Jinsi Marekani ilivyoizuia China ili Israel ifanikiwe katika shambulizi la vifaa vya mawasiliano (pagers)

Jinsi Marekani ilivyoizuia China ili Israel ifanikiwe katika shambulizi la vifaa vya mawasiliano (pagers)

Xi Jinping

JF-Expert Member
Joined
Jun 14, 2023
Posts
3,651
Reaction score
11,548
Kwanza kabisa, mnamo Februari 2024 kiongozi wa Hezbollah, Hassan Nasrallah, aliwaamuru wanachama wake kuacha kutumia simu kwa sababu zinaweza kunaswa kwa urahisi na kufuatiliwa na majasusi wa Israeli.

Miezi 2 baada ya agizo la mkuu wao yaani April 2024 wakaagiza hizo pagers ndivyo hata BBC na Reuters zimeripoti.

20240922_005148.jpg
20240922_005135.jpg

BBC na Reuters zimeripoti kuwa pagers zilinunuliwa miezi 5 iliyopita kutoka sasa yaani April

Turudi hadi mwezi April mwaka huu tuone mfuatano wa matukio ulivyokuwa:

April 2, 2024
  • Marekani ilizuia kampuni ya China ya kutengeneza pagers ya Hytera isiuze pagers zake katika soko la dunia. Hiyo hukumu ilitolewa kufuatia kesi ambayo mwaka 2017 Motorola ilifungua dhidi ya Hytera katika masuala ya intellectual property.

  • Sawa hatukatai kuhusu uamuzi wa kesi hiyo ila bado swali linabaki; Kwa nini mahakama ya Marekani itoe hukumu mwezi uleule ambao Hezbollah walikuwa na uhitaji mkubwa wa pagers?
  • Ikumbukwe kipindi hicho ndicho ambacho Hezbollah walihitaji sana pagers. Kwa kuwa za China zilikuwa zimepigwa ban ikabidi wanunue za kutoka Taiwan.​

April 17, 2024
  • Siku 15 tu baadaye yaani April 17 mahakama nchini Marekani ikaondoa ban kwa kampuni ya Hytera na ikaruhusiwa kuanza tena kuuza pagers zake katika soko la dunia. Wakati huo Hezbollah walikuwa tayari wameshanunua mzigo wa pagers kutoka Taiwan. Unaweza kujionea mchezo uliofanyika hapo.​

Kwa nini kumekuwa na sintofahamu kuhusu ni nani mtengenezaji wa hizo pagers?
Kwa kuwa taifa la Lebanon lina vikwazo vya kiuchumi mataifa na makampuni mengi yanaogopa kufanya nao biashara direct hivyo huwa wanatumia third party.
  • Ndio maana unaona suala la mtengenezaji na muuzaji wa pagers limekuwa na danadana nyingi. Kampuni ya Taiwan Gold Apollo inakana kuwa yenyewe haikutengeneza hizo pagers bali iliweka tu logo lakini hawakushiriki kwenye kuunda, kutengeneza wala kuziuza bali wanadai waliipa license kampuni ya Hungary iitwayo BAC kutengeneza pagers, kampuni ambayo nayo haieleweki kwani taarifa zake haziko wazi. Ni wazi kuwa kuna black market fulani ilifanyika.

Kwa mujibu wa taarifa za kiuchunguzi zilizofanywa na Al Jazeera ni kuwa order hiyo ya pagers kutoka Taiwan haikwenda moja kwa moja nchini Lebanon ilipitia Hungary.

Sasa hapo Hungary ndipo inaonekana mchezo mzima wa kupandikiza vilipukizi ulifanywa kisiri na Israel. Kwa nini tunasema hivyo?

Mzigo huo wa pagers ulikaa bandarini kwa miezi mitatu ukisubiri clearence ndipo uende Lebanon. Katika hiyo miezi mitatu ya kusubiria Mossad waliitumia vizuri kupandikiza vilipukizi.

Ikiwa vifaa vya kielektroni vinaweza kufanyiwa mchezo kama huu vikiwa kwenye usafirishaji au supply chain je, kuna usalama wa watumiaji wa vifaa hivyo duniani?

 
Hezbollah sasa hivi wakiona Radio calls, au simu au ipad au paper pagers wanakimbia as if wameona bomu linataka kulipuka, yaani Hezbollah communications yao ni ngumu mnoo, huku wakicheki angani Israelis warplanes zinawamaliza, na niwaambie vita vyovyote ukikosa mawasiliano ndio umemalizwa..!! Wayahudi watu hatari sana tokea enzi na enzi..!!
 
Hezbollah sasa hivi wakiona Radio calls, au simu au ipad au paper pagers wanakimbia as if wameona bomu linataka kulipuka, yaani Hezbollar communications yao ni ngumu mnoo, huku wakicheki angani Israelis warplanes zinawamaliza
Nimecheka kinoma.

Hii wamakonde wanakwambia "Ukisimama nchale, ukiinama nchale"
 
Ukiisha pigwa maelezo yako huwa hayasikilizwi, unaonekana unajitetea. bondia mshindi ndiye hushangiliwa, ila aliyepigwa hata kocha wake huwa hamuelewi, hata ndugu ukitaka kujieleza wanaona unatafuta faraja tu.
Hizi ni bluh bluh tu.
Sawa na mtu asiye na pesa kwenye kikao Cha ukoo. Hata aseme ana upako hakuna atakayemsikikiza.
 
Hezbollah sasa hivi wakiona Radio calls, au simu au ipad au paper pagers wanakimbia as if wameona bomu linataka kulipuka, yaani Hezbollar communications yao ni ngumu mnoo, huku wakicheki angani Israelis warplanes zinawamaliza
Baadhi ya vikundi vimeanza kununua pagers kutoka kwa suppliers wengine ambao hawana uhusiano na Marekani
 
Ukiisha pigwa maelezo yako huwa hayasikilizwi, unaonekana unajitetea. bondia mshindi ndiye hushangiliwa, ila aliyepigwa hata kocha wake huwa hamuelewi, hata ndugu ukitaka kujieleza wanaona unatafuta faraja tu.
Hizi ni bluh bluh tu.
Lengo la huu uzi ni kutokuwa na mlengo wowote

Wengine watalizungumzia kishabiki lakini ukweli ni kwamba usalama wa watumiaji wa vifaa vya kielektroni duniani uko mashakani kama kuna mchezo kama huu.

Je, unajua kifaa chako kimewekewa nini kikiwa kwenye supply chain mpaka kukufikia?

Katika shipping kuna delay huwa ziko kwenye bandari vipi siku mzigo wa vifaa vya kielektroni unaokuja kwenye taifa lako watu wenye nia mbaya wakafanya mchezo kama huu?

Kama mbinu hii imewezekan kwa Lebanon je, itashindikan kufanywa kwa wengine huenda isiwe kwa lengo la kuweka vilipukizi vipi ikiwa ni kuchukua taarifa binafsi za watu?

BBC na Al Jazeera kufanya uchunguzi kujua huu mchezo sio wajinga

Inaweza kuwa mbinu mpya ya kigaidi au ya kiujasusi kuanza kutumiwa


SOMA PIA
www.jamiiforums.com/threads/kulipuka-kwa-pagers-radiocalls-lebanon-ni-pigo-kubwa-kwa-sekta-ya-uchukuzi-na-usafirishaji-duniani.2258252/

Conquistador Teslarati Frank Wanjiru
 
Hao hizbollah na washirika wake, wanaishi kama panya mashimoni kwa sasa maana hawajui kitu gani kitalipuka muda wowote.
Ni shambulizi la kigaidi kutekelezwa na Israel kwa sababu watumiaji wa vifaa vya kielektroni sio tu ambao Israel iliwalenga yaani Hezbollah

Hata raia wa kawaida wamepatwa na milipuko hiyo. Unafikiri kilichofanywa ni sawa?

Weka kwanza ushabiki pembeni
 
Ni shambulizi la kigaidi kutekelezwa na Israel kwa sababu watumiaji wa vifaa vya kielektroni sio tu ambao Israel iliwalenga yaani Hezbollah

Hata raia wa kawaida wamepatwa na milipuko hiyo. Unafikiri kilichofanywa ni sawa?

Tuweke tu ushabiki pembeni
Wako sawa kwa mtazamo wao, maana vita haina macho.
Hata hao Hizbollah na washirika wake, kutwa kurusha mabomu ndani ya ardhi ya Israel bila kujali nani ataangukiwa.

Tukumbuke lile tukio la October 7, 2023 la Hamas kufanya mauaji na utekaji Israel, wahanga wakubwa wa tatizo hilo siyo wahusika.

Hakuna vita iliyowahi kuwa fair hapa duniani na haitakuja kutokea vita hiyo.
 
Wako sawa kwa mtazamo wao, maana vita haina macho.
Hata hao Hizbollah na washirika wake, kutwa kurusha mabomu ndani ya ardhi ya Israel bila kujali nani ataangukiwa.

Tukumbuke lile tukio la October 7, 2023 la Hamas kufanya mauaji na utekaji Israel, wahanga wakubwa wa tatizo hilo siyo wahusika.

Hakuna vita iliyowahi kuwa fair hapa duniani na haitakuja kutokea vita hiyo.
Kwa hiyo tunakubaliana kuwa ni ugaidi?
 
Hezbollah sasa hivi wakiona Radio calls, au simu au ipad au paper pagers wanakimbia as if wameona bomu linataka kulipuka, yaani Hezbollar communications yao ni ngumu mnoo, huku wakicheki angani Israelis warplanes zinawamaliza
Kabla ya hiki kisa, sikujua na hadi sasa kwa uhakika sijaelewa hivyo vifaa paga(pagers) vinafanyaje kazi za kimawasiliano.
Kama unauzoefu kidogo navyo mkuu, nipe mwanga.
 
Kwa hiyo wanawake na watoto waliolipuliwa walikuwa wanatumia au wanakaa na vifaa vilivyoingizwa kwa matumizi ya kijeshi ya kikundi cha wapiganaji!
hao hua wanatumika kama human shield na magaidi. popote alipo gaidi mwanamke na mtoto ndo anakua mbele yake ndio maana wao ndio wanaanza kufa, unajua maana ya ngao? yenyewe ndio inaanza kuumia kabla yako
 
Kwa hiyo tunakubaliana kuwa ni ugaidi?
Vyovyote tukubaliane au tusikubaline kama ni ugaidi au laa, ila kinachoendelea huko ni vita kama vita nyinginezo ambazo hupelekea vifo na maafa mengi kwa pande zote zinazohusika.

Kwa ujumla, Ugaidi ni tafsiri ambayo hutegemea mtu aonavyo, mfano wapo waonao Boko haram ni magaidi huku wengine wakiwaita wakombozi na mashujaa.
 
Vyovyote tukubaliane au tusikubaline kama ni ugaidi au laa, ila kinachoendelea huko ni vita kama vita nyinginezo ambazo hupelekea vifo na maafa mengi kwa pande zote zinazohusika.

Kwa ujumla, Ugaidi ni tafsiri ambayo hutegemea mtu aonavyo, mfano wapo waonao Boko haram ni magaidi huku wengine wakiwaita wakombozi na mashujaa.
Screenshot_20240922-072217_Chrome.jpg
 
Back
Top Bottom