Jinsi polisi walivyonusuru maisha yangu last night

Jinsi polisi walivyonusuru maisha yangu last night

Hapana mkuu, japo niliwahi kuzaa na msauzi, lkn mke wangu ninaeishi nae huku ni mbongo. Ila tayari tumeshazaa nae watoto wawili, mmoja anaingia darasa la tatu mwakani, na mdogo ataingia la kwanza.

Elimu ya hapa inafaida kubwa kwa nchi yoyote ya Afrika. Hivyo naona bora niendelee kupambana ili kuwapatia watoto wangu elimu bora kwa maisha yao ya baadae.

Pia huyo mtoto niliezaa na mzawa kwa sasa yupo kwenye mikono yangu namsomesha na ashafika la 5. Huyu pamoja na kwamba simtegemei sana kama nitaweza kurudi nae nyumban pale itapobidi kurudi, lkn naona ni damu yangu, siwezi kuacha kumpa haki yake ya msingi kwa ajili ya maisha yake ya baadae hata ntakapokuwa sipo hapa.

Sababu yeye hakupenda au kupanga kujileta mwenyewe dunia, bali ni starehe za sisi wawili (mimi na mama yake) ndio zilizosababisha ujio wake. Hivyo ni lazima nimpambanie kwa ajili ya dreams zake.

Nikiona presha inazidi nitahamia mji mungine, maana nchi hii ni kubwa na kila mji au kila sehemu kuna fursa zake.
Yaani umemzalisha mwanamke mzawa na kumtelekeza? wewe hawakuachi.
 
Sawa brother ila hakuna ruhusa ya Polisi wa SA kukimbiza gari na raia wanachokifanya ni kutoa taarifa kwenye radio call na wanawatafuta kwa mawasialiano kama wana hatari sana wanaweza kutafutwa kwa Chopa upo sawa na pia sijui ulipita wapi ila kutoka Airport Robot ya kwanza ni hiyo hapo East Gate Mall kama ulitoka na R 24 na ukaunga baadae na Albertina Sesulu Road na hapo chini kushoto mara nyingi wazee ndio huwa wanapenda kukaa hapo East Gate na wengine walikua wale Polisi wezi wanawazuia watu hapo wanaotoka Airport kwa kujifanya Polisi na kuwaibia Mali zao...ili uwe salama mara nyingi unatakiwa uingie kama unaingia kwenye hiyo Mall then unakata kulia unaendelea na safari ili kuwakwepa hao wezi wa kwenye mataa wa usiku..
 
Pole sana! Na hongera kuwa makini. Mara nyingi watu wanaotoka Airport au Shopping malls wanakuwa wanawindwa sana na vibaka.Mungu akulinde Ndugu. Kitambo sana hapo Hillbrow Flamingo Hotel, wape high majita wote hapo the pertz na mitaa mingine
Asante sana mkuu kwa maombi na dua yako kwangu. Kuhusu salam kwa masela nitawafikishia tu mkuu wangu.

Mungu akubariki ndugu yangu
 
Pole mzee, SAUZI ni nchi ya hatari sana kuishi.
Ongeza umakini kuanzia unapoamka mpaka unaingia kulala.
Ikiwezekana fuatilia tu upate kibali uwe na cha moto.
Nimeona umesema kupata kibali ni changamoto, pambana upate mzee.
 
Yah mwanume ninlazima kupambana , ila lazima uwe na exit plan , nimeona unasema hapo kuwa umeshaanzisha familia huku Sa , hapo sasa your hands are tied . katika vitu niliapa sitafanya ni kuanzisha familia kwa kaburu. Yani huko kutengeneza yatima ni dakika tu . Nimeingia sa mwaka 1999 na final goodbye ilikuwa mwaka 2008 . huwa naenda na kurudi . nimepata matukio mengi sana ya kupoteza pesa na kuibiwa na vibaka nikiwa kwa kaburu.
Wanasema south africa uzunguni pamekuwa pagumu mno kuingilika na vibaka kwai io siku iz vibaka shughuli za ukabaji wamezihamishia kwa weusi wenzao
 
Tatizo watu wa nje( hasa wanigeria na watanzania) wanafanya biashara haramu ya unga, wizi, utapeli, ndio kinachowakera wazawa wa huko
South Africa kuna mchanganyiko mkubwa sana wa wahamiaji kutoka karibu nchi zote za hapa.duniani. Ndio nchi pekee ktk bara la Afrika yenye wahamiaji wengi zaidi, na hii imekuwa sababu mojawapo ya kuongezeka kwa matukio ya uhalifu kwenye nchi hiyo due to the "scramble of scarce resources."
 
Sawa brother ila hakuna ruhusa ya Polisi wa SA kukimbiza gari na raia wanachokifanya ni kutoa taarifa kwenye radio call na wanawatafuta kwa mawasialiano kama wana hatari sana wanaweza kutafutwa kwa Chopa upo sawa na pia sijui ulipita wapi ila kutoka Airport Robot ya kwanza ni hiyo hapo East Gate Mall kama ulitoka na R 24 na ukaunga baadae na Albertina Sesulu Road na hapo chini kushoto mara nyingi wazee ndio huwa wanapenda kukaa hapo East Gate na wengine walikua wale Polisi wezi wanawazuia watu hapo wanaotoka Airport kwa kujifanya Polisi na kuwaibia Mali zao...ili uwe salama mara nyingi unatakiwa uingie kama unaingia kwenye hiyo Mall then unakata kulia unaendelea na safari ili kuwakwepa hao wezi wa kwenye mataa wa usiku..
Yah ni kweli ulichoongea kuhusu robot ya kwanza hapo Eastgate, lkn hao polisi hawakuwa maeneo ya robotini bali walikuwa wametinga nyuma kabisa karibu na ile barabara inayopandisha kushoto kuelekea Eastgate Mall kama unatokea Albertina Susulu.

Kuhusu askari kukimbiza gari na raia hilo pia linafanyika. Kuna siku moja week end asubuhi nilienda kunyoa sehemu (salon). Sasa wakati nikiendelea kunyolewa, mimi pamoja na wateja wengine tukaanza kusikia risasi zinalia nje, ikabidi wote tutoke nje kuangalia nini kinaendelea. Wakati tunatoka kuangalia, tukaona jamaa mmoja anatoka ndani ya gari yake (ilikuwa hiace quantum) akiwa na bomba mkononi akijaribu kurusha na yeye risasi kuelekea upande wa mbali kidogo ambapo kulikuwa na gari nyingine tena aina ya X5 ikiwa na jamaa wawili waliokuwa wakimshambulia jamaa kwa risasi pia bila mafanikio wala kumjeruhi (nahisi zilikuwa beef zao) hivyo sisi wote tulivyoona jamaa anaelekea upande wetu tukawahi kufunga mlango wa salon na kukimbilia uwani, lengo ni kutaka jamaa asiingie mle salon maana pengine jamaa wangemfata na kusababisha vifo na kwetu pia.

Sasa yule jamaa akapitiliza hadi Spar, maana salon ilikuwa karibu na Spar ambapo kuwalikuwa na askari wamekuja kununua vitu Spar, alaf muda wote huo walikuwa hawajui hili wala lile. Jamaa akakimbilia ndani ya Spar na kuwataarifu askari, wale jamaa walipoona yule mtu kaingia za Spar wakageuza kurudi kwenye gari yao. Jamaa nae akawataarifu askari kuwa kuna watu wanamkimbiza. Hivyo wazee walichofanya wakampakia jamaa kwenye gari lao na kutoka nae kwa kasi sana lengo la kuwawahi na kuwa tight jamaa eneo la tukio. Kwa bahati mbaya walipotoka wakakuta ile gari ya wale majamaa imeshaondoka tayari. Hivyo ikabidi waende na jamaa kituoni wakaandike maelezo ya kilichotokea.

Hiki kilikuwa ni kile kipindi cha mabeef ya madereva texi (mabasi) wenyewe kwa wenyewe.

Hivyo muda mungine raia anaweza kusaidia kuwapata wale wanaomtafuta wamuue kama anawafahamu vizuri wauaji.
 
Pole mzee, SAUZI ni nchi ya hatari sana kuishi.
Ongeza umakini kuanzia unapoamka mpaka unaingia kulala.
Ikiwezekana fuatilia tu upate kibali uwe na cha moto.
Nimeona umesema kupata kibali ni changamoto, pambana upate mzee.
Asante sana mkuu. Itabidi nipambane kwa namna yoyote ili nipate kitu cha kunilinda.
 
Pole mzee, SAUZI ni nchi ya hatari sana kuishi.
Ongeza umakini kuanzia unapoamka mpaka unaingia kulala.
Ikiwezekana fuatilia tu upate kibali uwe na cha moto.
Nimeona umesema kupata kibali ni changamoto, pambana upate mzee.
Asante sana mkuu. Itabidi nipambane kwa namna yoyote ili nipate kitu cha kunilinda.
 
South Africa kuna mchanganyiko mkubwa sana wa wahamiaji kutoka karibu nchi zote za hapa.duniani. Ndio nchi pekee ktk bara la Afrika yenye wahamiaji wengi zaidi, na hii imekuwa sababu mojawapo ya kuongezeka kwa matukio ya uhalifu kwenye nchi hiyo due to the "scramble of scarce resources."
Huu ni ukweli ambao haupingiki mkuu.
 
Back
Top Bottom