Jinsi mapenzi ya mtoto wa Kizulu Durban South Africa yalivyotaka kunitoa roho

Jinsi mapenzi ya mtoto wa Kizulu Durban South Africa yalivyotaka kunitoa roho

picha ikitupiwa humu,lazima wabongo watoe kasoro sana.

watakueleza mbona demu wa kawaida sana.

kuna mapimbi hayajui kutofautisha picha za Photoshop na zile za kupiga kawaida

kuna mademu n pisi kali sana,lakini ukimpga picha ya kawaida anaonekana wa kawaida

nakushauri konda msafi,usitupie picha,tuache tuendelee kutengeneza picha zetu vichwani,ndo tunaupata utamu wa khumbu
Dah!!! [emoji30] [emoji30] [emoji30] Mawazo ya kijinga kabisa haya....
 
Kabla hatujaendelea na matukio ya Khumbu hebu jaribuni kuigoogle "the workshop mall" ili muweze ku-visualize ile park(garden) niliyoenda kukaa na kuanza kutokwa machozi bila kupenda, huenda hata mkapaona hiyo sehemu niliyokaa ndugu yenu hahahaha!

Haya tuendelee,
Baada ya kujiapiza kuwa huyu anayeutesa moyo wangu lazima nifanye rebound ya kufa mtu ili nimle hata mara moja ya mwisho, na siku akijiroga aingie kwenye 18 zangu nitakachomfanya hatanisahau. Ikawa kama namtaka Khumbu kwa ajili ya kumkomesha na si kwa ajili ya kumpenda. Of course deep down nilikuwa nampenda ila tayari moyo wangu ulikuwa umejawa hisia za kumkomesha.

Hapa nikawa natafakari nini cha kufanya ili nitimize dhamira yangu. Cha kwanza nilichokifikiria ni kumpigia simu jamaa yangu don wa unga anitoe hii sehemu niliyokuwa naishi ili nikakae kwenye mijengo yake maana alikuwa na mijengo kibao ya kufanyia mambo yake. Unajua wauza ngada huwa na machimbo tofauti tofauti.

Yaani huwa wanakodisha majumba sehemu tofauti tofauti tena maeneo wayayokaa watu wenye pesa zao mjini kwa ajili ya kufanyia biashara zao. Humu ndimo shughuli ya kufunga mzigo tayari kwa kuupeleka streets hufanyika. Hilo wazo nikaona halifai. Nikafikiria nikija kudakwa kwenye hizo yumba za sembe si na shule itaishia hapo. Of course kufungwa nisingefungwa maana don angenitoa fasta tu ila hii kesi ikifika chuo lazima nitimuliwe, so nikaona idea ya kwenda kuishi huko haifai.

Idea ya pili nikawaza labda nipambane nitafute hata part time job maana documents nilizokuwa natumia zilikuwa zinaniruhusu kusoma na kufanya kazi. Nipambane nipate mjengo wa maana wa kuishi peke yangu. Hii idea tena nikaona kama itakuwa ngumu. Kuishi mjengo wa maana peke yako kwa South Africa inahitajika hela ndefu sana, so hata kama nikipata kazi sidhani kama itakidhi haya ninayoyapanga. Nikawa kama nimevurugwa vile maana moja haikai, mbili haikai. Anyway nikajiambia acha niyapeleke mambo taratibu mbele ya safari nitapata tu njia ya kutokea na hatimae kumtia Khumbu mikononi.

Itaendelea...
Ile we mwanaume....ndo unawaadithia wenzako kila kitu cha Durban.

No wonder sandile alikua hataki tuwe kwenye relationship.
 
Kuanzia juzi hapa JF pamekuwa patam sana, kuna nyuzi kama 3 hivi nkiingia lazima nizipitie.
1.hii ya khumbu
2.Jamaa anaye mkataa mtoto rasmi.
3.ya mzee wetu Mwitore na bi mdogo wake.

Yaani mambo ni Hot no Stress.
Mkuu nipe link ya hiyo #2 nami niisome tafadhali. #1 na #3 nafuatana nazo tayari.
 
Back
Top Bottom