Jinsi polisi walivyonusuru maisha yangu last night

Jinsi polisi walivyonusuru maisha yangu last night

Mkeo msouth?nimewahi sikia wanawake wa South Africa...mwanamume mgeni akipata hela wanachonga mchongo anauwawa ili wabebe mali
Hapana mkuu, japo niliwahi kuzaa na msauzi, lkn mke wangu ninaeishi nae huku ni mbongo. Ila tayari tumeshazaa nae watoto wawili, mmoja anaingia darasa la tatu mwakani, na mdogo ataingia la kwanza.

Elimu ya hapa inafaida kubwa kwa nchi yoyote ya Afrika. Hivyo naona bora niendelee kupambana ili kuwapatia watoto wangu elimu bora kwa maisha yao ya baadae.

Pia huyo mtoto niliezaa na mzawa kwa sasa yupo kwenye mikono yangu namsomesha na ashafika la 5. Huyu pamoja na kwamba simtegemei sana kama nitaweza kurudi nae nyumban pale itapobidi kurudi, lkn naona ni damu yangu, siwezi kuacha kumpa haki yake ya msingi kwa ajili ya maisha yake ya baadae hata ntakapokuwa sipo hapa.

Sababu yeye hakupenda au kupanga kujileta mwenyewe dunia, bali ni starehe za sisi wawili (mimi na mama yake) ndio zilizosababisha ujio wake. Hivyo ni lazima nimpambanie kwa ajili ya dreams zake.

Nikiona presha inazidi nitahamia mji mungine, maana nchi hii ni kubwa na kila mji au kila sehemu kuna fursa zake.
 
Ulichoongea kina ukweli wa 100% mkuu, maana hata unapotoka hizo sura unazokutana nazo zinakupa sign fulani kichwani.

Sema ndo hivyo sisi hatukuwa na chochote ndomaana sikuwa na wasi wasi wowote wa kuondoka pale usiku as long as najijua nipo na usafiri wa kunifikisha nyumban muda wowote.
Nakumbuka mwishoni mwa mwezi Septemba, 2017 tuliwasili hapo OR Tambo International Airport Saa 6 usiku, nilishangaa kuona Wanajeshi wengi pamoja na Askari Polisi wengi pia wakiwahutubia Abiria na Wageni wanaowasili kwamba wasitoke nje ya uwanja huo kwani kuna tukio kubwa la ujambazi limetokea usiku huo eneo la Four Ways Jhb ambako Watalii kutoka Ujerumani waliporwa kila kitu na Majambazi. Watalii hao walikodisha basi kubwa ili liwafikishe hotelini, majambazi waliovalia Yunifomu za Polisi walisimamisha basi hilo na Kisha kuwaweka watalii wote at gun-point na kuwapora kila kitu, mabegi na simu zao zote zilichukuliwa. Ni hatari sana kuwasili OR Tambo usiku na Kisha kuchukua usafiri wa gari bila escort ya ulinzi mkali wa silaha.
 
Wahalifu wanakufata kwa sababu fulani , miongoni mwa sababu hizo ni inawezekana una kitu cha thamani, au una ugomvi nao, au kuna deal haramu unafanya nao na mmepishana sehemu

Hao ambao wanakufata kwasababu una kitu cha thamani huwa hawawezi kukurudia kama hawana connection na mtu wako wa karibu, ila hao waliobaki kama una watu unafanya nao deals haramu na umepishana nao, au una kisasi na mtu hao hawawezi kukuacha watakutafuta sana

Kwahiyo ni muda wa kutulia na kujitafakari na kuwa standby muda wote
 
Nakumbuka mwishoni mwa mwezi Septemba, 2017 tuliwasili hapo OR Tambo International Airport Saa 6 usiku, nilishangaa kuona Wanajeshi wengi pamoja na Askari Polisi wengi pia wakiwahutubia Abiria na Wageni wanaowasili kwamba wasitoke nje ya uwanja huo kwani kuna tukio kubwa la ujambazi limetokea usiku huo eneo la Four Ways Jhb ambako Watalii kutoka Ujerumani waliporwa kila kitu na Majambazi. Watalii hao walikodisha basi kubwa ili liwafikishe hotelini, majambazi waliovalia Yunifomu za Polisi walisimamisha basi hilo na Kisha kuwaweka watalii wote at gun-point na kuwapora kila kitu, mabegi na simu zao zote zilichukuliwa. Ni hatari sana kuwasili OR Tambo usiku na Kisha kuchukua usafiri wa gari bila escort ya ulinzi mkali wa silaha.
Aisee kipindi hiki huku huwa ni hatari sana.
 
Wahalifu wanakufata kwa sababu fulani , miongoni mwa sababu hizo ni inawezekana una kitu cha thamani, au una ugomvi nao, au kuna deal haramu unafanya nao na mmepishana sehemu

Hao ambao wanakufata kwasababu una kitu cha thamani huwa hawawezi kukurudia kama hawana connection na mtu wako wa karibu, ila hao waliobaki kama una watu unafanya nao deals haramu na umepishana nao, au una kisasi na mtu hao hawawezi kukuacha watakutafuta sana

Kwahiyo ni muda wa kutulia na kujitafakari na kuwa standby muda wote
Ulichoandika kina ukweli mkuu, ila binafsi nafanya shughuli zangu halali.

Japokuwa duniani kuwa watu hawapendi kuona wengine wakipiga hatua kuwazidi. Watu hao huwa tayari kufanya lolote aidha kukuroga, kukusingizia kesi mbaya ili upotezwe au kukuuwa kabisa.
 
Yani nlipata mchongo wa biashara na kampuni glani south Africa lakni Kila nikiifkria Ile nchi nashindwa kabisa ,
Nimeamua ntafute kampuni zengne Austria na ulaya huko Mana hii nchi so mchezo naiogopa balaaa.
Hta stamani kwenda hata buree
 
Yani nlipata mchongo wa biashara na kampuni flani south Africa lakni Kila nikiifkria Ile nchi nashindwa kabisa ,
Nimeamua ntafute kampuni zengne Austria na ulaya huko Mana hii nchi so mchezo naiogopa balaaa.
Hta stamani kwenda hta bure
 
Labda una gari kali sana🙂
Yani hapo ndo nashindwa kuelewa kama lengo lilikuwa ni gari au kitu gani.

Lakini kama ni gari kali mbona kuna wanaoendesha kali zaidi ya hili langu mkuu!

Anyway sio mimi au wewe anaeweza kujua lengo la wale jamaa isipokuwa mwenye kufahamu malengo yao ni Mungu pekee.
 
Wahalifu wanakufata kwa sababu fulani , miongoni mwa sababu hizo ni inawezekana una kitu cha thamani, au una ugomvi nao, au kuna deal haramu unafanya nao na mmepishana sehemu

Hao ambao wanakufata kwasababu una kitu cha thamani huwa hawawezi kukurudia kama hawana connection na mtu wako wa karibu, ila hao waliobaki kama una watu unafanya nao deals haramu na umepishana nao, au una kisasi na mtu hao hawawezi kukuacha watakutafuta sana

Kwahiyo ni muda wa kutulia na kujitafakari na kuwa standby muda wote
Kwa nchi ya Afrika ya Kusini hususani kwenye miji mikubwa zaidi kama vile Jhb, Cape Town au Durban, kufuatiliwa na Wahalifu au Majambazi ni kitu cha kawaida kabisa, wala siyo ajabu. Kitu cha msingi ni kuwa mwangalifu sana muda wote unapokuwa safarini barabarani.
 
Mkuu una uhakika hawajakariri plate no pamoja na rangi ya gari wakakuwinda mitwa hiyo uliyokuwa unakatiza wwkati wanakufatilia?

Pole sana chief, umakini uongezeke zaidi.
 
Mnadhulumiana kwenye biashara...
Mnachukuliana mademu..
Hampendani wahamiaji.

Huyo jamaa mliyemsindikiza huenda aliwaset. Trust nobody.
Japo hayo hutokea kwa baadhi ya watu, lkn mimi sio mmoja wao mkuu.

Na jamaa niliemshindikiza hawezi kufanya huo mchongo kwani yeye hapa ni mgeni kutoka cape town, na mimi ndio nilikuwa mwenyej wake, alaf ni ndugu wa damu kabisa.
 
Kwa nchi ya Afrika ya Kusini hususani kwenye miji mikubwa zaidi kama vile Jhb, Cape Town au Durban, kufuatiliwa na Wahalifu au Majambazi ni kitu cha kawaida kabisa, wala siyo ajabu. Kitu cha msingi ni kuwa mwangalifu sana muda wote unapokuwa safarini barabarani.
Hakika wewe unaifahamu vizuri nchi hii, na ushauri wako uliotoa ni wa kuzingatiwa.

Tatizo wengi ambao hawajawahi kuishi nchi hii hawajui kama hayo mambo yapo kila siku, na hutokea kwa mtu yoyote haijalishi unafanya dili za hatari, unatembea na wake za watu au unaishi peace na watu.

Wakikuotea ndo hivyo tena inabidi utafute namna ya kuwaepuka au kukabiliana nao tu kama ilivyokuwa kwangu na kwa watu wengine walionusurika.
 
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Kwanza napenda kumshukuru mw/Mungu kwa kuendelea kunipa nafasi nyingine ya kuishi hapa duniani. Naelewa kila mtu atakufa kwa kifo cha namna yake hapa duniani, lkn katika maisha yangu nimekuwa nikimuomba Mungu siku akinihitaji kurudi kwake, basi kifo changu kiwe cha amani mfano kiwe cha usingizini, cha nyumbani nikiwa nimekaa nk.

Vifo vya kufa kwa kuuwawa mara nyingi huwa sio vizuri. Ni vya mateso na maumivu makali, japo dini hutuambia kwamba wale wanaouwa wenzao kwa namna yoyote, na wao adhabu yao huwa kubwa kwa Mungu, na pia hapa duniani kwa sheria za nchi husika. Hivyo inapotokea mtu umenusurika kifo cha kuuwawa na mtu/ watu, basi ni bora kutumia muda mwingi kumshukuru Mungu na yule/ wale waliokuwa sababu ya kukuokoa.

Let's go to the mada husika hapo chini 👇

Wakuu mimi ni mbongo nilieamua kuhamishia maisha yangu Kaburu longtime ago, japo mara nyingi huwa nakuja bongo kwa mambo yangu binafsi na kuondoka.

Usiku wa kuamkia leo, kuna ndugu yangu alikuwa anasafiri na ndege ya usiku, kutoka hapa Afrika kusini kuelekea Tz (nyumbani). Huyu ndugu yangu ni mwenyeji wa Cape Town, hivyo alivyofika hapa mimi ndio nilikuwa mwenyeji wake.

Alikuwa anaondoka na ndege ya saa tisa alfajiri, hivyo ikabidi mimi na rafiki yangu tumpeleke uwanja wa ndege wa Oliver Tambo saa sita usiku, ili awahi kufanya process zake zingine za usafiri nk, na pia na sisi angalau tuwahi kurudi kupumzika kwa ajili ya kesho (leo asubuhi) kazini. Basi baada ya kufika kule na kupiga story mbili tatu za kuagana, na baadae kufanya process zake za usafiri, sisi mida ya saa saba na nusu tukaanza safari ya kurudi nyumbani.

Wakati nakanyaga mafuta katika highway ya kutoka Kempton park kuelekea Johannesburg town, nikaona kama kuna gari fulan ndogo inatufuata kwa nyuma. Mwanzo tulijua ni gari tu ya kawaida au maybe askari wanataka watusimamishe wakague gari yetu (huo ni utaratibu wao), lkn kila nilipokuwa naongeza mwendo na wao pia waliongeza kimya kimya.

Nilivyofika sehemu fulani kuna mjengo mkubwa umeandikwa "Builders Warehouse" Edenvale, nikaingia kushoto kuelekea Edenvale road ila mimi nikakunja kushoto kuelekea upande wa Germiston road, kuangalia nyuma naona na wao wanaelekea upande ule ule ninaoelekea mimi. Sasa nikawa nishajua kwamba jamaa wanatufuata ni sisi na tukifanya masihara tutagawa maisha yetu kwa shetani (nasema ivi kwa sababu mtu anaetaka kukufanyia uovu anakuwa connected moja kwa moja na shetani) hivyo nikabidi nizidishe speed bila kujali mshale unasoma ngapi kibaoni.

Nilivyokunja pale Edenvale road kuelekea Germiston road nikavuka robot ya kwanza (mataa), nikavuka ya pili kuna daraja la highway ya gari zinazotoka Pretoria, alaf mbele nikakunja kulia jamaa wako na sisi tu japo tayari tulikuwa tushawaacha distance kadhaa. Nikakamua kweli kweli mpaka tukakutana na highway wa Albertina Sisulu, jamaa hawakati tamaa wako na sisi tu.

Tukatambaa na highway mpaka mitaa ya karibu na Eastgate Mall. Pale tukakuta kuna gari ya askari imepaki pembeni wanafanya ukaguzi wa kawaida, tukasema hapa hapa ndo tutapopatia usalama wetu. Japo hawakutaka kutusimisha, lkn ikabidi sisi wenyewe tusimame, ili tuwape maelezo ya ile gari inayotufatilia.

Wakati nimepaki pemben nashuka kwenda kuwapa maelezo wale askari tukaona ile gari nayo inakuja wangu wangu.., ila walipoona kuna askari, na sisi tumepaki tukiongea na askari, jamaa wakapandisha kwa njia ya juu kushoto inayoelekea Eastgate kwenyewe na kutokomea kusikojulikana.

Sasa kwa vile ni usiku na tulikuwa kwenye kukimbizwa na watu hatari, hatukuweza kui mark gari yenyewe wala namba za gari, hivyo ikawa ngumu kwa sisi na askari kuwakamata, kwani tulijaribu kuwafuatilia kwa nyuma na gari yetu tukiongozana na ile ya askari, lkn hola hatukuwapata, na ukizingatia J'burg ni mji mkubwa na una barabara nyingi mno. Basi tukarudi home na kulala hadi asubuhi.


Hii imenikumbusha, week 2 zilizopita, kuna mkongo mmoja alifuatiliwa hivyo hivyo kutoka Yeoville hadi kwake Bez alley. Inasemekana kuwa mkongo baada ya kufika kwake alifungua mlango fasta, na kuingia kwake. Ila bahati mbaya (au naweza kusema siku zake zilikuwa zimefika) hakuwa amebana vizuri gate la kuingilia kwake, na jamaa wakawa wameshafika na kuona nyumba aliyoingia. Jamaa wakapush mlango, wakaingia ndani na kukuta watu wakiwa hawana hili wala lile, jamaa wakiwa na "double 9" mkononi wakauliza yule mtu aliekimbilia humu yuko wapi? Mpopo (nigeria guy) mmoja akajibu hatujamuona, kabla hajamaliza kauli akapigwa ya Paja, na kuelekezewa nyingine kichwani, akaambiwa tunauliza kwa mara ya mwisho, bila jibu sahihi tunafumua ubongo na kukamata mungine mpaka tutawamaliza. Walivyouliza kwa mara ya pili, wote wakajibu pamoja kwamba amejificha chooni.

Ndo wakamwambia mpopo akawaoneshe chooni, kweli Ile kuingia wakakuta jamaa kajificha anatetemeka. Wakamtoa nje mbele ya familia yake, wakamuomba funguo za gari na simu, akawa funguo akasema hana simu. Basi jamaa wakafumua kichwa kwa risasi 4 mbele ya ndugu zake, alafu funguo ya gari wakaachana nayo wakatoka nje na kutokomea kusikojulikana.

So na sisi tulivyokuwa tunafuatwa, basi nilihisi na mimi yanakwenda kunikuta yale ya mkongo. Kwamba huenda jamaa wamepewa dili tu kama ilivyotokea kwa yule mkongo au labda walikuwa ni majambazo wa magari nk.

Huu ndio unakuaga mwezi mgumu, na hatari kuliko miezi yote hapa Kaburu. Wengi huwa tunaweka mbele maombi na dua mbali mbali ili kuuvuka salama mwezi huu.
Daaa
 
Mkuu una uhakika hawajakariri plate no pamoja na rangi ya gari wakakuwinda mitwa hiyo uliyokuwa unakatiza wwkati wanakufatilia?

Pole sana chief, umakini uongezeke zaidi.
Hili ndio nina wasi wasi nalo. Kama sio majambazi basi ni watu waliotumwa au wanaonifahamu kati ya mimi au jamaa niliekua nae.

Na kama ni hivyo basi tayari watakuwa washaifahamu au wanaifahamu gari yangu. Hivyo nimeamua niipaki uani huku nikiangalia utaratibu wa kumtafuta mtu tusiefahamiana nae nimuuzie.
 
Back
Top Bottom