Jinsi polisi walivyonusuru maisha yangu last night

Jinsi polisi walivyonusuru maisha yangu last night

Kwenye makasino ya wacheza kamari **** msemo mmoja maarufu sana" winners knows when to quit. "
South africa na uzuri wake katika utafutaji wa pesa nyie wahusika mnatakiwa muwe na ratiba ya kutoka na kurudi nyumbani kuwekeza .
Tukio zima lililokutokea jana mimi limeahawahi kunitokea miaka 17 nyuma na nilisha wahi leta story hapa . enzi hizo nokiishi hillbrow at its best.
Ni shida sana mkuu. Ila hilo swala la kuwekeza nyumban ni zuri, maana kuna leo na kesho, mtu huwezi jua.

Ku risk maisha huku ni jambo la kawaida, maana hata mimi hii sio mara yangu ya kwanza. Imeshanitokea babkubwa zaidi ya hii mwaka 2008, ila nimeahidi hapo juu kwenye comment za juu kwamba siku nikipata muda nitakuja kuandika kilichonitokea.

By the way maisha ya mwanaume ni kuhangaika, na katika kuhangaika huko kuna risk nyingi unakutana nazo kama hivi.
 
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Kwanza napenda kumshukuru mw/Mungu kwa kuendelea kunipa nafasi nyingine ya kuishi hapa duniani. Naelewa kila mtu atakufa kwa kifo cha namna yake hapa duniani, lkn katika maisha yangu nimekuwa nikimuomba Mungu siku akinihitaji kurudi kwake, basi kifo changu kiwe cha amani mfano kiwe cha usingizini, cha nyumbani nikiwa nimekaa nk.

Vifo vya kufa kwa kuuwawa mara nyingi huwa sio vizuri. Ni vya mateso na maumivu makali, japo dini hutuambia kwamba wale wanaouwa wenzao kwa namna yoyote, na wao adhabu yao huwa kubwa kwa Mungu, na pia hapa duniani kwa sheria za nchi husika. Hivyo inapotokea mtu umenusurika kifo cha kuuwawa na mtu/ watu, basi ni bora kutumia muda mwingi kumshukuru Mungu na yule/ wale waliokuwa sababu ya kukuokoa.

Let's go to the mada husika hapo chini 👇

Wakuu mimi ni mbongo nilieamua kuhamishia maisha yangu Kaburu longtime ago, japo mara nyingi huwa nakuja bongo kwa mambo yangu binafsi na kuondoka.

Usiku wa kuamkia leo, kuna ndugu yangu alikuwa anasafiri na ndege ya usiku, kutoka hapa Afrika kusini kuelekea Tz (nyumbani). Huyu ndugu yangu ni mwenyeji wa Cape Town, hivyo alivyofika hapa mimi ndio nilikuwa mwenyeji wake.

Alikuwa anaondoka na ndege ya saa tisa alfajiri, hivyo ikabidi mimi na rafiki yangu tumpeleke uwanja wa ndege wa Oliver Tambo saa sita usiku, ili awahi kufanya process zake zingine za usafiri nk, na pia na sisi angalau tuwahi kurudi kupumzika kwa ajili ya kesho (leo asubuhi) kazini. Basi baada ya kufika kule na kupiga story mbili tatu za kuagana, na baadae kufanya process zake za usafiri, sisi mida ya saa saba na nusu tukaanza safari ya kurudi nyumbani.

Wakati nakanyaga mafuta katika highway ya kutoka Kempton park kuelekea Johannesburg town, nikaona kama kuna gari fulan ndogo inatufuata kwa nyuma. Mwanzo tulijua ni gari tu ya kawaida au maybe askari wanataka watusimamishe wakague gari yetu (huo ni utaratibu wao), lkn kila nilipokuwa naongeza mwendo na wao pia waliongeza kimya kimya.

Nilivyofika sehemu fulani kuna mjengo mkubwa umeandikwa "Builders Warehouse" Edenvale, nikaingia kushoto kuelekea Edenvale road ila mimi nikakunja kushoto kuelekea upande wa Germiston road, kuangalia nyuma naona na wao wanaelekea upande ule ule ninaoelekea mimi. Sasa nikawa nishajua kwamba jamaa wanatufuata ni sisi na tukifanya masihara tutagawa maisha yetu kwa shetani (nasema ivi kwa sababu mtu anaetaka kukufanyia uovu anakuwa connected moja kwa moja na shetani) hivyo nikabidi nizidishe speed bila kujali mshale unasoma ngapi kibaoni.

Nilivyokunja pale Edenvale road kuelekea Germiston road nikavuka robot ya kwanza (mataa), nikavuka ya pili kuna daraja la highway ya gari zinazotoka Pretoria, alaf mbele nikakunja kulia jamaa wako na sisi tu japo tayari tulikuwa tushawaacha distance kadhaa. Nikakamua kweli kweli mpaka tukakutana na highway wa Albertina Sisulu, jamaa hawakati tamaa wako na sisi tu.

Tukatambaa na highway mpaka mitaa ya karibu na Eastgate Mall. Pale tukakuta kuna gari ya askari imepaki pembeni wanafanya ukaguzi wa kawaida, tukasema hapa hapa ndo tutapopatia usalama wetu. Japo hawakutaka kutusimisha, lkn ikabidi sisi wenyewe tusimame, ili tuwape maelezo ya ile gari inayotufatilia.

Wakati nimepaki pemben nashuka kwenda kuwapa maelezo wale askari tukaona ile gari nayo inakuja wangu wangu.., ila walipoona kuna askari, na sisi tumepaki tukiongea na askari, jamaa wakapandisha kwa njia ya juu kushoto inayoelekea Eastgate kwenyewe na kutokomea kusikojulikana.

Sasa kwa vile ni usiku na tulikuwa kwenye kukimbizwa na watu hatari, hatukuweza kui mark gari yenyewe wala namba za gari, hivyo ikawa ngumu kwa sisi na askari kuwakamata, kwani tulijaribu kuwafuatilia kwa nyuma na gari yetu tukiongozana na ile ya askari, lkn hola hatukuwapata, na ukizingatia J'burg ni mji mkubwa na una barabara nyingi mno. Basi tukarudi home na kulala hadi asubuhi.


Hii imenikumbusha, week 2 zilizopita, kuna mkongo mmoja alifuatiliwa hivyo hivyo kutoka Yeoville hadi kwake Bez alley. Inasemekana kuwa mkongo baada ya kufika kwake alifungua mlango fasta, na kuingia kwake. Ila bahati mbaya (au naweza kusema siku zake zilikuwa zimefika) hakuwa amebana vizuri gate la kuingilia kwake, na jamaa wakawa wameshafika na kuona nyumba aliyoingia. Jamaa wakapush mlango, wakaingia ndani na kukuta watu wakiwa hawana hili wala lile, jamaa wakiwa na "double 9" mkononi wakauliza yule mtu aliekimbilia humu yuko wapi? Mpopo (nigeria guy) mmoja akajibu hatujamuona, kabla hajamaliza kauli akapigwa ya Paja, na kuelekezewa nyingine kichwani, akaambiwa tunauliza kwa mara ya mwisho, bila jibu sahihi tunafumua ubongo na kukamata mungine mpaka tutawamaliza. Walivyouliza kwa mara ya pili, wote wakajibu pamoja kwamba amejificha chooni.

Ndo wakamwambia mpopo akawaoneshe chooni, kweli Ile kuingia wakakuta jamaa kajificha anatetemeka. Wakamtoa nje mbele ya familia yake, wakamuomba funguo za gari na simu, akawa funguo akasema hana simu. Basi jamaa wakafumua kichwa kwa risasi 4 mbele ya ndugu zake, alafu funguo ya gari wakaachana nayo wakatoka nje na kutokomea kusikojulikana.

So na sisi tulivyokuwa tunafuatwa, basi nilihisi na mimi yanakwenda kunikuta yale ya mkongo. Kwamba huenda jamaa wamepewa dili tu kama ilivyotokea kwa yule mkongo au labda walikuwa ni majambazo wa magari nk.

Huu ndio unakuaga mwezi mgumu, na hatari kuliko miezi yote hapa Kaburu. Wengi huwa tunaweka mbele maombi na dua mbali mbali ili kuuvuka salama mwezi huu.
Mmh pole sana mkuu hiyo nchi kila nikisoma matukio yake ya uhalifu kwenye social networks huwa na appreciate nchi yetu sana
 
Ni shida sana mkuu. Ila hilo swala la kuwekeza nyumban ni zuri, maana kuna leo na kesho, mtu huwezi jua.

Ku risk maisha huku ni jambo la kawaida, maana hata mimi hii sio mara yangu ya kwanza. Imeshanitokea babkubwa zaidi ya hii mwaka 2008, ila nimeahidi hapo juu kwenye comment za juu kwamba siku nikipata muda nitakuja kuandika kilichonitokea.

By the way maisha ya mwanaume ni kuhangaika, na katika kuhangaika huko kuna risk nyingi unakutana nazo kama hivi.
Yah mwanume ninlazima kupambana , ila lazima uwe na exit plan , nimeona unasema hapo kuwa umeshaanzisha familia huku Sa , hapo sasa your hands are tied . katika vitu niliapa sitafanya ni kuanzisha familia kwa kaburu. Yani huko kutengeneza yatima ni dakika tu . Nimeingia sa mwaka 1999 na final goodbye ilikuwa mwaka 2008 . huwa naenda na kurudi . nimepata matukio mengi sana ya kupoteza pesa na kuibiwa na vibaka nikiwa kwa kaburu.
 
Yah mwanume ninlazima kupambana , ila lazima uwe na exit plan , nimeona unasema hapo kuwa umeshaanzisha familia huku Sa , hapo sasa your hands are tied . katika vitu niliapa sitafanya ni kuanzisha familia kwa kaburu. Yani huko kutengeneza yatima ni dakika tu . Nimeingia sa mwaka 1999 na final goodbye ilikuwa mwaka 2008 . huwa naenda na kurudi . nimepata matukio mengi sana ya kupoteza pesa na kuibiwa na vibaka nikiwa kwa kaburu.
Dah aisee pole sana mkuu. Mimi nilianzisha familia huku baada ya kuona umri umeruhusu mimi kufanya hivyo.

Na obvious mara ya kwanza niliishi na mzawa tukapata mtoto mmoja, ila baadae tukashindwana kutokana na tabia na wivu wake usiokuwa na msingi, hivyo nikaruka mara 1 nyumban nikachukua jiko na kuja nalo huku ambapo nimezaa nae watoto wawili. Mmoja mwakani ataingia darasa la 3 na mungine ambae mdogo ataingia la kwanza.

Huyu niliezaa na mzawa alizaliwa mwaka 2013, kwa sasa ni darasa la 5 japo naamini kuwa hapa nimepoteza mbegu yangu, lkn inanibidi nimsapoti tu kwa ajili ya maisha yake ya baadae, kwani sio yeye aliepanga kujileta duniani, bali ni starehe zetu mimi na mama yake ndio zilizosababisha leo yeye kuwepo.

Hata hivyo huku elimu yao ni bora mara 100 ya elimu yetu, au ya nchi yoyote nyingine ya Afrika. Ndomaana nimeendelea kukaza tu ili watoto wapate elimu ya kuwasaidia hapo baadae hata tutapoamua kurudi nyumbani baada ya wao kumaliza shule.
 
Mimi nipo cape town hii ishu kama Yako ilinitokea mwezi wa 4 mwaka huu ilichonisaidia ni chuma niliipiga juu wakastop gari Yao ilikua saa Tano usiku mshukuru mungu sana ulikua unakufa
Asante mkuu, dah pole sana na wewe kwa kunusurika kifo cha aina hii.
 
Rabda kama sijaelewa. Lakini Nakushauri Rudi tu Nyumbani. Kwanini uteseke roho??
Mkuu japo ushauri wako mzuri, lkn tayari nina familia. Kurudi nyumban sasa hivi ni sawa na kuuwa ndoto za wanangu.

Labda nihame mji niende kuishi mji mungine 👇
Dah aisee pole sana mkuu. Mimi nilianzisha familia huku baada ya kuona umri umeruhusu mimi kufanya hivyo.

Na obvious mara ya kwanza niliishi na mzawa tukapata mtoto mmoja, ila baadae tukashindwana kutokana na tabia na wivu wake usiokuwa na msingi, hivyo nikaruka mara 1 nyumban nikachukua jiko na kuja nalo huku ambapo nimezaa nae watoto wawili. Mmoja mwakani ataingia darasa la 3 na mungine ambae mdogo ataingia la kwanza.

Huyu niliezaa na mzawa alizaliwa mwaka 2013, kwa sasa ni darasa la 5 japo naamini kuwa hapa nimepoteza mbegu yangu, lkn inanibidi nimsapoti tu kwa ajili ya maisha yake ya baadae, kwani sio yeye aliepanga kujileta duniani, bali ni starehe zetu mimi na mama yake ndio zilizosababisha leo yeye kuwepo.

Hata hivyo huku elimu yao ni bora mara 100 ya elimu yetu, au ya nchi yoyote nyingine ya Afrika. Ndomaana nimeendelea kukaza tu ili watoto wapate elimu ya kuwasaidia hapo baadae hata tutapoamua kurudi nyumbani baada ya wao kumaliza shule.
 
FAIDA ZA VIFURUSHI VYA T!G∅ POSTPA!D.

1. GB NYINGI PESA KIDOGO.

2. UKISHAPEWA KIFURUSH MWEZI WA KWANZA MIEZ INAYOFUATA KILA TAREHE 1 UNAPEWA KIFURUSH KISHA UNALIPIA SIKU UOYOTE UKIWA NA HELA

3. UNAPEWA KIFURUSHI KISHA UNAWEZA KULIPIA KIDOGO KIDOGO KIFURUSH ULICHOCHUKUA.

4. VIFURUSHI VINADUMU MWEZI MZIMA NA KINAJIRUDIA KILA TAREHE 1 KWA MIEZ 24.YANI MIAKA MIWILI YOTE.

5. UKIWA NA DENI LA NIWEZESHE, UKIJIUNGA HUDUMA HIZI DENI LINASAMEHEWA.

6. KUNA USALAMA UNAPOJIUNGA HUWEZI KUTAPELIWA NA MTU MANA MALIPO UNAFANYA YANAENDA T!G∅ MOJA KWA MOJA, HUMTUMII MTU YOYOTE HELA.

7. MKIWA WATU WA5 AU ZAID MNAPEWA OFFER YA KUWASILIANA NYIE KWA NYIE BUREE BILA KUKATWA CHOCHOTE YANI HATAKAMA UNA SALIO 0 NA DAKIKA 0 UNAMPIGIA MWENZAKO MNAONGEA MUDA WOWOTE.

MCHANGANUO

15000 UNAPATA 15GB KILA MWEZI.

30000 UNAPATA GB 35 KILA MWEZI.

40000 UNAPATA GB 48 KILA MWEZI.

60000 UNAPATA GB 72 KILA MWEZI

100000 UNAPATA GB 120 KILAMWEZI

NJOO NIKUPE MAELEKEZO BURE UJIUNGE MWENYEWE.

KAMA NILISHAWAHI KUKUUNGA NILETEE WENZAKO NDUGU MARAFIKI WAJIUNGE THEN NIKULIPE.

NICHEKI WHATSAPP 0717700921

kama una swali karibu!!
Ok mkuu, ngoja wateja wa tigo waje wasome na kukupa mrejesho.
 
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Kwanza napenda kumshukuru mw/Mungu kwa kuendelea kunipa nafasi nyingine ya kuishi hapa duniani. Naelewa kila mtu atakufa kwa kifo cha namna yake hapa duniani, lkn katika maisha yangu nimekuwa nikimuomba Mungu siku akinihitaji kurudi kwake, basi kifo changu kiwe cha amani mfano kiwe cha usingizini, cha nyumbani nikiwa nimekaa nk.

Vifo vya kufa kwa kuuwawa mara nyingi huwa sio vizuri. Ni vya mateso na maumivu makali, japo dini hutuambia kwamba wale wanaouwa wenzao kwa namna yoyote, na wao adhabu yao huwa kubwa kwa Mungu, na pia hapa duniani kwa sheria za nchi husika. Hivyo inapotokea mtu umenusurika kifo cha kuuwawa na mtu/ watu, basi ni bora kutumia muda mwingi kumshukuru Mungu na yule/ wale waliokuwa sababu ya kukuokoa.

Let's go to the mada husika hapo chini 👇

Wakuu mimi ni mbongo nilieamua kuhamishia maisha yangu Kaburu longtime ago, japo mara nyingi huwa nakuja bongo kwa mambo yangu binafsi na kuondoka.

Usiku wa kuamkia leo, kuna ndugu yangu alikuwa anasafiri na ndege ya usiku, kutoka hapa Afrika kusini kuelekea Tz (nyumbani). Huyu ndugu yangu ni mwenyeji wa Cape Town, hivyo alivyofika hapa mimi ndio nilikuwa mwenyeji wake.

Alikuwa anaondoka na ndege ya saa tisa alfajiri, hivyo ikabidi mimi na rafiki yangu tumpeleke uwanja wa ndege wa Oliver Tambo saa sita usiku, ili awahi kufanya process zake zingine za usafiri nk, na pia na sisi angalau tuwahi kurudi kupumzika kwa ajili ya kesho (leo asubuhi) kazini. Basi baada ya kufika kule na kupiga story mbili tatu za kuagana, na baadae kufanya process zake za usafiri, sisi mida ya saa saba na nusu tukaanza safari ya kurudi nyumbani.

Wakati nakanyaga mafuta katika highway ya kutoka Kempton park kuelekea Johannesburg town, nikaona kama kuna gari fulan ndogo inatufuata kwa nyuma. Mwanzo tulijua ni gari tu ya kawaida au maybe askari wanataka watusimamishe wakague gari yetu (huo ni utaratibu wao), lkn kila nilipokuwa naongeza mwendo na wao pia waliongeza kimya kimya.

Nilivyofika sehemu fulani kuna mjengo mkubwa umeandikwa "Builders Warehouse" Edenvale, nikaingia kushoto kuelekea Edenvale road ila mimi nikakunja kushoto kuelekea upande wa Germiston road, kuangalia nyuma naona na wao wanaelekea upande ule ule ninaoelekea mimi. Sasa nikawa nishajua kwamba jamaa wanatufuata ni sisi na tukifanya masihara tutagawa maisha yetu kwa shetani (nasema ivi kwa sababu mtu anaetaka kukufanyia uovu anakuwa connected moja kwa moja na shetani) hivyo nikabidi nizidishe speed bila kujali mshale unasoma ngapi kibaoni.

Nilivyokunja pale Edenvale road kuelekea Germiston road nikavuka robot ya kwanza (mataa), nikavuka ya pili kuna daraja la highway ya gari zinazotoka Pretoria, alaf mbele nikakunja kulia jamaa wako na sisi tu japo tayari tulikuwa tushawaacha distance kadhaa. Nikakamua kweli kweli mpaka tukakutana na highway wa Albertina Sisulu, jamaa hawakati tamaa wako na sisi tu.

Tukatambaa na highway mpaka mitaa ya karibu na Eastgate Mall. Pale tukakuta kuna gari ya askari imepaki pembeni wanafanya ukaguzi wa kawaida, tukasema hapa hapa ndo tutapopatia usalama wetu. Japo hawakutaka kutusimisha, lkn ikabidi sisi wenyewe tusimame, ili tuwape maelezo ya ile gari inayotufatilia.

Wakati nimepaki pemben nashuka kwenda kuwapa maelezo wale askari tukaona ile gari nayo inakuja wangu wangu.., ila walipoona kuna askari, na sisi tumepaki tukiongea na askari, jamaa wakapandisha kwa njia ya juu kushoto inayoelekea Eastgate kwenyewe na kutokomea kusikojulikana.

Sasa kwa vile ni usiku na tulikuwa kwenye kukimbizwa na watu hatari, hatukuweza kui mark gari yenyewe wala namba za gari, hivyo ikawa ngumu kwa sisi na askari kuwakamata, kwani tulijaribu kuwafuatilia kwa nyuma na gari yetu tukiongozana na ile ya askari, lkn hola hatukuwapata, na ukizingatia J'burg ni mji mkubwa na una barabara nyingi mno. Basi tukarudi home na kulala hadi asubuhi.


Hii imenikumbusha, week 2 zilizopita, kuna mkongo mmoja alifuatiliwa hivyo hivyo kutoka Yeoville hadi kwake Bez alley. Inasemekana kuwa mkongo baada ya kufika kwake alifungua mlango fasta, na kuingia kwake. Ila bahati mbaya (au naweza kusema siku zake zilikuwa zimefika) hakuwa amebana vizuri gate la kuingilia kwake, na jamaa wakawa wameshafika na kuona nyumba aliyoingia. Jamaa wakapush mlango, wakaingia ndani na kukuta watu wakiwa hawana hili wala lile, jamaa wakiwa na "double 9" mkononi wakauliza yule mtu aliekimbilia humu yuko wapi? Mpopo (nigeria guy) mmoja akajibu hatujamuona, kabla hajamaliza kauli akapigwa ya Paja, na kuelekezewa nyingine kichwani, akaambiwa tunauliza kwa mara ya mwisho, bila jibu sahihi tunafumua ubongo na kukamata mungine mpaka tutawamaliza. Walivyouliza kwa mara ya pili, wote wakajibu pamoja kwamba amejificha chooni.

Ndo wakamwambia mpopo akawaoneshe chooni, kweli Ile kuingia wakakuta jamaa kajificha anatetemeka. Wakamtoa nje mbele ya familia yake, wakamuomba funguo za gari na simu, akawa funguo akasema hana simu. Basi jamaa wakafumua kichwa kwa risasi 4 mbele ya ndugu zake, alafu funguo ya gari wakaachana nayo wakatoka nje na kutokomea kusikojulikana.

So na sisi tulivyokuwa tunafuatwa, basi nilihisi na mimi yanakwenda kunikuta yale ya mkongo. Kwamba huenda jamaa wamepewa dili tu kama ilivyotokea kwa yule mkongo au labda walikuwa ni majambazo wa magari nk.

Huu ndio unakuaga mwezi mgumu, na hatari kuliko miezi yote hapa Kaburu. Wengi huwa tunaweka mbele maombi na dua mbali mbali ili kuuvuka salama mwezi huu.
OR Tambo Airport ni hatari sana kutoka nje kwa mida ya usiku. Ni hatari zaidi kwa kipindi hiki cha mwisho wa mwaka (Peak Season). Majambazi wengi huwa wanakuwa hapo sehemu ya watu wanaowasili (arrivals) wakichora ramani ya wageni wanaowasili ambao Wana fedha nyingi ili wawafuatilie na kuwapora.
Aidha, majambazi hao pia Wana connection na wale watu wa "bureau de change" zilizopo hapo ndani airport.
 
Shukran sana kwa ushauri mzuri kaka yangu The Boss ila kabla ya kuhamia huko inabidi mtu ujipange. Mimi kwa sasa nina familia hapa SA, hivyo siwezi kuhamia huko kichwa kichwa bila connection au kujipanga sawa sawa.
Mkeo msouth?nimewahi sikia wanawake wa South Africa...mwanamume mgeni akipata hela wanachonga mchongo anauwawa ili wabebe mali
 
Back
Top Bottom