maombi na upuuzi ufananao na kuabudu eti kumkemea shetan na uharibifu wa dunia, basi hayo maovu na madhaifu yangepungua kama sio kuisha.

Waulizeni babu zenu kabla ya dini za kizushi kuja afrika, hakukuwa na magonjwa kama leo hii, hakukuwa na mmomonyoko wa maadili kma leo hii, hakukuwa na uzandiki kma mlio nao wafia dini, je hayo maombi yenu mnayemuomba hawasikii??

Acheni kupoteza muda kwenye dini za kizushi, Mungu wa dini zote ni mmoja na ndiye huyo huyo shetan ktk majina ya vificho[emoji23].

Bitter truth.
 
Ndio MAANA NABII NA MTUME MWAMPOSA KABLA AJAANZA IBADA UTASIKIA AKISEMA" PAZAA SAUTI YA SHUKRANI ,PAZA SAUTI YA SHUKRANI ,MWAMPOSA YEY ANAFAHAMU SIRI HYO wengi hawajui washukuru VIP na atamke nni mbele za bwana
 
Sahihi kabisa.
Sema imani nyingi zimeingiliwa na watafuta shortcuts .
Mwamposa kbla hajanza ibada yake UTASIKIA AKISEMA PAZAA SAUTI ya SHUKRANI ,paza sauti ya SHUKRANI ,Kweli Ni Mara nyingi Sana mtume mwamposa akihimiza watu kushukuru
 
Tumezoea kudhani kuwa maombi yanakuza Imani. Ni kweli tumesisitizwa kuomba, lakini asilimia karibu 99 ya Sala zako hazipaswi kuwa Maombi Bali Shukrani.

Kuombaomba na mbaya Zaidi kuombewa kunapumbaza na kushusha Imani.

NINI KITAONGEZA IMANI YAKO?

SHUKRANI.
Unatakiwa kushukuru Muda mwingi Kwa vitu ambavyo huna kana kwamba tayari unavyo.

KWA NINI USHUKURU NA SIO KUOMBA?
Tayari Mungu karibu Kila unachokiomba ameshasema amekupa. Badala ya kuomba shukuru Kwa kupewa Kisha Anza kuchukua hatua za kivitendo bila shaka kana kwamba tayari hicho kitu kipo na unacho.


Mfano, Yesu hakuomba ili mikate5 na samaki 3 vilishe watu 5000 (wanaume). Alishukuru Kwa sababu tayari Kuna andiko linasema Kila chenye Mwili akipa chakula chake Zaburi 136:25.

Kiwango chako Cha imani kinapimwa hivi.

Kuombewa ----Mtoto mchanga kiimani.
Kuomba ------Mvulana au msichana kiimani.
Kushukuru nakusifu ---- Mtu mzima na mkomavu kiimani.


Kama umeelewa, andika Amina.


Muebrania
Mitale na Midimu
Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote angekuwepo, kungekuwa hakuna haja ya kuomba wala kushukuru.

Hizi habari za kuomba na kushukuru kuwepo zinaonesha Mungu huyo hayupo.

Na habari za kuwepo kwake zimetungwa na watu tu.
 
Tumezoea kudhani kuwa maombi yanakuza Imani. Ni kweli tumesisitizwa kuomba, lakini asilimia karibu 99 ya Sala zako hazipaswi kuwa Maombi Bali Shukrani.

Kuombaomba na mbaya Zaidi kuombewa kunapumbaza na kushusha Imani.

NINI KITAONGEZA IMANI YAKO?

SHUKRANI.
Unatakiwa kushukuru Muda mwingi Kwa vitu ambavyo huna kana kwamba tayari unavyo.

KWA NINI USHUKURU NA SIO KUOMBA?
Tayari Mungu karibu Kila unachokiomba ameshasema amekupa. Badala ya kuomba shukuru Kwa kupewa Kisha Anza kuchukua hatua za kivitendo bila shaka kana kwamba tayari hicho kitu kipo na unacho.


Mfano, Yesu hakuomba ili mikate5 na samaki 3 vilishe watu 5000 (wanaume). Alishukuru Kwa sababu tayari Kuna andiko linasema Kila chenye Mwili akipa chakula chake Zaburi 136:25.

Kiwango chako Cha imani kinapimwa hivi.

Kuombewa ----Mtoto mchanga kiimani.
Kuomba ------Mvulana au msichana kiimani.
Kushukuru nakusifu ---- Mtu mzima na mkomavu kiimani.


Kama umeelewa, andika Amina.


Muebrania
Mitale na Midimu
Umeandika point kubwa sana, lakn mtu mwenye imani ya kurisishwa ama kukariri hawezi kukuelewa
 
Mwamposa kbla hajanza ibada yake UTASIKIA AKISEMA PAZAA SAUTI ya SHUKRANI ,paza sauti ya SHUKRANI ,Kweli Ni Mara nyingi Sana mtume mwamposa akihimiza watu kushukuru
Sijawahi kumsikiliza hiyu Bwana, Ila ninachojua wengi wa aina yake Huwa wanachanganya.
Unaweza kuona baada ya kushukuru Tena aliowaaminisha wanamagonjwa na wamefungwa.
Niliwahi kfuatilia mmoja anaitwa Kuhani, anawaaminisha waumini wamelogwa na wako kwenye vyama vya wachawi, anawaambia wakili hivyo.
Wakati huohuo anawaambia wameokoka. hayo tunayaita Satan and not Christ Conscious churches

Kama wanaaminishwa kupata Kwa Kushukuru, watakuwa ni waumini imara Sana wasio na hofu.
 
Tumezoea kudhani kuwa maombi yanakuza Imani. Ni kweli tumesisitizwa kuomba, lakini asilimia karibu 99 ya Sala zako hazipaswi kuwa Maombi Bali Shukrani.

Kuombaomba na mbaya Zaidi kuombewa kunapumbaza na kushusha Imani.

NINI KITAONGEZA IMANI YAKO?

SHUKRANI.
Unatakiwa kushukuru Muda mwingi Kwa vitu ambavyo huna kana kwamba tayari unavyo.

KWA NINI USHUKURU NA SIO KUOMBA?
Tayari Mungu karibu Kila unachokiomba ameshasema amekupa. Badala ya kuomba shukuru Kwa kupewa Kisha Anza kuchukua hatua za kivitendo bila shaka kana kwamba tayari hicho kitu kipo na unacho.


Mfano, Yesu hakuomba ili mikate5 na samaki 3 vilishe watu 5000 (wanaume). Alishukuru Kwa sababu tayari Kuna andiko linasema Kila chenye Mwili akipa chakula chake Zaburi 136:25.

Kiwango chako Cha imani kinapimwa hivi.

Kuombewa ----Mtoto mchanga kiimani.
Kuomba ------Mvulana au msichana kiimani.
Kushukuru nakusifu ---- Mtu mzima na mkomavu kiimani.


Kama umeelewa, andika Amina.


Muebrania
Mitale na Midimu
Nakubaliana nawe kwa sehemu kubwa tu ni kweli kushukuru kuna nguvu kubwa sana lakini baada ya kuomba. Ombeni mtapewa, tafuteni mtapata, pigeni hodi mtafunguliwa.
 
Na ni Mungu huyo huyo aliyesema usiseme uongo

Sasa kama wewe ni masikini halafu mnamdanganya kuwa we ni tajiri huoni kwamba hiyo ni dhambi?

Ibrahimu hakuamini atarudi na mtoto wake kwasababu lilikuwa ni agizo LA Mungu na hakujua kama hill no jaribio amepewa

Ukisema aliamini atarudi na Issack maana yake alijua exactly kuwa anaenda kujaribiwa

Na Abraham akishajua kuwa hili ni jaribio maana yake hiyo inakuwa ni cheating amefanya na majibu yanayopatikana hapo hayawezi kuwa sahihi

Na Mungu angejua kuwa huyu Abraham amekwishajua lengo la yeye sio kumuamuru amchinje mwanae basi agizo hilo lisingetumika kama kipimo cha imani
Ibrahim aliamini atarudi na mtoto, hata kama angemchimja na kumchoma. Mungu angemrudisha Kwa manjia elfu aliyonayo.
Ndio maana anaitwa Baba wa Imani.
Ushahidi
Waebrania 11:19
[19]akihesabu ya kuwa Mungu aweza kumfufua hata kutoka kuzimu; akampata tena toka huko kwa mfano.
Accounting that God was able to raise him up, even from the dead; from whence also he received him in a figure.

Ni sahihi kumwambia maskini ni aseme ni tajiri. Ushahidi wa utajiri wake sio vitu vya kugusika alivyonavyo, ushahidi ni neno la Mungu lililosema hivyo. Imani ni uhakika wa usichonacho, uhakika hup ni neno la Mungu usilolitilia mashaka.
Kila mkristo anayejitambua ni Tajiri kuliko Elon Musk Kwa sababu, unafanyika mtoto wa Ufalme na mrithi wa Vyote alivyonavyo Mungu. Hata kama Hauna Sasa vitakuwa vyako siku akirudi.

Ni dhambi mkristo kukili huna kitu, maana imeandikwa.
Wafilipi 4:19
[19]Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu.
But my God shall supply all your need according to his riches in glory by Christ Jesus.

Ni KOSA mkristo kukiri udhaifu, maana imeandikwa.
Yoeli 3:10
[10] aliye dhaifu na aseme, Mimi ni hodari.
... let the weak say, I am strong.

Pia udhaifu wako (kiuchumi, kiroho,kimahusiano ndio kigezo Cha kufanywa imara. Udhaifu ni advantage.) Paulo aliandika katika udhaifu ndipo nakuwa imara.

Kwa Nini watu hawapati au hawaoni. Wengi hatujua maana ya tajiri Kwa mtazamo wa biblia. Ni kuwa na financial freedom hata unaishi chini ya Dola Moja. Pia wanavunja kanuni nyingine mfano. Utajiri wa Mungu inahitaji bidii , ndio maana anasema Wenye bidii watakaa na wakuu
 
Wengi awajui nguvu kuu iliyomo kwenye kushukuru.
Kushukuru ni kuiruhusu positive energy ijae mwilini mwako.
Positive energy ikizalishwa vya kutosha uchochea ukuaji na matokeo uonekana kwenye ulimwengu wa mwili.
 
Wengi awajui nguvu kuu iliyomo kwenye kushukuru.
Kushukuru ni kuiruhusu positive energy ijae mwilini mwako.
Positive energy ikizalishwa vya kutosha uchochea ukuaji
Hata kama huna dini. Hii ni kanuni. Ukiitumia inazaa matunda.
Wakristo wengi wanaahangaika eti wamefungwa kumbe midomo yao ndio imewafunga Kwa kutokushukuru na kubaki wakitazamia kuona Mungu atafanya kitu katikati ya bidii zao. Huku wakiepuka negativity Kwa gharama zote.

Haya ni maarifa, tu watu wanatakiwa kuyatest.
 
Back
Top Bottom